Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kairudia tu haijaendelea
Hapana kuna moja mpya..hii ya ulinzi shirikishi ulikua umeisoma? Na kuugua kwa mke wa steve usiku?? Mi ndo naiona leoNdio lkn naona ni marudio ya juzi
Haaaaah kweli Ile ya kumi na moja eeh nmesoma ccy tena ngoja niirudie maan sikuelewa nilikua kweny purukushaniHapana kuna moja mpya..hii ya ulinzi shirikishi ulikua umeisoma? Na kuugua kwa mke wa steve usiku?? Mi ndo naiona leo
Mhh hapana sa hv bebe wangu ananinubulia pipi za bei mbaya sio hizo mara pipi ukwaju, mara pipi pilipili sitak mie
Ahh wacha nkusikitisheWe Sista mawigi Antonnia dada yako Lovelovie kanisikitisha sana, angejua hiyo 500 nilivyoisotea kwa boss Bantu Lady . angeipokea kwa mikono na miguu yote, maana nimedeki mpaka bahari ili wageni wa Bantu Lady wasikasirike.
Malimao yanakata shombo kweny mboga wala nisingekunywa ningetunza nikatumia polepole kweny upishTena Lovelovie shukuru MUNGU, asingekuwa my boss Bantu Lady kuangusha hizo 50 basi ningekunywesha juisi ya malimao coz umezidi utukutu. Haya we sista mawigi Antonnia njoo uone hiki
Anajiita Kobis Kikala mista romanticBIG atawakana mchana kweupe [emoji23]View attachment 2512531
Mbona sikuelewi Kwan ndo umeshaniacha au?Vina muda basii mtaachana tu
Jamani hii ilotumwq na mlatino ndo yule yule steve mollel?SteveMollel
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida – 11
KATIKATI ya usiku mke wangu alianza kuongea mwenyewe, mwanzoni nilidhani ni masikio yangu pengine yanasikia vibaya lakini nilipofungua macho kutazama nilibaini kile nilichokisikia kilikuwa ni kweli, mwanamke huyo alikuwa anaongea akiwa usingizini, maongezi ambayo kwa muda kidogo sikufahamu anachokimaanisha.
Kidogo, nikiwa namtazama na kumskiza, akakurupuka toka usingizini, aliponikuta namtazama akakurupuka tena zaidi kabla ya kutulia. Alikuwa ameparwa na hofu sana, macho ameyatoa akihema. Nilimuuliza ni nini kimemsibu lakini kabla hajaniambia kitu alinyoosha mkono wake kwenye swichi akawasha taa alafu akaniambia kwa kunong’ona, “kuna mtu mlangoni.” Akarudia tena akiwa amenishika mkono, “kuna mtu mlangoni.”
Nikatoka kwenda sebuleni kutazama, niliwasha taa nikaufungua mlango lakini huko sikuona kitu. Nilipogeuza uso kumtazama mke wangu nilimwona akiwa amesimama kwenye mlango wa chumbani ananitazama kwa macho ya hofu, nikamwambia hamna mtu hapa mlangoni wala koridoni kisha nikarejea naye chumbani, huko hakutaka tuzime taa abadan, alisema anaogopa sana.
Aliniambia alisikia mtu mwenye sauti kama ya kwake akiwa anagonga na kubisha hodi vilevile kama alivyokuwa anabisha hodi muda ule kwenye mlango wa BIGI. Alijaribu kuniamsha lakini sikuamka, punde kidogo ndo’ akasikia mlango unafunguliwa sebuleni.
Kwa kumtuliza, nikamwambia hiyo ni ndoto tu na jambo hilo ameliota maana alikuwa akilifikiria sana, cha muhimu apuuzie kisha alale hamna chochote kitakachotokea, kishingo upande akalala lakini akinisisitiza tena nisizime taa. Kama baada ya lisaa hivi akapitiwa na usingizi, lakini hakukucha mpaka asubuhi akawa anashtuka shtuka, si kwa kuota tena bali kwa uoga wake binafsi. Alikuja kulala kwa amani jua lilipomea.
