JK Hatembei na Fuko La Fedha

JK Hatembei na Fuko La Fedha

Ile siasa yetu ya kujitegemea tumeicha wapi? Au ilikuwa ni wimbo tu, rais anaenda nje kuomba na wananchi wanamuomba rais!
Kwa ambao hamjakaa vijijini mtalaumu, ila hizi shule kata zimefanywa mashamba ya watu, ukifika tu kijijini hata kama umeenda msibani utaambiwa uchangie ujenzi!

Serikali kupitia halmashauri ya wilaya hutoa mabati nondo cement na mbao. wananchi hutakiwa kusomba mchanga na mawe tu, ambapo vijijini mawe yanapatikana bure, mchanga husombwa kwa kichwa na akinamama.

Sasa wanaposema nguvu zimaisha inamaana walikuwa wagonjwa au walikuwa na njaa!

Mkuu alitegemea aulizwe habari za epa, umeme na maji, sio kuambiwa hawana nguvu za kubeba mawe, sasa walitaka abebe yeye mabegani?

Mbona tarime hawachangishwi hela na shule zinajengwa kama kawaida, waende wakajifunze huko sio kumlalamikia mkuu wa kaya.

Inawezekana kabisa kuwa raia walifanya makosa kumuuliza mkuu aina hilo la swali.Lakini kuna namna ya kujibu kiasi cha kuwafurahisah watu, pia kuna namna ya kudela na viongozi wa chini.Kwani inaonyesha hawana vikao vya mara kwa mara.Maswali haya yanaonyesha pia kuwa wananchi pamoja na wabunge wao wamekata tamaa.

Shule au miradi mingi kweli inafanywa na wananchi wenyewe serikali ni kuongeza nguvu haijalishi miradi hiyo ni mikubwa au midogo kiasi gani.WATANZANIA WANAPASWA KUPEWA FARAJA HATA YA MANENO TU!
 
Mbona nahisi kama kuna mtu/watu wamedekezwa!?

Upo Right kama hisia zako na zangu ziko sawa ni kwamba. Hawa jamaa wamezoea kila kitu Siasa tu, Rais atoe mchango kinyume na taratibu za Fedha mradi tu ionekane ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani Ya Chama. Na hasa mbunge alitaka kujionesha kuwa yeye yupo karibu na Mkuu wa Nchi ili 2010 apate ubwete.
 
Subirini msikie Rostam kaenda njombe kuwatuliza wananchi na kutoa mchango wa kujenga shule na zahanati!
 
Tangu lini FISADI akaombwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa???????????? Tutamlaumu Prezidaa bure tunasahau prezidaa wetu ni FISADI mweupe. FISADI anaombwa pesa nyingi kama kufungulia mradi wa MGODI wa MADINI, Mradi wa kusambaza UMEME Tanzania nzima na nchi jirani, Mdadi wa kununua RADA au kutengeneza sare za vyombo vya dola. Since FISADI madau yake ni makubwa makubwa, hakuona umuhimu wa kuchangia ujenzi wa madarasa wanetu waweze kusoma. Anyway, aliona hapati gain yoyote hata kama angetoa mchango. Maake FISADI akitoa anategemea kupata money back.

Mtaamini kama ni FISADI wa madau makubwa asipo-APOLOGIZE kwa wananchi kutokana na kauli hiyo. Yangu masikio.
 
hamjiulizi kwanini mkuu alikuwa mkali katika sehemu zile imalinyi na ilembula..kumbuka imalinyi ni kijiji anachotokea adui wake wa kisiasa philip mangula na siku yenyewe ya tukio mangula alikuwa miongoni kwa viongozi waliokuwepo kumlaki.ndio maana akawa mkali pale muungwana pamoja na kuchangia milioni mbili alizosema hatembei nazo.

watu wa vijijini hawajaelemishwa hata hiyo siasa ya ujamaa na kujitegemea,kwasababu kila jamii miaka hii imejiingiza katika biashara zaidi ya kukuza maendelea ya vijiji ndio maana hawawezi kuipa kipaumbele hiyo siasa ya kusaidiana kujenga vijiji vya ujamaa kama enzi za mwalimu.vijiji hivi bila kuwezeshwa nyenzo mbalimbali,raslimali uchumi havitaendelea kamwe na zitabaki kuwa omba omba hata baada ya miaka 100
 
