John Bocco aandaliwe kama golikipa wa akiba

John Bocco aandaliwe kama golikipa wa akiba

Hoja fukunyuku.

Sitegemei Simba kusajili kipa mwingine msimu huu. Nadhani wanafuatilia kwa ukaribu uponyaji wa Aishi Manula na naona kuna juhudi zinafanyika za kuboresha viwango vya Ally Salum na mwenzake Ferooz. Kwa sababu dirisha la usajili halijafungwa, maamuzi ya mwisho bado hayajafanyika.

Kuleta kipa kutoka nje halafu umlipe milioni 15 za kukaa benchi, huo utakuwa ni ufujaji wa fedha. Nafasi ya golikipa siyo ya kufanya rotation kwa hiyo tusitegemee Manula kuja kushea namba na mtu ila timu bado inahitaji uwe na kipa wa ziada wa gharama nafuu ambaye unaweza kumtegemea kwa asilimia fulani.

Safu ya mbele pale Simba sasa hivi haimpi nafasi tena John Bocco kucheza. Mimi nadhani kama tuko tayari, wamfanyie mazoezi ya ukipa awe msaidizi wa Salum/Ferooz hadi hapo Manula atakaporudi.

Bocco ana kimo na mwili mzuri kwa nafasi ya kipa. Akiwa tayari kuurusha na kuutupa mwili wake mara kwa mara kama majukumu ya kipa yanavyotaka, na kuongezewa uwezo wa kudaka, hili wazo linaweza kujaribiwa. Na huwa naamini ukiwa mshambuliaji, ni rahisi kucheza beki/kipa na kinyume chake pia maana unakuwa unajua uchezaji na ufikiriaji wa mtu wa nafasi hiyo.

Pia kwa haraka haraka naona kama Ferooz anaweza kuwa bora zaidi ya Salum ingawa sijawahi kumuangalia katika mechi. Akiongeza utayari, apewe nafasi.

ZIADA: Mwezi wa 2 niliwahi kutoa wazo la Israel Mwenda kuchezeshwa kama beki wa kushoto nikaonekana hamnazo lakini mwishoni mwa ligi alijaribiwa hiyo nafasi na hivi sasa Simba wanaamini wanaweza kweli kumtumia kwenye nafasi hiyo.
Hoja mzuri ila umemvunjia heshima Bocco
 
Ungesema tu kuna haja ya Simba ya kuwa na golikipa ingetosha sana na ningekuelewa/ tungekuelewa ila kumhusisha Bocco hapo umemvunjia heshima.. Maneno haya yangeandikwa na Utopolo ningeelewa ila wewe mshabiki/mpenzi/ mwanachama kindakindaki hapa Jf na hata huko mtaani...Nimeshangaa..labda Bocco mtani wako.
Kwa nini unadhani hivyo?
 
Ungesema tu kuna haja ya Simba ya kuwa na golikipa ingetosha sana na ningekuelewa/ tungekuelewa ila kumhusisha Bocco hapo umemvunjia heshima.. Maneno haya yangeandikwa na Utopolo ningeelewa ila wewe mshabiki/mpenzi/ mwanachama kindakindaki hapa Jf na hata huko mtaani...Nimeshangaa..labda Bocco mtani wako.
Dah sikuwa na nia hiyo kabisa. Ni nia njema kabisa. Mbona nafasi ya golikipa ni nafasi muhimu sana katika timu, inakuwaje inakuwa dharau? Ngoja nikuulize, kuna mpango gani wa kuwakuza kina Salim na Ferooz kama replacement ya baadae ya Manula au wataendelea kuwa makipa wa akiba maisha yao yote?

Kwa mtazamo wangu unapokuwa mchezaji unayeheshimika katika timu, utafanya kila uwezalo ili kuhakikisha timu inabaki imara. Ndiyo maana nikatoa mfano mimi nilipokuwa nacheza, nilikuwa naangalia sehemu gani katika timu ina mapungufu siku hiyo naenda kuicheza ile nafasi na naicover vizuri tu. Bocco siku hizi akiingizwa anaonekana kupambana sana kwa ajili ya timu ingawa mwili ndiyo hivyo unakataa, ndiyo maana nikatoa ushauri huo ajifue na afuliwe ili likitokea la kutokea, tusijikute Salim kama option pekee tuliyonayo. Kuna kitu kinaniambia ukiacha labda mwili wake kuwa umechoka, Bocco anaweza kuicover hiyo nafasi kuliko wengi tunavyodhani.

Vilevile kule mbele kumejaa, yaani miamba yote ile ituangishe?
 
Bado muda upo kwa wazo langu kufikiriwa. Mambo mengine yanahitaji tu kujiamini baasi
 
Back
Top Bottom