Jinsi gani uliweza kuendelea baada ya kuachana na mpenzi uliyekuwa unampenda sana?

Unapoteza muda wako bure, kama mtu haswa mwanamme kakuacha ni kwa sababu kakuona haufai maishani mwake na ndiyo maana hakufikirii. Don't force yourself kwenye mahusiano mengine ya haraka, kaa chini na ujifikirie nini tatizo. Usihofu keep yoursef busy, Yes - it will take time lakini utafika tu na kuna uwezekano utapata mtu wako sahihi atakayekupenda na mapungufu yako.
 
Hiii unaweza kukusaidia kumove on.
Sikia,
Kumkumbuka ex sio kuwa hujamove on aiseeh.

Unamkumbuka kwa kuwa yupo maisha uliwa kuwa nayo pamoja nae.
Hii inatosha kabisa kutomsahau.

Kutokumove on ni pale, bado unamtamani, bado unaumia kumuona ana mahusiano mengine, bado unamfuatilia issue zake.

Lakini kumkumbuka tu nimetoka kitu mutual mlifanya ndo uone hujamove on.
Relax, huwa inaenda na muda.

Kikubwa ishi mama, katika kuishi unaona maisha yalivyo bado yana furaha na yanahitaji kuyafurahia kuliko kuumia na vilivyokwisha pita.

Ila, nakuelewa.
 
Nimebarikiwa na neno nkamu. Msiseme nimeanza ubaguzi

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu umenikumbusha jinsi nilivyo mpenda mrembo huko kijijini nilimpenda sana kupitiliza,sku moja mama yeke mzazi akaugua ilibidi niuze baisekeli yangu ili mama yake akatibiwe lakini niliachwa kisa umasikini nilikonda kabisa,nika amua kukimbilia mjini tukapotezana kabisa miaka ikasonga,ili nichukua mda sana kumsahau,baada ya miaka kadhaa kupita nikaenda kijijni msibani akaniona eti akajiliza umenenepa umependeza mara nisamehe turudiane nikawa na mcheki tu,baada ya msiba kuisha nikaanzisha na ujenzi kabisa hapo nyumbani ujenzi ukaenda halaka,akaja kuomba kibarua cha kusaidia mafundi nikamwambia aongee na fundi mm si husiki akawa ananisema eti nimepata pesa kidogo nimeaanza kuringa,nikawa namshangaa tu wakati huo namona sio saiz yangu tena maana alikua amepigwa na maisha amechoka,ila namshukuru asinge niacha ningekua bado kijijini mpaka leo.
 
Mkuu kila jambo linalotokea linakuwa na sababu...cha msingi ni kumshukuru Mungu kwa kila jambo pasipokujali ni kiasi gani linatuumiza, (na hapa ndipo huwa tunapokosea maana badala ya kushukuru tunaanza kulalamika na kulaumu).
 
alinitumia text whatsapp "mpenzi kukweli nmejitahid sana ila naona sina hisia za kimapenz na ww".

baada ya muda kidogo akaweka clip status jamaake mpya anamfundisha kuendesha gari nikawa nasikia "baby siku 3 mbele ntakuachia uwe unaendesha mwenyew unaonekana una kichwa chepesi" demu wangu akajibu kwa madeko huku akikanyaga mafuta "thawa sweetheart"


sikilizia ayo maumivu.
 
Hahahaha...."Eti thawa sweetheart"

Hajaachwa bado?
 
Pole Sana.
Mambo gani yanakufanya ushindwe kumtoa kichwani????
Je,umezaa naye?
Umejenga naye?
Alishakutolea mahari? n.k

Ni Heri uchumba uliovunjika kuliko ndoa mbovu.
Uchumba siyo ndoa,lolote linaweza kutokea.

Mapenzi ya kweli hayalazimishwi.

Mshukuru Mungu kwa yote na muombe akusaidie kuendelea mbele.
Kufikiria Sana hakutatatua tatizo lako.
 
Hahahhahah nimecheka kama mazuri. Daah kuna watu wanajua kuumiza wenzao; naamini ulishapona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…