JKT kurejeshwa, wazo zuri au limepitwa na wakati?

JKT kurejeshwa, wazo zuri au limepitwa na wakati?

Wakuu nimesoma mahali kwamba serikali ina mpango wa kurudisha JKT kwa "wasomi wetu" naomba nieleweshwe vizuri kwa wale wenye data. Na pia je kuna umuhimu kweli katika kipindi hiki?
Eh! Hivi JKT haipo tena. Si lilikuwa Jeshi la Kujenga Taifa, sasa Taifa linajengwa na nani!? OMG!
 
Watu wako desperate kufikiria channels za kupitisha mikwanja ya kampeni mwakani... nyie angalieni tu
 
JKT ilifutwa na Mwinyi ili wanae wasiende huko. Leo ajabu mwanae ati ni waziri wa ulinzi.
Umuhimu wa JKT ulikuwepo na utaendelea kuwepo. Kama si mafunzo ya jeshi JKT inaweza kusaidia kuwapa skills vijana wanaomaliza shule katika kazi kama vile kilimo cha kisasa, useremala, na ujasiriamali. Najua Tanzania si nchi ya kivita lakini unakuta nchi kama Israel ina lazima ya vijana kwenda jeshini kwa miaka miwili, angalau.
 
kuna umuhimu sana wa kurudisha JKT ambao ni kujenga utaifa, umoja na utamaduni ambao umeporomoka sana baada ya kufuta JKT.

Kwa wale amboa tumepitia JKT ukiacha ile karinyekarinye ukafanya uchambuzi "objectively" utaona JKT ilitujenga kwa kutufanya tuje kuwa raia wema na kujiona wote ni ndugu bila kujari umetokea familai gani, kabila gani, mkoa gani au una rangi gani.

I FULLY SUPPORT REINTRODUCTION OF JKT with minor improvements
 
iliondolewa kwa sababu na sidhani inaumuhimu wa kuirudisha

pesa za kupeleka JKT wangeupgrade JWTZ na taasisi zinginezo za kiusalama
 
JKT ilifutwa na Mwinyi ili wanae wasiende huko. Leo ajabu mwanae ati ni waziri wa ulinzi.
Umuhimu wa JKT ulikuwepo na utaendelea kuwepo. Kama si mafunzo ya jeshi JKT inaweza kusaidia kuwapa skills vijana wanaomaliza shule katika kazi kama vile kilimo cha kisasa, useremala, na ujasiriamali. Najua Tanzania si nchi ya kivita lakini unakuta nchi kama Israel ina lazima ya vijana kwenda jeshini kwa miaka miwili, angalau.

Unaona sasa....umekuwa kidingi kinoko na wewe. JKT haina umuhimu wowote zaidi ya kutesa watu
 
JKT, of the compulsory kind, was not useful. What do we have to show for it? I wasted a year in Mafinga and Masange JKT camps. It was time that should have been spent in a university.

There is order in JKT, but there is absolutely no discipline. Too many people mistake the order there for discipline. Morally speaking, the JKT that I experienced deformed rather than formed youths. The main activity of its barely educated crop of officers was to sexually harass the female inmates.

JKT could not even feed itself. The institution was too morally corrupt to be productive. It had to be fed by the overworked and overexploited farmers and peasants of Tanzania.
 
Uzalendo na Umoja wa Kitaifa tunaojivunia sasa ulichangiwa na kurutubishwa sana na JKT. Pale mlikuwa mnakutana Watanzania wa kada zote, watoto wa viongozi, watoto wa wakulima, watoto waliokwenda shule, watoto walioishia darasa la saba tu,mnajifunza kuishi kila aina ya maisha...
Sasa hivi mtoto anazaliwa kijijini, anasomea kijijini kwake hadi kidato cha sita hapo kwenye KATA yake, hakutani kabisa na Watanzania wenzake wa maeneo mengine ya Nchi yetu hadi anapobahatika kwenda vyuoni. Hali hii sio kwamba inachochea UKABILA bali pia inavuruga sana UMOJA wa Taifa letu.
Ambao hamuifahamu JKT hamuwezi kutambua haraka umuhimu wake hadi mtakapofika kule.
 
