Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Hizi sarafu hata niione njiani siiokoti
mwaka 2017 nilikuwa soko la moshi mjini MBUYUNI nikamwona mmama ameangusha chini sarafu kwa makusudi, pembeni kulikuwa na muhuni akaiokota ile sarafu alaf akamfuata yule mama akamwambia mama ela yako hii umeitupa pale chini, yule mama aliikataa katakata, yule muhuni akamshikisha mkononi kinguvu aah yule mama wa kichaga aliwaka kinoma akawa anakwepesha mkono adi akashikishwa akaitupa chini,

lile tukio mimi nilikuwa nalishuhudia kwa macho yangu. sijui aliimbilizia nin kwenye ile sarafu, na sijui yule mwamba aliyeishika alidhurika ama lah
 
Nilikua namwambia kuhusu hii ya Big ila kuna ile nyingine ya Tukibaki hai tutasimulia ni nzuri sana kaipitie uisome japo Steve hakuimalizia..

Sasa badae alivotulia nikamuuliza pale jikoni ulikua unavutana na Nani??? Akasema Alivomaliza kupika hio kabegi kuitua toka jikoni kuiweka chini tu ile sasa anataka kuibeba ile ananyanyua tu alishangaa anaona mara kuku mara hapohapo anakua ng'ombe mara anageuka kuwa bibi kizee Huku yanamvuta kwanguvu!!
Ile khali sana!
 
Hizi sarafu hata niione njiani siiokoti
Juzi nimetoka dukani na mtoto wangu akaokota 200 njiani. Nilipokumbuka huu uzi niliogopa nikamwambia aiache hukohuko nje tusiingie nayo ndani. Hapa nimetoka kuiangalia ipo pale pale tulipoiacha.
Kuna roho tuu iliniambia hiyo hela usiingie nayo ndani wala usichanganye na hela nyingine
 
Yule Jirani yangu wa Goba, hakuwa mtu wa kawaida - MWISHO.



Siku mbili baada ya kumwona Bembela akiwa na shangazi yake usiku ule wamebebela mfuko nisijue wapi walipotokea na nini walibebelea, nilipigiwa simu na Mwenye nyumba majira ya mchana nikiwa kazini.

Bwana huyo baada ya kunisalimu na kuniuliza mambo ya nyumbani, aliniuliza kama kuna watu wamefika pale nyumbani kumuulizia bwana BIGI, nikamwambia sifahamu, binafsi sikuona mtu labda wapangaji wengine, baada ya hapo nikamuuliza hali za wale wagonjwa, akanieleza hali zao ni bora ya jana yake, siku hiyo alipitia asubuhi hospitali kabla ya kwenda kwenye shughuli zake akakutana na hali mbaya sana ya bwana BIGI.

Alinambia, "yule bwana sijui sasa kama kuna kupona. Amepooza mwili wake mzima, ni wa kugeuza na kumfuta tu, sasa wanataka kumpatia rufaa!"

Aliniambia hofu yake endapo bwana huyo akifa maana hamjui mtu wake hata mmoja na wala hana mawasiliano nao, achilia mbali hata mkataba naye hana, sijui ataeleza kitu gani akaeleweka mbele ya vyombo vya usalama, lakini pia hata mkewe ambaye alikuwa anategemea atapoa ili amhudumie mumewe na kutoa taarifa kwa watu wao wa karibu naye hali yake haikuwa inaeleweka, tangu amefikishwa hapo hospitali hajapata kuonekana akifungua macho wala kutoa ishara yoyote ya mawasiliano, amepimwa kila kitu, hamna kinachosoma na hitilafu ila fahamu hazimo, ajabu gani?

Aliniaga akiniambia alimwacha yule bwana, mpangaji aloongozana naye siku ile kwenda naye hospitali, baadae atampigia kumuuliza maendeleo, baada ya hapo akakata simu nikaendelea na shughuli zangu.

Kesho yake majira ya jioni nikiwa natoka kazini, nikakutana na huyo mpangaji mwenzangu kwenye geti dogo akiwa anarejea nyumbani, bwana huyo alikuwa ametoka kwenye mihangaiko yake ya hapa na pale, tulisalimiana kisha akanieleza ya kule hospitali.

Bwana yule akaniambia mambo ambayo Mwenye Nyumba hakupata kusema au pengine hakuwa anayajua.

Alisema: "Baada ya leo asubuhi kutoka kule, mimi sitokaa nirudi tena kule hospitali hata mwenye nyumba akiniomba na kunilamba miguu."

Nikastaajabu kweli na maamuzi hayo ambayo niliyaona ya ghafla, kabla sijamuuliza kulikoni, akaniambia mwanamke yule alokuwapo hospitali hakuwa mgonjwa, mwanamke yule ni mzima kila ifikapo usiku, maneno hayo yakanifanya nimuulize: "ushawahi kuwa kule hospitali majira ya usiku?"

Akanijibu "lah!" na kusema kamwe hajawahi lakini alionana, asubuhi ya siku hiyo, na nesi alokuwa anaingia zamu usiku, nesi huyo alimwita kando akamuuliza mwanaume yule yaani BIGI ni ndugu yake? Akamwambia ndio na yule mwanamke ni shemeji yake, basi akamwambia mwanamke yule huenda ndo' amemuadhiri ndugu yake mpaka kufikia vile.

