Jinsi Ninavyopambana na Gharama za Usafi wa Nyumba na Mwili

Jinsi Ninavyopambana na Gharama za Usafi wa Nyumba na Mwili

Tuwekee na gharama ya kiasi cha pesa unachotumia kwenye manunuzi ya hivyo vifaa vya usafi kwa wastani wa siku au wiki.
 
Ndio namaliza muda huu kusafisha maliwato yangu na nimetumia dakika 30,dakika 10 ni kuyaacha madawa na sabuni yanyonye uchafu sakafu na masinki na vyoo na dakika 20 ni kusugua,kusafisha na kukausha.Pametakata na sote mie na mke wangu tumefurahi.Yeye anajiandaa kwenda job mimi leo na darasa la tution.Sasa kuna kuna kitu sikukueleza kwenye maandishi ya yangu ya awali juu ya somo hili,nacho ni:
Usafi wa masikio
Natilia mkazo sana usafinwa masikio na huu siwezi kuufanya mimi ni lazima nimpe mke wangu,aufanye,anatumia earbuds ambazo huichovya kwenye spirit na kusafisha uchafu fulani hivi ambao hutokea kwenye masikio na akimaliza,kuchukua mkasi na kutoa nywele zinazoota kwenye masikio na huwa anatumia mashine fulani hivi,ambayo huja kwenye set,unanyoa ndevu,sharubu na nywele za kwenye pua na masikio,baada ya hapo ndio naoga,navaa na kuangalia kazi za siku
 
Usafi uwe kwa kiasi, maana muda unaotumika kwenye usafi usizidi ule wa mambo mengine, kila jambo kwenye routine zetu tulipe muda......
 
Leo nawaletea changamoto nyingine ninayokumbana nayo baada ya kuzungumzia gharama za maji ya kunywa na umeme. Safari hii ni kuhusu gharama za usafi wa nyumba na mwili:

a) Usafi wa Nyumba (Eneo la Maliwato)

Eneo la maliwato, ambalo lina choo na bafu, kwa Waingereza huitwa self-contained. Kwenye sehemu hii, natumia vifaa na bidhaa mbalimbali kama:
  • Sabuni za unga na maji,
  • Madawa ya kuua wadudu kama Jik na Dettol,
  • Sabuni zenye harufu nzuri, na
  • Pafyumu za hewa nzuri, za kupulizia na zile zisizohitaji kupulizwa.
Nyumbani kwetu tuna vyoo vya aina tatu:

1. Choo cha kukaa,
2. Choo cha kukojolea wanaume, na
3. Choo cha kukojolea wanawake.

Hii tumeweka ili kuzuia maambukizi kama UTI. Tunashirikiana na mke wangu kutumia choo cha kukaa pekee. Changamoto kubwa ni kwamba mimi nina passion ya usafi, hivyo kila siku nafanya usafi wa:
  • Choo,
  • Chumba cha kulala, na
  • Kitanda.
Baada ya kila saa mbili, husafisha sakafu ya maliwato kwa madawa na sabuni. Kila choo kikitumika (cha kike, cha kiume, au cha kukaa), nakisafisha tena kwa sabuni, madawa ya kuua wadudu, na kumalizia na sabuni zenye harufu nzuri. Baada ya hapo, napulizia pafyumu ya kuleta hewa safi.

Hii hali inagharimu sana. Watoto wangu hufadhaika na kuhoji matumizi makubwa ya sabuni na vifaa. Wanapokuja na wake au waume zao, huniuliza jinsi ninavyohakikisha usafi wa kiwango hiki. Ninawaeleza hatua kwa hatua huku mke wangu akicheka.

Pesa nyingi hutumika kwa bajeti ya vifaa hivi. Sipendi kabisa harufu mbaya, ndiyo maana nawekeza sana kwenye usafi wa eneo hili.

b) Usafi wa Mwili

Hapa, matumizi yangu ni makubwa pia. Ninatumia pesa kununua:
  • Vifaa vya kunyolea, sabuni yake, na aftershave,
  • Taulo za aina tatu (uso, mgongo na tumbo, na sehemu za siri),
  • Dawa ya mswaki na dawa za kusukutua mdomo.

