Jiunge nami kusema hapana kwa udhalilishaji na ubaguzi anaoufanya mmliki wa clock tower café Iringa

Jiunge nami kusema hapana kwa udhalilishaji na ubaguzi anaoufanya mmliki wa clock tower café Iringa

Hii ndo tabu ya kuishi mikoani mji mdogo karibu watu wote wanajuana sasa wewe umefunga unabanwa vipi na mkojo hahahah
 
Wakili weka mambo sawa hapo ubaguzi warangi yako umeingia vipi ww kakuzuia kwenda kumjazia choo ambacho hakipo kwa ajili ya umma sasa uwarabu na uhindi umeviunganishaje

Wewe ndio utakua mbaguzi
Heshimu biashara Za wenzako wacha ujanja ujanja bwana Wakili
 
Daaa! Kumbe hapo sikuhizi ni Mgahawa? Tunashukuru kwa taarifa Mh. Wakili,lkn kwa maelezo yako mwenyewe unasema ofc yako ni jirani na mgahawa huo,Sasa kwani hapo ofcn kwako hamna choo ya ofc? Na kwanini unaenda kushusha mzigo kwenye choo Cha mwenzio Tena sehem ya biashara? Pia Jambo lenyewe ni fupi ila wewe umeandika maelezo mengi mengi na mengine hayana msingi,utanisamehe aisee ila kwa bandiko hili unatakiwa ujipike sana kwenye melezo/ kuandika ur still poor in this area.
 
Nashukuru kuwa umenipa taarifa juu ya Mgahawa huo Mpya... Nilizoea kwenda Lulu's Cafe
 
huyo mwenye hiyo cafe chama gani ? kama ni chadema hapo Iringa tunaye mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa anaitwa Msigwa , ni suala la kumjulisha tu na hatua zitafuatwa
 
Hahaha mimi nimecheka kwa sababu SIJAUONA UBAGUZI wowote hapo. Huwezi kulazimisha kutumia choo cha mtu mwingine bila idhini yake kwa sababu ya rangi yako. Kwani hapo Iringa kuna choo mahali hapo tu Clock Tower café? Kama kuna nyumba jirani na hiyo Café kwanini hukwenda kuomba kujisaidia huko kama huyo mmiliki wa café kakataa? Kubanwa na haja iwe kubwa au ndogo ni matatizo yako, kama yalivyo binafsi kwa kila binadamu. Lakini huwezi kulifanya hili likawa tatizo la ubaguzi wa rangi, Eti wewe ni mwanasheria, mwanasheria unalazimisha kutumia mali ya mtu bila ridhaa yake? Kwanini usilishitaki jiji la Iringa kukosa VYOO VYA UMMA?! Choo binafsi ni mali ya mmiliki na choo cha umma ni mali ya wote kwasababu kinajengwa kuhudumia umma wote na kwa kutumia pesa za kodi zetu.

Umenishangaza mwanasheria kudai kutumia mali ya mtu kwa lazima, hili limenishangaza sana. choo ni kwa ajili ya wateja wake, wewe siku hiyo hukuwa mteja wake, huwezi kujipa uteja kwanguvu, yeye hawezi kukumbuka wateja wote wa siku za nyuma.
Ulipoingia ulipaswa kueleza shida yako kwao, siyo kama ulivyofanya wewe , uliwasalimia ukapitiliza kwenda chooni, huo siyo ustaarabu. Ustaarabu ni kueleza shida yako kwa mmiliki, kwamba umebanwa na unaomba ujisaidie chooni. Lakini ulijipa uteja kwa nguvu na uliona unahaki kutumia choo cha café kama mali ya umma, hiyo siyo halali. Swaumu yako haina uhusiano na choo chake, na uwakili wako hauna haki kutumia visivyo vyako. Utaratibu ni kuomba, kasha unapewa au kunyimwa.
Acha kulazimisha ubaguzi hata mahala pasipokuwa na ubaguzi.
 
