Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Screenshot_20220211-194631_Snapchat.jpg
 
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.

Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.

Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.

Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.

Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.

Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.

Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.

Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.

Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.

Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.

"Habari?" Tukionana.

"Asante." Tukiagana.

Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.

Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.

Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.

Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.

Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.

Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.

Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.

Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"

Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.

Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.

Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.

Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?

Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.

Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.

Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.

Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.

Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.

Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.

Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.

Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.

Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.

Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.

Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.

Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.

Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.

Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.

Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.

Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.

Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!

Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?

Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.

***
Beb moneytalk
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida - 06

Sikupoteza muda, nilijiandaa upesi nikaongozana na jirani mmoja wa kiume mpaka hospitali Mwananyamala tulipoambiwa kuwa ndipo alipo bwana Tarimo. Tulipofika huko, tulipokelewa na mke wa bwana huyo akiwa na uso ulioparama kwa majonzi.

Mwanamke huyo hakuwa anaweza kuongea hata maneno mawili kwa usahihi, kila alipotoa neno moja ni kama vile alitoneshwa upya kidonda akaishia kunyamaza akiufunika uso wake, alikuwa anatia huruma kwelikweli na alinifanya niamini kuwa hali haikuwa shwari huko ndani. Mama huyo pembeni yake alikuwa akifarijiwa na mmoja wa ndugu yake Tarimo, ndugu ambaye mimi sikuwa namfahamu kwani alikuwa mgeni machoni pangu.

Ndugu huyo, kwasababu angalau yeye alikuwa anajiweza, basi ndo’ akawa anaongea na sisi kutupatia taarifa ya kinachoendelea hapo, kwa maelezo yake bwana Tarimo alikuwa amevunjika miguu yote miwili, mkono mmoja, kiuno na taya pia! Kwa namna hiyo bwana Tarimo alikuwa anangojea tu rufaa apelekwe Muhimbili.

Baada ya muda kidogo wa kungoja nilipata nafasi ya kumwona bwana huyo, kwakweli hakuwa anatamanika, ajali ilimchakaza sana, lilikuwa ni jambo la kheri sana kumwona bado yu hai, pale niliamini kweli kama siku yako ya kwenda haijafika basi hautaenda hata iweje.

Tulikaa hapo kwa muda wa lisaa limoja hivi kabla hatujageuza kurejea nyumbani. Tulipanga siku ya kuja kumwona tena bwana Tarimo huku tukisihi maombi mengi yanahitajika bwana huyo apate kusimama kwa mara nyingine. Kuja kufika nyumbani, majira ya saa nane hivi ya usiku, sikufanya kitu kingine nikaoga na kupumzika usiku wake nikiwaza kumhusu bwana Tarimo.

Yale yote aliyotaka kuniambia yaligeuka mawe … kweli hamna mtu anayeijua kesho yake, niliwaza nikijigeuza huku na kule pale kitandani. Sasa kitu pekee ambacho bwana Tarimo alikuwa ameniachia kikawa ni mawazo makubwa kumhusu bwana BIGI, kwanini bwana huyo aliniambia tufanye kila linalowezekana ili BIGI ahame pale? Ni nini aliona mpaka akafikia hitimisho kama hilo? Kwakweli nilitamani sana kujua kama kuna mtu ameyaona zaidi ya yale ambayo mimi nimeyaona.

Nikiwa naendelea kuwaza, akili yangu ikipiga mbizi katika dimbwi hilo la mawazo, mara usingizi ukanibeba msobemsobe nisijue nimepotelea humo saa ngapi, ni baadae ndo’ nilikuja kugutuka baada ya kusikia ndoo ikianguka chini huko nje puuuh, nikaamka upesi kuangaza dirishani. Bila shaka ndoo ile ilikuwapo kibarazani ndo’ maana kuanguka kwake kukawa na kishindo.

Niliitazama ndoo ile ikiwa inazungukazunguka pale chini mpaka ikatulia kabisa. Kimya. Sikuona mtu wala kitu cha kutilia shaka. Nilitazama lile geti dogo, geti jipya, nalo nikaliona limefungwa basi nikarejea kitandani nikiamini ndoo ile iliangushwa na upepo wa huko nje.

Nilitazama saa kwenye simu yangu, ilikuwa ni saa tisa, nikajilaza kuutafuta usingizi tena lakini kabla sijapotelea kwenye njozi nilisikia tena ndoo ikipigwa, nikashtuka. Mlio niliousikia ni kana kwamba mtu ameipiga teke ndoo ile, taratibu nikafungua pazia la dirisha kutazama.

Niliona ndoo ile ikiwa karibu na geti dogo, hapo inazungukazunguka kwenda kushoto na kulia, kulia na kushoto, alafu ikatulia tuli.

Nilitazama kando na kando lakini sikumwona mtu, kulikuwa kimya na kumetulia sana, nikajiuliza ni masikio na macho yangu ndiyo yananidanganya ama? Au ni usingizi na sijapata muda wa kutosha kupumzika? Sikupata majibu … niliendelea kutazama ile ndoo na pande zingine zote kwa muda wa dakika tano hivi, nilipoona hamna kitu niliachia pazia nikajilaza, sikusikia tena kitu mpaka jua linakucha na ndo’ mimi nikalala kwa amani.

