John Butler Walden (1939 - 2002) a.K.a ''Black Mamba''- A legend in the Tanzanian army (author unknown)

John Butler Walden (1939 - 2002) a.K.a ''Black Mamba''- A legend in the Tanzanian army (author unknown)

RIPs
General Abdallah Twalipo
Brigedier Chitete"Supersonic"
Kanali Yunus Abdallah
Mhandisi Brigedier R R R Rajab
Brigedier Lupembe
Kanali Lusimbi"Kamanda Radi"
Major General Silas Mayunga"Mti mkavu"
Brigedier Imran Kombe"Kamanda Ngono"
Brigedier Himid Mansour
Kanali Ferderico Nshimanyi
Brigedier Herman Lupogo

Hawa na wengine wana nafasi yao ktk historia ya nchi hii lkn wengi wao walikufa maskini baada ya kutoka vitani Uganda!Kwa sasa anayeifaidi Tanzania ni Riziwani Kikwete na Paul Makonda,vijana ambao HAWAIJAIFANYIA chochote Tanzania!!

Inauma sana!!
Sahihisho huyu sio kanali Lusimbi ni kanali Tumbi alipewa jina la kamanda radi kwa vile alikuwa mkuu wa kikosi cha mizinga.Mizinga yake ndio ilimtia Amini adabu kuna mahali waganda waliibatiza jina la sabasaba maana waliamini Nyerere ndio alikuwa akiifyatua tokea uwanja wa sabasaba Dar maana walikuwa wanashangaa mabomu yake yalikuwa yanawapata maadui tu sio raia
 
Nafahamu nyumbani kwake Iwambi Mbeya.
Mashujaa wetu hawa tuwaenzi kwa nguvu zetu zote.
Nimekaa naye pale mtaani sasa alikuwa ana majaribu balaa, mzee alikuwa anakushikisha msumari wa nchi sita anakwambia weka kichwani ushikirie halafu anaenda umbali kama mita 15 hivi anachukua bastola yake anafyatua halafu analenga tu msumali utasikia kriiiiiii msumali haupo mkononi!!!!alikuwa na shabaha ajabu!! Basi bwana tulifaidi nyama pori akiendaga kuwinda anarudi na minyama anagawa pale jirani aaaah mungu mlaze mahala anapostahili!!
 
Ngongo,
Hiyo taazia/makala sikuandika mimi.
Mwandishi simjui lakini nimeomba jina lake.

Nimeikuta kwenye group yetu moja nika CnP.
Kihiyo mie nitaandika nini cha maana kaka?
Hongera sana kwa historia hii sikutegemea nawe waweza kuandika vitu vyenye mashiko,Tumezoea kukuona ukikomalia UDINI tu,Hongera sana!!!!
 
Hongera sana kwa historia hii sikutegemea nawe waweza kuandika vitu vyenye mashiko,Tumezoea kukuona ukikomalia UDINI tu,Hongera sana!!!!
Echolina,
Hakuna udini wowote katika yale ninayoandika.
Ninaandika historia kueleza mambo kama yalivyotokea.

Ikiwa wewe unaona huo ni Uislam basi ni bahati mbaya.
Hiyo makala sikuandika mimi nilichofanya ni kuandika
utanguliza wake.
 
Echolina,
Hakuna udini wowote katika yale ninayoandika.
Ninaandika historia kueleza mambo kama yalivyotokea.

Ikiwa wewe unaona huo ni Uislam basi ni bahati mbaya.
Hiyo makala sikuandika mimi nilichofanya ni kuandika
utanguliza wake.
Bwana Mkubwa Uislamu umeutaja wewe mimi sikusema hayo lakini nazidi kukupa Hongera kwa kuiandika vizuri sana historia ya Mwanajeshi mwenzangu vizuri sana,uandishi kama huo ndiyo tunaoutaka hapa maana unaelimisha jamii nzima bila kujali itikadi.
 