Nina tabia ya kupiga mswaki mara tatu kwa siku na kusukutua pia mara tatu kwa siku. Kabla ya kutoka kwenda mjini, humuomba mke wangu aninuse mdomo ili kuhakikisha uko safi.

Huu ni ugonjwa wangu wa usafi ambao unanigharimu pesa nyingi sana. Watoto wangu huchukua jukumu la kununua vifaa hivyo kwa zamu huku wakicheka kuhusu tabia yangu ya usafi.

Ingawa usafi huu unanigharimu, najivunia kuwa na mazingira safi na mwili uliotunzwa. Ni changamoto inayohitaji bajeti kubwa, lakini inanipa utulivu wa akili na furaha ya maisha.
Hongera sana kwa usafi. Ni kinga thabiti ya magonjwa mengi, hususan ya tumbo, ngozi na UTI
 
Ndio namaliza muda huu kusafisha maliwato yangu na nimetumia dakika 30,dakika 10 ni kuyaacha madawa na sabuni yanyonye uchafu sakafu na masinki na vyoo na dakika 20 ni kusugua,kusafisha na kukausha.Pametakata na sote mie na mke wangu tumefurahi.Yeye anajiandaa kwenda job mimi leo na darasa la tution.Sasa kuna kuna kitu sikukueleza kwenye maandishi ya yangu ya awali juu ya somo hili,nacho ni:
Usafi wa masikio
Natilia mkazo sana usafinwa masikio na huu siwezi kuufanya mimi ni lazima nimpe mke wangu,aufanye,anatumia earbuds ambazo huichovya kwenye spirit na kusafisha uchafu fulani hivi ambao hutokea kwenye masikio na akimaliza,kuchukua mkasi na kutoa nywele zinazoota kwenye masikio na huwa anatumia mashine fulani hivi,ambayo huja kwenye set,unanyoa ndevu,sharubu na nywele za kwenye pua na masikio,baada ya hapo ndio naoga,navaa na kuangalia kazi za siku
Unaijua kazi ya hivyo vinywele unavyovitoa ndani ya pua? Kwa kuvinyoa mzee wangu
 
Ndio namaliza muda huu kusafisha maliwato yangu na nimetumia dakika 30,dakika 10 ni kuyaacha madawa na sabuni yanyonye uchafu sakafu na masinki na vyoo na dakika 20 ni kusugua,kusafisha na kukausha.Pametakata na sote mie na mke wangu tumefurahi.Yeye anajiandaa kwenda job mimi leo na darasa la tution.Sasa kuna kuna kitu sikukueleza kwenye maandishi ya yangu ya awali juu ya somo hili,nacho ni:
Usafi wa masikio
Natilia mkazo sana usafinwa masikio na huu siwezi kuufanya mimi ni lazima nimpe mke wangu,aufanye,anatumia earbuds ambazo huichovya kwenye spirit na kusafisha uchafu fulani hivi ambao hutokea kwenye masikio na akimaliza,kuchukua mkasi na kutoa nywele zinazoota kwenye masikio na huwa anatumia mashine fulani hivi,ambayo huja kwenye set,unanyoa ndevu,sharubu na nywele za kwenye pua na masikio,baada ya hapo ndio naoga,navaa na kuangalia kazi za siku
Nywele za pua na masikio zina kazi maalum.

Nywele za pua ni kusafisha hewa unayovuta
Nywele masikio ni kunasa vumbi na wadudu watakao ingia masikioni

Kamasi na Nta za masikio vyote vipo kwa ajili ya kazi maalum uvitoe kwa kiasi
 
Hahah aisee sijawahi kuwa busy na maisha kiasi hiko.

Hongera mzee wetu mstaafu maisha ni kuchagua na wewe umechagua fungu lako uliloliona jema.
 
Back
Top Bottom