Jiunge nami kusema hapana kwa udhalilishaji na ubaguzi anaoufanya mmliki wa clock tower café Iringa

Bado ana kariri mambo ya USA, na vile aliepambana nae ni muarabu , akajua ni racism
 
Inaonekana mara kadhaa umejisaidia hapo na hasira zimempanda hata hukuwasalimia aidha kwa kuwa ni msomi au ulikuwa umebanwa sana (yote yanawezekana)

Kuhusu Ulaya na sehemu zingine utaratibu ni huo huo kama sio mteja wana haki ya kukukataza kujisaidia hilo halina mjadala (for customer only)
Sioni ubaguzi hapo kabisa kwani kama ni ubaguzi usingekuwa unaenda hapo, mbaguzi halafu kila siku mnaongea nae na unamjua miaka mpaka baba yake.

Siku nyingine hata kama umevaa suit yako ni wajibu ukiwakuta watu uwasalimie na kuomba kuwa unaenda kujisaidia
 
Sasa kama mwanasheria analialia mbele za watu je sisi wakulima tutafanyaje?amedhalilisha taaluma yake na ndo hapo nazidi kupata mashaka na wasomi wetu wa Tanganyika
 
Binadamu yeyote ameumbwa na udhaifu, wewe unapoona udhaifu wa mwenzako kupitiliza chooni ni sahihi kupewa maneno makali ya kashfa na kuzuiwa kuingia eneo hilo tena, kuwa ni jambo sahihi kunasiku utajuta kuzaliwa kwa litakalokukuta kwenye hii dunia. Maana unapoweka interest binafsi katika kutetea ujinga ukumbuke dunia ni mzunguko, kunasiku mwanao au mkewako atashikwa na hali mbaya mjini akaingia pasipokupenda katika choo cha watu anapotoka na kukutana na watu wasio na utu wenye itikadi mbaya za ubaguzi kama hao wala usiende kulia kuwa ametukanwa. Kunahekima yakuongea na mtu, daima watakuwepo watu ambao kiburi cha mafanikio ndio kimeijaza midomo yao na hekima imefichwa mbele za mioyo yao wasijue namna yakuteat binadamu aliyeumbwa na Mungu anayewanyweshea mvua matajiri na masikini.
 
Vyoo vya kulipia viko kibao ungeenda huko.Choo Cha hoteli Ni kwa ajili ya wateja wanaonunua chochote Sasa mtu unaenda tiu kujaza choo ya watu hununui kitu SI sawa wakati unajua anagharimia maji ,wafanyakazi wa kusafisha,kuvuta kikijaa nk SI sahihi .Yuko sahihi choo chake Sio Cha umma
 
Huyu bwana anatangaza kazi yake ya UWAKILI, kiustaarabu ukibanwa haja nenda choo cha Umma hapo stendi ya mabasi
 
Huyu bwana anatangaza kazi yake ya UWAKILI, kiustaarabu ukibanwa haja nenda choo cha Umma hapo stendi ya mabasi
Mwenye cafe choo chake ni haki yake kuamua Nani aingie na nani asiingie.Kwani alimsaidia kujenga? Angeondoka kimya kimya.Analazimisha Kama vile lazima ajisaidie humo.Kujuana Sio leseni ya kutaka kwenda kujisaidia bure..Ile Ni biashara.Principle ya biashara Ni I know you but my business doesn't know you if you are not a customer who buys something!!! Huyu wakili anataka kuchanganya kujuana binafsi na biashara!!!! Biashara ni biashara ukienda kwenye biashara nenda kwa biashara Sio kwenda kujisaidia bure na kutoka bure.No no no.Hayuko pale na wahudumu hawapo pale kuhudumia wajisaidia chooni bure!!! Naungana na mwenye cafe huyo wakili asirudi hapo tena kwenye hiyo cafe.Niko pamoja na mwenye cafe
 
Kuishi kwa mazoea ndo kumetufisha hapa, kwasababu umeenda kupata huduma sehemu mara moja unaleta uodinary kama hujaomba hata mimi nakubalasa,hakuna sehemu ambayo utatanguliza ustaarabu ukapatiwa maudhi.
 
Duh pole sana wakili, Umeomba watu wakuunge mkono, waone umedhalilishwa, naona wote waliochangia wanakupinga. Hapo ulipofungua ofisi ni muhimu kuwa na Choo, sasa ukiwa na wateja, wakishikwa na haja huwa unawaelekeza waende wapi.
 
Madhali ww ni wakili nenda kamfungulie mashtaka tu na sio kulilia hapa
 
Usipende kuhudumiwa chakula kwa mtu ambaye umegundua hakupendi tofauti na hapo sumu ya panya inakuhusu
 
Nyie wanasheria huwa mnajifanya wajuaji sana, lazma utakuwa umezngua huko afu unataka mharbia mwenzako biashara
 
SASA bwana wakili ulitaka ukate gogo free of charge kisa mnafahamiana?? Hivi wananchi wote hapo iringa kila mmoja akaenda kukata gogo free of charge hapo si kitajaa ndani ya muda mfupi??

Acha hizo bwana wakili, kwako kwenye umeweka kufuli chooni kwako.
 
Sasa kama mwanasheria analialia mbele za watu je sisi wakulima tutafanyaje?amedhalilisha taaluma yake na nendeleedo hapo nazidi kupata mashaka na wasomi wetu wa Tanganyika
aiseee chalii yangu endeleeni kulima tu na mdhulumiwe mazao yenu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…