Hatunaga kabaya Mamy..Ubaya mliuanza wenyewe 😅
ndomaana tunawalea kama watoto..
ila ndo hvo mnatuvuruga vichwa vyote
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hatunaga kabaya Mamy..Ubaya mliuanza wenyewe 😅
Kawaida hamna kesi hapo,,Atapoteza muda na pesa Bure,Bora asamehe TU mkuu!akaripoti polisi Kwa ushahidi tu halafu aiache jamhuri kama itahangaika na hiyo kesi!!
Mkuu mbna unaongea Kama mepesi hivyoKawaida hamna kesi hapo,,
wangu baada ya kusomesha miaka 2.
Kanipiga na chuma kizito Mwisho katimua na milion.
Napata habari binti yako ana mimba huko.
Tumeongea kashazaa tayari,na huyo bwana katoka baru.
Mpk sasa sina hamu.
Binti mwenyewe ukiongea nae anakwambia 'mbona we ulimtia mimba mamaangu bado kijana mkanizaa mimi?"
Unatoa mimacho🙄.
Nna kajukuu sasa,
poa tu na single maza yupo
Aliyemzalisha ntamtafuta alipe gharama zangu zoote kabla sijafa.
NI kweli mkuuPole mkuu na changamoto.... Wanawake washenzi huaribu sana future za watoto hasta wa kike.
Asante mkuu kwa USHAURI mzuriMkuu huu sasa ndio wakati wakuonyesha kuwa wewe ni BABA, Bahari yenye mawimbi ndio hupima ubora wa Nahodha.
BABA sio jina la ubatizo, ni Majukumu na kupambana na matatizo yote yanayokuja mbele yako. Mtoto ameshazingua, so what? malalamiko na masikitiko hayatakupa matokeo yoyote mapya.
USHAURI: Kwanza kubali kuwa ulikosea kumpeleka kwa Mama yake, na pia utambue haya mambo yanawatokea Binadamu(You are not special). Mtunze Binti yako hadi atakapojifungua kisha uangalie namna ya kupambana na yanayokuja mbele yako.
Be a Man, Focus na kutafuta maisha na pesa kwa ajili ya uzee wako, Hili la Binti yako lisivuruge Utafutaji wako au kukupa pressure na magonjwa ya moyo.
Yaani poleWanawake ni watu wa hovyo sana zaidi ya sindano ya ncha kali jichoni ngoja nikupe mkasa niliokuwa nao hivi sasa
Nilikuwa na Ex wangu nilifanikiwa kuzaa naye mtoto mmoja kipindi hicho ndo damu ilikuwa bado mbichi (balehe) yule dada alijifungua akapata mtoto Ila kiukweli niliona si mwanamke sahihi wa kuoa
Mtoto kakaa naye hadi katimiza mwaka na nusu huku natuma pesa ya matumizi kufika miaka mitatu yule mtoto akaniletea nyumbani kwangu mie nipo kazini
Ikumbukwe hapo ndo nimeoa sina muda mrefu wife ni mjamzito kaja kambwagia wife mtoto huku akimwachia ujumbe kwamba mtoto kamshinda kumlea kwa kuwa amepata mume wa kumuoa na hataki mtoto nyumbani kwake basi kaamua amlete kwa baba yake
Mie narudi kazini sina hili wala lile nakuta mabegi yapo mlangoni huku wife yupo kwenye kiti ananingoja anikabidhi funguo kwa jinsi nilivyomuona nikajua hapa usalama hakuna. Nikimsalimia pale lakini hakuitikia kumuuliza kulikoni akanambia nenda ndani kamfungulie neti mgeni wako
Laaahaula naingia ndani nakuta mtoto kumuangalia vizuri namuona Farida nikasema leo nishafedheheka
Nikarudi kwa mama mtu kumuuliza kulikoni mbona kile kiumbe kipo hapa akanipa mkasa wote
Kufupisha story yule mtoto nikamlea na wife akanielewa akamlea mtoto kama wake akamfunza maadaili yote ya mtoto anatakiwa awe nayo nashukuru Mungu yule mtoto kamaliza kidato cha nne lakini hakupasi vizuri mwaka huu amerudia mitihani.