......naomba nieleweshwe vizuri kwa wale wenye data. Na pia je kuna umuhimu kweli katika kipindi hiki?

Mkodoleaji na wenzako,
Umuhimu wa kuwa na JKT ni mkubwa sana kuliko wengi wanavyodhani. Enzi za JKT, wanafunzi walifundishwa, mbali ya ukakamavu, mbinu za kilimo bora, ufugaji bora, utengenezaji wa fenicha, ujenzi na mbinu nyingine nyingi za uzalishaji mali. Washiriki kutoka mikoa mbali mbali walikutana katika kambi moja, hivyo kujenga moyo wa uzalendo kwa nchi yao.
Wahitimu wa masomo kama vile ya sekondari, uuguzi, ualimu na fani nyingine walikutana na kubadilidhana uzoefu, walifahamiana na kujenga mahusiano, kuondoa hisia za ukabila (kwa kukaa na kufanya kazi pamoja na watu wa kabila mbalimbali) na mambo mengine mengi mazuri. Mafunzo haya yaliwapa washiriki hawa ujasiri wa kufanya kazi popote pale nchini, tofauti na vijana wa sasa ambao hawataki kufanya kazi katika maeneo ya vijijini na kusababisha kujazana mijini.
Kwa mtazamo wangu, ningependa sana serikali irudishe mafunzo haya, kwani yatasaidia sana kujenga stadi za kazi na ukakamavu kwa wanafunzi wanaohitimu sekondari na vyuo mbalimbali. Enzi za JKT, ilikuwa huwezi kupata nafasi katika chuo iwapo hujapitia depo. Kuwepo kwa JKT kutasaidia kujenga stadi za kazi kwa makundi ya vijana wasio na ajira Tanzania. Tazameni mfano wa SUMA JKT


...Misallocations of our meager resources!..

Sikubaliani na wazo lako, kwamba kurudisha JKT ni kutumia vibaya rasilimali chache tulizonazo. Sababu nimeziandika hapo juu!

Haitaluwa na maana. Awamu hii ya nne ya kifisadi nadhani watoto wa mafisadi watakwepa JKT kwa kusaidiwa na wazazi wao, na kama vipi wataenda kusoma nje.

Kwenda kusoma nje sio kwa sababu ya kukwepa JKT, walisoma nje walikuwepo tangu enzi za Mwalimu na JKT walikwenda pia.

Eh! Hivi JKT haipo tena?
JKT ipo, ila mafunzo ni ya kujitolea zaidi kuliko lazima na nafasi ni za kuomba, si kupelekwa!

JKT ilifutwa na Mwinyi ili wanae wasiende huko.
Wow! Tuambie zaidi mkuu.


Umuhimu wa JKT ulikuwepo na utaendelea kuwepo. Kama si mafunzo ya jeshi JKT inaweza kusaidia kuwapa skills vijana wanaomaliza shule katika kazi kama vile kilimo cha kisasa, useremala, na ujasiriamali. Najua Tanzania si nchi ya kivita lakini unakuta nchi kama Israel ina lazima ya vijana kwenda jeshini kwa miaka miwili, angalau.

Nakuunga mkono kwa 100%

kuna umuhimu sana wa kurudisha JKT ambao ni kujenga utaifa, umoja na utamaduni ambao umeporomoka sana baada ya kufuta JKT.

Kwa wale amboa tumepitia JKT ukiacha ile karinyekarinye ukafanya uchambuzi "objectively" utaona JKT ilitujenga kwa kutufanya tuje kuwa raia wema na kujiona wote ni ndugu bila kujari umetokea familai gani, kabila gani, mkoa gani au una rangi gani.