Huyu jamaa sio yule alikuwa anaishi nyumba fulani maeneo ya chang'ombe umuhimu, alikuwa mwanajeshi na alikuwa na watoto kama wazungu wazungu fulani, na hata yeye alikuwa chotara, ila labda TPDF machotara walikuwa wengi
 
Huyu jamaa sio yule alikuwa anaishi nyumba fulani maeneo ya chang'ombe umuhimu, alikuwa mwanajeshi na alikuwa na watoto kama wazungu wazungu fulani, na hata yeye alikuwa chotara, ila labda TPDF machotara walikuwa wengi
Ndio maana hawakubaguliwa na waliaminiwa kwamba nao ni Watanzania. Ilikuwa Tanzania ya Watanzania wote ndio maana hata Brayson alikuwa Kinondoni na hakuna aliyembagua siku hizi utanzania na uzalendo ni rangi. (sakata la Manji na kunyang'anywa udiwani!!!)
 
Bwana Mkubwa Uislamu umeutaja wewe mimi sikusema hayo lakini nazidi kukupa Hongera kwa kuiandika vizuri sana historia ya Mwanajeshi mwenzangu vizuri sana,uandishi kama huo ndiyo tunaoutaka hapa maana unaelimisha jamii nzima bila kujali itikadi.
Echolima,
Utakuwa mtu wa ajabu sana katika utafiti wangu kwani kinachosemwa
''udini,'' ni pale Uislam unapoonekana.

Nilikuwekea hiyo kwa makusudi nikutoe ulikojificha.
Makala hiyo sikuandika mie mimi nimeandika utangulizi.
 
RIPs
General Abdallah Twalipo
Brigedier Chitete"Supersonic"
Kanali Yunus Abdallah
Mhandisi Brigedier R R R Rajab
Brigedier Lupembe
Kanali Lusimbi"Kamanda Radi"
Major General Silas Mayunga"Mti mkavu"
Brigedier Imran Kombe"Kamanda Ngono"
Brigedier Himid Mansour
Kanali Ferderico Nshimanyi
Brigedier Herman Lupogo

Hawa na wengine wana nafasi yao ktk historia ya nchi hii lkn wengi wao walikufa maskini baada ya kutoka vitani Uganda!Kwa sasa anayeifaidi Tanzania ni Riziwani Kikwete na Paul Makonda,vijana ambao HAWAIJAIFANYIA chochote Tanzania!!

Inauma sana!!
Mkuu Kwanini General Imran Kombe aliitwa kamanda ngono ??
Pia naomba kujua wasifu wake binafsi: Alikuwa ni mtu wa aina gani.
 
Huyu jamaa sio yule alikuwa anaishi nyumba fulani maeneo ya chang'ombe umuhimu, alikuwa mwanajeshi na alikuwa na watoto kama wazungu wazungu fulani, na hata yeye alikuwa chotara, ila labda TPDF machotara walikuwa wengi
Yeah TPDF imekua na machotara wengi .....wengi toka Iringa ..ambako kuna jamiii hiyo pia yumo.

Maj Gen Louis ambaye alifariki akiwa mkuu wa utumishi jeshini ,a very brave commander
Mdogo wake alikuwa fighter jet Pilot
Col(brig gen) aloyce louis

Capt zacharia Hans Pope (huyu baba yake alikuwa SACP Hans Pope alikufa vitani wakati uvamizi ulipotokea na majeshi ya Amin yakachukua maiti yake eti ushahidi kuwa Nyerere anasaidiwa na Cuba ,,
UGANDA ilipokombolewa maiti yake ni kati ya ambazo zilikutwa State Reseach Bureau zikiwemo.za wapinzani wa amin na maofisa usalama jeshi wa tanzania ambao bahati mbaya waligundulika na kutekwa na SRB) na wengine
Chotara wa Kihindi col Kashmir ambaye at one point alikuwa the second most senior wakati wa brig gen sarakikya (gen)....na kuna hisia kuwa hakupewa u.gen kwakua tu ni muhindi na mwalimu alimpatia kazi...nyingine,naona bado kulikua na hisia za afrikanization

Kuna kitu TPDF wanatakiwa kufanya kwenye usaili ili huhakikishai linaendelea kuvutia minority races kama machotara kujiunga na jeshi...kwa heshima ya utumishi wa mashujaa kama hawa..ni muda mrefu sijaona machotara cadets
 
Labda tunaweza kusema zipo sababu kuu mbili.