Tatizo limeanza pale mama mzazi wa yule mtoto alikuwa anaumwa kaumwa sana kiasi Cha kulazwa kuchunguzwa aliambiwa ana uvimbe kwenye uzazi inabidi afanyiwe upasuaji yule mzazi mwezangu akaniomba yule binti aje amsaidie kumuhudumia na vile hakubahatika mtoto AISEEE hilo ndo kosa kubwa nililolifanya maishani mwangu kumruhusu yule binti yangu kwenda kwenye himaya ambayo hakutakiwa kuishi kwa umri alokuwa nao yaaani najuta mpaka kesho Kama baba nilishindwa kumfanyia maamuzi sahihi binti yangu
Yule binti alienda kumuhudumia mama yake kwa usaidizi wa mambo madogo pale nymbn ambako asubuhi anaenda shule jioni akirudi anamwangalia mama yake ilapita wiki mbili yupo kule mwezi nikijua bado yupo na mama yake nikimpigia mzazi mwezangu ananiambia hajambo anaendelea vizuri huku akinipa moyo binti yetu atamrudisha muda si mrefu
Nikakaa nikasema mbona siku zishakuwa nyingi na hakuna dalili ya mtoto kurudi nikaenda kule anapoishi yule mzazi mwezangu kufika pale nikagonga mlango kimya kuchungulia ndani taa hazijawashwa kiufupi hamna dalili ya kuwepo mtu ikabidi nizunguke kwa jirani niulize hawa watu wako wapi AISEEEE jibu nililolipata niliishiwa na nguvu
Yule jirani kanambia huyo dada hayupo kaenda zake kwao kikijini kuvuna nikamuuliza vipi yule binti yake yupo wapi akanambia yule binti kampeleka kwa shoga yake akakae mpaka arudi. Yaani nilipandwa na hasira maradufu lakini nikapiga moyo konde nikasema ngoja nimpgie muhusika inawezekana haya sio ya kweli
Kumpgia simu akapokea nikamuuliza uko wapi akanambia kaenda harusini kwa rafiki yake nikaguna kidogo mana jibu lile halikuniridhisha nikamwambia mie nakungoja hapa kwako mana nimekuja kukujulia hali na kumuona mwanangu alichonijibu sasa eti we nenda mie Leo sirudi Kama haurudi vpi kuhusu mtoto atalala wapi akanambia mtoto kampeleka kwa rafiki yake nilijihisi joto la ghafla sikuishia hapo nilitaka nimchimbe zaidi nikamwambia bhas nielekeze ulipo nije nikuone mara moja mie nirudi zangu nyumbani
Akasema sio rahisi kuonana Leo kiukweli kwa maneno Yale nilihakikisha asilimia mia huyu mtu hayuko mkoa huu nikakata simu
Huku nikjiuliza hivi huyu mwanamke yupo timamu kweli binti kamchukua kwangu kama alikuwa anasafari zake na hawezi kuwepo nyumbn kwanini asimrudishe nyumbani kuliko kumuachia uhuru mtto afanye anachojiskia na istoshe yule binti yupo katika majaribu ya usichana wake nikashindwa kupata jibu
Ikabidi nimpgie simu nimuambie ukweli kwamba kila kitu nishaambiwa na majirani zake mie Sina shida na yeye anielekeze mwanangu alipo nimrudishe nyumban akanambia atampigia simu shoga yake amwambie mtoto arudi zake nyumbn tukamalizana hvyo
Kesho yake mchana binti yangu anarudi nyumbani namuona binti yangu kabadilika kuanzia mavazi rangi mpaka maongezi yake kiufupi mwanangu kaja na kiguo utasema changudoa rangi yake nyeusi ya kuvutia yote imepotea kawa wa njano Kama papai hata ile furaha ya kurudi kwao hana kila nikiangalia uwezekano tena wa kusoma haupo mtoto kajazwa maneno na mama yake huyu mke wangu aliyemlea yule mtoto anaonekana mbaya mtoto kukaa nyumbn akatulia hawezi tena muda wote simu mkononi mguu na njia yaani ile miezi minane ilitosha kabisa kumbadilisha mwanangu na kuwa kiumbe tofauti kabisa wiki hii ninavoongea na nyinyi binti yangu amebainika mjamzito kumbana ananiambia ni rafiki wa mama yake ndo aliyemtia ujauzito ule.