I FULLY SUPPORT REINTRODUCTION OF JKT with minor improvements
Nakuunga mkono kwa 100%

iliondolewa kwa sababu na sidhani inaumuhimu wa kuirudisha....

Sikubaliani na wewe (na sio kosa kutokubaliana na wewe). Sababu zio hapo juu, katika post za Boma na Jasusi.
Jamani tufikirie kichanya chanya, JKT ni nzuri.
 
umuhimu upo sana, kuna watu wanasoma hizi academia wanalemaa sana.....jeshi linamuongezea mtu kujitambua na kujiamini.nchi kama Marekani kujiunga na jeshi ni kipimo cha uzalendo ndo sababu watu wa taaluma zote utakuta kuna wakati alikuwa jeshini.
 
Mkodoleaji na wenzako,
Umuhimu wa kuwa na JKT ni mkubwa sana kuliko wengi wanavyodhani. Enzi za JKT, wanafunzi walifundishwa, mbali ya ukakamavu, mbinu za kilimo bora, ufugaji bora, utengenezaji wa fenicha, ujenzi na mbinu nyingine nyingi za uzalishaji mali
Mkuu, uzoefu wangu unaonyesha tofauti na haya unayoyasema. Mimi nilikwenda JKT, nilianzia Ruvu baadaye nikapelekwa Chita. Sikufundishwa chochote miongobni mwa hivyo ulivyoviorodhesha. Nilipokuwa Ruvu maafande walikuwa wanatupa mbinu za kuwaibia mayai ya kuku. Chita ilikuwa ni kama utumwa, watu 100 tulitakiwa kupalilia mpunga (kwa kung'oa magugu) kwenye shamba la ekari 100! CO aliomba dawa za kuua magugu (nadhani hicho ndicho kilimo bora) akanyimwa. bahati nzuri na yeye alikuwa mwelewa, akatuongoza katika mgomo wa kupalilia hadi madawa yalipoletwa, tena ilikuwa too late, hatyukuweza kupalilia hata robo ya mashamba tuliyokuwa tumepanda.Hiyo ndiyo JKT niliyopitia mimi, labda wewe mwenzetu una uzoefu tofauti
 
Mkuu, uzoefu wangu unaonyesha tofauti na haya unayoyasema. Mimi nilikwenda JKT, nilianzia Ruvu baadaye nikapelekwa Chita. Sikufundishwa chochote miongobni mwa hivyo ulivyoviorodhesha. Nilipokuwa Ruvu maafande walikuwa wanatupa mbinu za kuwaibia mayai ya kuku. Chita ilikuwa ni kama utumwa, watu 100 tulitakiwa kupalilia mpunga (kwa kung'oa magugu) kwenye shamba la ekari 100! CO aliomba dawa za kuua magugu (nadhani hicho ndicho kilimo bora) akanyimwa. bahati nzuri na yeye alikuwa mwelewa, akatuongoza katika mgomo wa kupalilia hadi madawa yalipoletwa, tena ilikuwa too late, hatyukuweza kupalilia hata robo ya mashamba tuliyokuwa tumepanda.Hiyo ndiyo JKT niliyopitia mimi, labda wewe mwenzetu una uzoefu tofauti
Nadhani unaongelea JKT iliyokuwa inakaribia kukata roho, yaani miaka ya mwisho ya 80 kuelekea 90. Mapungufu yapo na yataendelea kuwepo hata itakaporudishwa tena. Tunachelewa kuirudisha JKT iliyotupunguzia sana "maselule".
 
iliondolewa kwa sababu na sidhani inaumuhimu wa kuirudisha

pesa za kupeleka JKT wangeupgrade JWTZ na taasisi zinginezo za kiusalama
Ni kama nafikiri ingeweza kuwa recruiting ground ya vyombo hivyo nyeti vya usalama kwa sababu ya mchanganyiko mkubwa wa watu wenye haiba na mitazamo tofauti tofauti. Halafu kwa wengine it was a turning moment..they could discover other potentials they had which in some cases other environment could not reveal.
Kwa upande mwingine, ni nchi zipi bado zina utaratatibu kama wa JKT na zina benefit nini?
 
