Job Ndugai: Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Job Ndugai: Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Mpaka Muda huu ilitakiwa Katibu Mkuu wa Bunge ajiuzulu Kama aliendelea kumlipa Mtu Mshahara wakati hayupo eneo la Kazi Na Hakuna taarifa yoyote ya kimaandishi ya kutokuwepo kazini Na Sasa hivi anaonekana anazurura Kwenye Channel Za Kimataifa anachafua Nchi
Anachafuaje nchi iliyokwisha kuchafuliwa na serikali iliyoko madarakani? Anyway, hata katika hili la mshahara sheria itachukua mkondo wake!
 
Nimefanya utafiti mdogo kupitia maisha ya Mbunge Tundu Lissu kupitia maisha yake tangu ashambuliwe kwa risasi na watu wasiojulikana. Matibabu yake sasa yanakaribia Bilioni moja.

Jambo jingine ni kuwa kupitia interviews zake anazofanya na vyombo vya habari vya kimataifa kuonyesha kwamba, mambo hayapo sawa Tanzania, hasa kukosekana kwa demokrasia na haki za binadamu, akiweza kuishawishi Jumuiya ya Kimataifa kusitisha misaada kwa nchi yetu, huenda tukakosa asilimia 40% ya pesa ambazo hupata kutoka mataifa shirika, na hivyo kukosa karibu shilingi trillion 13.

Kwa hesabu rahisi ni kwamba thamani ya uhai wa Tundu Lissu ni 13 trillion + 1 billion.
 
Kuna kitu watu hamkielewi bado,na sijui shida iko wapi,Yani bado mnaamini hizi ni order za spika bado?Tuwe serious kidogo.
There is a third part in this drama.
Ila Spika akisimamisha mshahara wake ndio anamwagia petrol kwenye moto,bora akae kimya tu.
The genie is out of the bottle
 
Kwa hiyo huko nyuma mlikokua mkimlipa mshahara kulikua na barua ya daktari aliyo waandikia? Au ni sasa hivi mmeitaka barua japo hamjawahi kuwa nayo moja kwa sababu tu Lissu anaongea ukweli wa kile watesi wake walichomfanyia?
Sasa hivi hamuongei na Lissu kama Lissu maana kwa zile risasi 16 zilizomwingia mwilini huyu angepaswa awe ni marehemu.
Sasa mnaongea na malaika yule aliyemkinga Lissu na ni kwa kusudi maalum. Atawatesa sana maana yeye hajui uongo ila kweli tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hajashiriki gharama za matibabu sembuse Mshahara...dawa imeingia mpaka imemchanganya...hii straight talk imewaumiza wengi
 
Lissu kwasasa hana cha kupoteza, Mshahara kwake si kitu....

Yeye Ndugai kama Spika anapaswa kujua hali ya Lissu bila hata Lissu kumtaarifu.

Sent using Jamii Forums mobile app


Lunch ni kwa bill yangu kabisa. huyo ndugai alitakiwa kabisa ajue ratiba ya Lissu na stage zote za matibabu na siku za mazoezi alitakiwa awe anajua. ila kwa kuwa ni wa upinzani hataki kujua.

Amini nakuambia Ndugai kuna maisha baada ya uspika sidhani kama wewe una kinga ya kushatakiwa
 
Ipo haja ya kusimamisha mshahara wa Tundu Lissu kwa sababu hayupo jimboni, Bungeni na hospitalini na sijapewa taarifa ya Daktari

Swali toka kwa Mwanahabari Huru: Je -Waliompiga Lissu risasi wameshapatikaka?

-CCTV ulishawai kuhoji nani amezitoa?

-Lissu alipigwa risasi akiwa Jimboni au kazini Hapo Dodoma?

Ukiwa kiongozi Ushabiki ni mbaya

=====================

Spika wa Bunge Bw.Job Ndugai amesema atasimamisha Mshahara na Malipo yote ya Mbunge wa Singida Mashariki Mhe.Tundu Lisu kuanzia mwezi huu kutokana ana Ofisi yake kutokuwa na Taarifa sahihi ya mahali alipo kwasasa na anachokifanya huko. Hii ina maana Lissu hatalipwa mshahara tena kuanzia sasa hadi pale Spika atakapojisikia.

#MyTake:
Hawa ndio wale Balozi Masilingi alisena wameumizwa sana na shambulio la Lissu. Yani waliumizwa sana lakini hawajahangaika kujua aliyeng'oa camera za CCTV. Waliumizwa sana wakaondoa ulinzi siku ya shamvulio la Lissu. Wakaumizwa sana lakini wakamnyima hela za matibabu ili afe, lakini Mungu akamuokoa kwa neema. Sasa wameumizwa sana wameamua kumsimamishia mshahara. Hivi bado tunahangaika kutafuta waliomshambulia Lissu kwa risasi?
Hawamjui Lissu vizuri. Wanafikiri anatafuta faida ya kifedha kama wao.
 
Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema kuna haja ya kusimamisha mshahara wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu kwa sababu hayupo bungeni, jimboni kwake wala hospitalini, na hajapewa taarifa zozote na daktari. #GlobalHabariUpdates.
1549533994699.png
 
Ukiona mshahara mesitishwa ujue ndio mwanzo wa Lissu ku-bid bye bye Bungeni. Pengine atasubiri kugombea urais ambao nao ni mawili kwa kuwa kuna mashaka iwapo atatimiza lengo hili maana E. N Lowasa, mwansiasa mwenye ushawishi mkubwa ndani na nje ya Chadema amekuwa kwenye maandalizi hayo hayo tangu 2015. Who knows, it could be such an unceremonious end of punch politics of Tundu Antipasi Magwai Lissu.
 
Back
Top Bottom