Niliishiwa na nguvu kabisa nisijue nimfanye nini yule mtoto na mama yake kumbe wakati mama yake kasafiri yule mtoto na rafiki ya mama ake alikuwa akizalimishwa wazagamuane mpaka yule mtoto huo mchezo ukamkolea yaaani mpaka nakosa nguvu za kulikabili hili jambo.
Naungana na weweHaikuwa na sababu ya kumuacha miezi miwili atange tange kwa shoga yake natamani nimfanye kitu kibaya yu mwanamke
Ajifungue au aitoe?????? yash_ed hakikisha unamtoa hiyo mimba.Ingekuwa Busara kama ungetumia neno la Baadhi ya wanawake, kwa sababu sio wote wenye tabia kama hiyo.
Lakini pole kwa yote. Mtoto bado ana nafasi ya kubadilika.
Muache ajifungue na umrudishe shuleni.
Pole sana mkuu ila bado kosa ni lako mkuu, wewe ndo ulimchagua, wewe ndo ukazaa nae, wewe ndo ukamtelekeza, wewe ndo ukampa mtoto alee na wewe ndo ukampa tena mtoto kwa miezi sijui nane blla kumfatilia.Mjukuu Hana kosa na Wala siezi mnyooshea kidole mjukuu
Tatizo mama mzazi wa mtto unanuacha vp binti yako kigoli kwa rafiki yako wa kiume
Ukumbuke mama yake nilifata process kwa wazazi wake Ila yeye alinionesha picha sio nikasita kuoa
Huyo rafiki wa mzazi mwenzio umeshampeleka Mahakamani kwa kumpa ujauzito mwanafunzi?Nikjiuliza Hilo swali nakosa jibu
Zingatia ushauri huuMkuu huyo bazazi mpige tukio la kubaka mwanafunzi kama binti Yuko tayari kutoa ushirikiano!!
Kakimbia mjiHuyo rafiki wa mzazi mwenzio umeshampeleka Mahakamani kwa kumpa ujauzito mwanafunzi?
NI kitu kabisa mie nna mchango wa kumtumbukiza mwanangu hukoPole sana mkuu ila bado kosa ni lako mkuu, wewe ndo ulimchagua, wewe ndo ukazaa nae, wewe ndo ukamtelekeza, wewe ndo ukampa mtoto alee na wewe ndo ukampa tena mtoto kwa miezi sijui nane blla kumfatilia.
Nipo navizia akirudi jijini amazangu amazakeNaungana na wewe
Mtie kilema hata Cha kidole tu kumkata inaumiza sana
Huyo Binti usimkatie tamaa please
Mkuu kwa tabia zake za hovyo majiran wako mstari wa mbele kunipa ushirikianoKwa Nini ulitoa source ya taarifa kuwa majirani ndio wamekuambia?. Hii tabia mbovu Tena wanayo wanaume wasio na misimamo unapewa taarifa wewe unatoa Siri nani kakupa, umenikera mno katika hili. Unadhani akirudi uhusiano wake majirani utakuwaje?. Yaani mpaka hapa na mengine ya mbeleni yatakushinda. Sina ushauri kwako.