Siku hiyo kama nilivyokuwa nimepanga, nilienda kumwona Tarimo kule hospitali, huko nikakutana na ndugu yuleyule ambaye nilimkuta siku ile kule Mwananyamala, ndugu huyo alikuwa pamoja na mke wa Tarimo, niliongea naye mambo kadha wa kadha kumhusu mgonjwa na nilipoona ni vema nikondoka zangu kurejea nyumbani. Nilipofika, hata sikupoa, nikapata taarifa kuwa mtoto wa Bembela, yule mwanamke mama ntilie, alizidiwa hoi bin taabani akafanya kuwahishwa hospitali ya Massana!
Yule jirani, mwanamke ambaye nilimdhania kuwa ni yeye ndiye alimpa maneno Bembela jana yake, alirejea majira ya jioni akitokea hospitali alipokuwapo na Bembela na mgonjwa akatuambia yale yaliyokuwa yamejiri, mtoto yule aliamka akiwa na homa kali tangu asubuhi na kutwa akilalamika mwili mzima unamuuma. Alimpatia dawa za kutuliza maumivu akidhani atapoa lakini kadiri muda ulivyoenda hakupata nafuu, ikambidi ampigie simu mama yake aje upesi waende hospitali. Maneno mengine aliyoyasema niliamini ni chumvi tu ya kwetu waswahili, sikuyatilia sana maanani mpaka pale kesho yake asubuhi mimi mwenyewe nilipopata kupitia hospitali ya Massana baada ya kupata upenyo mdogo kazini majira ya mchana, muda wa lunch. Hospitali hiyo haikuwa mbali na eneo ninapofanyia kazi, yaani hapo GOIG, hivyo haikuniwia ugumu kufika upesi kisha nikaendelea na mambo yangu mengine.
Hapo hospitali nilimkuta Bembela akiwa na mwanae kitandani anampatia chakula. Mtoto huyo alionekana hana nguvu, amevalia khanga aliyoifunga shingoni na uso wake unaugulia maumivu. Mwanamke yule, yaani Bembela, akanieleza ya kwamba usiku wa kuamkia siku ile mwanaye alikuwa anasumbuka sana na ndotoni, na mara mbili alikurupuka akisema kuna mtu anampiga, mtu asiyemwona, kwa maelezo hayo akaamini mwanaye anaota yale yaliyotokea siku ile.
Asubuhi ilipowasili, aliondoka kwenda kuendelea na shughuli zake za kawaida, hakuona kama jambo lile ni ishu kubwa, lakini ajabu majira ya baadae ndipo alipigiwa simu na shoga yake akaambiwa hali ya mtoto imekuwa mbaya, aliporejea akamkuta mtoto amevimba na baadhi ya sehemu zake za mwili zimevilia damu, kama haitoshi homa yake ilipanda sana na tena anatapika damu mara kwa mara. Jambo hilo likamshtua maana mpaka anaondoka ile asubuhi hakupata kuona kama kuna cha ajabu kumhusu mwanaye.
Mtoto alipimwa ikabainika ana majeraha ya ndani, lakini pia maumivu yake makali, kwa mujibu wa daktari, hayakusababishwa na kitu kingine isipokuwa kipigo, swala hilo likafanya daktari amtake Bembela kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi kwanza kwa kuhofia huenda mtoto yule alikuwa ni mhanga wa ukatili wa majumbani, naye akafanya hivyo lakini akiwa tayari ameshamkabidhi mtoto kwa ajili ya huduma. Lakini ajabu ni kwamba sisi sote tulikuwa tunafahamu kilichomtokea mtoto yule, tukio lililomtokea halikuwa cha kiasi hicho cha kumtia hali mbaya namna ile, hayo mambo ya kuvilia na kutapika damu yalikuwa yanashangaza sana.
Nilipomaliza kumwona mgonjwa nikaenda nyumbani na huko nikaeleza kwa wengine hali ya mtoto. Kesho yake, jumatatu, asubuhi nikiwa kazini nikapigiwa simu kuwa mtoto yule amefariki usiku, hivyo nyumbani kuna msiba. Jambo hilo likanishtua sana kwani sikutegemea kama lingetokea haraka hivyo, ndio mtoto yule alikuwa anaumwa lakini sikudhani kwa jinsi nilivyomwona siku ile basi angelifariki usiku wake. Wenyeji wa yale maeneo watakuwa wanaukumbuka msiba huu vema.
