Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Haya maneno kaongea yeye???
Sasa 2025 itaamua. Mkitoa waliopo sawa. Waje watakaokuwa kazi yao kwenda kukopa endepo hiyo ndo namna ya kuendesha Nchi

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Ndugai nae kichwa cha mgogo hakina akili, leo ndio anashtuka deni ni kubwa?
Kama anajua nchi yetu imelemewa na madeni, angekataa kabisa kabisa mradi hatari wa Bagamoyo, ambao kwa historia za nchi za kiafrika, huo mradi utakuwa ni deni na mzigo mkubwa sana kwetu.

Mradi wa Bagamoyo, ni karibu $ 10 bil, sawa na tshs 23 trillions ambazo wawekezaji watawekeza, of which hatujui hatma yake kwa nchi yetu, narudia, kwa historia za nchi zote za Afrika, miradi kama hii imegeuka kitanzi na kaburi zao.

Mh. Speaker angejua deni kubwa, mradi kama huo wa Bagamoyo angekaa mbali nao.
 
Wanakumbuka Shuka Kumekucha ,endeleeni kugonga meza tu huko mjengoni.
CCM ilishapoteza dira kitambo sana.
 
Spika wa Bunge ameonya kitendo cha serikali kuendelea kutegemea mikopo kutoka nje kuendesha nchi kitu ambacho kimefanya deni la taifa kuwa kubwa maradufu "Ipo siku hii nchi itapigwa mnada,kopeni tu".

View attachment 2060343
Nchi hii ina ela ila inaishia mifukoni mwa watu na matumizi yasiyo na tija na bado wanataka watutoze ili tuendelee kugharamia lifestyle lao.
Just imagine sasa mawaziri wako dar badala ya dodoma, hivyo wana makazi dar na dodoma gharama nyingine hiyo ya kuendesha magari na makazi yao.
Ela nyingi inaishia kwenye mifuko yao
 
Spika wa bunge la jamhuri ya muungano JOB NDUGAI amedai kuwa kulingana na mwenendo wa deni la taifa kufikia trilion 70 ipo siku nchi ya Tanzania itapigwa mnada amenena maneno hayo baada ya kusema kwamba tozo zote zamiamala ya simu zilizopitishwa na bunge zilipitishwa kwa lazima kwani wananchi hawakuridhia kama inavyosema na baadhi ya wanasiasa.

Kwa maneno hayo naona kuna mambo yanaendelea huko Lumumba yapo mambo hayajakaa sawa ukiona spika anaanza kulalamikalalamika! Alianza kuhusiana na serikali kuhamia Dodoma kuwa kwa sasa kazi zote za serikali na makongamano zimerudishwa Dar-es-Salaam.

Mheshimiwa Ndugai popote ulipo nakwambia hivi wewe na viongozi wako mnaifanyia nini hii nchi mbona mnakaa mnalalamika lalamika wakati chama ni cha kwenu na chama chenu ndicho kimeunda serikali.?

=====

UPDATES;

=====

=> Watu wengi wanatulaumu sana, ninyi ndio Wasomi. Hebu fikiria, Juzi mama kaenda kukopa 1.3 Trilioni deni.

=> Na tuna majengo hivi sasa ya Madarasa, ya Vituo vya afya, ambayo yanajengwa kwa tozo. Hivi ipi bora? Sisi Watanzania wa miaka 60 ya Uhuru tuendelee kukopa na Madeni au tubanane banane hapa tujenge wenyewe bila madeni Makubwa yasiyoeleweka? Ni lini tutajenga wenyewe?

=> Tutembeze bakuri ndo heshima? na tukishakopa tunapiga makofi! Sisi wa kukopa kila siku?

=> Tukasema pitisha Tozo, anayetaka asiyetaka, pitisha Tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? Yupo wapi huyo Mjomba? Tukapitisha Tozo.

=> Sasa 2025 itaamua. Mkitoa waliopo sawa. Waje watakaokuwa kazi yao kwenda kukopa endepo hiyo ndo namna ya kuendesha Nchi.