Bwana wakili biashara haitaji mazoea iyo ni kazi kama ilivyo kaz yako mtu hawezi kukurupuka tu , bila utaratibu kisa amekuzoea akakwambia nna kesi yangu twende maakaman ukawe wakili wangu bila utaratibu maalum.
 
1. Mkiwa katika sehemu au eneo ambalo liko confined kama hapo Iringa ni rahisi kukwazana wakati mwingine bila kujua kwa sababu gani, labda
a. Itikadi za vyama
b. Mapenzi
c. Maslahi ya kikazi, inawezekana unamtetea hasimu wake
d. Majungu
e. Marafiki, coincidentally adui yake ni rafiki yako

2. Take it simple, dont complicate so far wewe sio uliolianzisha ni weakness yake yeye SIO WEWE calm down, smile, take it easy, thank God

3. Nahisi ulikosa Courtesy, ulipaswa kwanza usalimie kisha uombe kuingia msalani sidhani kama haya yote yangetokea

4. Ingawa amekuumiza mbele za watu lakini SAMEHE, haigharimu kitu. Sana sana inapunguza kutembea na mizigo ISIYOKUHUSU
 
Baada ya kumkata kelebu wewe unaleta uzi hapa wa kulalamika, kama mambo yenyewe ndio haya tutakuwa watumwa. Mpaka mwisho wa dunia hii, sasa wewe wakili mpeleke mahakamani na umfugulie shitaka la ubaguzi na udhalikishaji.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Umeandika/Umecopy Mkeka mrefu sanaa
Jinsi wabongo walivyo wavivu,watakuwa Wamesoma na ilipofika Juu juu Waka scroll.

In summary

Hilo bandiko Linahusu Ubaguzi (kwa mujibu Wake)
Muandishi Ni mwanasheria/wakili
anaishi Iringa.
Ni mteja mzuri sana wa Mgahawa uliopo Clock Tower Iringa dodoma road.
Akiwa katika harakati Zake za Kuweka mkono kinywaji,alibanwa na haja Sasa kwa Kuwa Ni mteja wa pale na Ni mwez mtukufuku (ramadhani) akaon ngoja nikaji sitili pale (kujisaidia japo hajasema Kama ilikuwa kubwa au ndogo haha yamkini Kubwa).

wakati kashamaliza kuji hajabisha,ghafla mhudumu akamuambia Kuwa "Yeye c Mteja mzuri na anatakiwa asikanyage Tena pale"

na hiyo ndiyo hoja yake Kuwa. aliambiwa asikanyage Tena hapo.bila sababu ya Maana.
so akaona Kuwa ame baguliwa (C unajua Wanasheria tena?!).

Kupitia Ubaguzi wake akatumia ref za wakati wa ukoloni jinsi watu walivyokuwa wanabaguliwa katika nchi yao.

Ni Hayo TU.
Hata hii sijamaliza
 
Ilivyokua iringanet cafe mmilik alikua feisal mtoto wa amani store, kama bado mmilik ni yule mwarabu bas mtoa mada atakua sahihi yan jamaa ni mvuta bangi na mlevi had jamii ya kiarabu ilimtenga
 
JIUNGE NAMI KUSEMA HAPANA KWA UDHALILISHAJI NA UBAGUZI ANAOUFANYA MMLIKI WA CLOCK TOWER CAFÉ IRINGA.

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
Nimekuwa mteja wa mgahawa wa Clock Tower Café uliopo barabara ya Dodoma/Uhuru Avenue katika Manispaa ya Iringa tangu uanzishwe mwaka jana. Nimekuwa nikipata huduma ya chakula katika Mgahawa wa Clock Tower nikiwa ama peke yangu au nikiwa na wageni au wateja wangu kwa kuwa ofisi yangu ya Uwakili ipo jirani tu na mgahawa huu. Hata hivyo jana tarehe 9 mwezi Mei mwaka 2019 limetokea tukio ambalo limenisononesha na kunifanya nisiwe tena na hamu ya kupata huduma ya chakula katika mgahawa wa Clock Tower Café wa hapa Iringa.

