Jinsi ya kufanikiwa kiuchumi, Kijamii, kisiasa, kiroho, kirahisi kabisa

Jinsi ya kufanikiwa kiuchumi, Kijamii, kisiasa, kiroho, kirahisi kabisa

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam, Shalom!!

Salamu hapo juu itoshe kukujulisha kuwa walengwa wa HOJA hapo juu ni Wana wa Mungu, ni wale ambao wanahangaika,wanafanya KAZI Kwa bidii, wanajitenga na UOVU, walipao ZAKA nk nk, lakini Bado malengo Yao hayafanikiwi Kwa hatua za kuridhisha.

Neno la Mungu lasema katika
( Yakobo 4:3)
"Mwaomba Wala hampati, Kwakuwa Mwaomba vibaya, Ili mvitumie Kwa tamaa zenu wenyewe"!!


Ujumbe huo hapo juu haukuandikwa Kwa ajili ya wapagani, Bali Wana wa Mungu,

Hivi kijana, unasugua goti ukiomba Mungu akujaalie upate deal zuri katika KAZI zako Ili upate gari Kwa ajili ya kumfurahisha mchumba wako, Unadhani utajibiwa kirahisi?

Unapiga goti ukimwomba Mungu akutajirishe Ili maadui wako wakuheshimu, Unadhani utajibiwa kirahisi?

Mwingine uko kitandani unaumwa cancer au gonjwa hatari, ukimwi Kwa Mfano, unamwomba Mungu akuponye lakini huweki AGANO nae kuwa ukiponywa utafanya nini Kwa ajili ya Mungu, sahau kujibiwa.

Mimi Rabbon, nilipooa, nilikuwa napata shida sana Kila Jumapili sababu palikuwa na shida sana ya USAFIRI, nilimwomba Mungu anijalie nipate gari Ili gari Hilo linisaidie kuwahi Kanisani jumapili na litumike kusaidia huduma Kanisani, na nilimwomba Mungu anijalie ninunue gari Hilo baada ya mwaka mmoja sababu sikuwa na pesa za kutosha, Cha kushanga nilipata gari ndani ya miezi SITA tu.

JINSI YA KUJIBIWA MAOMBI YAKO KIRAIHISI!!

1. SIASANI
Ikiwa umepanga kugombea, na ungependa Mungu akusaidie kushinda Udiwani, ubunge, Urais nk nk, weka AGANO na Mungu, Mwambie hivi, Mungu wangu ukinifanikisha kuwa mbunge, nk nk, nitahakikisha Ufalme wako Mungu unaingia bungeni, nitahakikisha HAKI inatawala ndani ya bunge na Kwa wananchi, utafanikiwa kirahisi.

2. KIUCHUMI
Wengi mmefungua biashara na mnamwomba Mungu awatajirishe, lakini hamsemi mkipata utajiri mtafanya nini Kwa ajili ya INJILI. Hamuweki AGANO na Mungu kuwa mtatumia vipi utajiri wenu kuhakikisha watoto mitaani wanaishi vizuri na kupata mahitaji Yao, wajane nk nk!!

3. KIJAMII
Wengi mnatamani mfanikiwe katika huduma mzifanyazo, mnatamani kufahamika, lakini hamweki AGANO na Mungu kuhusu jinsi mtakavyitumia kufahamika kwenu kuwaleta wengi Kwa kristo, kamwe hamtatoboa msipofanya hivyo, sababu mnaomba vibaya Ili mpate hayo Kwa tamaa zenu.

4. MAHUSIANO NA NDOA.

Ulipokuwa single, bachelor ulimtumikia Mungu vizuri, ukaomba Mungu akupe NDOA, Kweli Mungu kakupa mume/ mke mzuri, Cha ajabu tangu umeoa, Kanisani huendi tena, maombi hufanyi tena, huduma huendi tena,

Sasa Kwa kuwa Mungu anapenda umtumikie kama zamani, ataruhusu huyo mume akutese vilivyo, huyo mke akutoe JASHO Kwa kukupiga matukio, Ili urudi tena Kanisani, urudi magotini ujue yupo Mungu na urudi kumtumikia, makinika!!