Bwana yule alisema: "nilimuuliza nesi kwanini anawaza hivyo akaniambia yeye ana uzoefu na hayo mambo ya hospitali, anajua mambo ya kutibiwa hospitali na mambo ya kutafuta njia zingine mbadala, na hili la kwetu ni la njia mbadala, tena tufanye upesi kabla hatujampoteza ndugu yetu."

Bwana yule akaniambia nesi huyo alishawahi kumshuhudia mwanamke yule,kama kivuli, akiwa anatembea wodi ya watoto na wazazi nyakati za usiku, na anaamini ni kweli alichoona sio mauzauza ama kiini macho, lakini alipoenda kutazama kitanda chake bado akamkuta mwanamke huyo hapo, mwili wake umetulia kitandani, na jambo hilo si mara moja bali mara mbili.

Ajabu kule kote mwanamke huyo alikokatiza, kesho yake paliongokea msiba ya watoto kwenye vitanda viwiliviwili, kwa siku mbili wakapoteza watoto wachanga wanne!

"Ndugu yangu," bwana yule aliita kisha akasema, "kuanzia leo mimi sitahusika kwa namna yoyote na wale mabwana, hata iweje, yote nimewaachia wale ndugu zao walokuja hapa kuhani msiba."

Nikahamaki,

"Ndugu hao uliwaona?"

Akanambia hapana ila kama walikuja wakati wa msiba basi waje pia na kuwatazama huko hospitali, nikabaini bwana huyo amepandwa na jazba, niliagana naye akaondoka zake, kesho yake asubuhi ya mapema nikiwa najiandaa kwenda kazini mwenye nyumba akanipigia simu, akaniambia amepitia hospitali asubuhi ya siku hiyo akapata taarifa bwana BIGI amefariki dunia!

Alisema: "Kifo chake kimetokea usiku wa kuamkia leo kwahiyo hapa tunapoongea, mwili wake umehifadhiwa."

Kuhusu mkewe, alinambia bado hali yake iko vilevile, hamna afueni wala ahueni, namna alivyoletwa ndo' namna alivyo, lakini kabla hatujamaliza maongezi akaniomba ningoje mara moja atanirejea, akakata simu.

Yakapita masaa kama mawili, hakunipigia, nishafika kazini na ninaendelea na mambo yangu lakini kule nyumbani kabla sijaondoka nilishaacha taarifa ya msiba, baada ya masaa hayo nlosema, mwenye nyumba alinipigia akaniambia muda ule alokata simu, kuna watu walikuja hapo hospitali wakisema wao ni ndugu zake na BIGI, akaniuliza kuna mtu niliyempa taarifa kuwa BIGI yuko hospitalini hapo? Nikamjibu hapana, akasema;

"Basi itakuwa Muddy, nampigia hapokei simu yangu, sijui yuko wapi?"

Muddy ni yule jamaa jirani aloongozana na mwenye nyumba kwenda naye kule hospitali, mwenye nyumba aliponieleza anampigia bwana huyo hampati nikakumbuka moja kwa moja maneno alosema yule bwana jana yake usiku nilipokutana naye, pengine alihisi mwenye nyumba anamtafuta ili aende hospitali, kitu ambacho yeye hakukitaka tena abadani.

Lakini kama ndiye Muddy alisema kuhusu BIGI kuwa kule hospitali, je alikutana na hao majaa lini? Mimi sikuamini kabisa hilo jambo. Na kama kweli hao majamaa wamemjuaje mwenye nyumba ukizingatia mwenye nyumba hata kwenye msiba hakuwapo?

Sikukaa nikayajua.

Baadae jioni niliporejea nyumbani, nilimkuta baba mwenye nyumba akiwa pamoja na Mjumbe, vijana wawili wa ulinzi shirikishi na mabwana wawili ambao sikuwatambua. Tulisalimiana kisha mwenye nyumba akanieleza kinachoendelea hapo ya kwamba mabwana wale wawili ni ndugu zake na BIGI na wamekuja hapo kubeba vitu vyao.

Alinieleza mabwana wale ndo' waliofika kule hospitali kujumuika naye, kama haitoshi, walisimamia kila kitu kuhusu gharama za matibabu na kitanda alicholalia BIGI muda wote ule wa kuuguzwa.

Lakini mimi nikabaki na maswali, sawa mabwana hao wameibuka na kubeba majukumu, lakini tuna uhakika gani kama wao ni ndugu halisi wa BIGI? Nilijiulizia moyoni...

Vitu vyote vya BIGI vilitolewa nje, kweli hakukuwa na cha maana, yaani ungeweza kubeba vitu hivyo kichwani ukaondoka navyo kwa miguu, kulikuwa ni mifuko mifuko, viroba, nguo na mavitu mengine kadhaa ambayo kwakweli sikuona kama yana tija, ajabu ni kwamba mabwana wale hawakubakiza hata kitu, kila kilichochao walibeba, hata yale ambayo unaweza dhania ni taka, yote hayo walikuwa wanakusanyia katika kiroba chao kikubwa walichokuja nacho.

Wakiwa wanafanya hivyo mimi nikaona moja ya 'toy' la mwanangu, nikawaambia hiki ni changu hamna kwenda nacho, hapo ukaibuka mzozo, mabwana wale hawakuwa tayari kuacha kitu, nami kuona vile nikapata mashaka juu ya kwanini wanang'ang'ania vile vitu kiasi hiko, mpango wao ni nini?