Jana ilikuwa ni siku ya tatu/ya nne ya mwezi wa Ramadhan. Nami nilikuwa katika saumu lakinijana wakati natoka mahakamani wakati napita Clock Tower Café nilijisikia haja nikaona niinge ili nijisaidie. Mnamo saan 4.00 asubuhi hivi niliingia Clock Tower Café. Nilipoingia nilimkuta Mmiliki wa Clock Tower Café, Iringa akiwa na mfanyakazi wake wa muda mrefu tangu enzi eneo hilo lilipokuwa Iringanet ikitoa huduma za mtandao wa internet. Kama ilivyo desturi niliwasalimia na kuingia ndani nikapita chooni.

Wakati nataka kutoka Clock Tower Café, niliwakuta Mmiliki na mfanyakazi wake wakiwa eneo lile lile na Mmiliki alinikabili kwa ujeuri na katika hali ya udhalilishaji na kashfa kwangu. Mbele ya wateja na wafanyakazi wa Clock Tower Café Iringa alinionyesha kwa sauti ya ukali kama vile mimi ni motto mdogo sana poster yenye maneno “Management reserves the right to refuse admission” iliyobandikwa ukutani. Maneno hayo ya Kiingereza yanamanisha: “Utawala unayo haki ya kumkataza mtu yoyote kuingia”. Na kisha kwa maneno makali akaniambia eti mimi ni mteja mbaya na kamwe hataki kuniona nikiingia au kununua chochote katika mgahawa wake wa Clock Tower Café Iringa na kwamba choo chake sio choo cha umma.

Kwa kweli nilifedheheka sana na kuvunjiwa heshima yangu katika jamii kwa tukio hili na sikuamini kinachotokea. Nimekuwa ninamfahamu Mmiliki huyo wa Clock Tower Café Iringa kwa miaka mingi sana name nimekuwa nikimchukulia kwamba ni jamaa yangu na yeye ananifahamu kwa kina na kazi ninazofanya hapa Iringa na hata baba yake namfahamu na tuna mahusiano mazuri tu kwa miaka mingi. Nimemfahamu Mmiliki huyu wa Clock Tower Cafe Iringa tangu mwaka 2015 nilipokuwa nafanya kazi Iringa na nikiwa mteja wa Iringanet tangu ilipokuwa jingo la Ghorofa pale Mshindo hadi anahamia hapa Barabara ya Dodoma. Kwa upole, nilimsihi na kumkumbusha kwamba tuko ndani ya mwezi wa Ramadhani na si vizuri kunifanyia kitendo cha udhalilishaji lakini alibaki na msimamo wake kuwa hanihitaji mimi wakla wananihusu kuwa wateja wa Clock Tower Café na kwamba niondoke na kamwe nisiingie tena Clock Tower Café Iringa. Ilibidi niondoke kwa aibu kimya kimya kwa unyonge mithili ya mbwa aliyemwagia maji akiogopa hata kubwekawa. Na jambo hili lilinishangaza sana kwa sababu sehemu ya biashara ni sehemu ya umma ambapo kila mtu anaweza kuingia na kutoka.

Kwa kweli tukio hili lininsononesha, kunidhalilisha na kunikumbisha si tukio lilimtokea mmoja wa wagombe Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alipoingia katika Hotel moja Mjini Dar es Salaam, Uongozi wa Hotel ulikataa hata kumhudumia maji ya kunywa na pia unakumbusha madhila ya siku za ukoloni ambapo watu waafrika licha ya kuwa ndiyo wenyeji wa nchi hii walikuwa wanabaguliwa kwa rangi na hadhi yao na kukatazwa kuingia katika mahoteli au migahawa ya watu weupe. Pale jijini Tanga ilikuwa rahisi mbwa kuingia Planters Hotel lakini si Mwaafrika. Na marehemu Mzee Erasto Mang’enya katika kitabu chake kimoja anaeleza madhila haya ya ubaguzi kwa waafrika pamoja na elimu yake na kuwa mjumbe wa Mamlaka ya Mji alikuwa haruhusiwi kuingia katika Hotel za watu weupe kwa kuwa tu alikuwa ni Mwaafrika.