Nilikuja kuamka baadae majira ya mchana baada ya kusikia sauti za watoto huko nje wakiwa wanacheza na kukimbizana. Nilitoka nikaenda kuoga kisha nikaketi sebuleni pamoja na tarakilishi yangu kufanya kazi za hapa na pale, muda si mwingi alikuja jirani mmoja aliyegonga mlango na kuniambia kuna zoezi la kuchangia pesa kwaajili ya kuifariji familia ya Tarimo na mkasa uliowapata.

Jirani huyo alikuwa ameshikilia daftari, peni, noti na sarafu lukuki mkono wake wa kushoto ambazo bila shaka alikuwa ameziokoteza kwa majirani wengine. Aliniambia Tarimo ameshahamishwa kwenda Muhimbili kwaajili ya matibabu zaidi na hizo pesa wanazozichanga si kwamba wameombwa na familia ya wahanga, lah, bali ni jitihada za kuonyesha umoja wetu nyakati za matatizo, nikaona vema.

Nilitoa pesa akanipatia peni kuandika jina langu pamoja na sahihi, sikuona haja ya lile jambo lakini kwasababu nililazimika basi nikafanya hivyo, niliandika jina langu na kiasi nilichotoa, katika karatasi lile nikapata kuona majina matano hivi ya majirani wengine waliokwisha kutoa, sikuyatilia maanani majina hayo wala kiasi walichotoa, ila kitu kilichonishangaza ni wingi wa sarafu zile alizokuwa amezishikilia bwana mchangaji, sarafu nyingi mno za hamsini hamsini, nikamuuliza kwa utani,

“Ndugu yangu, umekuwa kondakta?”

Bwana yule alitabasamu kwanza alafu akaniambia sarafu zingine anazo mfukoni, kweli nilipotazama nikaona mfuko wake umenenepa haswa. Nilistaajabu, yeye akaongezea kutabasamu kabla hajaniambia kuna jirani amempatia sarafu hizo na kwa ujumla wake zilikuwa yapata alfu ishirini! … baada ya hapo alienda zake kuendelea na zoezi la kuchanga pesa na mimi nikaendelea na shughuli zangu nilizokuwa nafanya.

Majira ya mchana, kwasababu ya kuboreka kukaa nyumbani tangu asubuhi, niliona ni vema nikanyoosha miguu kwa kutembea hapa na pale. Nilifikiria nielekee wapi, mwishowe nikakata shauri kwenda ‘bar’ fulani hivi ambayo ni mashuhuri kwa kuuza mbege kwani ilikuwa ni muda mrefu sijapata kinywaji hicho na nilihisi kiu chake. Nilichukua chupa ya lita moja na kiasi fulani cha pesa kisha nikashika njia kuelekea huko.

Ukiwa unatumia njia ya lami ya Goba kwenda mwelekeo wa Mbezi Mwisho, kuna kituo kinaitwa kwa Ndambi, kituo cha nyuma yake na cha Kontena ambacho ndipo kina sisi wa Goba Mashuka huteremkia. Ukishukia hapo kwa Ndambi kuna njia kubwa ya vumbi mkono wa kushoto, njia hiyo ukiifuata moja kwa moja, kwa kama dakika sita hivi, mkono wa kushoto utaiona bar hiyo niliyokuwa naiendea, hapo wanauza vinywaji vyote lakini pia wameandika kibao ‘Mbege Ipo’.

Ili kuifikia Bar hiyo kwa sisi ambao tunatokea Goba kwa Mashuka unalazimika kutembea umbali mrefu kukwea kilima mpaka kituo cha Kontena alafu urudi kituo cha nyuma cha Kwa Ndambi, vinginevyo, kwa njia fupi zaidi ya miguu, unakatiza kwenye lile korongo kubwa kuibukia ng’ambo ambako huko ndo’ kwa Ndambi, yaani kwa Ndambi na hapo Mashuka pametenganishwa tu na korongo hilo, korongo ambalo si njia rasmi bali watu hulitumia tu kwaajili ya kupunguza umbali wa safari.

Korongo hilo majira ya usiku huwa na kiza totoro, bila ya kutembea na kurunzi huwezi kuona unapokanyaga na kwasababu hiyo watu hawapendi kutumia njia hiyo, hata majira hayo ya mchana ni watu wachache wachache wangependa kupita hapo.

Nilikatiza korongoni nikipiga mahesabu ya kwenda na kuwahi kurudi kabla ya giza halijawa kubwa kwani sikutaka kutumia njia ndefu zaidi ya ile. Nilipomaliza korongo hilo, nilitumia kama dakika sita tu kufika katika ile bar, hapo nilikuta mziki mtamu na laini ukipiga kuburudisha wateja, tena ule muziki usiokuwa na fujo wala purukushani, nikaona ni vema sana nikipumzika hapo. Watu wachache na muziki usiokuwa na fujo ni moja ya mandhari zangu pendwa kabisa.