5. UJENZI.

Unaomba Kila kukicha, unamwomba Mungu akusaidie Ili upate nyumba Yako Ili kuondokana na adhaa akupazo mwenye nyumba wako wa sasa. Utachelewa sana, maana unakosea kuomba.

Omba hivi, EE Mwenyezi Mungu, ukinijalia kujenga nyumba nzuri, kubwa, nitahakikisha natenga chumba special Kwa ajili ya maombi, nitatenga chumba/ nyumba special Kwa ajili ya Wageni ambao ni watumishi wa Mungu, nyumba hiyo itakuwa na standard zote za nyumba Bora Ili wahubiri wajapo katika Kanisa letu, wasilale nyumba za wageni zinazotumika na watu wengi wasio waaminifu, nitahakikisha, nyumba yangu / chumba changu Kwa ajili ya kupokelea watumishi wa Mungu ni kisafi na kitakatifu, ambatisha AGANO lako na sadaka.

Amini nakuambia, Mungu hawezi kataa offer hiyo, atakufanikisha haraka sana.

Yatosha Kwa sasa, mbarikiwe🙏

Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako, fuatisha Sala hii;

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AMEN

Karibuni 🙏.
 
Mada nzuri ila umezingua uwasilishaji wake, sote tunajua Mungu anaanza kwa kila kitu, then ili tufanikiwe ni juhudi zetu wenyewe ambazo ndio nilitarajia kusikia hizo tactics
 
Je nikitaka kufaulu masomo na kupata kazi ?
Soma Kwa bidii.

Mwombe MUNGU akupe uelewa na ufahamu Toka juu, weka AGANO nae kuwa:

EE Mwenzezi Mungu, ukinisaidia nikasoma na kufaulu, nikapata KAZI nzuri yenye kipato kizuri, nitahakikisha Ufalme wako unaingia kazini.

Nitahakikisha wafanyakazi wenzangu, wanafunzi wenzangu wote wanamjua Mungu. Nitahakikisha ofisi hainuki RUSHWA,HAKI itatamalaki katika utumishi wangu, Upendo utazidi nk nk

Ubarikiwe!!
 
Mada nzuri ila umezingua uwasilishaji wake, sote tunajua Mungu anaanza kwa kila kitu, then ili tufanikiwe ni juhudi zetu wenyewe ambazo ndio nilitarajia kusikia hizo tactics
Umenena vyema,

Ningeingia huko kipaelezea, mada ingekuwa Pana sana. Next time tutafika huko.

Lakini pia kufanya KAZI Kwa bidii Si kubarikiwa, Kuna wengi tu wanajibidiisha sana katika KAZI lakini mifuko Yao imetobolewa!! (Hagai 1:6-7)
 
Soma Kwa bidii.

Mwombe MUNGU akupe uelewa na ufahamu Toka juu, weka AGANO nae kuwa:

EE Mwenzezi Mungu, ukinisaidia nikasoma na kuifaulu, nikapata KAZI nzuri yenye kipato kizuri, nitahakikisha Ufalme wako unaingia kazini.

Nitahakikisha wafanyakazi wenzangu, wanafunzi wenzangu wote wanaujua Mungu.

Ubarikiwe!!
Asante MTUMISHI barikiwa Sana tunajifunza
 
Je dhamiri na nadhiri na agano haya mambo yametofautiana kivipi

Dhamiri -
Nadhiri-
Agano-
 
Je dhamiri na nadhiri na agano haya mambo yametofautiana kivipi

Dhamiri -
Nadhiri-
Agano-
DHAMIRI

Ni kipawa Cha binadamu kinachowezesha kuamua kuhusu Uadilifu au UOVU wa Tendo Fulani analolikabili au analolipenda.

