Jinsi nilivyothibitisha Uchawi, hutoamini nakwambia!

Jinsi nilivyothibitisha Uchawi, hutoamini nakwambia!

Hakuna uchawi. Uchawi haupo.

Ni watu wapumbavu [blithering idiots] tu wanaoamini uchawi upo.

Sasa ukichanganya ujinga na upumbavu, unapata uzuzu.

Siku hizi kuna drones ambazo hazionekani kwa rada.

Mtu akirusha stealth drone yake yenye uwezo wa kufanya mashambulizi na kumlenga adui na kumuu bila kujua hizo risasi zimetoka wapi, mazuzu wanasema huo ni uchawi kumbe ni sayansi tu na teknolojia.

Ni rahisi sana kuwadanganya Watanzania.
 
Hakuna uchawi. Uchawi haupo.

Ni watu wapumbavu [blithering idiots] tu wanaoamini uchawi upo.

Sasa ukichanganya ujinga na upumbavu, unapata uzuzu.

Siku hizi kuna drones ambazo hazionekani kwa rada.

Mtu akirusha stealth drone yake yenye uwezo wa kufanya mashambulizi na kumlenga adui na kumuu bila hizo risasi zimetoka wapi, mazuzu wanasema huo ni uchawi!

Ni rahisi sana kuwadanganya Watanzania.
Sikia mkuu unaongea kwa sababu hujawahi kutana na TUKIO ZITO wewe, na hujawa exposed to maisha
 
ni kweli uchawi upo,na ndo manake BIBLIA au MUNGU anasema"usimwache mwanamke mchawi kuishi" na ata QURAN tukufu inasema "acheni USHIRIKINA!!!,,,,,,,,,,okay ata mimi nilishawai kukutana na jirani yangu mwanamke shambani saa nane usiku!!! akiwanga,juu kavaa kaniki nyeusi,chini kavaa kaniki nyekundu,huku akirukaruka!!
Mkuu elezeaa vizuri
 
images (2).jpeg
 
Hakuna uchawi. Uchawi haupo.

Ni watu wapumbavu [blithering idiots] tu wanaoamini uchawi upo.

Sasa ukichanganya ujinga na upumbavu, unapata uzuzu.

Siku hizi kuna drones ambazo hazionekani kwa rada.

Mtu akirusha stealth drone yake yenye uwezo wa kufanya mashambulizi na kumlenga adui na kumuu bila kujua hizo risasi zimetoka wapi, mazuzu wanasema huo ni uchawi kumbe ni sayansi tu na teknolojia.

Ni rahisi sana kuwadanganya Watanzania.
Vipi kama huo uchawi ni jina la teknolojia ya kiafrika ambayo huwezi kuiona kwa macho kama ambavyo unajua una malaria ila huwezi kuviona vimelea kwa macho bila kupitia microscope..

Sasa kama wewe unaaminishwa unaumwa malaria kwa dalili tu pasipo kuthibitisha kwa microscope "mwenyewe" Kwa sababu huna utaalamu huo, kwa nini umuone mtu mwendawazimu kwa kuamini anarogwa na akaponywa na mtaalamu kwa sababu tu "hujauona huo uchawi kwa macho"..
 
Hakuna uchawi. Uchawi haupo.

Ni watu wapumbavu [blithering idiots] tu wanaoamini uchawi upo.

Sasa ukichanganya ujinga na upumbavu, unapata uzuzu.

Siku hizi kuna drones ambazo hazionekani kwa rada.

Mtu akirusha stealth drone yake yenye uwezo wa kufanya mashambulizi na kumlenga adui na kumuu bila kujua hizo risasi zimetoka wapi, mazuzu wanasema huo ni uchawi kumbe ni sayansi tu na teknolojia.

Ni rahisi sana kuwadanganya Watanzania.
Yeah. Ni kweli kwani watanzania ni wepesi kuamini badala ya kuchunguza, kudadisi au kutafakari kwa kina kwanza; wengi wakikosa jawabu, haraka wao hukimbilia jawabu rahisi i.e. ni Uchawi. Ukimwambia akuelezee huo uchawi ukoje anaishia kukwambia "we hayajakukuta".
 