Na ni jambo la kusikitisha zaidi kuona kuwa baada ya zaidi ya nusu karne ya nchi yetu ya Tanzania na pia Visiwa vya Unguja na Pemba kuwa nchi huru, bado wapo watu kama Mmiliki wa Clock Tower Café Iringa ambao wanaona wanayo haki ya kumnyanyasa Mtanzania na kwamba Mwaafrika kwao ni mtu dhalili asiye na hadhi au haki ya kupata huduma katika biashara zao. Jambo hili halivumiliki hata kidogo na kamwe siwezi kukaa kimya katika hili kuona mtu kwa sababu yeye ni Mwaarabu au Mweupe anayo haki ya kumnyanyasa mtu mweusi katika ardhi ya mababu zake. Je mtu mwenye rangi nyeupe akiingia Clock Tower Café kwenda choo kujisaidia na kasha kutoka bila ya kupata huduma yoyote, je Mmiliki huyu angemsemesha katika kama alivyonisemesha mie kijeuri?

Kama Mtanzania na Mwaafrika naona fahari kuwa nimepata bahati ya kutembelea au kuishi katika nchi zingine za Afrika Mashariki, Ulaya (Norway) na Marekani (USA) lakini katika kutembea kwangu kote huko sijawahi kukatazwa kupata huduma hata ya kujisaidia chooni katika mgahawa au Hotel yoyote kokote kule duniani isipokuwa hapa Iringa katika mgahawa huu wa Clock Tower Café. Kote nilipopata huduma hotelini au mgahawani nimekuwa nikipata heshaima ya utu wangu kwa usawa bila ya kujali hali yangu, rangi yangu au Utaifa wangu hata kama nilikuwa Mwaafrika pekee mahali hapo. Kamwe sijawahi kutokewa na tukio la kubaguliwa na kuonekana dhalili na nisiye na hadhi yoyote isipokuwa jana mbele ya Mmiliki, wafanyakazi na wateja wa Clock Tower Café Iringa ndani ya Mji na nchi yangu. Jambo hili halivumiliki na ni lazima kwa vitendo tulikemee.

Msimamo wangu ni kwamba tukio lililonitokea jana kamwe lisimtokee mkazi au mtu yoyote anayetembelea Iringa. Rai yangu ni kuwa wakazi na watu wote wanaotembelea Iringa kamwe tusiingie kupata huduma Clock Tower Café Iringa kwani Mmili hatuhitaji sisi anao wateja wake wenye hadhi ya kupata huduma ya chakula chake na sio sisi wakazi na watu wanaotembelea Iringa. Tusimmudhi tuwache Mmiliki huyu awahudumie wateja wake anaowataka kwa raha zake.

Tuungane pamoja kusema hapana kwa udhahlilishaji na ubaguzi anaoufanya Mmiliki wa Clock Tower Café katika nchi yetu na mji wetu!

Tafadhali mhabarishe na mwingine!

ZUBERI HAMISI NGODA
Iringa, Tanzania
Simu: +255 655 200 200
E-Mail: advocate.ngoda@gmail.com
May 10 , 2019

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
sijaona hoja ya msingi ,maana ya mfungo unaijua,?mojawapo ni kushinda vishawishi kwa maana hiyo mfungo wako haukua na mantiki kama ulishindwa kukabiliana na hasira kwa kutumia imani yako,katika kipindi cha mfungo wa kweli lazma ukutane na majaribu /vishawishi kupima imani yako,ulipaswa kitumumia hekima kukabiliana na jamaa huyoo..aksante
 
NIMESOMA SIJAONA UBAGUZI HAPO!!😳

Anadai alienda kujisaidia, Ghafula anaambiwa usiingie Tena kwenye hiyo hotel !!!! Inawezekana kweli ndivyo ilikuwa?


Mtoa Mada pamoja na kwamba NI Wakili uwezo wake NI mdogo Sana sijui hata kesi huwa anashinda!!

Kwa mfano kilikuwa na sababu gani kutaja Mambo ya mfungo, meeting Ramadhani na kwenda kujisaidia?

We unafikiri watu wote wanaujua au kuutambua mwezi wa Ramadhani?

Sikuona hoja yoyote iliyokusababusha uanze kuingiza Mambo ya mwezi wa Ramadhani na tendo la kujisaidia!!!

Halafu unadai umebaguliwa !!! Sasa hapo umebaguliwa kutoka kwenye kundi lipi?

MIMI SIUNGANI NA WEWE KABISAA KULAANI HUO UBAGUZI UNAODAI KUFANYIWA, SIJAONA UBAGUZI. HALAFU HATUWEZI KUSIKILIZA UPANDE MMOJA HALAFU TUTOE HUKUMU, WE MWANASHERIA YA WAPI UNAYEMALIZA KESI KWA KUSIKILIZA UPANDE MMOJA? WANASHERIA WENYE MTAZAMO KAMA WAKO NDO MAWAKILI WA SERIKALI MNAOITAABISHA SERIKALI KWA USHAURI MBOVU.
 
Haha kama ni ngoda ni mtata kwa asili niliwahi kupata taarifa za kutaka kumpiga mwenyekiti wa baraza la nyumba na Ardhi hapo Iringa. (District Land and Housing Tribunal ) .

Badilika mkuu Ngoda, it is not that late.
 
JIUNGE NAMI KUSEMA HAPANA KWA UDHALILISHAJI NA UBAGUZI ANAOUFANYA MMLIKI WA CLOCK TOWER CAFÉ IRINGA.

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
Nimekuwa mteja wa mgahawa wa Clock Tower Café uliopo barabara ya Dodoma/Uhuru Avenue katika Manispaa ya Iringa tangu uanzishwe mwaka jana. Nimekuwa nikipata huduma ya chakula katika Mgahawa wa Clock Tower nikiwa ama peke yangu au nikiwa na wageni au wateja wangu kwa kuwa ofisi yangu ya Uwakili ipo jirani tu na mgahawa huu. Hata hivyo jana tarehe 9 mwezi Mei mwaka 2019 limetokea tukio ambalo limenisononesha na kunifanya nisiwe tena na hamu ya kupata huduma ya chakula katika mgahawa wa Clock Tower Café wa hapa Iringa.

Jana ilikuwa ni siku ya tatu/ya nne ya mwezi wa Ramadhan. Nami nilikuwa katika saumu lakinijana wakati natoka mahakamani wakati napita Clock Tower Café nilijisikia haja nikaona niinge ili nijisaidie. Mnamo saan 4.00 asubuhi hivi niliingia Clock Tower Café. Nilipoingia nilimkuta Mmiliki wa Clock Tower Café, Iringa akiwa na mfanyakazi wake wa muda mrefu tangu enzi eneo hilo lilipokuwa Iringanet ikitoa huduma za mtandao wa internet. Kama ilivyo desturi niliwasalimia na kuingia ndani nikapita chooni.

Wakati nataka kutoka Clock Tower Café, niliwakuta Mmiliki na mfanyakazi wake wakiwa eneo lile lile na Mmiliki alinikabili kwa ujeuri na katika hali ya udhalilishaji na kashfa kwangu. Mbele ya wateja na wafanyakazi wa Clock Tower Café Iringa alinionyesha kwa sauti ya ukali kama vile mimi ni motto mdogo sana poster yenye maneno “Management reserves the right to refuse admission” iliyobandikwa ukutani. Maneno hayo ya Kiingereza yanamanisha: “Utawala unayo haki ya kumkataza mtu yoyote kuingia”. Na kisha kwa maneno makali akaniambia eti mimi ni mteja mbaya na kamwe hataki kuniona nikiingia au kununua chochote katika mgahawa wake wa Clock Tower Café Iringa na kwamba choo chake sio choo cha umma.

Kwa kweli nilifedheheka sana na kuvunjiwa heshima yangu katika jamii kwa tukio hili na sikuamini kinachotokea. Nimekuwa ninamfahamu Mmiliki huyo wa Clock Tower Café Iringa kwa miaka mingi sana name nimekuwa nikimchukulia kwamba ni jamaa yangu na yeye ananifahamu kwa kina na kazi ninazofanya hapa Iringa na hata baba yake namfahamu na tuna mahusiano mazuri tu kwa miaka mingi. Nimemfahamu Mmiliki huyu wa Clock Tower Cafe Iringa tangu mwaka 2015 nilipokuwa nafanya kazi Iringa na nikiwa mteja wa Iringanet tangu ilipokuwa jingo la Ghorofa pale Mshindo hadi anahamia hapa Barabara ya Dodoma. Kwa upole, nilimsihi na kumkumbusha kwamba tuko ndani ya mwezi wa Ramadhani na si vizuri kunifanyia kitendo cha udhalilishaji lakini alibaki na msimamo wake kuwa hanihitaji mimi wakla wananihusu kuwa wateja wa Clock Tower Café na kwamba niondoke na kamwe nisiingie tena Clock Tower Café Iringa. Ilibidi niondoke kwa aibu kimya kimya kwa unyonge mithili ya mbwa aliyemwagia maji akiogopa hata kubwekawa. Na jambo hili lilinishangaza sana kwa sababu sehemu ya biashara ni sehemu ya umma ambapo kila mtu anaweza kuingia na kutoka.

Kwa kweli tukio hili lininsononesha, kunidhalilisha na kunikumbisha si tukio lilimtokea mmoja wa wagombe Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alipoingia katika Hotel moja Mjini Dar es Salaam, Uongozi wa Hotel ulikataa hata kumhudumia maji ya kunywa na pia unakumbusha madhila ya siku za ukoloni ambapo watu waafrika licha ya kuwa ndiyo wenyeji wa nchi hii walikuwa wanabaguliwa kwa rangi na hadhi yao na kukatazwa kuingia katika mahoteli au migahawa ya watu weupe. Pale jijini Tanga ilikuwa rahisi mbwa kuingia Planters Hotel lakini si Mwaafrika. Na marehemu Mzee Erasto Mang’enya katika kitabu chake kimoja anaeleza madhila haya ya ubaguzi kwa waafrika pamoja na elimu yake na kuwa mjumbe wa Mamlaka ya Mji alikuwa haruhusiwi kuingia katika Hotel za watu weupe kwa kuwa tu alikuwa ni Mwaafrika.

Na ni jambo la kusikitisha zaidi kuona kuwa baada ya zaidi ya nusu karne ya nchi yetu ya Tanzania na pia Visiwa vya Unguja na Pemba kuwa nchi huru, bado wapo watu kama Mmiliki wa Clock Tower Café Iringa ambao wanaona wanayo haki ya kumnyanyasa Mtanzania na kwamba Mwaafrika kwao ni mtu dhalili asiye na hadhi au haki ya kupata huduma katika biashara zao. Jambo hili halivumiliki hata kidogo na kamwe siwezi kukaa kimya katika hili kuona mtu kwa sababu yeye ni Mwaarabu au Mweupe anayo haki ya kumnyanyasa mtu mweusi katika ardhi ya mababu zake. Je mtu mwenye rangi nyeupe akiingia Clock Tower Café kwenda choo kujisaidia na kasha kutoka bila ya kupata huduma yoyote, je Mmiliki huyu angemsemesha katika kama alivyonisemesha mie kijeuri?