DHAMIRI hiyo hiyo inashinikiza daima kutenda lililo adilifu na kukwepa ovu,

Katika falsafa ya Maadili, wengi wanaokubali kwamba uamuzi wa DHAMIRI inategemea UKWELI ambao upo nje ya mhusika na ambao Yeye anatakiwa kuutambua.

Uamuzi wa DHAMIRI unategemea zaidi malezi na mang'amuzi.
Source: wikipedia dictionary.


NADHIRI.

Ni AHADI aitoayo mtu Kwa Mungu, kuwa atafanya jambo Fulani pindi akipata anachokitafuta.

AGANO.

AGANO ni kama tu nadhiri, lakini AGANO ni Pana na kubwa zaidi maana inahusisha mifumo ya kisheria, inahusisha vizazi na vizazi, nadhiri Ina mwisho, lakini AGANO halina ukomo, ni endelevu, no end.

Katika mada hapo juu AGANO limetumika sababu ni kitu Cha milele, vizazi na vizazi,

Mtu angependa afanikiwe Si Yeye pekeake, Bali Yeye na vizazi nyuma yake.

Hapo ndipo AGANO linapokuwa advanced ya nadhiri.

Ubarikiwe.
 
Salaam, Shalom!!

Salamu hapo juu itoshe kukujulisha kuwa walengwa wa HOJA hapo juu ni Wana wa Mungu, ni wale ambao wanahangaika,wanafanya KAZI Kwa bidii, wanajitenga na UOVU, walipao ZAKA nk nk, lakini Bado malengo Yao hayafanikiwi Kwa hatua za kuridhisha.

Neno la Mungu lasema katika
( Yakobo 4:3)
"Mwaomba Wala hampati, Kwakuwa Mwaomba vibaya, Ili mvitumie Kwa tamaa zenu wenyewe"!!


Ujumbe huo hapo juu haukuandikwa Kwa ajili ya wapagani, Bali Wana wa Mungu,

Hivi kijana, unasugua goti ukiomba Mungu akujaalie upate deal zuri katika KAZI zako Ili upate gari Kwa ajili ya kumfurahisha mchumba wako, Unadhani utajibiwa kirahisi?

Unapiga goti ukimwomba Mungu akutajirishe Ili maadui wako wakuheshimu, Unadhani utajibiwa kirahisi?

Mwingine uko kitandani unaumwa cancer au gonjwa hatari, ukimwi Kwa Mfano, unamwomba Mungu akuponye lakini huweki AGANO nae kuwa ukiponywa utafanya nini Kwa ajili ya Mungu, sahau kujibiwa.

Mimi Rabbon, nilipooa, nilikuwa napata shida sana Kila Jumapili sababu palikuwa na shida sana ya USAFIRI, nilimwomba Mungu anijalie nipate gari Ili gari Hilo linisaidie kuwahi Kanisani jumapili na litumike kusaidia huduma Kanisani, na nilimwomba Mungu anijalie ninunue gari Hilo baada ya mwaka mmoja sababu sikuwa na pesa za kutosha, Cha kushanga nilipata gari ndani ya miezi SITA tu.

JINSI YA KUJIBIWA MAOMBI YAKO KIRAIHISI!!

1. SIASANI
Ikiwa umepanga kugombea, na ungependa Mungu akusaidie kushinda Udiwani, ubunge, Urais nk nk, weka AGANO na Mungu, Mwambie hivi, Mungu wangu ukinifanikisha kuwa mbunge, nk nk, nitahakikisha Ufalme wako Mungu unaingia bungeni, nitahakikisha HAKI inatawala ndani ya bunge na Kwa wananchi, utafanikiwa kirahisi.

2. KIUCHUMI
Wengi mmefungua biashara na mnamwomba Mungu awatajirishe, lakini hamsemi mkipata utajiri mtafanya nini Kwa ajili ya INJILI. Hamuweki AGANO na Mungu kuwa mtatumia vipi utajiri wenu kuhakikisha watoto mitaani wanaishi vizuri na kupata mahitaji Yao, wajane nk nk!!

