Jinsi wenye magari wanavyopigwa na mafundi

Jinsi wenye magari wanavyopigwa na mafundi

Nimekubali brother ukijua kucheza na schematic diagrams na kuzielewa components mambo si magumu hasa kwa sasa teknolojia ilipofika.

Ila kuna jamaa wana mambo ya kipumbavu sana sasa unakata waya ili iweje yani Africa bana ni basi tu.

Kukata wire ni kitu kimoja...

Usiombe mtu aswap wires kwenye gari yako....

Ni disaster.
 
Labda kwa kuanza nieleze kisa kilichomkuta jamaa yangu.

Jamaa ana Subaru Forester 2006 2.0L

Usiku wa kuamkia 9 january 2023 zilinyesha sana mvua na kuna maeneo mjini yalijaa maji, sasa bahati mbaya wakati anaenda mishemishe kuna mahali alifika maji yakawa mengi.

Katika kupita maji yakawa yameingia mpaka ndani ya gari.

Sasa baadae kuna jamaa akawa amewapelekea ili watoe seat na makapeti ndani ili wayakaushe.

Jioni alipoenda kuchukua gari alipoendesha kidogo ikaanza kuwaka Check engine.

Akarudi wa wale jamaa wanamkaushia vitu vya ndani, wakacheck weeee mwisho wa siku wakasema Control box (ECU) imelowana hivyo inabidi ikakaushwe na bei ya kukaushwa ni Tsh. 150,000/=. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].

Basi jamaa akanipigia, kuniuliza kuhusu hayo aliyoambiwa na hao jamaa. Nikamuambia ninachokifahamu kuhusu check engine kwamba kuna chances kuna connectors maji yameingia na hivyo kupelekea kuwaka kwa hiyo check engine.

Lakini pia nikamshauri alete gari tuangalie kama kweli control box imeingia maji, me nitaikausha na hot air gun.

basi akaja jioni hiyohiyo, Kufanya diagnosis shida ikatokea P0037 HO2S heater circuit low(B1S2). Hii ni O2 sensor ya nyuma au baada ya masega(CAT converter).
View attachment 2525315


Nikasema labda maji yameingia kwenye connector ya Oxygen Sensor nikacheck connector iko poa, pia nikacheck connector zingine mpaka kwenye ecu wala hakuna maji.

Basi nikamuambia atembelee kama haitazima basi sensor inaweza kuwa imeshaleta shida,

Katembelea almost a week bila check engine kuzima basi akarudi tukatafuta Oxygen sensor tukaona bei mlima (180k sensor used, ndugu zangu wa Subaru poleni sana).

Basi tukafikia hitimisho kwamba tuagize tu nje. Lakini kabla ya kuagiza nikasema nijiridhishe tena na wiring ya ile gari. Hiyo ilikuwa ni jana.

Oxygen sensor ina waya 4, nikaanza na waya mmoja baada ya mwingine. Diagram yake hii hapa chini.

View attachment 2525288


View attachment 2525290

Hapo wire mbili za heater circuit, mmoja signal line na mmoja ni ground.

Signal line na ground niliziconfirm haraka sana kwa kutumia signal generator. Yaani naingiza signal kutoka kwenye wiring ya o2 sensor halafu naangalia kwenye live data inasomaje. Nikaona inavyosoma kwenye signal generator ndio inavyosoma kwenye live data.

Wire za Heater circuit, kuna mmoja unatoka kwenye Main relay na unakuwa na Voltage ya battery. Huu nao ulikuwa poa.

Huu mmoja uliobaki wa heater circuit unaenda straight kwenye ecu, nikaanza kuufatilia kama unafika kwenye ECU, nikajaribu pin zote kwenye connectors za ECU hamna kitu. Basi jana nikaishia hapo sababu muda ulikuwa umeenda.

Kazi ya leo ikawa kufatilia huo waya mmoja umekatika wapi maana signal haifiki kwenye ecu.

Nikaspend muda mwingi sana kuangalia hizo diagrams baada nilivyoenda kule mbele mahali ambapo connector ya oxygen sensor inaingia nikanote vitu viwili.