Nikapambana mpaka nilipohakikisha 'toy' ile haiendi kokote, swala hilo likawafanya majirani wengine nao wasogee kuziangatia vitu vile vinavyobebwa, hamaki majirani watatu wakapata nguo zao humo, tena wawili kati yao walipata nguo zao za ndani!

Hamna aliyejua ni namna gani nguo hizo zilifika humo, lakini kila mtu alikiri zilipotea kambani baada ya kuanikwa juani. Baada ya kila kitu kuwa sawa, mabwana wale walifunga kiroba chao kisha mmoja wao akasema, tena kwa sauti kuu:

"Kama kuna mtu yeyote mwenye kitu cha (akataja jina halisi la bwana BIGI) basi naomba akirejeshe hapa ... Kama vile mlivyodai vyenu, basi na vya kwake vyote virejeshwe, kama sivyo basi mwenye nacho atakuja kupata matatizo hapo baadae na sisi hatutabeba lawama."

Kimya,

Hakuna kilichorejeshwa, Bwana huyo akarudia tena maneno yake, kama kuna yeyote alowahi kubeba mali yoyote ya bwana BIGI basi airejeshe, la sivyo atakuja kujilaumu.

Kimya.

Mabwana wale walipoona kila kitu ni sawa, wakampatia mwenye nyumba mkono wa kheri na kisha Mjumbe, alafu wakasema msiba wa bwana BIGI utakuwapo maeneo ya Chanika eneo ambalo sikumbuki linaitwaje, baada ya hapo wakaenda zao na kile kiroba chao kikubwa, huo ukawa ndo' mwisho wa BIGI na mambo yake pale Goba. Baada ya hapo sikuwahi kumsikia wala kumwona tena bwana huyo. Sikumbuki kama kuna jirani yoyote aloenda kuhani msiba huo huko Chanika, laiti ingelikuwa hivyo basi ningelipata taarifa fulani.

Ikapita siku moja, siku ya pili, bila ya bwana BIGI, kila kitu kikiwa shwari, wiki moja na wiki ya pili, kila kitu kimetulia, hamna maisha ya usiku wala vimbwanga vyake, baada ya mwezi kukoma Bembela alihama pale nyumbani nisijue wapi alipoelekea, lakini sehemu yake ya biashara ilibakia kuwa ni ileile, nyuma ya kituo cha Goba Kontena.

Hapo mara kadhaa nilikuwa namkuta akiwa anahudumia watu, hata ameajiri wadada wawili wa kumsaidia maana wateja walikuwa wengi sana. Siku moja, nadhani ni baada ya kama mwezi kupita tangu amehama pale nyumbani, nilipita pale katika eneo lake la biashara kumsalimu, siku hiyo nilikuwa mwenyewe nyumbani maana mke wangu alikuwa ameenda huko Ugweno, Kilimanjaro, kwao kusalimu pamoja na mtoto, hivyo nilivyokuwa nikirejea nyumbani nilikuwa napitia hapo kupata chakula cha usiku kabla ya kwenda kulaza mazima ninaposhuka kule Mashuka.

Nilifanya hivyo mara kadhaa, kama majuma matatu hivi, nikikutana na Bembela kila siku na kila mara tukiongea naye mambo ya hapa na pale. Nilishawahi kumuuliza shangazi yuko wapi, akaniambia ameshakwenda zake Tanga lakini anashukuru kwani maisha si haba, kila kitu kinaenda sawa, sasa alikuwa anatazamia kumalizia nyumba yake aliyokuwa anajenga maeneo ya Kimara, Temboni.

Bembela, kwakweli, hakuwa yule Bembela wa zamani, kitendo cha kuajiri wasichana wawili na yeye akiwa wa tatu katika shughuli ile ya mama n'tilie ilionyesha namna gani alivyokua amepiga hatua kubwa kiuchumi.

Ilikuja kufikia pahali hata mimi nilokuwa naenda pale kupata chakula, zamani nikihudumiwa kama mfalme, sasa nikawa napanga foleni tena mpaka niwe nasisitiza mara mbili au tatu ndo' sahani ipate kuja mezani!

Nikatambua kweli maisha yanabadilika, na mengine, kama bahati, yanabadilika mbele ya macho yetu ya nyama, yaani tunapata kuyashuhudia yakiwa yanatokea tangu mwanzo wake mpaka mwisho wake.

Lakini mpaka leo, mimi binafsi, sijawahi kujua ni nini haswa kilichokuja kutokea katikati ya majuma na miezi kadhaa baina ya Bembela na yule shoga yake ... lakini mwanamke yule, yaani shoga yake na Bembela, ambaye tulikuwa tunaendelea kuishi naye pale nyumbani, ndiye baadae alikuja kugeuka kuwa mdomo wa kusema kuwa Bembela anamtumia yule mtoto na mke wa BIGI kwenye mafanikio ya biashara yake.

Sasa amepata mali na pesa, hakuna anayemjali na kumkumbuka, hata yeye alokuwa naye karibu katika yale yote alopitia ....