Mkuu elezeaa vizuri
Ata musa naharuni walivoagizwa kwa farao ili awaachie wana wa israil[waliagizwa na MUNGU,]MUNGU aliwapa fimbo akamwambia musa,ukifika farao atatuma wachawi waje wawajaribu wakitupa fimbo zao na wewe tupa fimbo yako,basi walipofika kule walifanya ivo,wachawi walipotupa fimbo zao za kichawi zikageuka nyoka,musa nae akatupa fimbo alopewa na MUNGU,basi fimbo ya musa ikageuka nyoka,na nyoka wa musa akameza fimbo za wachawi
 
Ata musa naharuni walivoagizwa kwa farao ili awaachie wana wa israil[waliagizwa na MUNGU,]MUNGU aliwapa fimbo akamwambia musa,ukifika farao atatuma wachawi waje wawajaribu wakitupa fimbo zao na wewe tupa fimbo yako,basi walipofika kule walifanya ivo,wachawi walipotupa fimbo zao za kichawi zikageuka nyoka,musa nae akatupa fimbo alopewa na MUNGU,basi fimbo ya musa ikageuka nyoka,na nyoka wa musa akameza fimbo za wachawi
Kwa mantiki hiyo, ina maana kwamba Mungu ni mchawi zaidi sio?
 
Ndugu zangu wa JamiiForums, napenda kushiriki nanyi tukio la kushangaza lililotokea maishani mwangu, ambalo lilinionyesha wazi kuwa uchawi upo! Mpaka leo nikikumbuka usiku ule, mwili hunisisimka na maswali hayaishi kichwani mwangu.

Usiku wa Ajabu

Ilikuwa ni usiku wa manane, saa nane hivi. Nyumba ilikuwa kimya kabisa, kila mtu amelala, lakini ghafla niliamka nikiwa na hisia ngeni. Kulikuwa na ukimya wa ajabu, ukimya ambao hukufanya usikie hata sauti ya mapigo ya moyo wako. Nilihisi kama kuna mtu au kitu ndani ya chumba changu, ingawa mlango ulikuwa umefungwa na madirisha yakiwa salama.

Niliinama kidogo nikatazama chini ya kitanda—hakukuwa na kitu. Nikanyanyuka taratibu na kuwasha taa ya simu yangu, kisha nikapeleka macho dirishani. Ndipo nikamuona mtu akisimama nje ya nyumba yangu, umbali wa kama mita tano, akiwa hana kiatu na amevalia mavazi meupe yaliyochafuka. Uso wake haukuwa wazi, lakini mwili wake ulikuwa umetulia kimya bila hata kusogea.

Nilihisi hofu ikianza kunizidia, lakini nikajipa ujasiri. “Labda ni mwizi,” nilijiambia, nikachukua fimbo yangu ndogo niliyokuwa nayo chumbani. Nikaamua kumfuata taratibu ili nione kama kweli ni mtu wa kawaida au kuna jambo lingine.

Tukio Lisiloeleweka

Nilipofungua mlango na kutoka nje, cha kushangaza ni kuwa mtu yule alionekana kama vile anateleza ardhini badala ya kutembea! Hakutembea kwa miguu kama binadamu wa kawaida. Niliendelea kumfuata kwa tahadhari, lakini kila nilipomsogelea, alionekana kusogea mbali zaidi bila hata kukimbia.

Nilipojaribu kupiga kelele ili majirani wasikie, sauti yangu haikutoka! Nilihisi kama koo langu limefungwa ghafla, kama mtu aliyebanwa na mkono wa ajabu! Hofu ilinizidi, nikaanza kurudi nyuma haraka kuelekea ndani. Nilipofika mlangoni na kugeuka kutazama tena, yule mtu alikuwa ametoweka ghafla—kana kwamba hakuwahi kuwepo!

Ushahidi wa Ajabu

Siku iliyofuata asubuhi, nilipowaeleza majirani kuhusu tukio hilo, baadhi yao waliniambia kuwa jirani yetu mmoja alifariki usiku huo huo nikiwa napambana na kiumbe kisichoeleweka! Inasemekana mtu huyo alikuwa anahusishwa na vitendo vya ushirikina na alishawahi kushukiwa kuwa mchawi wa mtaa.

Kwa hakika, tangu siku hiyo, niliamini kuwa kuna vitu ambavyo akili ya kawaida haiwezi kuelewa. Mpaka leo, sijui yule mtu alikuwa nani hasa, wala alitowekaje bila hata kusikika. Uchawi upo ndugu zangu, na mimi nimeshuhudia kwa macho yangu!

Je, umewahi kukutana na tukio kama hili? Niambie!
Wewe unalala njaa ndio maana unaota ndoto za ajabu
 
Back
Top Bottom