Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tayukwa Lucha Valentina Kalpana Watu8 atlas copco LovelovieYule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11
"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."
Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.
Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.
Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.
Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.
Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.
Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.
Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."
Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.
Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."
Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.
Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:
"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."
Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.
Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.
Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"
Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!
Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.
Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.
Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.
Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.
Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.
Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.
Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.
Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.
Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.
Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.
Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.
Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.
Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.
Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."
Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.
Kwani,
Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.
Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.
Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.
Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.
Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,
"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."
Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.
Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
Assnte, nawaza nguvu ya kumbeba kumueka kwenye gari ningeitoa wapi
Mzee asante sanaYule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11
"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."
Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.
Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.
Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.
Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.
Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.
Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.
Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."
Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.
Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."
Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.
Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:
"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."
Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.
Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.
Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"
Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!
Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.
Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.
Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.
Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.
Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.
Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.
Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.
Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.
Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.
Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.
Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.
Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.
Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.
Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."
Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.
Kwani,
Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.
Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.
Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.
Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.
Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,
"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."
Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.
Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
Ndio mwisho au kuna mwendelezo?Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11
"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."
Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.
Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.
Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.
Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.
Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.
Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.
Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."
Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.
Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."
Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.
Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:
"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."
Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.
Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.
Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"
Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!
Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.
Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.
Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.
Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.
Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.
Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.
Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.
Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.
Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.
Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.
Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.
Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.
Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.
Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."
Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.
Kwani,
Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.
Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.
Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.
Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.
Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,
"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."
Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.
Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
Shukrani sana.Mzee asante sana
Mkuje Shunie Kalpana Mideko Kanali_ bilu97 MAKULUGA Kelsea moneytalk atlas copco Annonymous
Atakuambia jumapili usiku.Aiseeh,tunaendelea lin tena mkuu?
Ebwana eeh daah huyo Big kabisa huyoJirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida - 06
Sikupoteza muda, nilijiandaa upesi nikaongozana na jirani mmoja wa kiume mpaka hospitali Mwananyamala tulipoambiwa kuwa ndipo alipo bwana Tarimo. Tulipofika huko, tulipokelewa na mke wa bwana huyo akiwa na uso ulioparama kwa majonzi.
Mwanamke huyo hakuwa anaweza kuongea hata maneno mawili kwa usahihi, kila alipotoa neno moja ni kama vile alitoneshwa upya kidonda akaishia kunyamaza akiufunika uso wake, alikuwa anatia huruma kwelikweli na alinifanya niamini kuwa hali haikuwa shwari huko ndani. Mama huyo pembeni yake alikuwa akifarijiwa na mmoja wa ndugu yake Tarimo, ndugu ambaye mimi sikuwa namfahamu kwani alikuwa mgeni machoni pangu.
Ndugu huyo, kwasababu angalau yeye alikuwa anajiweza, basi ndo’ akawa anaongea na sisi kutupatia taarifa ya kinachoendelea hapo, kwa maelezo yake bwana Tarimo alikuwa amevunjika miguu yote miwili, mkono mmoja, kiuno na taya pia! Kwa namna hiyo bwana Tarimo alikuwa anangojea tu rufaa apelekwe Muhimbili.
Baada ya muda kidogo wa kungoja nilipata nafasi ya kumwona bwana huyo, kwakweli hakuwa anatamanika, ajali ilimchakaza sana, lilikuwa ni jambo la kheri sana kumwona bado yu hai, pale niliamini kweli kama siku yako ya kwenda haijafika basi hautaenda hata iweje.
Tulikaa hapo kwa muda wa lisaa limoja hivi kabla hatujageuza kurejea nyumbani. Tulipanga siku ya kuja kumwona tena bwana Tarimo huku tukisihi maombi mengi yanahitajika bwana huyo apate kusimama kwa mara nyingine. Kuja kufika nyumbani, majira ya saa nane hivi ya usiku, sikufanya kitu kingine nikaoga na kupumzika usiku wake nikiwaza kumhusu bwana Tarimo.
Yale yote aliyotaka kuniambia yaligeuka mawe … kweli hamna mtu anayeijua kesho yake, niliwaza nikijigeuza huku na kule pale kitandani. Sasa kitu pekee ambacho bwana Tarimo alikuwa ameniachia kikawa ni mawazo makubwa kumhusu bwana BIGI, kwanini bwana huyo aliniambia tufanye kila linalowezekana ili BIGI ahame pale? Ni nini aliona mpaka akafikia hitimisho kama hilo? Kwakweli nilitamani sana kujua kama kuna mtu ameyaona zaidi ya yale ambayo mimi nimeyaona.