***
Asante mkuu kwa stori nzuri. Ila huko ulikoenda kuoa daah.
anyway mungu akupiganie.
 
Vipi kuhusu Tarimo alipona? Na kuhusu jambo alilokua akihitaji muonane mpaka anapata ajali alikuambia?
Ila kweli hapa stevemollel ili bidi atuambie...maana alisema Tarimo anaendelea vzuri kiasi cha kutaka kuruhusiwa kurudi nyumbani...nilikuwa na shauku sana ya kujua Tarimo alitaka kusema nn kuhusu Big mtu mbadi? Anyway labda SteveMollel labda aliona haina tena haja baada ya kuona Big ashahama ulimwengu kabisa na sio nyumba tu [emoji1] [emoji38] [emoji1787].
 
Yule Jirani yangu wa Goba, hakuwa mtu wa kawaida - MWISHO.



Siku mbili baada ya kumwona Bembela akiwa na shangazi yake usiku ule wamebebela mfuko nisijue wapi walipotokea na nini walibebelea, nilipigiwa simu na Mwenye nyumba majira ya mchana nikiwa kazini.

Bwana huyo baada ya kunisalimu na kuniuliza mambo ya nyumbani, aliniuliza kama kuna watu wamefika pale nyumbani kumuulizia bwana BIGI, nikamwambia sifahamu, binafsi sikuona mtu labda wapangaji wengine, baada ya hapo nikamuuliza hali za wale wagonjwa, akanieleza hali zao ni bora ya jana yake, siku hiyo alipitia asubuhi hospitali kabla ya kwenda kwenye shughuli zake akakutana na hali mbaya sana ya bwana BIGI.

Alinambia, "yule bwana sijui sasa kama kuna kupona. Amepooza mwili wake mzima, ni wa kugeuza na kumfuta tu, sasa wanataka kumpatia rufaa!"

Aliniambia hofu yake endapo bwana huyo akifa maana hamjui mtu wake hata mmoja na wala hana mawasiliano nao, achilia mbali hata mkataba naye hana, sijui ataeleza kitu gani akaeleweka mbele ya vyombo vya usalama, lakini pia hata mkewe ambaye alikuwa anategemea atapoa ili amhudumie mumewe na kutoa taarifa kwa watu wao wa karibu naye hali yake haikuwa inaeleweka, tangu amefikishwa hapo hospitali hajapata kuonekana akifungua macho wala kutoa ishara yoyote ya mawasiliano, amepimwa kila kitu, hamna kinachosoma na hitilafu ila fahamu hazimo, ajabu gani?

Aliniaga akiniambia alimwacha yule bwana, mpangaji aloongozana naye siku ile kwenda naye hospitali, baadae atampigia kumuuliza maendeleo, baada ya hapo akakata simu nikaendelea na shughuli zangu.

Kesho yake majira ya jioni nikiwa natoka kazini, nikakutana na huyo mpangaji mwenzangu kwenye geti dogo akiwa anarejea nyumbani, bwana huyo alikuwa ametoka kwenye mihangaiko yake ya hapa na pale, tulisalimiana kisha akanieleza ya kule hospitali.

Bwana yule akaniambia mambo ambayo Mwenye Nyumba hakupata kusema au pengine hakuwa anayajua.

Alisema: "Baada ya leo asubuhi kutoka kule, mimi sitokaa nirudi tena kule hospitali hata mwenye nyumba akiniomba na kunilamba miguu."

Nikastaajabu kweli na maamuzi hayo ambayo niliyaona ya ghafla, kabla sijamuuliza kulikoni, akaniambia mwanamke yule alokuwapo hospitali hakuwa mgonjwa, mwanamke yule ni mzima kila ifikapo usiku, maneno hayo yakanifanya nimuulize: "ushawahi kuwa kule hospitali majira ya usiku?"

Akanijibu "lah!" na kusema kamwe hajawahi lakini alionana, asubuhi ya siku hiyo, na nesi alokuwa anaingia zamu usiku, nesi huyo alimwita kando akamuuliza mwanaume yule yaani BIGI ni ndugu yake? Akamwambia ndio na yule mwanamke ni shemeji yake, basi akamwambia mwanamke yule huenda ndo' amemuadhiri ndugu yake mpaka kufikia vile.

Bwana yule alisema: "nilimuuliza nesi kwanini anawaza hivyo akaniambia yeye ana uzoefu na hayo mambo ya hospitali, anajua mambo ya kutibiwa hospitali na mambo ya kutafuta njia zingine mbadala, na hili la kwetu ni la njia mbadala, tena tufanye upesi kabla hatujampoteza ndugu yetu."

Bwana yule akaniambia nesi huyo alishawahi kumshuhudia mwanamke yule,kama kivuli, akiwa anatembea wodi ya watoto na wazazi nyakati za usiku, na anaamini ni kweli alichoona sio mauzauza ama kiini macho, lakini alipoenda kutazama kitanda chake bado akamkuta mwanamke huyo hapo, mwili wake umetulia kitandani, na jambo hilo si mara moja bali mara mbili.

Ajabu kule kote mwanamke huyo alikokatiza, kesho yake paliongokea msiba ya watoto kwenye vitanda viwiliviwili, kwa siku mbili wakapoteza watoto wachanga wanne!

"Ndugu yangu," bwana yule aliita kisha akasema, "kuanzia leo mimi sitahusika kwa namna yoyote na wale mabwana, hata iweje, yote nimewaachia wale ndugu zao walokuja hapa kuhani msiba."

