Jiongeze: Mheshimu sana House girl anayebaki na mtoto wako, unapokuwa haupo hakuna kinachomzuia yeye kulipizia kisasi kwa mtoto

Jiongeze: Mheshimu sana House girl anayebaki na mtoto wako, unapokuwa haupo hakuna kinachomzuia yeye kulipizia kisasi kwa mtoto

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
nani anaependa kukaripiwa?
nanj anaependa kupigwa?
nani anapenda kugombezwa?
nani anapenda kupigwa?
nani anapenda kunyanyaswa?

HAKUNA!!!!

Inanishangaza sana kuona kuna baadhi ya wazazi hawaheshimu kabisa mahouse girl wanaobaki na watoto wao, huwaona kama wanadamu wa toleo la pili.

House girl anaweza kuyaficha mengi sana moyoni, wewe ukaona kwamba hajaumia lakini ana vitu vingi sana kakuvumilia ni vile tu hajaamua kubrespond wazi wazi, ndio hapo sasa humuona mtoto wako kama balozi wako, atakachokifanya kwa mtoto wako huendana na unavyoishi nae.

kama unaishi nae vizuri basi kwa kiasi kikubwa nae ataishi na mtoto wako vizuri ila kama unamnyanyasa nakwambia atakuwa anakuchekea usoni ama kujifanya kuchukulia poa unachomfanyia ila unapoondoka asubuhi kwenda kwenye shughuli zako, hapo mtoto wako ndio atatumiwa kulipizia kisasi, nadhani wengi sio wageni wa zile video za siri zinazorekodiwa ma house girl wakiwa peke yao na watoto, huwafanyia watoto unyama ambao unatisha sana.

Ishi vizuri na house girl wako anaekulelea watoto, kumnyanyasa, kumtukana, kumgombeza, kumpiga, n.k ni sawa na kutukana mamba kabla hujavuka mto.....Kisasi humwendea mtoto wako ambae hawezi kulalamika.

House girl wako anaekulelea mtoto hakikisha yupo kwenye mood nzuri, akiwa na mood mbaya inakuwa hatari sana kwa mtoto, kama ni mshahara mlipe kwa wakati, kama ni nguo mnunulie, kama ni kazi basi muwe mnasaidiana sio mambo ya kuamshana saa 11 asubuhi kila siku huku wewe unachapa usingizi, kama mnaenda out muwe mnaenda wote, msimtenge, n.k. akianza kujihisi tu kwamba mnamchukulia kama mwamadamu wa daraja la mwisho hii huwa inamjengea stress, hata kama hamumpigi ama kumtukana ama kumnyanyasa bado inampa stresa kuona anadharauliwa na hana thamani, kwa hizi stress zinamuondolea umakini kwenye kuwalelea mtoto wenu.

JIONGEZEEE!!
 
House girl anaekulelea mtoto inabidi apewe uzito wa hali ya juu sana kuliko house girl anaewasaidia kazi pekee,,,,,Mtoto wenu sio wa kumchukulia poa hata kidogo
 
mie huwa namtoaga na 10k - 20k ambayo iko njee kabsaa ya mshaharaaa

namwambia mtumie mama akooo ya sukari etc
Una akili sana, inabidi awe na mood nzuri, kuna muda hata kama humkaripii ama kumnyanyasa, anaona kwao wanateseka huku yeye anawaona matajiri hamteseki alafu mnashindwa hata kusaidia, hii huwa inamuharibu kisaikolojia
 
ndio maana tunawafanya small wife....sababu huduma yake ni njema......na dogo anampenda balaa....so dingi lazima umpe mahaba......akutuzie vema....
 
Jamaa kampima house girl kagundua ameathirika, alianza kumyanyapaa akijiandaa kumrudisha kwao. Akiwa na watoto wake wadogo alimkata mmoja kucha kisha akamkata kidogo akaunganisha na damu yake. Alimhurumia tu angewakata wote. Bosi hana habari ila baada ya kumrudisha nyumbani aligundua kuwa mtoto wake mmoja ana virusi. Hayo ndio mambo ya house girl
 
mie huwa namtoaga na 10k - 20k ambayo iko njee kabsaa ya mshaharaaa

namwambia mtumie mama akooo ya sukari etc
Hapo hata mtoto akilia tu anabembelezwa that's all kumteka ki saikolojia housgirl it's showing love to her she Will pas that love to ya son and viservesa
 
Jamaa kampima house girl kagundua ameathirika, alianza kumyanyapaa akijiandaa kumrudisha kwao. Akiwa na watoto wake wadogo alimkata mmoja kucha kisha akamkata kidogo akaunganisha na damu yake. Alimhurumia tu angewakata wote. Bosi hana habari ila baada ya kumrudisha nyumbani aligundua kuwa mtoto wake mmoja ana virusi. Hayo ndio mambo ya house girl
It's a pity
 
Jamaa kampima house girl kagundua ameathirika, alianza kumyanyapaa akijiandaa kumrudisha kwao. Akiwa na watoto wake wadogo alimkata mmoja kucha kisha akamkata kidogo akaunganisha na damu yake. Alimhurumia tu angewakata wote. Bosi hana habari ila baada ya kumrudisha nyumbani aligundua kuwa mtoto wake mmoja ana virusi. Hayo ndio mambo ya house girl
Pauka pakawa hadith yetu ya shabani robert
 
Nasisitiza.. tuwaheshimu na kuwapenda wadada wa kazi
 
Back
Top Bottom