Nikiwa naendelea kuwaza, akili yangu ikipiga mbizi katika dimbwi hilo la mawazo, mara usingizi ukanibeba msobemsobe nisijue nimepotelea humo saa ngapi, ni baadae ndo’ nilikuja kugutuka baada ya kusikia ndoo ikianguka chini huko nje puuuh, nikaamka upesi kuangaza dirishani. Bila shaka ndoo ile ilikuwapo kibarazani ndo’ maana kuanguka kwake kukawa na kishindo.
Niliitazama ndoo ile ikiwa inazungukazunguka pale chini mpaka ikatulia kabisa. Kimya. Sikuona mtu wala kitu cha kutilia shaka. Nilitazama lile geti dogo, geti jipya, nalo nikaliona limefungwa basi nikarejea kitandani nikiamini ndoo ile iliangushwa na upepo wa huko nje.
Nilitazama saa kwenye simu yangu, ilikuwa ni saa tisa, nikajilaza kuutafuta usingizi tena lakini kabla sijapotelea kwenye njozi nilisikia tena ndoo ikipigwa, nikashtuka. Mlio niliousikia ni kana kwamba mtu ameipiga teke ndoo ile, taratibu nikafungua pazia la dirisha kutazama.
Niliona ndoo ile ikiwa karibu na geti dogo, hapo inazungukazunguka kwenda kushoto na kulia, kulia na kushoto, alafu ikatulia tuli.
Nilitazama kando na kando lakini sikumwona mtu, kulikuwa kimya na kumetulia sana, nikajiuliza ni masikio na macho yangu ndiyo yananidanganya ama? Au ni usingizi na sijapata muda wa kutosha kupumzika? Sikupata majibu … niliendelea kutazama ile ndoo na pande zingine zote kwa muda wa dakika tano hivi, nilipoona hamna kitu niliachia pazia nikajilaza, sikusikia tena kitu mpaka jua linakucha na ndo’ mimi nikalala kwa amani.
Nilikuja kuamka baadae majira ya mchana baada ya kusikia sauti za watoto huko nje wakiwa wanacheza na kukimbizana. Nilitoka nikaenda kuoga kisha nikaketi sebuleni pamoja na tarakilishi yangu kufanya kazi za hapa na pale, muda si mwingi alikuja jirani mmoja aliyegonga mlango na kuniambia kuna zoezi la kuchangia pesa kwaajili ya kuifariji familia ya Tarimo na mkasa uliowapata.
Jirani huyo alikuwa ameshikilia daftari, peni, noti na sarafu lukuki mkono wake wa kushoto ambazo bila shaka alikuwa ameziokoteza kwa majirani wengine. Aliniambia Tarimo ameshahamishwa kwenda Muhimbili kwaajili ya matibabu zaidi na hizo pesa wanazozichanga si kwamba wameombwa na familia ya wahanga, lah, bali ni jitihada za kuonyesha umoja wetu nyakati za matatizo, nikaona vema.
Nilitoa pesa akanipatia peni kuandika jina langu pamoja na sahihi, sikuona haja ya lile jambo lakini kwasababu nililazimika basi nikafanya hivyo, niliandika jina langu na kiasi nilichotoa, katika karatasi lile nikapata kuona majina matano hivi ya majirani wengine waliokwisha kutoa, sikuyatilia maanani majina hayo wala kiasi walichotoa, ila kitu kilichonishangaza ni wingi wa sarafu zile alizokuwa amezishikilia bwana mchangaji, sarafu nyingi mno za hamsini hamsini, nikamuuliza kwa utani,
“Ndugu yangu, umekuwa kondakta?”
Bwana yule alitabasamu kwanza alafu akaniambia sarafu zingine anazo mfukoni, kweli nilipotazama nikaona mfuko wake umenenepa haswa. Nilistaajabu, yeye akaongezea kutabasamu kabla hajaniambia kuna jirani amempatia sarafu hizo na kwa ujumla wake zilikuwa yapata alfu ishirini! … baada ya hapo alienda zake kuendelea na zoezi la kuchanga pesa na mimi nikaendelea na shughuli zangu nilizokuwa nafanya.