Nikahamaki,

"Ndugu hao uliwaona?"

Akanambia hapana ila kama walikuja wakati wa msiba basi waje pia na kuwatazama huko hospitali, nikabaini bwana huyo amepandwa na jazba, niliagana naye akaondoka zake, kesho yake asubuhi ya mapema nikiwa najiandaa kwenda kazini mwenye nyumba akanipigia simu, akaniambia amepitia hospitali asubuhi ya siku hiyo akapata taarifa bwana BIGI amefariki dunia!

Alisema: "Kifo chake kimetokea usiku wa kuamkia leo kwahiyo hapa tunapoongea, mwili wake umehifadhiwa."

Kuhusu mkewe, alinambia bado hali yake iko vilevile, hamna afueni wala ahueni, namna alivyoletwa ndo' namna alivyo, lakini kabla hatujamaliza maongezi akaniomba ningoje mara moja atanirejea, akakata simu.

Yakapita masaa kama mawili, hakunipigia, nishafika kazini na ninaendelea na mambo yangu lakini kule nyumbani kabla sijaondoka nilishaacha taarifa ya msiba, baada ya masaa hayo nlosema, mwenye nyumba alinipigia akaniambia muda ule alokata simu, kuna watu walikuja hapo hospitali wakisema wao ni ndugu zake na BIGI, akaniuliza kuna mtu niliyempa taarifa kuwa BIGI yuko hospitalini hapo? Nikamjibu hapana, akasema;

"Basi itakuwa Muddy, nampigia hapokei simu yangu, sijui yuko wapi?"

Muddy ni yule jamaa jirani aloongozana na mwenye nyumba kwenda naye kule hospitali, mwenye nyumba aliponieleza anampigia bwana huyo hampati nikakumbuka moja kwa moja maneno alosema yule bwana jana yake usiku nilipokutana naye, pengine alihisi mwenye nyumba anamtafuta ili aende hospitali, kitu ambacho yeye hakukitaka tena abadani.

Lakini kama ndiye Muddy alisema kuhusu BIGI kuwa kule hospitali, je alikutana na hao majaa lini? Mimi sikuamini kabisa hilo jambo. Na kama kweli hao majamaa wamemjuaje mwenye nyumba ukizingatia mwenye nyumba hata kwenye msiba hakuwapo?

Sikukaa nikayajua.

Baadae jioni niliporejea nyumbani, nilimkuta baba mwenye nyumba akiwa pamoja na Mjumbe, vijana wawili wa ulinzi shirikishi na mabwana wawili ambao sikuwatambua. Tulisalimiana kisha mwenye nyumba akanieleza kinachoendelea hapo ya kwamba mabwana wale wawili ni ndugu zake na BIGI na wamekuja hapo kubeba vitu vyao.

Alinieleza mabwana wale ndo' waliofika kule hospitali kujumuika naye, kama haitoshi, walisimamia kila kitu kuhusu gharama za matibabu na kitanda alicholalia BIGI muda wote ule wa kuuguzwa.

Lakini mimi nikabaki na maswali, sawa mabwana hao wameibuka na kubeba majukumu, lakini tuna uhakika gani kama wao ni ndugu halisi wa BIGI? Nilijiulizia moyoni...

Vitu vyote vya BIGI vilitolewa nje, kweli hakukuwa na cha maana, yaani ungeweza kubeba vitu hivyo kichwani ukaondoka navyo kwa miguu, kulikuwa ni mifuko mifuko, viroba, nguo na mavitu mengine kadhaa ambayo kwakweli sikuona kama yana tija, ajabu ni kwamba mabwana wale hawakubakiza hata kitu, kila kilichochao walibeba, hata yale ambayo unaweza dhania ni taka, yote hayo walikuwa wanakusanyia katika kiroba chao kikubwa walichokuja nacho.

Wakiwa wanafanya hivyo mimi nikaona moja ya 'toy' la mwanangu, nikawaambia hiki ni changu hamna kwenda nacho, hapo ukaibuka mzozo, mabwana wale hawakuwa tayari kuacha kitu, nami kuona vile nikapata mashaka juu ya kwanini wanang'ang'ania vile vitu kiasi hiko, mpango wao ni nini?

Nikapambana mpaka nilipohakikisha 'toy' ile haiendi kokote, swala hilo likawafanya majirani wengine nao wasogee kuziangatia vitu vile vinavyobebwa, hamaki majirani watatu wakapata nguo zao humo, tena wawili kati yao walipata nguo zao za ndani!

Hamna aliyejua ni namna gani nguo hizo zilifika humo, lakini kila mtu alikiri zilipotea kambani baada ya kuanikwa juani. Baada ya kila kitu kuwa sawa, mabwana wale walifunga kiroba chao kisha mmoja wao akasema, tena kwa sauti kuu:

"Kama kuna mtu yeyote mwenye kitu cha (akataja jina halisi la bwana BIGI) basi naomba akirejeshe hapa ... Kama vile mlivyodai vyenu, basi na vya kwake vyote virejeshwe, kama sivyo basi mwenye nacho atakuja kupata matatizo hapo baadae na sisi hatutabeba lawama."