Msiba huo ulipelekwa nyumbani kwa wakina Bembela, maeneo ya Mbezi Mwisho, huko kwa wazazi wake. Wapangaji wote walihidhuria huo msiba isipokuwa bwana BIGI na familia yake. Hakuna aliyepata kuwaona mwanzo mpaka mwisho wa shughuli hiyo. Baadae, kwasababu ya kutokuwepo ama kushinda nyumbani muda mrefu wa siku, nilikuja kupata taarifa kuwa maafisa wa polisi walifika pale nyumbani kuwahoji baadhi ya watu kuhusu kesi ile ya mtoto. Walihitaji kuonana na bwana BIGI na familia yake lakini hakuwapo hata mmoja, wakaomba mawasiliano ya hao watu lakini hamna hata mtu mmoja alokuwa nayo, wengine walidhani mimi ningelikuwa nayo kwasababu ya yale madhali ya kipindi kile kuja naye na pikipiki lakini hata mimi sikuwahi kuwa nayo, basi wakachukua namba ya mwenye nyumba kisha wakajiondokea.
Baadae mimi nikiwa nipo nyumbani naambiwa hayo yaliyotokea, ndipo simu yangu inaita akipiga mwenye nyumba. Bwana huyo akaniambia ametafutwa na polisi anatakiwa atoe taarifa za bwana BIGI na ubaya ni kwamba yeye hana chochote kwani hakuwahi kupeana makaratasi yoyote na yule bwana, aliniuliza kama ninayo namba yake nikamwambia sina, mimi nilimshafikishia BIGI ule ujumbe wake kuhusu mkataba muda mrefu tu hivyo sikufahamu kama muda wote huo hawakupata kuonana, basi yule bwana aka-panick sana, alihofia atawaambia nini polisi wakamwelewa na vipi kama BIGI hatopatikana tena?
Zilipita siku kadhaa, kama mbili au tatu hivi, baadae nikaja kusikia tetesi kwa watu kuwa mtoto yule marehemu kabla ya kukumbana na kifo chake aliendelea kulalamika akiwa pale hospitali ya kwamba maumivu yanamzidi na kumzidi. Ni kana kwamba aliendelea kupigwa na kupigwa lakini alokuwa anampiga haonekani. Zoezi hilo lilidumu kwa muda kidogo tu akapoteza maisha.
Tetesi hizo zilisambaa sana pale nyumbani na zikajenga hofu kubwa kumhusu bwana BIGI, wengine wakarejea kauli ya Bembela akiwa pale mlangoni mwa BIGI kuwa kauli hiyo imemponza, na wengine wakasema bwana huyo hatokuja kurejea tena pale alipokuwa anaishi, kwamba ametoroka baada ya kufanya tukio.
Basi bwana, kama mchezo hivi, siku hiyo nikiwa natoka kazini na pikipiki, nikamwona bwana BIGI akiwa anashuka na begi lake mgongoni mwelekeo wake ni kule nyumbani. Sikujua kwamba ndo alikuwa anarejea nyumbani kutoka safari au alikuwapo tu hapa mjini, na kama anarejea kutoka safari mbona alikuwapo mwenyewe ingali pale nyumbani kwa maelezo ya majirani na polisi familia yake nzima haikuwapo? Au waliongea pasi na uhakika?
Nilimsalimu na kumtaka apande tumalizie safari yetu lakini alikataa, kabla ya kuachana nikamwambia anatafutwa sana na mwenye nyumba kuhusu swala lile la mkataba basi afanye namna wawasiliane, akaniambia anajua kila kitu, na anajua pia polisi wanamhitaji.
Baada ya hapo sikupata kuonana na bwana huyo kwa muda wa siku kadhaa, nilikuja kusikia polisi walionana naye na pia walimwona mtoto wake, yule mwenye utindio, lakini hamna cha maana na kikubwa kilichojiri. Kwa maneno ya yule shoga yake Bembela , maneno ambayo alipata kumwambia mke wangu, Bembela alikuwa amesafiri kwenda mkoani kuonana na mtaalam. Mwanamke huyo , yaani Bembela, hakupata kuwa sawa tena tangu tukio lile la mwanae na aliamini kabisa lina mkono wa mtu.
Lakini mbali na mwanamke huyo, hata mimi mwenyewe mke wangu hakupata kuwa sawa tena tangu siku ile. Hali ambayo ilikuja kupelekea hata baadae mimba yake kuharibika, hili ntakuja kulieleza hapo mbele, lakini punde kama siku chache mbele ya lile tukio, mke wangu alianza kuona siku zake pamoja na kuwa mjamzito.
