SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Waarabu wameshaonja utamu wa asali ya pesa za CAF kwa hiyo wamejijengea mtandao mkubwa wa kuhakikisha hakuna boya yoyote anakuja kuwanyang'anya asali na himaya yao.
Miaka ya hivi karibuni Simba na Yanga zimejitahidi kufanyafanya usajili na kujifunza mikakati michache ya ndani na nje ya uwanja na tumeanza kushuhudia kumbe Waarabu wanafungika vizuri tu tofauti na zamani, tena wakati mwingine hata nyumbani kwao.
Sasa mimi nadhani hiki ni moja ya kitu wanachofanya. Hawa jamaa wakisikia na wakiona kuna mtu anawasumbua wanakaa kwenye vijiwe vyao vya kahawa na halua halafu wanapanga njama za kumnyofoa pale mbaya wao ili asiendelee kusumbua.
Wanafanya hivyo kwa wachezaji, makocha na hata viongozi.
Wakiangalia katika vyungu vyao wakaisoma nyota ya Kibu wakaona haishikiki na anaenda kuwasumbua, wanawekeana pesa katika kibubu kwa kushirikiana (kumbuka hili ni muhimu) ili kufanikisha jambo lao. Ukiwa boya na vitamaa tamaa vyako unakimbia kufanya nao biashara kumbe ndo wamekumaliza.
Nimalizie kwa kuwauliza nyie waswahili, ukigundua chimbo lenye fursa, huwa unakimbia kuwaambia wengine au unatengeneza mazingira ya kulilinda ili ule mwenyewe na watu wako? Lishikeni hili litawasaidia.
Miaka ya hivi karibuni Simba na Yanga zimejitahidi kufanyafanya usajili na kujifunza mikakati michache ya ndani na nje ya uwanja na tumeanza kushuhudia kumbe Waarabu wanafungika vizuri tu tofauti na zamani, tena wakati mwingine hata nyumbani kwao.
Sasa mimi nadhani hiki ni moja ya kitu wanachofanya. Hawa jamaa wakisikia na wakiona kuna mtu anawasumbua wanakaa kwenye vijiwe vyao vya kahawa na halua halafu wanapanga njama za kumnyofoa pale mbaya wao ili asiendelee kusumbua.
Wanafanya hivyo kwa wachezaji, makocha na hata viongozi.
Wakiangalia katika vyungu vyao wakaisoma nyota ya Kibu wakaona haishikiki na anaenda kuwasumbua, wanawekeana pesa katika kibubu kwa kushirikiana (kumbuka hili ni muhimu) ili kufanikisha jambo lao. Ukiwa boya na vitamaa tamaa vyako unakimbia kufanya nao biashara kumbe ndo wamekumaliza.
Nimalizie kwa kuwauliza nyie waswahili, ukigundua chimbo lenye fursa, huwa unakimbia kuwaambia wengine au unatengeneza mazingira ya kulilinda ili ule mwenyewe na watu wako? Lishikeni hili litawasaidia.