JKT Ruvu kama hamkuwa tayari kupokea watoto wetu kulikuwa hamna haja ya kusumbua wazazi

JKT Ruvu kama hamkuwa tayari kupokea watoto wetu kulikuwa hamna haja ya kusumbua wazazi

Naona unalilia na kulazimisha mtoto wako aende kupoteza muda
 
Nimeona wazazi wanalalamika kuwa watoto wao wamekataliwa kupokewa Hapo JKT Ruvu. Nashauri kama JKT nao hawajielewi hawawezi jiendesha wapewe DP World tu waiendeshe. Hakuna kucheka cheka na watu kwa sasa.
Hakika tuwaombe hawa DP word watuendeshee jeshi letu. Watuletee na majasusi wa Rwanda kwa lengo la kuleta ufanisi kwa jeshi letu
 
Kwakweli kama unataka kujua kwamba Tz kila sekita imeoza njoo ujionee hapa jkt, jinsi wanavo pokea watu kwa kujuana, najuliza hu ndo uzalendo wa kufundisha watoto wetu, najutia kumpeleka ndg yangu hamna lolote rushwa, kujuana na majigambo, hi nchi muache mama awape wanao weza kutuletea faida kama jkt ni shida kiasi hiki, je zile sehemu nyeti kama bandari, TRA, uhamiaji, Tanapa, hapa nimejifunza kitu sana.
sisi tukisema kuwa hii nchi inahitaji wawekezaji walio serious tunaonekana wadini. ila ukitaka kujua tabia za watanzania fanya kazi selikalini yaani watu hawapo serious na kazi wanawaza kuiba tu.
 
Jeshi haliendeshwi kisiasa km hyo serikali yenu ya kijiji, huku ni nidhamu tu, mwisho ulikuwa tar 11.06.2023.
Nani kakwambia jeshi haliendeshwi kisiasa au umekaririshwa na wewe umekariri? huyo CDF anapokea maelekezo kutoka kwa mwenyekiti wa CCM na kawekwa kwenye hiyo nafasi ya mkuu wa majeshi na mwenyekiti wa ccm
Na maelekezo yote anapokea kutoka kwa mwenyekiti wa ccm huku anampigia salute kama amiri jeshi mkuu.
akipigiwa simu moja tu ni kutii amri bila kuuliza chochote unasemaje haliendeshwi kisiasa?
 
Inakera inakera kweli kweli wanafunzi wamesafiri kutoka mikaoni tangu jana ku report Jkt kwa mjibu wa sheria, wamefika alfajiri mna wakata eti wame chelewa mwisho ulikua jana saa sita usiku, nani asie jua usumbufu wa usafiri hapa nchini mtu atoke Geita una tegemea kufika Dar siku hiyo hiyo kweli?

Kama nafasi zomesha uzwa tuambieni watoto tuwatumie nauli warudi makwao kuliko kuka getini tangu alfajiri, hi nchi ina matatizo kweli kweli kila sehemu na hilo mpaka mtu ajuane na kiongozi wa juu ndo mwanae apokelewe viongozi ni wasumbufu bora wawekezaji weje tu.
Mkuu kuwa mkweli
Mtoto amechelewa kutoka nyumbani
Nchi hii hakuna mkoa unaoweza kusafiri siku nne kufika Pwani hata kama shida ya usafiri,hakuna kitu cha namna hiyo,
Changamoto ya usafiri imeambatana na yeye kijana kuchelewa kupewa nauli
 
Kamchukue, yaani mfuate mrudishe nyumbani.

Mwaka ule alienda binti yangu huko mlale alirudi amekonda hadi kichwa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ukitoka Jkt lazima ukondee, wengine walilia baada ya kuwaona watoto wao km skeleton.
 
Jeshi haliendeshwi kisiasa km hyo serikali yenu ya kijiji, huku ni nidhamu tu, mwisho ulikuwa tar 11.06.2023.
Kiongozi wenu mwanasiasa halafu unaongea utopolo hapa. Nafasi zimeuzwa, sababu zinatafutwa tu hapa Full stop.
 
Jeshi haliendeshwi kisiasa km hyo serikali yenu ya kijiji, huku ni nidhamu tu, mwisho ulikuwa tar 11.06.2023.
Nidhamu huwezi mfundisha mtu kabla hujakaa naye. Wamekwenda kufunzwa nidhamu ukiwafukuza hutimizi lengo. Usihusishe complications na nidhamu
 
kwani mlikuwa wapi hadi mnaenda jana???? aisee hata mimi nilizuiliwaa getini boraa ningerudi nyumbani tuuu..
 
Mkuu kuwa mkweli
Mtoto amechelewa kutoka nyumbani
Nchi hii hakuna mkoa unaoweza kusafiri siku nne kufika Pwani hata kama shida ya usafiri,hakuna kitu cha namna hiyo,
Changamoto ya usafiri imeambatana na yeye kijana kuchelewa kupewa nauli
Ndo akatazwe kuingia, wangapi wanachelewa shule wangapi wanachelewa kazini, waseme tu nafasi wamesha ziuza kwa wengine walio kosa nafasi au walio pangiwa Bush, hi nchi ina uwozo kila sehemu.
 