Kimya,

Hakuna kilichorejeshwa, Bwana huyo akarudia tena maneno yake, kama kuna yeyote alowahi kubeba mali yoyote ya bwana BIGI basi airejeshe, la sivyo atakuja kujilaumu.

Kimya.

Mabwana wale walipoona kila kitu ni sawa, wakampatia mwenye nyumba mkono wa kheri na kisha Mjumbe, alafu wakasema msiba wa bwana BIGI utakuwapo maeneo ya Chanika eneo ambalo sikumbuki linaitwaje, baada ya hapo wakaenda zao na kile kiroba chao kikubwa, huo ukawa ndo' mwisho wa BIGI na mambo yake pale Goba. Baada ya hapo sikuwahi kumsikia wala kumwona tena bwana huyo. Sikumbuki kama kuna jirani yoyote aloenda kuhani msiba huo huko Chanika, laiti ingelikuwa hivyo basi ningelipata taarifa fulani.

Ikapita siku moja, siku ya pili, bila ya bwana BIGI, kila kitu kikiwa shwari, wiki moja na wiki ya pili, kila kitu kimetulia, hamna maisha ya usiku wala vimbwanga vyake, baada ya mwezi kukoma Bembela alihama pale nyumbani nisijue wapi alipoelekea, lakini sehemu yake ya biashara ilibakia kuwa ni ileile, nyuma ya kituo cha Goba Kontena.

Hapo mara kadhaa nilikuwa namkuta akiwa anahudumia watu, hata ameajiri wadada wawili wa kumsaidia maana wateja walikuwa wengi sana. Siku moja, nadhani ni baada ya kama mwezi kupita tangu amehama pale nyumbani, nilipita pale katika eneo lake la biashara kumsalimu, siku hiyo nilikuwa mwenyewe nyumbani maana mke wangu alikuwa ameenda huko Ugweno, Kilimanjaro, kwao kusalimu pamoja na mtoto, hivyo nilivyokuwa nikirejea nyumbani nilikuwa napitia hapo kupata chakula cha usiku kabla ya kwenda kulaza mazima ninaposhuka kule Mashuka.

Nilifanya hivyo mara kadhaa, kama majuma matatu hivi, nikikutana na Bembela kila siku na kila mara tukiongea naye mambo ya hapa na pale. Nilishawahi kumuuliza shangazi yuko wapi, akaniambia ameshakwenda zake Tanga lakini anashukuru kwani maisha si haba, kila kitu kinaenda sawa, sasa alikuwa anatazamia kumalizia nyumba yake aliyokuwa anajenga maeneo ya Kimara, Temboni.

Bembela, kwakweli, hakuwa yule Bembela wa zamani, kitendo cha kuajiri wasichana wawili na yeye akiwa wa tatu katika shughuli ile ya mama n'tilie ilionyesha namna gani alivyokua amepiga hatua kubwa kiuchumi.

Ilikuja kufikia pahali hata mimi nilokuwa naenda pale kupata chakula, zamani nikihudumiwa kama mfalme, sasa nikawa napanga foleni tena mpaka niwe nasisitiza mara mbili au tatu ndo' sahani ipate kuja mezani!

Nikatambua kweli maisha yanabadilika, na mengine, kama bahati, yanabadilika mbele ya macho yetu ya nyama, yaani tunapata kuyashuhudia yakiwa yanatokea tangu mwanzo wake mpaka mwisho wake.

Lakini mpaka leo, mimi binafsi, sijawahi kujua ni nini haswa kilichokuja kutokea katikati ya majuma na miezi kadhaa baina ya Bembela na yule shoga yake ... lakini mwanamke yule, yaani shoga yake na Bembela, ambaye tulikuwa tunaendelea kuishi naye pale nyumbani, ndiye baadae alikuja kugeuka kuwa mdomo wa kusema kuwa Bembela anamtumia yule mtoto na mke wa BIGI kwenye mafanikio ya biashara yake.

Sasa amepata mali na pesa, hakuna anayemjali na kumkumbuka, hata yeye alokuwa naye karibu katika yale yote alopitia ....


***
Nmehama nyumba kadhaa yaan kila nikiamka nimechanjwa kila nikiamka nimechanjwa na ni maumivu makali sana nayapata wakati wa kuoga.Haijapita muda nmehama zangu hakuna mchanjo wala kuchanjana...kha mi uchawi sijui ushirikina sitak kbs.Yaan hata nikishajua kunamtu niko nae around ni mshirikina hatoniona karibu yake tena.Mchawi ni mtu mbaya sana.

Pole sana mr SteveMollel ndio maisha haya.Tusimuache Mungu na Tujitakase nafsi zetu.
 
Kuna members wawili wamenifuata inbox kunishirikisha visa vyao wakisema wao hawawezi kuyasimulia lakini wangependa visa hivyo kuruka na kusomwa hapa JamiiForums ili tupate kujifunza na kuburudika pia.

Nawaahidi wakivikamilisha, hata tu mmojawao, ntavirusha hapa mwanzo mpaka mwisho wake, na nitawatag kama wakiwa radhi.

Nimeamini kweli, ukidhani kwako panaungua, basi kwa mwenzako panateketea.
Haya tunashukuru! Hamia kule maana umeacha ngoma mbiiichi kabisa
Screenshot_20230221-224004.jpg
 
Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida - Night Shift.



NILIGONGA mlango kwa kama sekunde kumi hivi, kimya, hamna mtu aliyeongea ndani wala kuja kuufungua, nikagonga tena na tena na tena. Nilihakikisha nimetumia dakika kadhaa hapo lakini bado sikufanikiwa, hakuna aliyethubutu kufungua mlango ule, basi nikasema:

"Nataka tuongee,nina shida na wewe!"

Kwa muda huo nimeparwa na jazba. Damu inapita kwa kasi kweli mwilini,jasho linanichuruza. Yani naona kama nakawia kumwona bwana yule. Kichwani mwangu nawaza, sipati raha, kwanini nguo ya mwanangu aliichukua kuifanyia mambo yake? Anataka kumuua kama yule mtoto wa Bembela? Nikagonga nikiongea na mlango mwenyewe kama mwehu. Nilipoona nimefanya kila jitihada ya kugonga mlango na nimegonga mwamba, akili yangu ikanituma nitengue kitasa cha mlango ule.

Nikafanya hivyo ...

Kikweli sikutegemea kama mlango ule utafunguka, mimi nilichokuwa nimedhamiria ni kumshtua mtu alokuwemo ndani kama kweli yumo humo ili aitikie haja yangu ya kuja nje, ila hamaki mlango ukafunguka!

Uliachama mwanya mdogo nikapata kuona kwa kiasi chake yale yalokuwemo ndani japo si kwa ukamilifu kwasababu sebule ile ilikuwa na mwanga hafifu sana, madirisha yamefungwa,yani kama si mwanga mchache uloingia ndani sababu ya mimi kuufungua ule mlango, sidhani kama ningeshuhudia jambo lolote humo ...

Basi kwa macho yangu ya nyama, pale chini sakafuni, niliona miguu ya watu wawili ambao niliamini wamejilaza: miguu miwili ilikuwa ni ya mtu mzima na miwili ni ya mtoto! Miguu hiyo imetulia tuli wala haikutikisika pamoja na mimi kuufungua mlango kutazama.

Upesi nikaurejeshea mlango huo kama nilivyokuta, moyo wangu unanienda mbio, nikaondoka hapo kwa haraka kwenda kwa Mama Tarimo kwa madhumuni mawili: moja kumpa taarifa ya maendeleo ya mgonjwa ambaye tulimpeleka naye hospitali hapo awali na pili nimwone mwanangu ambaye nilimwacha hapo.

Dhumuni la kwanza likatimia lakini la pili halikutimia kiukamilifu kwani mtoto alikuwa amelala na mimi sikuona haya ya kumsumbua, nikaelekea kwenye makazi yangu ambapo nilifikia sebuleni kwenye kochi nikaketi hapo nikiyatafakari yale niliyoyaona kwenye ile sebule ya BIGI na pia yale mengine niliyoelezwa na Mama Tarimo.

Mama huyo, kama alivyofanya shoga yake Bembela, alinieleza yale yalosibu pale nyumbani nikiwa hospitali, akienda mbali kwa kusema Mjumbe alifika pale nyumbani kuhusu lile swala la taka korongoni, mjumbe huyo alikuwa ameshapewa taarifa na wale watu wa ulinzi shirikishi asubuhi ya mapema walipoenda kwake kukabidhi lindo hivyo alikuja kwa minajili ya kutujuza kuwa tumepigwa faini, kitu ambacho mimi kwakweli sikukubaliana nacho hata kidogo na sikuwa tayari kutoa hata sent'ano.

Nikiwa nayatafakari hayo, kwasababu ya uchovu wangu nilioulimbikiza toka usiku ule, nikajikuta nalala hapo fofofo bila kubadili chochote mwilini. Nilikuja kukurupuka baadae baada ya kusikia mtu akigonga mlango, kutazama simu ni majira ya saa nane ya mchana, niliufungua mlango nikamkuta shoga yake Bembela akiwa ameegamia ukuta mkononi ameshikilia simu.

Alinisalimu, "Habari za saa hizi, shemeji?"

Nikamwitikia salamu yake na kumkaribisha ndani, akasema hapana haina haja, amekuja hapo kwa dharura tu.

"Bembela anataka kuongea na wewe," alisema akinipatia simu yake alafu akaongezea, "atapiga muda si mrefu, nitakuja kuichukua simu yangu." Kisha akaenda zake, mimi nikaingia ndani na kweli si muda simu ile ikaita nikapokea. Kusikia tu sauti nikajua ninayeongea naye ni Bembela.

Alinisalimu tukajuliana hali kisha akanieleza kuwa kesho yake atakuwa njiani kuja Dar akitokea Tanga.

Aliniambia amepata habari zote zilizotokea nyumbani maana shoga yake ameshamweleza alivyompigia simu majira ya asubuhi, lakini pia akanieleza juu ya hofu yake kwangu kuhusu zile nguo za mwanangu kuonekana katika kile kiroba ambacho yeye aliamini kabisa kuwa ni cha bwana BIGI.

Alisema, "Baba fulani, nguo za mwananangu zilipotea hivyohivyo katika mazingira ya kutatanisha hata kabla ya kifo chake, na kufa kwake hakukuwa na mahusiano kabisa na ugomvi ulotokana na mwanaye huyo BIGI bali hiyo ndo' kanuni yake ya kuua, hammalizi mtu mpaka pale mjumbe anayemtumia atakapopata sababu ya kufanya hivyo, na atakapoipata sababu hiyo basi huitumia hiyohiyo kwenye maangamizi yake."