Majira ya mchana, kwasababu ya kuboreka kukaa nyumbani tangu asubuhi, niliona ni vema nikanyoosha miguu kwa kutembea hapa na pale. Nilifikiria nielekee wapi, mwishowe nikakata shauri kwenda ‘bar’ fulani hivi ambayo ni mashuhuri kwa kuuza mbege kwani ilikuwa ni muda mrefu sijapata kinywaji hicho na nilihisi kiu chake. Nilichukua chupa ya lita moja na kiasi fulani cha pesa kisha nikashika njia kuelekea huko.
Ukiwa unatumia njia ya lami ya Goba kwenda mwelekeo wa Mbezi Mwisho, kuna kituo kinaitwa kwa Ndambi, kituo cha nyuma yake na cha Kontena ambacho ndipo kina sisi wa Goba Mashuka huteremkia. Ukishukia hapo kwa Ndambi kuna njia kubwa ya vumbi mkono wa kushoto, njia hiyo ukiifuata moja kwa moja, kwa kama dakika sita hivi, mkono wa kushoto utaiona bar hiyo niliyokuwa naiendea, hapo wanauza vinywaji vyote lakini pia wameandika kibao ‘Mbege Ipo’.
Ili kuifikia Bar hiyo kwa sisi ambao tunatokea Goba kwa Mashuka unalazimika kutembea umbali mrefu kukwea kilima mpaka kituo cha Kontena alafu urudi kituo cha nyuma cha Kwa Ndambi, vinginevyo, kwa njia fupi zaidi ya miguu, unakatiza kwenye lile korongo kubwa kuibukia ng’ambo ambako huko ndo’ kwa Ndambi, yaani kwa Ndambi na hapo Mashuka pametenganishwa tu na korongo hilo, korongo ambalo si njia rasmi bali watu hulitumia tu kwaajili ya kupunguza umbali wa safari.
Korongo hilo majira ya usiku huwa na kiza totoro, bila ya kutembea na kurunzi huwezi kuona unapokanyaga na kwasababu hiyo watu hawapendi kutumia njia hiyo, hata majira hayo ya mchana ni watu wachache wachache wangependa kupita hapo.
Nilikatiza korongoni nikipiga mahesabu ya kwenda na kuwahi kurudi kabla ya giza halijawa kubwa kwani sikutaka kutumia njia ndefu zaidi ya ile. Nilipomaliza korongo hilo, nilitumia kama dakika sita tu kufika katika ile bar, hapo nilikuta mziki mtamu na laini ukipiga kuburudisha wateja, tena ule muziki usiokuwa na fujo wala purukushani, nikaona ni vema sana nikipumzika hapo. Watu wachache na muziki usiokuwa na fujo ni moja ya mandhari zangu pendwa kabisa.
Nilitafuta sehemu palipokuwa pweke, nikakaa hapo, muda mchache tu mhudumu akaja kunikirimu. Mhudumu huyo ndiye aliyekuwa mmiliki wa ile biashara hivyo alikuwa anafanya kazi kwa moyo wake wote.
“Karibu, kaka.”
“Ahsante,” nilimwitikia nikampatia chupa yangu na kumwambia: “nahitaji mbege lita moja.”
Mara akaufinyanga uso wake kwa kuhuzunika.
“Daah pole, mbege imeisha muda si mrefu. Hapa ni mpaka kesho tena!”
Basi kwasababu hiyo nililazimika kuagiza bia mbili za baridi ili safari yangu yote isiwe bure, nikawa nakunywa taratibu huku naperuzi simu yangu nikiingia hapa na kutokea pale, nikiingia pale na kutokea hapa, kwa mbali muziki ukiniburudisha vilivyo.
Niliagiza bia tena na tena, kwa namna nilivyokuwa ‘busy’ na simu sikuwa natambua hata bia zile zilikua zinaenda wapi, nilijikuta nakunywa chupa na chupa hata nisijali. Baadae nilipata ‘kampani’ ya bwana mmoja ambaye naye alikuwa mpenzi wa nyimbo zile zilizokuwa zinapigwa basi nikajikuta nazidi kulowea hapo, tunaongea hiki na kile, kuja kupata ufahamu ni saa mbili usiku, kinyume kabisa na muda niliopanga kuondoka!
Nilinyanyuka upesi nikalipia bili yangu kisha nikaanza kiguu na njia, mwelekeo ni uleule wa korongoni kwani sikuwa radhi kuzunguka na njia ndefu ya kule barabarani, baada ya dakika chache nikafika korongoni, nilipotazama humo nikahamaki kwa kiza chake, aisee, kulikuwa ni kweusi tiii! Ile miti ambayo inapeperuka kwa upepo nyakati za mchana iligeuka kuwa mavitu meusi marefu ambayo yanatisha kwelikweli, ilitaka moyo sana kupita humo.
Niliwaza kurudi nyuma lakini nilipofikiria umbali wa safari ile, mmmh, nikajipa moyo, nitapita humohumo, siwezi kurudi nyuma wakati mataa ya nyumbani nayaona yalee kwa macho yangu, basi nikaingia korongoni huku nikitumia mwanga wa tochi ya simu yangu.
Nilitembea taratibu nikiwa naangaza ninapokanyaga, ndani ya korongo hilo kupo kimya, cha zaidi unachosikia ni matawi ya miti pale upepo unapopuliza. Nikiwa katikati ya korongo hilo, mara nilisikia sauti ya kitu kinachotembea … kabla sijafanya jambo lolote, mara nikasikia kitu hicho kikimbia! Niligeuka kuangaza kwa macho na tochi ya simu yangu nikamwona paka mmoja akiwa anakimbia kama mwehu, ni kana kwamba paka huyo alishambuliwa na mtu ama aliona kitu cha hatari.
Nilimtazama namna anavyokimbia nikajikuta napatwa na hofu nisijue ni ya kitu gani. Paka yule alipoishia katika macho yangu, upande uleule alokuwa anakimbilia, nikapata kuona viroba vitatu vikiwa vimepangana … sikujua ni nini lakini viroba hivyo vilinikumbusha taswira ya bwana BIGI upesi mno!
Vipi kama vile viroba ndo’ vile anavyovibeba nyakati za usiku wa manane? Nilijiuliza.
Nilivitazama kwa sekunde kadhaa, nafsi yangu ikawa inanituma niende nikavitazame viroba hivyo vina nini ndani yake. Baada ya muda mchache wa kujiuliza nilikata shauri kwenda kutazama, nikakwea kingo ya korongo na kuvuta kiroba kimojawapo mpaka chini miguuni mwangu. Kiroba hicho kilikuwa cheupe na kimefungwa mdomo kwa kamba ya katani, niliposogeza uso wangu karibu na kiroba hicho nilihisi harufu kali ya kuoza, na harufu hiyo ikawa inaongezeka kadiri nilivyokuwa najaribu kufungua kamba ile kuona kilichomo ndani.
***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
sophy27Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11
"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."
Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.
Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.
Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.
Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.
Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.
Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.
Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."
Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.
Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."
Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.
Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:
"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."
Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.
Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.
Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"
Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!
Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.
Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.
Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.
Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.
Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.
Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.
Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.
Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.
Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.
Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.
Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.
Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.
Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.
Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."
Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.
Kwani,
Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.
Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.
Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.
Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.
Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,
"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."
Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.
Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
Ah nimeridhika sasa. Episode ina nyama nyama. AsanteYule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11
"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."
Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.
Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.
Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.
Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.
Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.
Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.
Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."
Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.
Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."
Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.
Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:
"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."
Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.
Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.
Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"
Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!
Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.
Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.
Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.
Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.
Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.
Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.
Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.
Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.
Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.
Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.
Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.
Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.
Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.
Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."
Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.
Kwani,
Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.
Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.
Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.
Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.
Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,
"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."
Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.
Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
,Get Rich ukujeYule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11
"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."
Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.
Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.
Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.
Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.
Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.
Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.
Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."
Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.
Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."
Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.
Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:
"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."
Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.
Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.
Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"
Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!
Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.
Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.
Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.
Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.
Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.
Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.
Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.
Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.
Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.
Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.
Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.
Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.
Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.
Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."
Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.
Kwani,
Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.
Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.
Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.
Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.
Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,
"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."
Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.
Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
Kirahisi hivyo? Hapo Bembela au Auntiye.Itakua li Big lime dead