Nidhamu ni nguzo ya kati jeshini, nidhamu ni pamoja na kuitikia wito kwa wakati.
Kwamba kruta anatoka mbali hiyo sio hoja, angeanza safari mapema.
 
Ndo akatazwe kuingia, wangapi wanachelewa shule wangapi wanachelewa kazini, waseme tu nafasi wamesha ziuza kwa wengine walio kosa nafasi au walio pangiwa Bush, hi nchi ina uwozo kila sehemu.
Jeshi sio shule wala kazini na ndio maana hakuna mtu ndani ya Jamhuri ya TZ anayeajiriwa jeshini.
Hizo unazosema ni akili za uraiani ambazo huwa zinafutwa mara moja jeshini
 
Jeshi sio shule wala kazini na ndio maana hakuna mtu ndani ya Jamhuri ya TZ anayeajiriwa jeshini.
Hizo unazosema ni akili za uraiani ambazo huwa zinafutwa mara moja jeshini
Pale ni jeshi au mgambo, usichanganye jkt walinzi na jwtz. Wewe ulishawahi kuona jeshi linalo fundishwa miazi mitatu tu.
 
Bora arudi tu maana huko mungu ndo anajua mm nilikuwa kambi moja nilitamani nitoroke usku wa manane
 
Nimeona wazazi wanalalamika kuwa watoto wao wamekataliwa kupokewa Hapo JKT Ruvu. Nashauri kama JKT nao hawajielewi hawawezi jiendesha wapewe DP World tu waiendeshe. Hakuna kucheka cheka na watu kwa sasa.
Tangazo lao liliorodhesha vifaa vifuatavyo
1. Bukta ya rangi ya 'dark blue' yenye mpira kiunoni, iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini, isiyo na zipu
2. T-shirt ya rangi ya kijani (green vest)
3. Raba za michezo zenye rangi ya kijani au blue
4. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari
5. Soksi ndefu za rangi nyeusi
6. Track suit ya rangi ya kijani au blue
7. Nyaraka zote zinazohitajika katika udahili wa kujiunga na Elimu ya juu, zikiwemo cheti cha kuzaliwa, vyeti vya kuhutimu kidato cha nne nk
Hata hivyo baada ya kufika kambini vijana katika baadhi ya kambi wameambiwa tangazo lililotoka halihusu kambi hilo hivyo wenyewe wana utaratibu wao wakaelekezwa wahakikishe vitu vifuatavyo vinapatikana haraka kama
1. Buti za maji au mvua (gum boot)
2. Mchango wa rambi rambi
3. Pesa ya matumizi
4. Rasketi ya kubebea vifaa
5. Pesa ya kwenda saluni!!
6. Karatasi na vifaa vingine vya stationery
7. Picha
8. Vitu vingine lukuki

Maswali yanaibuka kutoka kwa wazazi
1. Je, kwanini serikali imeitisha vijana wote waliomaliza kidato cha sita kwenda JKT kwa mjibu wa sheria huku wakiwabebesha gharama zote za vifaa vya kutumia wakati wana bajeti kwa ajili ya programu hiyo ya uzalendo?
2. Kwanini serikali kupitia jeshii la kujenga taifa ilitoa tangazo ambalo halijabeba mahitaji kwa kila kambi badala ya kuacha vijana mpaka wafike kambini kisha wapate usumbufu? Si bora wangeteua makundi kwa zamu kwa kulingana na uwezo wa kuwahudumia badala ya kuwabebesha wazazi gharama kwa masuala ambayo serikali ndio inataka kujenga maadili na uzalendo wa kizazi cha vijana wa sasa?
3. Je, serikali haijabaini kwamba vijana walioitwa kwa mafunzo hayo kiakili hawatakuwa sawa maana wanahisi wananunua kile watakacho funzwa hivyo hawatokuwa tayari kutumia kwa hiari mpaka walipwe pesa wakimaliza?

Mwisho
1. Serikali kupitia jeshi letu ambalo limejaa wataalamu wenye weledi wa kutosha tafadhali toeni wa mafunzo hayo bila kuwabebesha wazazi gharama zinazowaumiza kiasi ambacho kinawafanya walalamike na kuona hakuna faida yoyote vijana wao kwenda JKT
2. Utofauti wa mahitaji ya vifaa katika kila kambi ubebwe na serikali maana ndio waliowaita maana wazazi wao ni walipa kodi kodi wazuri hivyo waangalia jinsi bora ya kuendesha mafunzo hayo pasipo kusababisha mfadhaiko wa kisaikolojia

Nimewasilisha maoni haya kama mdau wa JKT niliyewahi kutumikia kwa mjibu wa sheria mwaka mzima miaka ya 80s ambapo tuliyafaidi kwa kupata mafunzo yaliyo bora yaliyotuwezesha kuwa mabingwa wa 'justle' katika changam,oto yoyote inayojitokeza maishani bila kukata tamaa.

MAJUKUMU MEMA jeshi la kujenga taifa.
 
Back
Top Bottom