3. KIJAMII
Wengi mnatamani mfanikiwe katika huduma mzifanyazo, mnatamani kufahamika, lakini hamweki AGANO na Mungu kuhusu jinsi mtakavyitumia kufahamika kwenu kuwaleta wengi Kwa kristo, kamwe hamtatoboa msipofanya hivyo, sababu mnaomba vibaya Ili mpate hayo Kwa tamaa zenu.

Yatosha Kwa sasa, mbarikiwe🙏

Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako, fuatisha Sala hii;

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AMEN

Karibuni 🙏.
Amen 🙏.
 
Dini huwa inasaidia kukufanya u behave, uwe na kiasi, uweze kuji control, kuachana na tabia ambazo zinaharibu uchumi.
Mfano ulevi, umalaya, ugomvi n.k ni baadhi ya tabia mbaya ambazo mara nyingi zinarudisha mtu nyuma.

Dini inasaidia usiishi kama mnyama.
 
Amen 🙏
Barikiwa mtumishi.

Ni vyema pia ukashare nasi experience Yako juu ya mchango wa maombi katika mafanikio Yako kiujumla ukiweka na Shuhuda ikikupendeza Kwa uelewa wa wengi.
 
Dini huwa inasaidia kukufanya u behave, uwe na kiasi, uweze kuji control, kuachana na tabia ambazo zinaharibu uchumi.
Mfano ulevi, umalaya, ugomvi n.k ni baadhi ya tabia mbaya ambazo mara nyingi zinarudisha mtu nyuma.

Dini inasaidia usiishi kama mnyama.
Umenena vyema.

Ila penye Dini, weka IMANI, itaeleweka vizuri zaidi.

Ubarikiwe.
 
DHAMIRI

Ni kipawa Cha binadamu kinachowezesha kuamua kuhusu Uadilifu au UOVU wa Tendo Fulani analolikabili au analolipenda.

DHAMIRI hiyo hiyo inashinikiza daima kutenda lililo adilifu na kukwepa ovu,

Katika falsafa ya Maadili, wengi wanaokubali kwamba uamuzi wa DHAMIRI inategemea UKWELI ambao upo nje ya mhusika na ambao Yeye anatakiwa kuutambua.

Uamuzi wa DHAMIRI unategemea zaidi malezi na mang'amuzi.
Source: wikipedia dictionary.


NADHIRI.

Ni AHADI aitoayo mtu Kwa Mungu, kuwa atafanya jambo Fulani pindi akipata anachokitafuta.

AGANO.

AGANO ni kama tu nadhiri, lakini AGANO ni Pana na kubwa zaidi maana inahusisha mifumo ya kisheria, inahusisha vizazi na vizazi, nadhiri Ina mwisho, lakini AGANO halina ukomo, ni endelevu, no end.

Katika mada hapo juu AGANO limetumika sababu ni kitu Cha milele, vizazi na vizazi,

Mtu angependa afanikiwe Si Yeye pekeake, Bali Yeye na vizazi nyuma yake.

Hapo ndipo AGANO linapokuwa advanced ya nadhiri.

Ubarikiwe.


Nashukuru naendelea kujifunza

Nimekuwa nikifanya maombi ya usiku ya kuombea watu na familia nnimeona matokeo hakika Mungu ni mwema na anatenda Sana.

Je kuhusu maombi ya usiku unayachukuliaje mkuu nahitaji kukua na kujifunza.
 
Nashukuru naendelea kujifunza

Nimekuwa nikifanya maombi ya usiku ya kuombea watu na familia nnimeona matokeo hakika Mungu ni mwema na anatenda Sana.

Je kuhusu maombi ya usiku unayachukuliaje mkuu nahitaji kukua na kujifunza.
Hakuna kitu shetani na ufalme wa Giza unaogopa kama maombi ya WATAKATIFU.

Maombi huambatana na Imani, ni HAKIKA na Kila ukiombacho na kukitamka kinatokea hapo hapo katika Ulimwengu wa Roho.

