Jogging pembeni ya barabara zinagharimu UHAI

Jogging pembeni ya barabara zinagharimu UHAI

Inahuzunisha sana adse ....hizi jogging ziangaliwe sana
 
Dah,hili kwakweli huwa ni changamoto,mimi ni muhanga pia wa kukoswa koswa na magari,kwani wakati mzuri wa kufanya mazoezi ya kukimbia huwa ni asubuhi au jioni,na mida hii mara nyingi kunakuwa na magari mengi sana barabarani,mfano,kuna magari unakuta ana taa moja tu,boda pia ni majanga mara nyingi katika kujihami na magari anakuja mpaka pembeni kabisa kwenye chaki,kuna magari yana overtake,hapa nadhani wanaokimbia watakuwa wananielewa nini huwa kinatokea,kuna boda nyingine hazina taa zenye mwanga wa kutosha,kuna wanaotembea na full light unaweza kumulikwa ukopoteza muelekeo,kuna boda zina beba mizigo mikubwa unaweza kuhisi yuko peke yake kumbe mzigo unatokeza pembeni,ni hatari sana kwakweli.Tatizo nchi yetu ina viwanja vichache sana vya kufanyia mazoezi,ukipiga hesabu za kwenda gym kila siku kwa uchumi huu wa kati si rahisi kwa wengi wetu,tumuombe tu Mungu atuepushe na ajali tunapokuwa kwenye mazoezi...
 
Mimi ni mkimbiaji sana sana jioni nashauri haya
1. Kimbia barabara zenye sehemu maalum ya watembea kwa miguu
2.Kimbia upande wa kulia wa barabara
3.Usikimbie wakati wa giza
4.Ukivaa headphone weka sauti ambayo ukiongea na mtu mnasikilizana au unasikia magari,honi etc
5.Ukiweza, epuka main roads, kimbia kwenye mitaa isiokuwa na magari mengi.

Binafsi huwa nakimbia Toure drive,Tanzanite bridge,Obama drive na mitaa ya ndani ndani Oysterbay na Masaki.
 
Ndugu zangu wafanya mazoezi pembezoni mwa barabara. Chukueni tahadhari hususani wakati wa alfajiri na jioni/usiku.

Nimepoteza rafiki wawili (mmoja Dar mwingine Mtwara) kwa ajali wakiwa mazoezini. Wameacha familia changa mno.

RIP
NB: Lipia gym uwe salama
Asaante kwa Uzi Juma1967 naomba kuchangia uzi kwa sababu mimi ni mdau mkubwa wa mazoezi hasa ya Jogging; Katika kufanya mazoezi hasa ya kufanya jogging ni vema sana kuchukua tahadhari kama ifuatavyo;

1. Kimbia upande wako wa kulia ili kuona kwa urahisi kinachokuja mbele yako.
2. vaa mavazi ya rangi inayoonekana kirahisi kama rangi ya Neon Green
3. Vaa reflectors Mikanda au Arms/Shoe Dim lights ambazo zitawaonesha watumiaji wengine wa barabara uwepo wako. hizi kwa Dar zinapatikana Swahili sweatshop pale Dar Free market, lkn unaeza agizia online kutoka nchi nyingie sio gharama sana.
4. Ikifaa usikimbie peke yako muda huo ili hata ikitokea dharura basi urahisi wa kusaidika uwepo.
5. Pendelea kukimbia route isiyo na magari mengi au route yenye barabara pana ingawa kwa baadhi ya sehemu hizi ni changamoto!!

pole sana kwa kuwapoteza friends, lkn kama wewe ni Mkimbiaji kuna Group la FAMILIA YA WAKIMBIAJI TANZANIA (FWT) ambayo inajumuisha wakimbiaji wengi Tanzania ambao tunasaidia katika Changamoto mbalimbali na tupo mbio kuanzisha FWT Foundation ambayo itasaidia kusomesha watoto wa wakimbiaji wenzetu wanapopatwa na Changamoto mbalimbali ikiwemo Kifo.

Kwa sasa hakuna Kiingilio chochote ukihitaji unaweza kuniona PM ukaja na Namba yako nikuunge kwenye Group la WhatsApp utakutana na taarifa zingine huko.

