Nchi hii ina ela ila inaishia mifukoni mwa watu na matumizi yasiyo na tija na bado wanataka watutoze ili tuendelee kugharamia lifestyle lao.Spika wa Bunge ameonya kitendo cha serikali kuendelea kutegemea mikopo kutoka nje kuendesha nchi kitu ambacho kimefanya deni la taifa kuwa kubwa maradufu "Ipo siku hii nchi itapigwa mnada,kopeni tu".
View attachment 2060343
Naye analalamika kama sisi. Ni sawa nchi haina bunge.Ina maana mikopo huwa haipati idhini ya bunge?
Angefanya hata comparison kabla hajafanya conclusion hata na majirani wetu kenya.Spika wa bunge la jamhuri ya muungano JOB NDUGAI amedai kuwa kulingana na mwenendo wa deni la taifa kufikia trilion 70 ipo siku nchi ya Tanzania itapigwa mnada amenena maneno hayo baada ya kusema kwamba tozo zote zamiamala ya simu zilizopitishwa na bunge zilipitishwa kwa lazima kwani wananchi hawakuridhia kama inavyosema na baadhi ya wanasiasa.
Kwa maneno hayo naona kuna mambo yanaendelea huko Lumumba yapo mambo hayajakaa sawa ukiona spika anaanza kulalamikalalamika! Alianza kuhusiana na serikali kuhamia Dodoma kuwa kwa sasa kazi zote za serikali na makongamano zimerudishwa Dar-es-Salaam.
Mheshimiwa Ndugai popote ulipo nakwambia hivi wewe na viongozi wako mnaifanyia nini hii nchi mbona mnakaa mnalalamika lalamika wakati chama ni cha kwenu na chama chenu ndicho kimeunda serikali.?
=====
UPDATES;
=====
=> Watu wengi wanatulaumu sana, ninyi ndio Wasomi. Hebu fikiria, Juzi mama kaenda kukopa 1.3 Trilioni deni.
=> Na tuna majengo hivi sasa ya Madarasa, ya Vituo vya afya, ambayo yanajengwa kwa tozo. Hivi ipi bora? Sisi Watanzania wa miaka 60 ya Uhuru tuendelee kukopa na Madeni au tubanane banane hapa tujenge wenyewe bila madeni Makubwa yasiyoeleweka? Ni lini tutajenga wenyewe?
=> Tutembeze bakuri ndo heshima? na tukishakopa tunapiga makofi! Sisi wa kukopa kila siku?
=> Tukasema pitisha Tozo, anayetaka asiyetaka, pitisha Tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? Yupo wapi huyo Mjomba? Tukapitisha Tozo.
=> Sasa 2025 itaamua. Mkitoa waliopo sawa. Waje watakaokuwa kazi yao kwenda kukopa endepo hiyo ndo namna ya kuendesha Nchi.
=> Hivi sasa deni letu ni 70 Trilioni. Hivi ninyi si Wasomi? Is that healthy? Kuna siku nyi itapigwa mnada hii. Madeni Madeni Madeni
=> Bajeti yetu Trilioni 30, Trilioni 10 kati ya hizo kwa Mwaka tunalipa Madeni.
=> Tumeenda Kukopa 1.3 Trilioni, Tunapiga Makofi. Tunawapa Wazungu Trilioni 10 Mariba Matupu. Wanatufanya Sisi Mazezeta. Hela yako Mwenyewe. Anachukua hela yako, halafu anakupa Kidogo Unashangilia.
=> Toza fanya hivi, tujitegemee, Tusimame wenyewe. Kuna ubaya gani? Hata msomi anatupinga.
View attachment 2060338
Kati ya hizo pesa za mikopo tunamdai BILION 26 na ushee zilizotumika kumtibia maradhi yake India na kumfanya kuwa mgonjwa ghali zaidi duniani anayetarajiwa kuingia kwenye kitabu cha Guiness book of world records
Magufuli alikopa kuliko wote kwa miaka mitano amekopa zaidi ya miaka 10 ya kikwete..
Sasa alikuwa anajitegemea kivipi?
Kujitegemea kupi wakati magufuli alikopa kuliko wote kwa miaka mitano tu alikopa kuliko miaka 10 ya kikwete..
Hela ipo ila usimamizi sio mzuri! Tatizo linalotukwamisha ni usimamiz wa rasilimali zetu tumewapa madaraka watu wa hovyo!Nchi hii ina ela ila inaishia mifukoni mwa watu na matumizi yasiyo na tija na bado wanataka watutoze ili tuendelee kugharamia lifestyle lao.
Just imagine sasa mawaziri wako dar badala ya dodoma, hivyo wana makazi dar na dodoma gharama nyingine hiyo ya kuendesha magari na makazi yao.
Ela nyingi inaishia kwenye mifuko yao
Hela ipo ila usimamizi sio mzuri! Tatizo linalotukwamisha ni usimamiz wa rasilimali zetu tumewapa madaraka watu wa hovyo!
Punguza kuwa Negative siku zote mkuu, wewe siku ukiigua ndugu na jamaa wakakuchangia ukapate matibabu wakikusema utajisikiaje.Kati ya hizo pesa za mikopo tunamdai BILION 26 na ushee zilizotumika kumtibia maradhi yake India na kumfanya kuwa mgonjwa ghali zaidi duniani anayetarajiwa kuingia kwenye kitabu cha Guiness book of world records
Sawa sawa😅Ngoja wasimamishe uchumi wao kwanza
Ila usiguse mfuko wake.Anaoneka kama anauchungu sana na taifa ila sasa.....
Sisiem ni chama cha wanafiki.Huyu jamaa mjinga tu, Sasa kama bunge hakukubaliana hoja ya nape ya kuundwa chomba cha kuchunguza madeni yatokanayo na mikopo kipindi cha magufuli tumweleweje??
Ndiyo wanavuna dhambi ya kuiba kura na kulifanya Bunge la kijani tupu lililosheheni vilaza kama kina Babu Tale na mazuzu wengine bila kuwasahau wale wahuni covid 19Aibu yake kageuka kuwa mpinzani ndani ya bunge lake mwenyewe.