Mosi ,General Kiwelu alitoka kanda ya Kaskazini Mkoa wa Kilimanjaro.Ikumbukwe wakati wa utawala wa Mwl maafisa wa jeshi waliotokea Kanda ya Kaskazini waliondolewa jeshini kwa tuhuma za kutaka kupindua serekali.General Sarakikya Mirisho alikuwa Mkuu wa majeshi wakati huo alipelekwa Nigeria kama Balozi,Capt Mushi alipelekwa Arusha kama General Manager Fiberboard Arusha,Col Metili sikumbuki vizuri kama alikwenda Mkonge au KAMATA shirika la mabas ya taifa na wengine wengi waliondolewa jeshini.

Wakati wa vita ya Kagera (Uganda na Tanzania) General Kiwelu aliandaa mipango ya kivita kabla ya kurejeshwa makao makuu.Wakati wa kipindi chote cha maandalizi aligoma kumpatia taarifa Waziri Mkuu wakati huo Edward Moringe Sokeine lini majeshi yetu yangevuka mpaka kuelekea Uganda (Mto Kagera).Kwa mujibu wa nukuu yake mwenyewe Sokoine alishangaa na kuuliza hata mimi (Waziri Mkuu) nafichwa taarifa za kivita.Nadhani watawala waliofuta walitishwa na ujasiri wa General Kiwelu iwapo angepewa ukuu wa majeshi labda ingekuwa vigumu kumdhibiti/kumpeleka peleka.
Ni kweli Tumainieli Kiwellu alikuwa na.mmoja wa makamanda wa juu wasomi wakati huo pamoja na wengine kama lt gen martin mwakalindile

Wakati CDF wa kwanza na mwanzilishi wa TPDF BRIG GEN saarakikya anaondolewa ..ile ilikua fitna na aliondoshwa na maofisa wa juuu akiwamo Kanali kashmir ,ambaye watu wengi wanaamini anastahiki hupewa.u.brig gen angalau kwa heshima...kama sarakikiya alivyopewa ungen baada ya kustaafu, pia alikuwapo Kanali Marealle,maj.chuwa ,..na wengine wengi ila baadaye iligundulika walipigwa tu fitna na Waziri wa Ulinzi Kawawa ambaye naye huenda alipewa taarifa za uongo ...baadaye wote Mwalimu aliwatafutia kazi...nzuri na waliitwa kusaidia miakakati wakti wa vita na hata kwenda mbele

GENEREALI tumainieli kiwelu kwa...kutambua mchango wake ndiye kamanda pekeee full general ambaye hakuwahi kuwa mkuu wa majeshi ....na ndiye pekee ambaye amekuwa CHIEF OF STAFF mara mbili kwa nyakati tofauti chini ya Musuguri na baadaye wakati wa KIARO
 
Mkuu Kwanini General Imran Kombe aliitwa kamanda ngono ??
Pia naomba kujua wasifu wake binafsi: Alikuwa ni mtu wa aina gani.
niliwahi kuambiwa aliitwa kamanda ngono kwakuwa aliongoza vikosi vya jwtz kuvuka mto ngono huko kagera,
imran kombe alikuja kuwa mkuu wa idara ya usalama wa taifa mpaka umauti ulipomkuta mwaka 1996 alipouwawa kwa bahati mbaya mjini moshi baada ya kudhaniwa ni jambazi sugu...
 
niliwahi kuambiwa aliitwa kamanda ngono kwakuwa aliongoza vikosi vya jwtz kuvuka mto ngono huko kagera,
imran kombe alikuja kuwa mkuu wa idara ya usalama wa taifa mpaka umauti ulipomkuta mwaka 1996 alipouwawa kwa bahati mbaya mjini moshi baada ya kudhaniwa ni jambazi sugu...
Mkuu hilo la Usalama wa Taifa naljua vizuri. Ninachotaka kujua ni kwamba aliiongozaje ile Idara ya Usalama wa taifa ? Nguvu zake kiuongozi zilikuwaje ?
 
Jeshi lilikuwa na mashombeshombe kadhaa enzi za mwalimu...na walikuwa na ka urafiki fulani...hata huyu nilimjua thru shombe shombe mwingine mjeshi, alikuwa jirani etu....ila ukiuliza kwao utasikia Iringa na mikoa mingine ya Kusini...

Ndio tujue sasa uzalendo si rangi...
 
Back
Top Bottom