Mimi Kuna siku nilikuwa nimekaa sebuleni, nikapata msukumo na mawazo ya kumuombea baba yangu aliye mbali huko kwetu,

Nilianza kuomba na nikajikuta namuombea Mungu amuokoe, na sikujua ni Kwa sababu Gani, nilijikuta namuombea Kwa zaidi ya masaa mawili Hadi usiku wa manane, na nilipolala pia nilijikuta naendelea kuomba katika Roho usingizini.

Palipokucha, nilipigiwa simu Toka nyumbani nikiambiwa, baba yangu alipata shambulio katika AFYA yake na alifikia hatua ya kuzimia na jambo Hilo lilileta HOFU kuu Kwa familia.

Nilipouliza muda wa tukio nikaambiwa, ni muda Ule Ule nilipokuwa nikiomba. Na baada ya nusu saa, alizinduka na akawa salama tena.

Maombi ni vita, inadhoofisha sana ufalme wa Giza, ndio maana ukipanga nyumba Kwa mchawi na ukawa unaamka kuomba lazima akuchukie, sababu maombi yanaharibu KAZI za Giza na waovu,

Si Rahisi kuomba, wengi hujaribu wasiweze,

Ikiwa umepata neema hiyo endelea kuomba na uwaombee wengine maana wengi sana huokolewa kupitia maombi ya wengine.

Mungu akuzidishie Ari ya kuomba zaidi na zaidi.

Ubarikiwe 🙏
 
Mwafrika ukimuona kanisani anamuomba Mungu ampe kazi,mwenza ,mafanikio kiuchumi,mke mme na akishajibiwa kanisani ugeuka kituo cha polisi umuoni tena hadi apate tena matatizo mfano ya kufukuzwa kazi,biashara imeyumba talaka nk.Mzungu uenda kanisani kumuomba Mungu akimaanisha kwa sababu wao hawaombi kuhusu sijui uchumi,mafanikio,kazi,kupata mme mke kwa sababu hivyo tayari vipo tu kwao.
 
Mwafrika ukimuona kanisani anamuomba Mungu ampe kazi,mwenza ,mafanikio kiuchumi,mke mme na akishajibiwa kanisani ugeuka kituo cha polisi umuoni tena hadi apate tena matatizo mfano ya kufukuzwa kazi,biashara imeyumba talaka nk.Mzungu uenda kanisani kumuomba Mungu akimaanisha kwa sababu wao hawaombi kuhusu sijui uchumi,mafanikio,kazi,kupata mme mke kwa sababu hivyo tayari vipo tu kwao.
Ni Kweli kabisa,

Mungu anajua akikupa utajiri kidogo tu, unakuwa bussy Hadi ibadani tena hapendi kwenda tena.

Ndio maana wengi wanaishia kupewa tu pesa ya kula, kulipia Kodi na ada za watoto baas!!

Mtu ukiomba utajiri Kwa kuweka AGANO na Mungu kuwa, ukinipa pesa, nitajenga vituo vya kutunza na kusomesha yatima Nchi nzima Ili waje kuwa baba Bora Kwa familia zao, wamjue Mungu,

Mungu anawezaje kukataa deal la aina hiyo? Ndomana wazungu wanafanikiwa.

Ukiomba kibinafsi, ni ngumu kujibiwa maombi na Mungu.
 
1. SIASANI
Ikiwa umepanga kugombea, na ungependa Mungu akusaidie kushinda Udiwani, ubunge, Urais nk nk, weka AGANO na Mungu, Mwambie hivi, Mungu wangu ukinifanikisha kuwa mbunge, nk nk, nitahakikisha Ufalme wako Mungu unaingia bungeni, nitahakikisha HAKI inatawala ndani ya bunge na Kwa wananchi, utafanikiwa kirahisi.
Very interesting.

Mkuu, itakuwa heri sana ugombee ubunge tuushuhudie huo muujiza wa kuingiza utawala wa Mungu na HAKI yake ndani ya bunge la CCM. Tafadhali.
 
Back
Top Bottom