1. Kulikuwa na tape mpya imefungwa, (mind you, hiyo gari haina hata miezi 6 toka iagizwe nje).

View attachment 2525300
Hapo baada ya kuitoa hiyo tape.

2. Waya niliokuwa naususpect kwamba una shida ulikuwa umetokeza kwa nje.

View attachment 2525301

Basi nikatoa hilo gamba jeusi na hiki ndio nilichokikuta ndani.

View attachment 2525302

Huo waya umekaatika kama hivyo, na siyo kwamba umekatika wenyewe, bali umekatwa.

Nikauunga huo wire na creamper pin.

View attachment 2525303

Nikarudishia gamba lake, nikapiga tape, nikarudisha kila kitu, nikawasha gari kwenda kutest, kila kitu kiko poa.

Jamaa alikuwa smart kwa waya alioukata sababu katika waya zote nne ndio waya mgumu kuufatilia,

Kiukweli kama ambavyo imekuwa ikishauriwa siku zote humu ndani kuhusu suala ya kuachia mtu gari halafu wewe unaenda kwenye mambo yako, Usimuamini mtu.

Trust get you killed.

Fine, umeamua kumpiga mtu basi angalau usimuharibie gari yake.
Mkuu umesahau kuweka namba ya simu wewe ni bonge la fundi. Binafsi huwa sipendi mafundi wanaotoa solution haraka.
Gari yangu ilikosa nguvu ikawa inaishia speed 60. Nikapeleka kwa fundi akaninunulisha fuel pump mpya kutest hakuna mabadiliko, akaanza kufuatilia kwa kuchomoa oxygen sensor gari ikawa na nguvu akasema sega limezima, nliishia kupigwa sega kija kuuliza nikaambiwa huwa yanasafishwa ila fundi aliniambia ukisafisha linaziba tena
 
Hiyo diagram hapo juu Kwa mafundi wa mtaani ni usiku wa Giza Tu...
Hata hivyo umeokoa pesa nyingi Sana kwenye matengenezo ya hiyo gari maana Kama angeagiza oxygen sensor mpya bado taa ingeendelea kuwaka Tu.

Big up mkuuuu!!!!
Hahaha hizo diagrams kama una ABC ya schematic reading unabaki kuona kama ramani tu kiukweli jamaa yupo vizuri kwa alivyoanza ku troubleshoot hadi kugundua shida ni wire kukatwa ilihitaji utulivu. Vinginevyo kama ulivyosema Sensor mpya ingeletwa na bado ingeindicate tatizo.
 
Mkuu umesahau kuweka namba ya simu wewe ni bonge la fundi. Binafsi huwa sipendi mafundi wanaotoa solution haraka.
Gari yangu ilikosa nguvu ikawa inaishia speed 60. Nikapeleka kwa fundi akaninunulisha fuel pump mpya kutest hakuna mabadiliko, akaanza kufuatilia kwa kuchomoa oxygen sensor gari ikawa na nguvu akasema sega limezima, nliishia kupigwa sega kija kuuliza nikaambiwa huwa yanasafishwa ila fundi aliniambia ukisafisha linaziba tena
Aiseee pole mkuu....

0621 221 606.
 
Sijaelewa kitu bado.

Lengo la kumfanyia huo uharibifu wao wangenufaika vipi?

okay labda nirudie tena.

Wewe umempelekea mtu gari yako ambayo uliingia nayo kwenye maji, aifungue ndani akukaushie viti na makapeti.

Umeenda nayo ukiwa unaiendesha, haina tatizo na haijawasha taa yoyote.

Baadae unaenda kuchukua gari inawaka check engine.

Unaamua kuwarudishia,

Wanaingalia wanakuambia shida ni control box imeloa na inatakiwa kukaushwa na bei ya kukausha ni 150,000/=.

Unaamua kuachana nao na kutafuta fundi mwingine, ambaye anakuja kugundua hiyo check engine inawaka kwa sababu kuna wire umekatwa....(tena umekatwa na kitu sharp kama mkasi au kisu).

Mpaka hapo nadhani umenielewa.

Rudia maneno niliyobold.
 
Back
Top Bottom