=> Hivi sasa deni letu ni 70 Trilioni. Hivi ninyi si Wasomi? Is that healthy? Kuna siku nyi itapigwa mnada hii. Madeni Madeni Madeni

=> Bajeti yetu Trilioni 30, Trilioni 10 kati ya hizo kwa Mwaka tunalipa Madeni.

=> Tumeenda Kukopa 1.3 Trilioni, Tunapiga Makofi. Tunawapa Wazungu Trilioni 10 Mariba Matupu. Wanatufanya Sisi Mazezeta. Hela yako Mwenyewe. Anachukua hela yako, halafu anakupa Kidogo Unashangilia.

=> Toza fanya hivi, tujitegemee, Tusimame wenyewe. Kuna ubaya gani? Hata msomi anatupinga.
View attachment 2060338
Angefanya hata comparison kabla hajafanya conclusion hata na majirani wetu kenya.

Kenya deni la taifa na uwiano na GDP ni 67% na Tanzania ni 35%.

Hata mataifa makubwa yana madeni makubwa sana kama wafanyabishara wakubwa sana cha muhimu ni kuhakikisha kunakuwa na transparency na monitoring nzuri ya hiyo mikopo.
 
suluhisho ni lipi sasa kama yeye spika analalamika na yupo kwenye chombo kikubwa cha maamuzi bunge ambalo ni mhimili wa nchi ..bila shaka anajua wananchi wanaumia kiasi gani kwa makosa wanayo yafanya ifike mahala waangalie na wajue wananchi ndio wenye nchi sio watu wachache walioko kwenye power ata maamuzi wayapembue kikamilifu kwa mustakabali wa wananchi.
 
Kati ya hizo pesa za mikopo tunamdai BILION 26 na ushee zilizotumika kumtibia maradhi yake India na kumfanya kuwa mgonjwa ghali zaidi duniani anayetarajiwa kuingia kwenye kitabu cha Guiness book of world records

IMG_20210923_152851_094.jpg
 
Nchi hii ina ela ila inaishia mifukoni mwa watu na matumizi yasiyo na tija na bado wanataka watutoze ili tuendelee kugharamia lifestyle lao.
Just imagine sasa mawaziri wako dar badala ya dodoma, hivyo wana makazi dar na dodoma gharama nyingine hiyo ya kuendesha magari na makazi yao.
Ela nyingi inaishia kwenye mifuko yao
Hela ipo ila usimamizi sio mzuri! Tatizo linalotukwamisha ni usimamiz wa rasilimali zetu tumewapa madaraka watu wa hovyo!
 
Hakuna lolote, roho mbaya tu inawasumbua
Leo ndio mumeona deni kuwa kubwa?
Mama kaa chonjo watu wanajipanga ujueeee
 
Kati ya hizo pesa za mikopo tunamdai BILION 26 na ushee zilizotumika kumtibia maradhi yake India na kumfanya kuwa mgonjwa ghali zaidi duniani anayetarajiwa kuingia kwenye kitabu cha Guiness book of world records
Punguza kuwa Negative siku zote mkuu, wewe siku ukiigua ndugu na jamaa wakakuchangia ukapate matibabu wakikusema utajisikiaje.

Jaribu kutumia kichwa kufikiria sio kila kitu unaandika kwa kufikiria matako tu.
 
Ndungai Ndungai Ndungai, nimekuita mara ngapi? Umeamua sasa kutoka hadharani kumkabili Samia kuonyesha kuwa sasa Sukuma Gang mko tayari kwa mpambano? Shauri yenu
 
Aibu yake kageuka kuwa mpinzani ndani ya bunge lake mwenyewe.
Ndiyo wanavuna dhambi ya kuiba kura na kulifanya Bunge la kijani tupu lililosheheni vilaza kama kina Babu Tale na mazuzu wengine bila kuwasahau wale wahuni covid 19
 
Back
Top Bottom