salimtevez
Senior Member
- Feb 26, 2014
- 186
- 16
Kwani wew mafisadi wamekupa shilingi ngapi? Mpaka umekua huyaki mabadiliko
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuuu mbona unatoa povu sana umetumwa uje uwatetete nini?think twice mkuu pia jipanga sio tu kukurupuka na kuchangia hoja au ndio buku 7 kazini?Mkuu wewe unaonesha kuwa hujasikiliza "maoni ya wachache" yaliyowasilishwa na "mwanasheria nguli!"
Mbunge Lissu atoke Bungeni maana Ubunge wake ni "BATILI!!"
CDM kumbe ni Chama BATILI mkuu, Lissu katutoa tongotongo!
Mbunge Lissu atoke Bungeni maana Ubunge wake ni "BATILI!!"
Batili hii kwa maoni yako unapendekeza ihalalishwe vipi?Utarekebishaje kwa utaratibu BATILI mkuu, maana mpaka sasa Bunge Maalum la Katiba ni BATILI, labda tumuulize "Mwanasheria Nguli" Tundu Lissu atuelimishe pa kuanzia!
Alichosema Lissu ni ukweli mtupu kuhusu Nyerere.
Kwa maana hiyo, alichosema Lissu kuhusu Muungano ni ukweli mtupu.Angalau kwa hilo tupo ukurasa mmoja. Naomba usiyumbe.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
You can do better than this!!
different people with different ways of understanding and internalizing issues , eti hakuna subsitences kwenye speech za TL, nani kakwambia ?Lissu anaanza kufanana na Lema..noises nyiingi but substance kidogo
Sasa wewe hizi kamasi zako ndio better? haishangazi kina Max wamekufukuza kazi ya umoderotor up stairs empty.
Kinachonishangaza ni pale Tundu Lissu anapomtunishi msuli Baba wa Taifa wakati yeye Tundu Lissu ameshiriki kutunga Sheria Batili, Kujiunga na Chama BATILI, nk!
mkuu huu waraka unamfaa huyo ndugu asiye na heshima kwa kazi za wazee wetu, huko ni kupungukiwa adabu tu, na kupenda sifa za magazeti
mkuu huu waraka unamfaa huyo ndugu asiye na heshima kwa kazi za wazee wetu, huko ni kupungukiwa adabu tu, na kupenda sifa za magazeti
Wakuu,
Haina shaka kwamba Hotuba ya Tundu Lissu imevuta hisia za washabiki wengi wa "Serikali 3/Nchi 3!" Pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa huyo kwa kuwasilisha maoni ya wachache na kuchambua Sheria akienda sambamba na historia ya Muungano wetu tangu kuundwa kwake mpaka leo.Mwanasheria huyo nguli, kama baadhi wanavyomwita ameenda mbali sana, bila kuuma maneno akidai kwamba Muungano wetu wa iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika na iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar hauna uhalali wowote wa kisheria kwa kuwa haukuridhiwa na Baraza la Wawakilishi, hata kama uliridhiwa na Bunge la Tanganyika tu!
Amedai pia kwamba kwa sasa tufute Sikukuu ya Muungano wetu na kuanzisha "Siku ya Shirikisho!"Kwa hoja hizo za Lissu mimi sina ubavu wa kuzipinga kwa kuwa ametaja na vifungu vya kisheria vya wakati huo, tukubali tu kwamba Muungano HAUNA UHALALI WOWOTE WA KISHERIA!
Hata hivyo, Tundu Lissu alifikiri kwamba hoja hiyo inamu-implicate tu Nyerere ambaye amemtaja mara nyingi kwamba mambo mengi ameyafanya kwa AMRI YA RAIS. Mambo hayo ni kamba vile:
1. Jina la Nchi,
2. Kuiua Tanganyika,
3. Nembo ya Taifa, nk.
Kama Muungano hauna uhalali wowote maana yake nini?
1. Ni kwamba Tundu Lissu alifanya makosa kugombea ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano "BATILI," kwa hiyo Ubunge wa Lissu mpaka sasa ni "BATILI!"
2. Kwamba, hata mchakato huu wa kuandika Katiba Mpya ni "BATILI" kwa kuwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba imetungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano" BATILI,"
3. Kwamba, Tundu Lissu amechangia kutunga Sheria "BATILI" za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa Bunge nalo ni "BATILI,"
4. Kwamba CHADEMA nacho ni chama "BATILI" kwa kuwa kimeundwa kwa Mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa ambayo imetungwa na Bunge "BATILI" la Muungano,
5. Kwamba, shughuli zote za kisiasa za Tundu Lissu hazina uhalali wowote wa Kisheria kwa kuwa zimefanywa kwa kufuata Sheria za Muungano "BATILI,"
6. Kama Lissu ana vyeti vya Shule za Tanzania navyo ni "BATILI" kwa kuwa vimetolewa na Serikali "BATILI,"
7. Kama Tundu Lissu amezaliwa baada ya Muungano na kupewa Cheti cha Kuzaliwa ahesabu kuwa ni "BATILI" mpaka sasa,
8. Kesi zote alizoshinda Tundu Lissu mahakamani ajue kwamba ni "UBATILI" mtupu maana" MUUNGANO HUU NI BATILI," kwa hiyo hata mahakama za Muungano ni "BATILI,"
9. Kama Tundu Lissu ameoa baada ya Muungano ajue kuwa ameumia, ni ndoa "BATILI" hiyo!!!
10..................
Hongera sana Tundu Lissu kwa Hotuba Murua...............Ila usiendelee kuwepo kwenye BUNGE hilo "BATILI" kwa kuwa limeundwa na Sheria "BATILI!!!" Tafadhali sana, I am not joking, this time around!
Mimi nimetoa pointi tupu, ndio maana hujakanusha hata moja, yaani umeshindwa pa kuanzia! Mimi nimekubali kuwa Muungano wetu ni BATILI, ila Lissu naye amechangia katika kuendeleza mambo BATILI. Au tuseme amegundua juzi tu wakati anaandaa Ripoti ya Wachache kuwa MUUNGANO WETU NI BATILI?
umeona ee halafu alivyojijaladia sijui mkewe hakumkagua maana ile suti ilikuwa imemvaa kama ya kuazima na tai la kijani.Lissu anaanza kufanana na Lema..noises nyiingi but substance kidogo