Pre GE2025 John Mnyika aeleza mikakati ya CHADEMA kukabiliana na Orodha Haramu ya Wapiga Kura Wasiokuwa Halali

Pre GE2025 John Mnyika aeleza mikakati ya CHADEMA kukabiliana na Orodha Haramu ya Wapiga Kura Wasiokuwa Halali

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika, ameeleza kuwa chama hicho kimejipanga vema kukabiliana na kile alichokieleza kama dhamira ovu ya kuhamisha orodha haramu ya wapiga kura wasiokuwa halisi. Mnyika amedai kuwa mbinu hii inatekelezwa kupitia mtandao wa mabalozi, ambao wamewekewa kikanuni kwamba waandikishaji ni watumishi wa umma.

Ameonya kuwa baadhi ya watumishi wa umma wasio waadilifu wanaweza kushawishiwa na mbinu hizi haramu kwa lengo la kuwahamisha wapiga kura wasio halali na kuwaingiza katika daftari la wapiga kura.

Kwa kukabiliana na hali hiyo, Mnyika amesema kuwa CHADEMA itakuwa na mawakala wao katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya kuhakikisha uangalizi wa karibu na kuhakikisha haki inatendeka.

Mnyika: Tukitaka kuongeza idadi ya wapiga kura imani katika mifumo ya uchaguzi iongezeke
Mnyika aitupia lawama TAMISEMI, adai ni Mpango wa CCM na TAMISEMI kutohamasisha Uandikishaji wa Wapiga Kura
Vyama vya siasa hamasisheni wapiga kura wenu wajitokeze kujiandikisha au kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la mpiga kura.
Jaji Mwambegele: Mawakala wa Vyama vya Siasa wataruhusiwa kuwepo katika Vituo vya Kuandikisha Wapiga Kura
 
Mnajidanganya tu hamna manpower ya kutosha kudhibiti hilo kwanza nani kawaambia watu wanampango huo mnashindwa kuhamasisha wanachama wenu wajiandikishe kwa wingi mnaanza kutafuta sababu wakati watu wenu hawajiandikishi kupiga kura
 
Nyie jikiteni kwenye chaguzi za ndani na kujifungia makanisani wakati CCM walikuwa busy kuhamasisha wanachama wao na wakereketwa subirini kitu kizito cha kichwa tuuuuuumh nyota nyota!
 
Nyie jikiteni kwenye chaguzi za ndani na kujifungia makanisani wakati CCM walikuwa busy kuhamasisha wanachama wao na wakereketwa subirini kitu kizito cha kichwa tuuuuuumh nyota nyota!
Punguani wahed.
 
Tutahakikisha hamfurukuti wajinga nyie!
Tukiamua kura tutazipigia na kuzihesabu maporini
1000012666.jpg
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mnyika, ameeleza kuwa chama hicho kimejipanga vema kukabiliana na kile alichokieleza kama dhamira ovu ya kuhamisha orodha haramu ya wapiga kura wasiokuwa halisi. Mnyika amedai kuwa mbinu hii inatekelezwa kupitia mtandao wa mabalozi, ambao wamewekewa kikanuni kwamba waandikishaji ni watumishi wa umma.

Ameonya kuwa baadhi ya watumishi wa umma wasio waadilifu wanaweza kushawishiwa na mbinu hizi haramu kwa lengo la kuwahamisha wapiga kura wasio halali na kuwaingiza katika daftari la wapiga kura.

Kwa kukabiliana na hali hiyo, Mnyika amesema kuwa CHADEMA itakuwa na mawakala wao katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya kuhakikisha uangalizi wa karibu na kuhakikisha haki inatendeka.

Mnyika: Tukitaka kuongeza idadi ya wapiga kura imani katika mifumo ya uchaguzi iongezeke
Mnyika aitupia lawama TAMISEMI, adai ni Mpango wa CCM na TAMISEMI kutohamasisha Uandikishaji wa Wapiga Kura
Vyama vya siasa hamasisheni wapiga kura wenu wajitokeze kujiandikisha au kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la mpiga kura.
Jaji Mwambegele: Mawakala wa Vyama vya Siasa wataruhusiwa kuwepo katika Vituo vya Kuandikisha Wapiga Kura
Yeye na Chadema yake wanapoteza muda wao bure kabisa.
CCM kuendelea kubaki madarakani au kushinda uchaguzi wa siasa hapa Tanzania haitegemei kupigiwa kura na mtu yoyote yule.
 
Yeye na Chadema yake wanapoteza muda wao bure kabisa.
CCM kuendelea kubaki madarakani au kushinda uchaguzi wa siasa hapa Tanzania haitegemei kupigiwa kura na mtu yoyote yule.
Good thinking, kwasasa kwa mfumo uliopo wa uchaguzi hakuna chama cha siasa kinaweza kuiondoa CCM madarakani
 
Hivi hawa sisiemu hawawezi kufanya uchaguzi bila wizi? Kila uchaguzi lazima wafanye mikakati ya wizi wa kura ,wao si wanajenga barabara,wanaleta maendeleo ,wanafanya mambo makubwa hadi wananchi wanawakubali ,sasa wizi wa kura wa nini?
 
Hivi hawa sisiemu hawawezi kufanya uchaguzi bila wizi? Kila uchaguzi lazima wafanye mikakati ya wizi wa kura ,wao si wanajenga barabara,wanaleta maendeleo ,wanafanya mambo makubwa hadi wananchi wanawakubali ,sasa wizi wa kura wa nini?
Bora wapinzani wangesusia tu huu uchaguzi maana huko mbeleni ni kilio tu

Ova
 
Back
Top Bottom