............MIMI NIJUAVYO RAIS YEYOTE ANATEMBEA NA FUKO LA PESA ...KAMA ANATAKA KUZIPIGA PANGA ASEME...KWENYE MSAFARA WA RAIS HAPAKOSEKANI PESA ....NA NDIO MAANA MARAIS WOTE WALIOTANGULIA ....AKIENDA MAHALI AKISHASOMEWA RISALA ...HUTOA PLEDGE YA CASH KUONGEZEA ANAPOTAKA...PESA IPO LIMITED NA MSHAURI WAKE WA PESA HUMSHAIRI KILA AENDAPO NI KIASI GANI ANAWEZA KUTOA MOJA KWA MOJA....HII NI KATIKA KUJENGA MAHUSIANO MEMA...INAPONEKANA PESA NYINGI ZA MFUKO WA RAIS..HUWA ANAZITUMIA ULAYA KUNUNUA MAWANI NA MAKOTI YA GUCCI.........WENZAKE KINA KIBAKI,MUSEVENI,KAGAME ets...wakienda vijijini huwa hawaoni hatari kuwa suprise wanakijiji kwa kumpatia mmoja wao kiasi cha pesa....kama ishara ya upendo!@!!...that is just a gesture ..but any empowerment programmes are meant to be sustainable...mabilioni ya kikwete is not one of the sustainable microeconomic programmes ..this was rather meant to reward presidents political suppporters ......and benefiting..remote bank managers and politician..while kikwete is just making hypocritical useless noises.........
 
Mwanakijiji,

..yaani Raisi ameshindwa kuzungumza na wananchi kwa njia za kiungwana anaamua kung'aka kwamba hatembei na fuko la fedha.

..vilevile kuna matukio mengi tu ambapo imetangazwa kwamba Raisi amechangia kiasi fulani cha fedha. kuna hata kipindi hapa tuliambiwa Mkuu wa Majeshi amechangia fedha mamilioni jimboni kwa Raisi.

..badala ya ukweli kuelezwa kwamba ni SERIKALI ndiyo imechangia wanasema Raisi/Waziri Mkuu/Mkuu wa Majeshi. hiyo ndiyo imezua dhana na mazoea kwamba wananchi wanaweza kumchomoa fedha Raisi.

NB:

..anayedekezwa hapa ni Raisi Kikwete. kauli hiyo ingetolewa na Mramba/Sumaye/Malecela ungesikia jinsi ambavyo wangepigwa vita

..si rais aliyenunua waandishi..hata resource zetu na walinzi wakitumika kulinda nyumba za ndogo hawaoni....kweli ..miaka ya shetani...teh ndio walisemaga CHAGUO LA SHETA... oooh sorry LA MUNGU!!!!
 
WANANCHI wa Wilaya ya Njombe, Mkoa wa Iringa, wameeleza kukerwa kwao na kauli ya Rais Jakaya Kikwete, kwamba hakutembea na fuko la fedha za kuwagawia.

Wakielezea kuhusu kauli hiyo ya Rais Kikwete, wananchi wa kada mbalimbali wilayani humo walisema wamechukizwa na kauli hiyo, wakidai kuwa ni ya kuwadhalilisha.
“Kwa kweli tumesikitishwa mno na kauli ya rais wetu. Hii ni dharau na udhalilishaji dhidi yetu, sisi si ombaomba, tunafanya kazi zetu kwa kujitegemea. Tumetumia rasilimali na nguvu zetu kujenga madarasa ya shule zetu, lakini hatukukamilisha kazi kwa sababu uwezo wetu ulifikia kikomo, hivyo tulimwomba msaada ili tukamilishe miradi yetu.
“Isitoshe hatukumwomba msaada wa fedha kutoka mfukoni mwake kama Kikwete binafsi, tumemwomba msaada akiwa rais wa nchi, ambaye tunajua ana fedha za umma za kusapoti nguvu za wananchi katika miradi ya maendeleo.
“Na hili si jambo jipya, marais waliomtangulia walikuwa wakifanya hivyo, na hata yeye amekuwa akichangia fedha katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi katika maeneo mbalimbali anapokuwa katika ziara za kikazi kama hii,” alisema mkazi wa Kijiji cha Imalinyi aliyekataa kutaja jina lake, kwa sababu ya kukwepa usumbufu.
Mwananchi mwingine kutoka Kijiji cha Ilembula, wilayani humo, ambaye pia hakutaka kutaja jina lake kwa sababu za kiusalama, alikuwa na maoni haya: “Kama rais hataki kusikiliza shida zetu, ni bora asingekuja kabisa, hakuna maana ya ziara yake kwetu. Anatuona sisi ombaomba, mbona yeye amekuwa akisafiri mara kwa mara nje ya nchi kuomba misaada - Marekani, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Canada, Denmark, Sweden, Uholanzi n.k.