Hapo ndo nikakumbuka yale maneno ya Bembela kwenye mlango wa BIGI, namna mwanamke huyo alivyokuwa anapiga kelele siku ile akiwa amemshika mwanaye pale koridoni akisema familia ya BIGI itoke kuendelea kumpiga mtoto wake, na kweli ikawa hivyo mpaka kifo cha mtoto yule!

Lakini zaidi nikakumbuka ndoto alizokuwa anaota mke wangu na kukurupuka nyakati za usiku: Ndoto za mtu kugonga mlangoni, mtu ambaye ana sauti ileile kama ya kwake, hapo ndipo nikafahamu kuwa jambo lile ni kwasababu ya yeye kuugonga ule mlango wa BIGI akimwita mtoto yule au yeyote aliyemo ndani baada ya huyo mtoto chizi kusababisha kadhia ya kumpiga mtoto wa Bembela.

Kumbe kwasababu hiyo, mjumbe wa mauaji anayetumiwa na BIGI aliutumia huo mwanya kumbishia hodi za kutisha mara nenda rudi kwenye ndoto zake, majira ya usiku mkubwa, mpaka pale alipoondoka na uhai wa kiumbe kilichokuwa tumboni mwake!

Bembela alinieleza kwenye simu, bwana huyo hawezi kumuua mtu kama hatokuwa na kitu binafsi cha mhanga wake, kwahiyo mbali na zile nguo za mwanangu nilizoziona pale nje, asingeweza kuangamiza kiumbe ambacho kipo tumboni mwa mke wangu kama asingekuwa na mali binafsi ya mke wangu.

Nikajihisi kuelemewa na maneno hayo. Kuna muda aliongea lakini sikumwelewa tena maana nilifurikwa na mawazo lukuki kichwani.

Kwanza huyo mjumbe wa BIGI ni nani? Je, ni yule mkewe? Kama ndio, atakuwa ni mjumbe wa aina gani huyo ambaye niliwahi kumpeleka hospitali alipozidiwa?

Nikamweleza Bembela kuhusu mwanamke huyo na safari yetu ya kwenda zahanati siku ile, namna nilivyokuwa nahisi karibu naye na pia yale yalotokea kule zahanati, akanichosha kabisa kwa majibu yake ...

Bembela aliniambia,

"Basi huyo ndo' mjumbe wake, na siku hiyo sikumpakiza mtu bali nilimpakiza kiumbe kilichokuwa kinaenda kutafuta damu na pumzi za wagonjwa, mimi pale nilitumika kama daraja tu. Na usiku huo lazima kuna watu ambao waliondolewa roho zao kule kwenye nyumba ya matibabu."

Hapo nikamkumbuka yule bibi kule zahanati binafsi ya kawe na yale maneno yake.

Lakini zaidi, tumbo liliniuma nilipokumbuka kuwa hata mimi siku hiyo nilienda kugonga na kufoka mlangoni mwa BIGI nikimtaka bwana huyo atoke nisemezane naye, tena kama haitoshi mwanamke yule ambaye nimeambiwa ni mjumbe akiwa ndani amejilaza.

Je, nitakuwa salama?

Bembela aliniaga akiniahidi akifika Dar tutayajenga zaidi na kwa kushirikiana tutamkabili bwana huyo kwa ukamilifu, dawa amekwishaipata, mimi nikamuaga na kukata simu lakini siku ile nzima nikawa naendelea kuyasikia yale maneno yote aloniambia kana kwamba ni kanda ya muziki inayojirudia!

Nilifanya ratiba yangu kama kawaida, kwenda hospitali na kupita baadhi ya mahali kwa mambo yangu binafsi, usiku nikarejea nyumbani nilipoungana na mwanangu kwaajili ya chakula na mapumziko.

Muda wote huo mpaka naenda kulala, usiku wa saa nane, sikuona alama wala viashiria vyovyote vya uwepo wa bwana BIGI, achilia mbali na kwamba yeye mwenyewe sikumwona, lakini hata taa ya makazi yake haikuwashwa kabisa.

Ajabu ni kwamba, majira ya usiku wa saa tisa, kwa mujibu wa saa ya simu yangu, nilikurupuka kusikia mtu anagonga mlangoni. Kabla sijajigusa, nikasikia mtu huyo akisema, "nataka tuongee, nina shida na wewe."

Vilevile kama nilivyosema mimi muda ule malangoni mwa BIGI!
Mmmh noma sana
 
Ninyi misukule ya Steve Mollel mnafanya nini humu ? Au mnasubiri kabegi na furushi la mizoga ya big ?
 
Nt
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.

Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.

Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.

Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.

Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.

Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.

Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.

Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.

Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.

Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.

"Habari?" Tukionana.

"Asante." Tukiagana.

Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.

Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.

Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.

Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.

Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.

Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.

Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.

Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"

Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.

Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.

Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.

Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?

Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.

Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.

Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.

Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.

Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.

Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.

Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.

Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.

Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.

Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.

Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.

Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.

Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.

Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.

Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.

Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.

Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!

Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?

Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.

***
Muendelezo soma Jirani yangu wa Kule Goba hakuwa mtu wa kawaida
Ntarudi kusoma
 
Back
Top Bottom