Pole sana Mkimbiaji kwa kupoteza Rafiki.
 
Ndugu zangu wafanya mazoezi pembezoni mwa barabara. Chukueni tahadhari hususani wakati wa alfajiri na jioni/usiku.

Nimepoteza rafiki wawili (mmoja Dar mwingine Mtwara) kwa ajali wakiwa mazoezini. Wameacha familia changa mno.

RIP
NB: Lipia gym uwe salama
Leo wakati natoka kwenye kibarua changu asubuhi nikiwa na rafiki yangu kituo cha vetenary nyuma kulikuwa na kundi la wanajeshi wamevaa nguo za kimichezo truck suit wakikimbia jogging nais ni wa jkt mgulani walitoka upande wa Tazara wakielekea sokota mim na mwenzangu tukavuka upande kutoka kulia kuelekea kushoto yaani kituoni kabisa na kusimama yule mwanajeshi kijana alikuwa kashika bendera nyekundu akiongoza kile kikundi alisimama ghafla na kutuambia rudi mara moja upande tuliotoka akituonesha kwa bendera "rudi haraka kabla sijakasirika atukubisha tukatoka upande wa kituoni na kurudi upande mwingine maana pembeni nliona kulikuwa na madimbwi ya maji lile kundi likapita baadae nikamuhuliza yule jamaa nliyekuwa nae kosa letu nin akasema akuna kosa uo ni ubabe wa kijeshi na tungebisha wangetutia aibu mbele ya abilia waliokuwa wamekaa kituoni
 
Binafsi huwa nakimbia Toure drive,Tanzanite bridge,Obama drive na mitaa ya ndani ndani Oysterbay na Masaki.
napigaga hiyo route Alhamis nikitokea Job maeneo ya Sokoine Drive, katika route ambazo ni nzuri kukimbia hiyo ya Toure ni moja wapo! anyway mjuba uje basi Jerusalem Children's marathon Kigamboni 23/07 baada ya hapo tukutane NBC tarehe 31/07 pale Dom.
#RUNFORbetterHEALTH #runyourpace
 
Kama unaweza bora ukimbie kwenye uwanja maalumu kama wa mpira, ulio karibu na makazi yako...ukiachana na ajali
huo moshi unaovutwa na wanamazoezi huku wanapumulia mdomo ni janga lingine
ni wazo zuri sana lakini kwa wakimbiaji ambao wamefanya mazoezi kama sehemu yao ya maisha ni ngumu kidogo maana, kuzunguka uwanja ukamilishe 10Kms aisee sio jambo dogo na ina bore sana imagine kila siku ufanye hivyo hadi ukamilishe target ya 200Km ya mwezi!!

Kukimbia ukiacha kuwa ni mazoezi pia ni adventure, so kila mara macho na ubongo vinataka ku explorer new look!
 
napigaga hiyo route Alhamis nikitokea Job maeneo ya Sokoine Drive, katika route ambazo ni nzuri kukimbia hiyo ya Toure ni moja wapo! anyway mjuba uje basi Jerusalem Children's marathon Kigamboni 23/07 baada ya hapo tukutane NBC tarehe 31/07 pale Dom.
#RUNFORbetterHEALTH #runyourpace
Ndani ya mwezi mmoja nimesikia matukio mawili moja limepelekea kupoteza maisha Kigamboni. Mmoja bodaboda imebeba geti ikamzoa, mwingine juzi nimesikia kagongwa na gari Ungindoni sijui anaendeleaje.
 
Ndani ya mwezi mmoja nimesikia matukio mawili moja limepelekea kupoteza maisha Kigamboni. Mmoja bodaboda imebeba geti ikamzoa, mwingine juzi nimesikia kagongwa na gari Ungindoni sijui anaendeleaje.
Yeah Tarehe 6/7 tulimpoteza mwenzetu mmoja hata hivyo yeye hakugongwa akiwa barabarani alikuwa amepakiwa kwenye Boda ambayo iligongwa na Mlevi mmoja akitoka misele yake town (Rest easy Dastan)

Yule aliyekatwa na gate kwa kweli sikuelewa sana maana hakuwa mwanachama wa kigamboni runners ila ninachosikia ni kwamba alikatwa na gate kifuani gate ambalo lilikuwa limebebwa na boda.