Nilitafuta sehemu palipokuwa pweke, nikakaa hapo, muda mchache tu mhudumu akaja kunikirimu. Mhudumu huyo ndiye aliyekuwa mmiliki wa ile biashara hivyo alikuwa anafanya kazi kwa moyo wake wote.

“Karibu, kaka.”

“Ahsante,” nilimwitikia nikampatia chupa yangu na kumwambia: “nahitaji mbege lita moja.”

Mara akaufinyanga uso wake kwa kuhuzunika.

“Daah pole, mbege imeisha muda si mrefu. Hapa ni mpaka kesho tena!”

Basi kwasababu hiyo nililazimika kuagiza bia mbili za baridi ili safari yangu yote isiwe bure, nikawa nakunywa taratibu huku naperuzi simu yangu nikiingia hapa na kutokea pale, nikiingia pale na kutokea hapa, kwa mbali muziki ukiniburudisha vilivyo.

Niliagiza bia tena na tena, kwa namna nilivyokuwa ‘busy’ na simu sikuwa natambua hata bia zile zilikua zinaenda wapi, nilijikuta nakunywa chupa na chupa hata nisijali. Baadae nilipata ‘kampani’ ya bwana mmoja ambaye naye alikuwa mpenzi wa nyimbo zile zilizokuwa zinapigwa basi nikajikuta nazidi kulowea hapo, tunaongea hiki na kile, kuja kupata ufahamu ni saa mbili usiku, kinyume kabisa na muda niliopanga kuondoka!

Nilinyanyuka upesi nikalipia bili yangu kisha nikaanza kiguu na njia, mwelekeo ni uleule wa korongoni kwani sikuwa radhi kuzunguka na njia ndefu ya kule barabarani, baada ya dakika chache nikafika korongoni, nilipotazama humo nikahamaki kwa kiza chake, aisee, kulikuwa ni kweusi tiii! Ile miti ambayo inapeperuka kwa upepo nyakati za mchana iligeuka kuwa mavitu meusi marefu ambayo yanatisha kwelikweli, ilitaka moyo sana kupita humo.

Niliwaza kurudi nyuma lakini nilipofikiria umbali wa safari ile, mmmh, nikajipa moyo, nitapita humohumo, siwezi kurudi nyuma wakati mataa ya nyumbani nayaona yalee kwa macho yangu, basi nikaingia korongoni huku nikitumia mwanga wa tochi ya simu yangu.

Nilitembea taratibu nikiwa naangaza ninapokanyaga, ndani ya korongo hilo kupo kimya, cha zaidi unachosikia ni matawi ya miti pale upepo unapopuliza. Nikiwa katikati ya korongo hilo, mara nilisikia sauti ya kitu kinachotembea … kabla sijafanya jambo lolote, mara nikasikia kitu hicho kikimbia! Niligeuka kuangaza kwa macho na tochi ya simu yangu nikamwona paka mmoja akiwa anakimbia kama mwehu, ni kana kwamba paka huyo alishambuliwa na mtu ama aliona kitu cha hatari.

Nilimtazama namna anavyokimbia nikajikuta napatwa na hofu nisijue ni ya kitu gani. Paka yule alipoishia katika macho yangu, upande uleule alokuwa anakimbilia, nikapata kuona viroba vitatu vikiwa vimepangana … sikujua ni nini lakini viroba hivyo vilinikumbusha taswira ya bwana BIGI upesi mno!

Vipi kama vile viroba ndo’ vile anavyovibeba nyakati za usiku wa manane? Nilijiuliza.

Nilivitazama kwa sekunde kadhaa, nafsi yangu ikawa inanituma niende nikavitazame viroba hivyo vina nini ndani yake. Baada ya muda mchache wa kujiuliza nilikata shauri kwenda kutazama, nikakwea kingo ya korongo na kuvuta kiroba kimojawapo mpaka chini miguuni mwangu. Kiroba hicho kilikuwa cheupe na kimefungwa mdomo kwa kamba ya katani, niliposogeza uso wangu karibu na kiroba hicho nilihisi harufu kali ya kuoza, na harufu hiyo ikawa inaongezeka kadiri nilivyokuwa najaribu kufungua kamba ile kuona kilichomo ndani.

***

Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
 
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.

Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.

Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.

Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.

Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.

Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.

Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.

Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.

Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.

Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.

"Habari?" Tukionana.

"Asante." Tukiagana.

Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.

Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.

Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.

Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.

Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.

Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.

Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.

Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"

Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.

Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.

Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.

Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?

Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.

Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.

Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.

Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.

Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.

Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.

Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.

Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.

Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.

Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.

Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.

Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.

Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.

Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.

Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.

Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.

Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!

Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?

Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.

***
Mwandishi mahiri pia, haki nasisimka nikiwa na soma kwa umahiri wako. Kongole kwako chief!

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom