Akifafanua kuhusu nguzo hiyo ya kwanza ya Bara la Afrika kutumia vizuri, kwa njia endelevu na erevu raslimali zake, Rais Kikwete amesema kuwa uchimbaji wa madini na mafuta katika Afrika lazima uwasaidie Waafrika.
Ni jambo lisilokubalika kuwa madini ama mafuta yanachimbwa katika Bara la Afrika, lakini jamii zinazozunguka machimbo hayo havinufaiki na uchimbaji huo. Baadhi ya makampuni ya uwekezaji katika machimbo yanathubutu hata kuagiza maji ya kunywa, ama kuagiza chakula, ama hata kukodisha malori ya kusomba mchanga kutoka nje ya Bara hili, amesema Rais Kikwete.