Hapa Presidaa alisema,


“Hivi mmejipanga kunieleza matatizo yenu kwa lengo la kunichomoa fedha? Mbunge wewe ndiye umewapanga watu wako waniombe fedha? Mmekosea sana, mimi sijatembea na fuko la fedha za kuwagawia.
“Elezeni matatizo makubwa ambayo yameshindikana kutatuliwa na uongozi wa ngazi ya wilaya na mkoa. “Nielezeni matatizo ya mbolea, maji, barabara na afya. Mambo ya ujenzi wa madarasa ya shule za sekondari na msingi yanaweza kutatuliwa na uongozi wa ngazi ya wilaya na mkoa,” alisema Rais Kikwete huku akionekana dhahiri kukasirika.

Hapa KWeli JK amesahau kuwa aliwaahidi Wakati alipokuwa anaomba "Kula" kila kitu alisema tutafanya meengine wala hayakuwepo kwenye ilani ya chama chake lakini sasa ameshapata anawapa majibu ya mkato.ama kweli alishiba hamjui mwenye Njaa.😱


Hii ni aibu.
 
Jk kwisha habari yake hata kuwajibu watu wa chini namna ile ameshindwa kabisa...sasa anategemea picha waliopata wale watu itawatoka karibuni mana wamemsikia wenyewe akiwajibu "kunya"....hata kujibu kisiasa wala kidiplomasia ameshindwa???
 
Kweli ashibaye kamwe hawezi kumkumbuka mwenye njaa. Huu ni msemo wa kawaida tu ila kwa alichokisema JK kwa wananchi hawa kinatakiwa kupewa tafakari ya kina. Amekuwa na hasira na wananchi wake waliomchagua kwanini???

Kwanza inawezekana kuna jambo liliomuudhi Mh. Rais, kiasi akashindwa kuhimili hasira zake. Lakini kama Rais hakutakiwa kung'aka namna ile. Kufanya vile kunapunguza imani ya wananchi wake kwa CCM na yeye mwenyewe binafsi. Ushauri wangu ni kwamba atumie njia ya kidemokrasia akanushe hilo kwamba hakumaanisha hivyo.
 
Huyu jamaa inabidi aingie studio tu atoke na album maanke mimi siungi mkono usanii wake uso na tija.

Mbona kipindi cha kampeni aliitwa mteule wa Mungu?

Mbona alikua anapita kwenye magari ya wazi na kusema sitawaangusha watanzania? Yaani leo hii imekua ni kejeli na hasira?

Mkuu,hapa katudharau sisi wananchi sasa sijui watu hao hao wataruhusiwa kuandamana kuilaani hiyo kauli yake? Si ni wanademokrasia sisi? au yeye na wafuasi wake hawaamini ktk demokrasia yaani kisiri siri wantumia udikteta
 
Pole sana mzee Mangula na wananchi wa Imalinyi lakini nina tatizo kidogo na huyu Yono Kevela, siasa si sehemu yake ila kaivamia tu kwa vile ana vijisenti lakini pia ninakiri kuwa mkoa wa Iringa kuna tatizo kwa sasa na wasipoangalia litaugawa ule mkoa vipande, uchaguzi wa 2005 na 2007 ccm umeendelea kuwagawa na 2010 tatizo litakuwa kubwa sana. Hawa jamaa CCM hawakuwa tayari kuwapoteza wale wazee NEC na Uenyekiti zaidi ya kuhujumiana ndani ya CCM wenyewe, sasa wameanza kujutia na kuwasaka wachawi hapo ndipo chokochoko inaporudi kisengerenyuma.

JK atakuwa alikuwa na sababu za msingi za kuwakaripia hawa ndg zetu, na ninathubutu kukiri kuwa mkoani Iringa na wilaya zake hakuna kuaminiana ndani ya CCM ukienda kwa wabunge huko ndio hatari. Kama wasaidizi wamemwambia akina Mangula wameandaa kumpiga maswali huko kijijini unategemea nini toka kwa muungwana? Ni lazima awe mkweli na lazima ukweli uume wakuu.

Poleni wana Njombe na pia Muungwana kwa shughuli pevu.
 
The sad thing is, even if there was a lesson to teach, and a discipline to instill the president bungled the occassion by his trademark colloquism and lack of communication skills.Reading him one would be excuse to think that this guy actually believes he is no mere politician and has attained the status of a demi god.
 
mbona huwa hawatoi maneno kama haya wakati wa kampeni?
 
hata kama nia ya rais ilikuwa ni kuwafunza wananchi kujaribu kutatua matatizo mengine wao wenyewe au kwa kutumia ngazi za wilaya, kuwakaripia hivyo kama watoto ni ukosefu wa heshima kwa raia wake.

inashangaza kuona aliyesema maneno ya aibu hivyo ni mwana diplomasia wa siku nyingi!
 
Back
Top Bottom