Kama Mtanzania na Mwaafrika naona fahari kuwa nimepata bahati ya kutembelea au kuishi katika nchi zingine za Afrika Mashariki, Ulaya (Norway) na Marekani (USA) lakini katika kutembea kwangu kote huko sijawahi kukatazwa kupata huduma hata ya kujisaidia chooni katika mgahawa au Hotel yoyote kokote kule duniani isipokuwa hapa Iringa katika mgahawa huu wa Clock Tower Café. Kote nilipopata huduma hotelini au mgahawani nimekuwa nikipata heshaima ya utu wangu kwa usawa bila ya kujali hali yangu, rangi yangu au Utaifa wangu hata kama nilikuwa Mwaafrika pekee mahali hapo. Kamwe sijawahi kutokewa na tukio la kubaguliwa na kuonekana dhalili na nisiye na hadhi yoyote isipokuwa jana mbele ya Mmiliki, wafanyakazi na wateja wa Clock Tower Café Iringa ndani ya Mji na nchi yangu. Jambo hili halivumiliki na ni lazima kwa vitendo tulikemee.

Msimamo wangu ni kwamba tukio lililonitokea jana kamwe lisimtokee mkazi au mtu yoyote anayetembelea Iringa. Rai yangu ni kuwa wakazi na watu wote wanaotembelea Iringa kamwe tusiingie kupata huduma Clock Tower Café Iringa kwani Mmili hatuhitaji sisi anao wateja wake wenye hadhi ya kupata huduma ya chakula chake na sio sisi wakazi na watu wanaotembelea Iringa. Tusimmudhi tuwache Mmiliki huyu awahudumie wateja wake anaowataka kwa raha zake.

Tuungane pamoja kusema hapana kwa udhahlilishaji na ubaguzi anaoufanya Mmiliki wa Clock Tower Café katika nchi yetu na mji wetu!

Tafadhali mhabarishe na mwingine!

ZUBERI HAMISI NGODA
Iringa, Tanzania
Simu: +255 655 200 200
E-Mail: advocate.ngoda@gmail.com
May 10 , 2019

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
Ujumbe wako nmekuelewa Kaka vizuri Sana.Ila tatizo nyie waislam huwa mnawaonaga waarabu Kuwa ni Mungu wenu wa pili Ila wao waarabu wanawadharau watu weusi na kuwaona kituko. Pole Ila nafikiri kuna kitu umejifunza kutoka kwa hawa jamaa. Waarabu na Wahindi ni watu tulioishi nao Tanzania miaka mingi Ila Wana Racism. Mimi niliwahi kusoma na Wahindi flani Thailand walikuwa very Racism.
 
Kikubwa usizoee sana ofisi za watu ,,choo kipo kwa ajili ya wateja tu na sio wapita njia ,Iringa vyoo ni vingi tu ,toa 200 acha kuzoea


Kuna hichi choo cha stand kimetazamana na mahala wamachinga wamepanga vitu ,,ukiwa mteja wa kila siku unatoa 100 tu.
Vatete [emoji28][emoji28][emoji28]
 
Siku nyingine ujifunze kwamba hao watu wenye asili ya (hasa) Asia huwa hawana urafiki wa kweli na wa kudumu. Wanapokuwa wanakuhitaji kwa maslahi yao utaona mema yote. Akimaliza uhitaji hana muda nawe. Halafu kuna maliwato pale Garden, Soko kuu na hata mahakamani kama ndipo ulipotokea.
KUKUKKUMBUSHA:
Iringa net haikuwa Mshindo. Pale ghorofani ni Kitanzini kwa Ngailo karibu na Masiti complex!
BAADAYE
nakupa pole kwa kujiaminisha urafiki na kufahamiana na watu wa sampuli hiyo na hongera kwa kujiongezea elimu ya tabia za wanadamu. Msamehe.
 
Back
Top Bottom