****
Ndio kila siku zuuu zuuuu nimeachiaaaMbona sikuelewi Kwan ndo umeshaniacha au?
Big kama nAmjua vileJirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida - 04
Kikao kilikwisha kwa pande zote mbili kuelewana, mwenye nyumba alisema baada ya siku tatu mafundi watakuja kwaajili ya kuanza ujenzi lakini pia hapohapo kabla kikao hakijaisha akasisitizia kuhusu kodi yake, hili nililijua tu litakuja, alisema na yeye atapata nguvu zaidi ya kuboresha miundombinu endapo sisi tutatoa pesa zake kwa wakati, baada ya kikao kuisha aliaga na kwenda zake na kila mtu akaendelea na shughuli zake, angalau sasa na mimi nikapumzika na macho ya yule shemeji, macho ambayo sikuelewa yanamaanisha nini zaidi ya kunitisha.
Zikapita siku mbili, mafundi hawakuja kama tulivyoambiwa, ikapita siku ya tatu na ya nne, hola, mpaka wiki nzima iliyoyoma si fundi wala mhandisi aliyekuja, mwenye nyumba anatupiga tu kalenda.
Siku moja nikiwa niko nyumbani, sikumbuki haswa zilipita siku ngapi tangu tufanye kile kikao, katika majira ya saa saba usiku nikasikia mtu anafungua mlango wake, sikujua ni nani maana mimi nilikuwa ndani sebuleni lakini ni bayana alikuwa ni jirani mmojawapo katika milango ile miwili, kidogo mlango wa grill ulifunguliwa kakaaa-kakaaaa kisha kukawa kimya, nami nikawa kimya nikiwaza huenda mtu anaenda maliwatoni hivyo nikaendelea na mambo yangu ya kutazama runinga.
Nilikaa kama nusu saa lakini sikusikia mlango ule wa grill ukifungwa, na kwa namna yoyote ile mlango ule usingeweza kufungwa bila kutoa sauti, hapo nikapata shaka. Nilitoka sebuleni nikaenda chumbani ili nipate kuchungulia nje kuna nini kinaendelea, nilipofungua pazia la dirisha kwanza nikatazama pikipiki yangu, nikaona kuna usalama, nikaangaza huku na kule lakini sikumwona mtu, nje kulikuwa kimya sana.
Nilitulia kusikiliza labda kuna mtu bafuni, napo sikusikia kitu, kila pembe ilikuwa kimya sana. Hapo nikapata wasiwasi. Niliufungua mlango nikaenda nje kutazama maana ule mlango wa grill kuwa wazi kwa muda wote huo haikuwa salama kabisa ukizingatia tulinusurika kupigwa tukio mara ya mwisho, huko nje nikatazama upande wa magharibi, hamna mtu, nikatazama upande wa mashariki nao hamna mtu, kabla ya kurudi ndani nikaenda kule bafuni, bafu zote zilikuwa zimezimwa taa hivyo nikahitimisha hamna mtu humo, basi nikarejea mlangoni na kuurejeshea ule mlango wa grill pasipo kuufunga na ufunguo ili kama kuna mtu huko nje basi ataingia na kuufunga mwenyewe, mimi nikareja sebuleni nikaendelea kutazama televisheni.
Nilitazama mpaka nilipohisi naelemewa na usingizi ndipo nikaenda zangu chumbani, huko nikajilaza na kuskilizia lakini muda wote huo sikusikia mlango wa grill ukifunguliwa, kulikuwa ni kimya tu kama hapo awali, nikajiuliza nini kinaendelea au ni mimi ndo' mwenye matatizo? Mpaka napitiwa na usingizi sikupata kusikia kitu, asubuhi palipokucha wakati naenda kuoga niende kazini, pale bombani, nilikutana na jirani yangu wa mlango mwingine ndani ya ile nyumba kubwa, mwanamke huyo alikuwa anafua nguo zake hapo nje, wanawake hawa huwa wana utaratibu wa kuamka mapema kufua kwaajili ya kuwahi kamba, baada ya kunisalimu aliniuliza,
"Shemeji, ni wewe ndo' uliacha mlango wa grill ukiwa wazi jana usiku?"
