Jinsi ya kupangalia chumba cha kulala kiwe na mvuto zaidi

Jinsi ya kupangalia chumba cha kulala kiwe na mvuto zaidi

Watu wasiojulikana wakivamia utakuwa unakodoa tu macho huna hata pini ya kumshindilia nayo mtu kwenye kalio
 
Kwa wenye uwezo wao ndio watafanya hivyo ila sisi makapuku ni tabu kweli

Najifariji kwa kusema usingizi ni uleule ila tu sehemu ya kumbonji ni tofauti
Hapana.

Chumba kikiwa katika hali nzuri hata usingizi pia utakuwa ni mzuri ila chumba kikiwa shaghala baghara basi usingizi utakaoupata utakuwa ni wa mang'amung'amu.
 
Hapana.

Chumba kikiwa katika hali nzuri hata usingizi pia utakuwa ni mzuri ila chumba kikiwa shaghala baghara basi usingizi utakaoupata utakuwa ni wa mang'amung'amu.
Hapo kwenye kiwe na Hali nzuri ndio nimekuelewa ila hizo zingine mbwembwe tu kunogesha usingizi
 
Sisi wengine tumeshazoea jiko la mkaa kwenye kona,jiwe la kusugulia uvunguni na kamba ya kuanikia vyupi
 
Pia umesahau.
Lazima kuwe na kitu maridadi kabisa cha kulaza kwenye hicho kutanda[emoji131][emoji131][emoji131]
 
hayo mambo ni huko kwenu upanga sijui mbezi beach. Sisi kwetu tandale chumba kina ndoo, majaba ya kutosha, jiko la gesi na mkaa, mswaki na ndoo la kuogea, na bodaboda yangu nailaza ndani yani kwa ufupi chumba changu kina kila kitu.
Watanzania 98% wanaishi store
 
Hamna chochote utakachosema kitanikatisha tamaa. Lazima nije.
Haha karibu pacha mimi wala sikukatishi tamaa nakupa tu picha halisi ya kwetu ujue kulivyo ili wakati wa kuja ujipange
 
Pole sana mkuu ila ndiyo vitu tunavyoweka mavyumbani mwetu

Ila huo mtiririko wa vitu nadhani ni wale wanaoishi masaki, mikocheni na sehemu kama hizo, lakini huku kajambana nani, kwanza rum kubwa hivyo ya kulala na kuweka vitu vyote hivyo unaitoa wapi
 
Ni kweli mkuu, mie mwenyewe chumbani kwangu ni panga na jambia.......
Hahaa nikiangalia avatar yako inanipa ugumu kidogo kuamini kama unaweza hata kuua mende
 
Back
Top Bottom