Jinsi ya Kuuza Bidhaa EBay na Amazon


Mkuu masoko yapo mf kaymu, jumia ila wabongo bado muamko na ndio kwanza wanakimbilia ya wamarekani
 
hiyo bank nayo inayouwezo wa kukuletea malipo bila usumbufu wa aina yoyote ile au kutapeliwa mtandaoni mana mm naongopaga biashara za mtandaoni kwa ajili ya matapeli wa mtandaoni
Hi! Usiogope sana kuibiwa maana woga ni adui wa mafanikio. Matapeli na wezi wapo hata hapo ulipo. Cha msingi ni kujifunza kipi unatakiwa kuangalia au kufanya kabla ya hujafanya transactions online."Knowledge is power"
 
Mkuu masoko yapo mf kaymu, jumia ila wabongo bado muamko na ndio kwanza wanakimbilia ya wamarekani

Hi!, Kama hoja yako hapo ni kuhusu "Masoko Yetu" nikwambie hata hayo uliyoyataja sio ya kwetu. e.g. Jumia is a Nigerian Company and even Kaymu is not ours. Hoja yangu kubwa hapa sio soko linamilikiwa na akina nani..my concern here is where there is a big market 'Market needs'. Kwa mfano Kaymu nilishawahi kuitumia sikuendelea nao due to some inconveniences siwezi kuanika hadharani(I'm saving their face). Thanks in advance.
 
Me nadhani hilo soko linawafaa wamarekani we uza bidhaa zako jumia,kaymu ndio panakufaaa pia itasaidia kutanua masoko yetu, anyway kama unaweza kudeliver bidhaa worldwide na kupambana na ushindani basi subiri wadau wafunguke

Tanzania ukiuza vitu vya culture utaishia kukata tamaa tu but kwa america I think unaweza ukatoka
 

Naona mpaka sasa hakuna mdau aliyekujibu swali lako hata mmoja, pole mkuu.
Kwa uzoefu wangu mfupi ebay unaweza kuuza, kikwazo kikubwa utakachokumbana nacho ni kwamba njia pekee ya malipo inayokubalika kule ni PAYPAL, na account za PayPal kwa Tanzania haziruhusu kupokea malipo hivyo hata ukicreate business account itakuwia vigumu kupokea malipo kutoka kwa wateja wako. Amazon sina hakika sana lakini wacha nifuatilie kidogo nitakujuza kidogo nitakachokipata. Na kuhusu kuibiwa hilo suala liko wazi lazima utalizwa mara chache, mtu atalipia mzigo utatuma kisha anarudi kuwalilia ebay kuwa hajapata mzigo wake, ebay wanaskiliza sana mteja kuliko muuzaji huyo mteja lazima atarudishiwa tu pesa yake akisisitiza kuwa hakupata mzigo, hiyo inakuwa imekula kwako,,,,lakini usiogope, hakuna bishara isiyo na hasara. Angalia bidhaa zilizo huku ambazo ni unique na zinaweza kuvutia walio nje, kuna dada mmoja Mghana huwa napiga naye story, anauza shanga za kuvaa kiunoni, shanga ya string mbili mpaka tatu anauza mpaka dola sitini...na anawateja wengi marekani na ulaya!! Sasa fikiria wewe hizi shanga za wamasai huku zinauzwa shngapi, ukipata wamama kadhaa wanaojua kudesign shanga nzuri unapata faida nzuri kisi kwamba ukipoteza mara mojamoja wala haiumi! Angalia vitu vya kiutamaduni, pia unaweza kufuatilia bei za vito vilivyochongwa vya mawe adimu kama Tanzanite kwa sonara, ukadesign na boksi zako unakuwa unahudumia maharusi wa huko mbele...eventualy brand yako inasimama wakati hujui hata kukata jiwe, mjini kulala na njaa kupenda!
 