Nikamweleza namna mambo yalivyotokea kuwa mimi sikuuacha wazi bali niliurejeshea tu baada ya kusikia mtu alitoka, ajabu akaniambia kuwa mumewe asubuhi ya mapema sana alipotoka aliukuta mlango ukiwa wazi kabisa, umeachama kama mdomo! Nikastaajabu kusikia hayo, nilijiuliza ni muda gani mlango ulifunguliwa lakini sikupata majibu, nikaenda zangu kuoga nikilenga kuwa siku n'takayokutana na BIGI nimuulize kuhusu jambo hilo, sikuwa najua ni lini ila nilitumai ndani ya wiki hiyo basi nitambahatisha.
Ikapita siku mbili, sikumwona BIGI wala mkewe, siku ya tatu yake nikiwa sebuleni majira yangu ya usiku mtulivu, siku hiyo sikuwa natazama televisheni bali namalizia kazi fulani kwenye laptop, nikasikia mtu akiufungua mlango na kisha akaufungua mlango wa grill kakakaaa-kaaakaa, nikakaa tenge, mara hiyo sikutaka kupuuzia nilinyanyuka upesi nikaenda chumbani kutazama, ile kufungua tu pazia nikamwona mtu akiishia kwa kulifunga geti dogo, sikumjua mtu huyo ni nani kwani nilichoambulia kukiona ni mkono tu tena kwa muda mchache mno, basi nikabaki hapo nikiendelea kutazama pengine nitaona kitu.
Ngoja lakini wapi! Nilitumia kama nusu saa hapo lakini sikuona kitu nami nilikuwa nina hamu sana ya kumwona mtu huyo kwani niliamini yeye ndiye yule aliyeacha geti wazi siku ile, nilitamani kujua anafanya nini muda huo na kwanini anaacha geti wazi?
Nilikaa hapo dirishani kwa muda mrefu pasipo kuona kitu nikakata shauri kwenda nje, nilipoufungua mlango wangu kudaka korido nilisikia sauti ya watu wakizungumza, nikasita nikiskiliza. Sauti hiyo ilikuwa inatokea kwenye chumba cha BIGI na nilipoisikiliza kwa kitambo kidogo tu nilibaini sauti hiyo haikuwa ngeni masikioni mwangu, nilishawahi kuisikia mahali, ila ni wapi?
Kidogo kuwaza nikaikumbuka, sauti hii ilikuwa ni ileile niliyoisikia siku ile kwenye mlango huuhuu nikajua ni ya televisheni, ina maana imejirudia au ni masikio yangu? Nilistaajabu, lakini kadiri nilivyoisikia sauti hiyo tena na tena, tena kwa umakini, nikaamini kabisa haikuwa sauti ya televisheni, sauti hiyo ilikuwa ya watu wanaozoza na kunong'ona kitu ambacho sikuwasikia vema nikaelewa.
Nikiwa naendelea kuskiza hapo, mara nikasikia kishindo cha hatua za mtu kibarazani alafu mlango wa grill ukafunguliwa kakaaa kaakaaa! Nikashtuka kweli kweli, ni kama vile moyo wangu uliruka pigo moja kwa fujo!
Upesi nilirejea karibu na mlango wangu nikayatupa macho kule langoni, punde nikamshuhudia BIGI akiingia ndani huku amebebelea kiroba kitupu mkononi, huku juu amevalia 'vest' yake ileile aliyokuja nayo wakati mke wake anaumwa, aliponiona alisimama akan'tazama, nahisi na yeye alishtushwa na uwepo wangu pale, alinitazama pasipo kusema kitu chochote ila mimi nikamsalimu, hakujibu, alisimama tu akiendelea kun'tazama, sijui alikuwa anawaza kitu gani, mapigo yangu ya moyo yalikuwa yanapiga kwa kasi sana, niliona ni busara kuingia ndani kwangu upesi nikaufunga mlango kwa funguo kisha nikasimama hapo kusikiliza, kimya, nlidhani nitasikia vishindo vya miguu vikijongea lakini sikusikia chochote zaidi ya sauti ya mlango ukifungwa kisha kukawa kimya tena.
Nilizima kila kitu changu nikaenda chumbani moja kwa moja mpaka dirishani. Nilitazama pale kibarazani nikaona mlango wa grill ukiwa wazi. Nilitamani kwenda kuufunga lakini nikawaza vipi kama bwana yule akawa bado hajamaliza shughuli zake? Nikaona ni stara nikitulia lakini niendelee kungoja kama atatoka tena.
