Jinsi ya Kushughulika na Mtoto Mwenye Milipuko ya Hasira

Jinsi ya Kushughulika na Mtoto Mwenye Milipuko ya Hasira

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Shikilia msimamo wako. Ikiwa unampa mtoto wako kila kitu anachotaka kwa sababu tu analipuka kwa hasira, yaelekea ataendelea kufanya hivyo kila mara anapotaka kitu fulani. Kwa utulivu mwonyeshe mtoto wako kwamba hutalegeza msimamo wako.

Elewa hali yake. Mtoto wako si mtu mzima. Kwa kuwa hajui jinsi ya kushughulika na hisia zake, anaweza kukasirika sana anapofadhaika. Jaribu kuona mambo kama yeye anavyoyaona.

Uwe mtulivu. Mtoto wako anapolipuka kwa hasira, kukasirika hakutakusaidia. Kwa kadiri inavyowezekana, puuza mlipuko wake wa hasira na udhibiti hisia zako. Kukumbuka kwa nini milipuko ya hasira hutokea kutakusaidia kuwa mtulivu.

Pia jaribu mambo yafuatayo:

Mlipuko wa hasira unapoanza mshikilie mtoto wako (ikiwa inawezekana) na, bila kumwumiza, mzuie asijigaragaze. Usimfokee mtoto wako. Subiri tu mpaka hali itulie. Hatimaye, mtoto atatambua kuwa kulipuka kwa hasira hakukumsaidia kwa njia yoyote.

Tenga mahali utakapomweka mtoto wako anapolipuka kwa hasira. Mwambie kwamba atatoka humo mara tu anapotulia, na kisha umwache humo.

Ikiwa mtoto wako analipuka kwa hasira mbele za watu, mwondoe hapo. Usimpe anachotaka eti kwa sababu tu amelipuka kwa hasira mbele za watu. Ukimpa, hilo linaweza kufanya afikiri kwamba ikiwa atalipuka kwa hasira, anaweza kupata chochote anachotaka.
 
Nina kamoja hako kana hii tabia! Kanambuliaga doze moja heavy Sana, Hadi nakaonea huruma baadae.,....Siwezagi kuvumilia ujinga naona Kama ananipima Imani! Anyway nitajaribu hii mbinu unaweza nifaa
 
Hii inawafaa kina Junia, sisi kina Zomboko mchafukoge ukijifanya kujilipua hasira kitakachofuata ni kula bakora za kutosha na unaambiwa kwenda kaoge, ukitoka kuoga unatumwa kazi zako kama kawaida.

Hao wa kupeti peti wapanda mabasi ya njano hongera zao
 
Upuuzi mtupu, zibua makofi, ning'iniza chapa sana,

Hao wazungu wanaodanganya hizo mbinu watoto wao wamewashindwa ndo wanataka kutuletea strategy hizi,

Tutatumia zile zile wazazi wetu walitumia, sisi siyo wazungu,

Kila mtu ashinde mechi zake, as far amezaliwa Africa, viboko atakula tu mpaka ashike adabu!!
 
Nina kamoja hako kana hii tabia!kanambuliaga doze moja heavy Sana,Hadi nakaonea huruma baadae.,....Siwezagi kuvumilia ujinga naona Kama ananipima Imani! Anyway nitajaribu hii mbinu unaweza nifaa
Mnawezaje kuwapiga jamani, mwenzenu siwezi kabisa kupiga na nashukuru sana Mungu wananielewa nikiongea tuu. sijui wangekua chakaramu ingekuwaje
 
Mnawezaje kuwapiga jamani, mwenzenu siwezi kabisa kupiga na nashukuru sana Mungu wananielewa nikiongea tuu. sijui wangekua chakaramu ingekuwaje
Maybe hujajaaliwa mtoto pasua kichwa,Mimi Nina boy na girl,huyu girl Ni msikivu na muoga Sana anaweza kuniangalia tu akajua mama kakasirika hivyo atabehave vizuri na ukimwambia Jambo anatii,Sasa Kuna huyo boy kwanza ukimuona utadhani Ni mpole maana Ni kivulana cheupee jamani Ni mkaidi,mtukutu hasikiii yaani Hadi apewe mimbata ndio anatulia kwa muda...hata sielewi.....mi mwenyewe sipendi mpiga Ila inanibidi tu Sina namna
 
Maybe hujajaaliwa mtoto pasua kichwa,Mimi Nina boy na girl,huyu girl Ni msikivu na muoga Sana anaweza kuniangalia tu akajua mama kakasirika hivyo atabehave vizuri na ukimwambia Jambo anatii,Sasa Kuna huyo boy kwanza ukimuona utadhani Ni mpole maana Ni kivulana cheupee jamani Ni mkaidi,mtukutu hasikiii yaani Hadi apewe mimbata ndio anatulia kwa muda...hata sielewi.....mi mwenyewe sipendi mpiga Ila inanibidi tu Sina namna
Pole sana aisee, mimi wa mwisho ndio kidogo mkorofi lkn bado nikimwambia aache anaelewa.
 
Ni fimbo tu
Huku mikoani sisi tunaotwa baba lakini wale wa dar wanao itwa dady inawahusu hii
 
Back
Top Bottom