Kwasasa mkataba kati ya paypal na ebay umevunjwa.
Ni makampuni mawili yanayojitegemea.
Unaweza kuruhusu payment ikafanyika directly from your card ila wengi hawataki kwasababu haina usalama kama amazon.
Ingia account yako ya amazon wametoa hiyo taarifa, isome kwa makini.
Amazon na Ebay inaruhusiwa kuuza ila means of payment bado ipo tatizo.
Unaweza kujaribu kutumia payoneer, transactions zote ziwe zinapitia huko.
 

Kwa mfanyabiashara PayPal ni nzuri kuliko njia hizo zingine, hizo njia nyingine utaibiwa sana. So far ebay bado malipo ni PayPal tu pamoja na kwamba zimekuwa kampuni mbili tofauti!
 
Thanks! I really appreciate your contribution let us keep on sharing.
 
Thanks Bavaria, nimeshafungua A/C ya Payoneer so I'm waiting their card. Nitaendelea kutoa updates
 
Bila PayPal au nyingine za namna hiyo ni vigumu saana kupata wateja. As ni wachache wanaweza kukupa namba za credit cards zao, mana ni hatari. Paypal na wengine kama hao wanakuhakikishia wewe na mteja wako kuwa taarifa zako za benki ziko salama. Mbinu zingine za malipo ni gharama zaidi.
 
I found that Tanzania is not among the listed Countries you can open Amazon Seller Account, Lina kwepeka hili?
Vipi biashara eBay inatoka kama amazon?
 
Hamna option ya kutransfer pesa kuja kwenye ATM card ?
 
Skrill netller
 
EBAY/PAYPAL NA AMAZON ZINAKUBALI WANUNUZI TOKA TANZANIA LAKINI HAIKUBALI WAUZAJI TOKA TANZANIA....KUNA KILA DALILI ZA KUHAMA NCHI
 
EBAY/PAYPAL NA AMAZON ZINAKUBALI WANUNUZI TOKA TANZANIA LAKINI HAIKUBALI WAUZAJI TOKA TANZANIA....KUNA KILA DALILI ZA KUHAMA NCHI
mkuu hili tatizo ni la tanzania au wenyewe. Nini kinatufanya tuendelee kuwa wajima katika hili?
 
mkuu hili tatizo ni la tanzania au wenyewe. Nini kinatufanya tuendelee kuwa wajima katika hili?
NAFIKIRI NI SERA/SHERIA ZA NCHI NDIO ZINATUWEKA UTUMWANI......KAMA SERIKAL HAIHUSIKI BAS HATUNA BANK INAYOAFIKIANA KTK HUDUMA IYO......KUMBUKA PIA SI BANK ZOTE ZINARUHUSU KUNUNUA ONLINE ILA CHACHE TZ......SO HIZI ZILIZOJITAHID KURUHUSU KUTOA PESA NJE(KUTUMA/KUNUNUA) BASI HUENDA WAKAJA TUBORESHEA TUKAPOKEA/LIPWA TOKA NJE.
 
Naitaji kununua vitu online tafadhali naombeni maelekezo, maana sijajua
 
wakuu huu uzi nimeusoma zaidi ya mara tatu kwa nyakati tofauti na aliyeuanzisha naona alifikiria mbali sana maana nimegundua soko ni kubwa sana la baadhi ya bidhaa toka nchi zetu mfano mboga za majani, madini na vingine vingi mie nimeona fursa ya kuuza mawe yenye thamani ya kati ila baada ya kuona kuwa hatuwezi kupokea hela toka paypal imenivunja moyo sana maana, ila ipo siku najua milango itafunguka na tutafanya makubwa, pia sisi hatuwezi kuuza vitu kwenda nchi ka china kwakutumia site nyingine? maana wao wanauza kwetu zaidi kwakutumia site kibao ka KIKUU, aliexpress, made in china, yani site kibao wanatumia tujuzane na tutafute haya masoko ya nje japo tupate hela nzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…