Tungetegemea wale waliopitia JKT ndo wawe mstari wa mbele kutetea maendeleo ya nchi yetu na kudhibiti UFISADI, lakini ndo wale wale waloshiriki kutuibia!!

All in All, muundo wa elimu ya secondary na vyuo umebadilishwa, wakati watoto wa masikini wakienda JKT, watoto wa wenye nazo wanawaingiza watoto wao vyuoni "direct entry" ndani ya nchi au nje. tayari tumepigwa bao!!!
 
Siungi hoja ya kurudisha JKT. Pamoja na kwamba inawafundisha vijana ukakamavu na kuleta mshikamano wa kitaifa, bado mazingira yetu kiuchumi na kiusalama kwa sasa haya halalishi uwepo wake.

Pendekezo langu badala ya kurudisha JKT, serikali yetu ianzishe Sports Academy za hali ya juu kila kanda za mikoa ya nchi yetu.

Tulifanya vibaya sana kwenye Olympics zilizopita. Tukiendeleza michezo yetu na kutengeneza mazingira ya kufaa, mafanikio yake naamini yatakuwa yenye manufaa makubwa kwa taifa letu kuliko hata hiyo JKT.

Otherwise, watumie fungu la pesa hizo kuwalipa mishahara inayostahili wana usalama wetu na kuendeleza miundo yao ya kazi kwa manufaa ya umma.

SteveD.
 
kuna umuhimu sana wa kurudisha jkt ambao ni kujenga utaifa, umoja na utamaduni ambao umeporomoka sana baada ya kufuta jkt.

Kwa wale amboa tumepitia jkt ukiacha ile karinyekarinye ukafanya uchambuzi "objectively" utaona jkt ilitujenga kwa kutufanya tuje kuwa raia wema na kujiona wote ni ndugu bila kujari umetokea familai gani, kabila gani, mkoa gani au una rangi gani.

I fully support reintroduction of jkt with minor improvements

so do i !!!
 
Nashauri hiki kinachoitwa JKT leo kiunganishwe tu na JW halafu kiwe ni kitengo cha PR kati ya JW na Raia. Wawe wanachukua watu wa kujitolea (volunteers) Kwa miaka kama miwili au mitatu. Volunteer wawe wanaingia waliomaliza kidato cha nne ila wamekosa nafasi za kuendelea (wengi wanakuwa hawajawa tayari kujitegemea mtaani). Hata drop-outs wa kidato cha sita na waliomaliza vyuo vyovyote ambao hawajapata ajira wawe wanachukuliwa. Wanaofanya vizuri wawe wanakuwa recruited katika majeshi mengine, Magereza, Polisi na JW kwenyewe. Wengine wawe wanapatiwa apprenticeship training katika fani mbali mbali tayari kwa kujiajiri wenyewe mitaani.

That will make sense.. Kuirudisha kwa style ya zamani haitasaidia hata kidogo. Wavu wa kuwaingiza watu huko una matobo mengi na itawaathiri watoto wa maskini tu. Nidhamu ya wakati ule haipo tena na JKT haiwezi kurejesha hiyo nidhamu.

Hata hivyo, ikiwa watu wote waliomo madarakani walipitia JKT, hatuuoni huo uzalendo unaopigiwa upatu hapa. Kwa hiyo tunaweza kusema wazi kuwa muda umetuthibitishia kuwa mfumo ule was a failure na hatuna sababu ya kuurejesha.
 
sidhani kama kuna umuhimu wowote, jamaa ana nyota ya kupendwa lakini siyo nyota ya kuleta mafanikio kwenye nchi. Kuna maswali mengi anatakiwa kujibu mwakani ndipo tumuweke kwenye uraisi, kama si hivyo, nakwambia robo tatu ya bunge itakuwa upinzani hata kama yeye atakuwa rais.
 
Back
Top Bottom