Wa Ungidoni aisee kwa kweli nadhani hakuna ukweli maana sisi kama Kigamboni Runnners Club inapotokea taarifa kama hiyo huifuatilia kwa kina lkn hadi sasa hatujabaini ukweli wowote!

hata hivyo kukimbia kwa taadhari bado ni jambo jema sana!!
 
Wanao kimbia barabarani wanafanya Show-Off wanajifanya wazungu Earphones masikioni na mbwembwe nyingine nyingi tu... Unatoka nyumban unaacha jirani yako kuna uwanja wa mpira kwanin usifanyie mazoez hapo..? Ila unataka ukakimbie barabarani dakika 10 urudi home...
😎 ILA UKWELI NI KWAMBA UKIONA MWANAUME ANAKIMBIA KIMBIA JIONI UJUE NGUVU ZIMEPUNGUA ANAJIBUSTI NGUVU ZIRUDI😂
Mazoezi ni afya mkuu. Si unaona mzee Mwinyi alivyofiti.
 
Huwajui bodaboda wewe. Kuna mmoja alipakia Geti kuzidi boda. Akamzoa mfanya mazoezi akamtupa mferejini
unaongelea ile ya kigamboni jamaa kaacha mke hata hawajazaa ndoa ya mwaka mmoja. mimi mwenyewe mtu wa jogging ila nako kaa hakuna migari mingi so mara nyingi nafanyia mazoezi uwanjani na mara chache sana barabara ya vumbi isiyokuwa na gari.
mazoezi muhimu asikwambaie mtu hasa ya asubuhi
 
Mimi ni mkimbiaji sana sana jioni nashauri haya
1. Kimbia barabara zenye sehemu maalum ya watembea kwa miguu
2.Kimbia upande wa kulia wa barabara
3.Usikimbie wakati wa giza
4.Ukivaa headphone weka sauti ambayo ukiongea na mtu mnasikilizana au unasikia magari,honi etc
5.Ukiweza, epuka main roads, kimbia kwenye mitaa isiokuwa na magari mengi.

Binafsi huwa nakimbia Toure drive,Tanzanite bridge,Obama drive na mitaa ya ndani ndani Oysterbay na Masaki.
Umehamia lini Oysterbay wakati tulikuwa tunaishi wote Buza.
 
Na vurugu zilivyo kubwa huku mijini, magari,pikipiki,baiskeli, wakimbiaji wanachangamana barabara moja hiyo hiyo, afadhali hata barabara zote zingekuwa na njia za watembea kwa miguu ila hamna, nimeshuhudia wengi wakilambwa pasi na magari, ni bora utafute barabara isiyokuwa na msongamano wa magari, pia kukimbia kwa kutumia upande wa kulia ni afadhali kidogo...
 
Kimbia in opposite direction na uelekeo wa magari,,kaa upande wa magari yanayokuja mbele yako
Jambo hili kiusalama ni muhimu sana lakini wengi hawalijui. Wakimbiaji na watembea kwa miguu wanapaswa kuwa upande wa kulia wa barabara, ili wayaone magari yaliyo karibu nao. Kutembea au kukimbia ukiwa kushoto ni hatari sana, kwani magari yatokayo nyuma yako mko nayo pamoja upende huo.
 
du ma
Umesema kweli kabisa. Dar maeneo mengi pembeni mwa barabara sio rafiki kwa jogging. Mimi muda wa jioni huwa nafanya mazoezi ya kutembea pembezoni mwa barabara na mara nyingi nimenusurika kugongwa. Barabara nyingi sehemu za waenda kwa miguu ndio packing hizo hizo, boda boda humohumo, hivyo kufanya jogging barabara za dar ni kuisogelea njia panda ya kuzimu
du hivi kutembea nako ni mazoezi,mimi huwa natoka kkoo mpaka gmboto kwa mguu,kukiwa na foleni kubwa ya daladala.
 
Back
Top Bottom