Nilingoja hapo kitandani kwangu mpaka usingizi ukanibeba, sikusikia kitu abadani. Kesho yake niliporejea tu kazini nikaelezwa kulitokea mjadala mkubwa hapo nyumbani juu ya swala la mlango wa grill kuachwa wazi kwa mara nyingine tena usiku ulopita, siku hiyo majira ya saa tatu hivi usiku kama sijakosea, nilikutana na jirani yangu yule wa dukani tukaongea mambo kadhaa kuhusu hapo nyumbani, moja kuhusu swala la ujenzi wa uzio na namna ambavyo mwenye nyumba haeleweki, na pili kuhusu swala la mlango wa grill kuachwa wazi nyakati za usiku. Bwana huyo alikuwa ndo' mtu wa kwanza kutoka asubuhi hivyo yeye ndiye aliyekuwa anaukuta mlango huo ukiwa wazi.
Kwa upande wangu nilimweleza yale niliyoyajua ya kuwa bwana BIGI ndiye anayeacha mlango huo wazi na basi kwa pamoja tukaazimia kumwambia endapo yeyote akipata nafasi hiyo. Siku zikapita, sijui kama yeye alifanikiwa kuonana na jamaa lakini mimi sikufanikiwa na uzuri mlango haukuachwa wazi tena.
Nakumbuka siku ambayo mafundi walikuja kwaajili ya ujenzi ndo siku ambayo nilipata kumwona bwana BIGI. Siku hiyo ilikuwa ni usiku kama wa saa nane hivi kama niko sawa, nilikuwa sebuleni kama kawaida yangu kabla ya kwenda kulala, televisheni inaongea lakini akili yangu yote ipo kwenye simu naperuzi mitandaoni, naingia instagram, whatsapp na JamiiForums.
Nilisikia mlango unafunguliwa na kisha mlango wa grill, nikanyanyuka kwenda kutazama dirishani. Hapo nilimwona BIGI akiwa amebebelea kiroba begani mwake anatoka kwenda geti dogo.
Kwasababu za ujenzi, geti hilo lilikuwa wazi tena limeegeshwa pembeni kabisa hivyo unaweza kuona mpaka nje. Nikamwona mtu huyo akitokomea huko mpaka kiza kikammeza!
Niliendelea kukaa hapo kwa muda kidogo lakini sikumwona akirudi, nikajua ni kama kawaida sitamshuhudia mpaka nitakapolala, lakini siku hiyo hali ilikuwa tofauti, baada ya kurudi kule sebuleni na kukaa kwa dakika kadhaa nilisikia kishindo cha mtu akikatiza koridoni alafu sauti ya mlango ikaita, nikawaza moja kwa moja atakuwa BIGI ndo amerejea lakini kwanini haufungi mlango wa grill? Nikaazimia ningoje kidogo hapo na nikiona kimya basi nitatoka nikaufunge mlango huo mwenyewe.
Kweli nilikaa hapo kwa kama nusu saa hivi, kimya, nilienda chumbani kutazama dirishani, hali ilikuwa shwari, nikauendea mlango wangu kuufungua lakini nilipotekenya tu funguo nikasikia mlango mwingine unafunguliwa, nikatulia kuskiza.
Vishindo vilipita koridoni nikahisi na kuamini kabisa alikuwa ni BIGI, vishindo hivyo vilipofifia nikaufungua mlango na kuchungulia nje, kweli alikuwa BIGI, nilimwona anatoka nje ya uzio akiwa na kiroba chake begani. Sikujua alikuwa anabebelea kitu gani humo lakini kilichonitatiza zaidi ni kwanini alikuwa anafanya zoezi hilo usiku wa manane?
Nilitoka nikatembea kwa upesi lakini pia kwa uangalifu mpaka kwenye geti dogo. Hapo nilirusha macho yangu kule kutazama, kwa mbali kwa msaada wa mataa mengine ya kule nje, nikamwona BIGI akiwa anayoyomea kuelekea kule korongoni, kule ambapo ndiyo wezi wanapokimbilia. Mwendo wake ulikuwa wa haraka sana na kwasababu ya uweusi wake basi kiroba ndo kilikuwa kinaonekana kikikata upepo, kile kinapepea, kilee kinapepea!
Niliijikuta nina hamu ya kwenda zaidi kutazama.
***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida