Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Wewe ndiomgonjwa mkuu..
Hadithi hujatunga wewe!
Husimulii wewe
Hujalazimishwa kusoma
Bando lakw
Sasa makasiriko ya Nini !?
Punguza umbea, soma uelewe kama hujaelewa nilicho maanisha mshirikishe hata mumeo ,usipende kukurupuka kuleta sonona zako humu. Angalia content binti ....ikbidi jikite zaidi kumuhudumia Mumeo..
 
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.

Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.

Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.

Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.

Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.

Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.

Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.

Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.

Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.

Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.

"Habari?" Tukionana.

"Asante." Tukiagana.

Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.

Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.

Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.

Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.

Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.

Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.

Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.

Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"

Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.

Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.

Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.

Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?

Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.

Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.

Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.

Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.

Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.

Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.

Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.

Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.

Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.

Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.

Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.

Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.

Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.

Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.

Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.

Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.

Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!

Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?

Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.

***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
Mmmm
 
Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11


"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."

Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.

Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.

Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.

Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.

Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.

Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.

Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."

Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.

Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."

Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.

Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:

"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."

Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.

Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.

Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"

Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!

Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.

Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.

Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.

Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.

Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.

Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.

Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.

Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.

Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.

Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.

Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.

Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.

Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.

Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."

Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.

Kwani,

Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.

Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.

Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.

Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.

Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,

"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."

Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.

Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
SteveMollel hongera kwa kurudi kwenye mstari, ile unatoa story, episode bila namba ulizingua kinyama chalii angu

NB: hizo bonus nazo zinachangia kuvuruga mtiririko wa simulizi yako mkuu
𝕕𝕠𝕟'𝕥 𝕨𝕠𝕣𝕜 𝕙𝕒𝕣𝕕,𝕨𝕠𝕣𝕜 𝕤𝕞𝕒𝕣𝕥
 
Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11


"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."

Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.

Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.

Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.

Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.

Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.

Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.

Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."

Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.

Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."

Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.

Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:

"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."

Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.

Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.

Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"

Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!

Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.

Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.

Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.

Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.

Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.

Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.

Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.

Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.

Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.

Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.

Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.

Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.

Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.

Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."

Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.

Kwani,

Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.

Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.

Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.

Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.

Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,

"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."

Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.

Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
Half american Get Rich atlas copco
Haya mje mambo tayari
 
Hii Story Inawafanya watu watuone Sisi ma BiG tuonekane sio ngoja nilale tuu...
20230216_082715.jpg
 
Back
Top Bottom