CHADEMA
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 490
- 2,471
Mbunge wa Kibamba kupitia CHADEMA, John Mnyika kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Twitter amesema kuwa Chadema Mdude amechukuliwa na Watu wenye silaha
Aidha, yeye mwenyewe amesema CHADEMA inafuatiloa suala hilo na taarifa zaidi itatolewa muda si mrefu
======
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA ZA AWALI KUHUSU TUKIO LA MDUDE NYAGALI (MDUDE CHADEMA)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), katika hali ya dharura, kinafuatilia kwa karibu, taarifa za Mdude Nyagali (Mdude Chadema) kuvamiwa kisha kuchukuliwa na watu ambao hawajatambulika, akiwa ofisini kwake, eneo la Vwawa, Mbozi, mkoani Songwe, katika tukio lenye dalili za utekaji.
Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda, majira ya jioni ya leo (saa 12 kuelekea saa 1) yalifika magari mawili katika eneo la ofisini kwa Mdude, Vwawa mjini, kisha wakatelemka takriban watu wanne, ambao walimkamata kijana mmoja aliyekuwa nje ya ofisi hiyo wakampeleka kwenye mojawapo ya magari waliyokuja nayo huku wengine wakiingia ndani ya ofisi, alikokuwa Mdude.
Imedaiwa kuwa baada ya muda mfupi kulisikika purukushani, watu hao wakijaribu kumkamata Mdude huku wakimpiga na yeye akipiga kelele za kupinga kitendo hicho na kuomba msaada.
Taarifa za awali ambazo Chama kimezipata kutoka kwa mashuhuda hao zimedai kuwa baada ya kusikika kwa purukushani na kelele hizo, baadhi ya wananchi walijitokeza kutaka kujua kinachoendelea na kutoa msaada, ghafla watu hao waliokuwa wakimpiga Mdude wakatoa silaha aina ya bastola na kuwatishia wananchi hao, kitendo kilichowaogofya wananchi na kukimbia kwa hofu. Imedaiwa kuwa watu hao walimuingiza Mdude kwenye 'buti' ya mojawapo ya gari hizo, wakamuachia yule kijana mwingine kisha wakaondoka na Mdude kuelekea kusikojulikana.
Tayari CHADEMA kupitia kwa Viongozi wa Chama katika eneo husika na Mbunge wa Mbozi Mashariki, Pascal Haonga, kimevitaarifu vyombo vya dola mkoani Mbeya, kwanza kutoa taarifa ya tukio hilo lenye mazingira ya utekaji pia kutaka kujua kama kuna askari waliopewa kazi ya kwenda kumkamata Mdude.
Hadi sasa haijulikani Mdude yuko wapi! Tupaze sauti zetu sote kulaani tukio hili na kutaka Mdude arudishwe au aachiliwe akiwa salama.
Katika hatua ya sasa, CHADEMA kwa nguvu zote kinalaani vikali tukio hilo. Tunavitaka vyombo vya dola, hususan Jeshi la Polisi lenye wajibu wa kulinda raia na mali zao, kufuatilia taarifa za tukio hilo kama zilivyoripotiwa kwa polisi katika eneo husika na kuhakikisha Mdude anapatikana na wahalifu waliotenda tukio hilo wanajulikana, kukamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
Tutaendelea kuwapatia taarifa zaidi kadri itakavyohitajika.
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
Zaidi, soma;
www.jamiiforums.com
www.jamiiforums.com
www.jamiiforums.com
www.jamiiforums.com
Aidha, yeye mwenyewe amesema CHADEMA inafuatiloa suala hilo na taarifa zaidi itatolewa muda si mrefu
======
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA ZA AWALI KUHUSU TUKIO LA MDUDE NYAGALI (MDUDE CHADEMA)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), katika hali ya dharura, kinafuatilia kwa karibu, taarifa za Mdude Nyagali (Mdude Chadema) kuvamiwa kisha kuchukuliwa na watu ambao hawajatambulika, akiwa ofisini kwake, eneo la Vwawa, Mbozi, mkoani Songwe, katika tukio lenye dalili za utekaji.
Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda, majira ya jioni ya leo (saa 12 kuelekea saa 1) yalifika magari mawili katika eneo la ofisini kwa Mdude, Vwawa mjini, kisha wakatelemka takriban watu wanne, ambao walimkamata kijana mmoja aliyekuwa nje ya ofisi hiyo wakampeleka kwenye mojawapo ya magari waliyokuja nayo huku wengine wakiingia ndani ya ofisi, alikokuwa Mdude.
Imedaiwa kuwa baada ya muda mfupi kulisikika purukushani, watu hao wakijaribu kumkamata Mdude huku wakimpiga na yeye akipiga kelele za kupinga kitendo hicho na kuomba msaada.
Taarifa za awali ambazo Chama kimezipata kutoka kwa mashuhuda hao zimedai kuwa baada ya kusikika kwa purukushani na kelele hizo, baadhi ya wananchi walijitokeza kutaka kujua kinachoendelea na kutoa msaada, ghafla watu hao waliokuwa wakimpiga Mdude wakatoa silaha aina ya bastola na kuwatishia wananchi hao, kitendo kilichowaogofya wananchi na kukimbia kwa hofu. Imedaiwa kuwa watu hao walimuingiza Mdude kwenye 'buti' ya mojawapo ya gari hizo, wakamuachia yule kijana mwingine kisha wakaondoka na Mdude kuelekea kusikojulikana.
Tayari CHADEMA kupitia kwa Viongozi wa Chama katika eneo husika na Mbunge wa Mbozi Mashariki, Pascal Haonga, kimevitaarifu vyombo vya dola mkoani Mbeya, kwanza kutoa taarifa ya tukio hilo lenye mazingira ya utekaji pia kutaka kujua kama kuna askari waliopewa kazi ya kwenda kumkamata Mdude.
Hadi sasa haijulikani Mdude yuko wapi! Tupaze sauti zetu sote kulaani tukio hili na kutaka Mdude arudishwe au aachiliwe akiwa salama.
Katika hatua ya sasa, CHADEMA kwa nguvu zote kinalaani vikali tukio hilo. Tunavitaka vyombo vya dola, hususan Jeshi la Polisi lenye wajibu wa kulinda raia na mali zao, kufuatilia taarifa za tukio hilo kama zilivyoripotiwa kwa polisi katika eneo husika na kuhakikisha Mdude anapatikana na wahalifu waliotenda tukio hilo wanajulikana, kukamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
Tutaendelea kuwapatia taarifa zaidi kadri itakavyohitajika.
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
Zaidi, soma;
Mdude Nyagali: Mnanunua ndege kwa pesa taslimu halafu mnaenda kukopa dawa za binadam Bohari Kuu. Tukiwambia mnavuta bangi bila malengo mnalalamika
Mnanunua ndege kwa pesa taslimu halafu mnaenda kukopa dawa za binadam bohari kuu.Tukiwaambia mnavuta bangi bila malengo mnalalamika hivi baba wa familia unawezaje kununua bia kwa pesa taslimu halafu chakula cha familia unaenda kukopa hulipi madeni mpaka unasitishiwa huduma?
Mdude wa CHADEMA amjibu mkuu wa mkoa wa Iringa kwenye twitter yake
Ni baada ya mkuu wa mkoa wa iringa ally hapy kuhitimisha ziara yake ndani ya mkoa huo na kutoa mrejesho wake.
Kamanda Mdude CHADEMA Nyagali ashinda kesi ya uchochezi baada ushahidi kukosekana
Leo tarehe 18 april 2017 ilikuwa hukumu ya kesi yangu ya uchochezi mimi na wenzangu wawili. Kesi hiyo ambayo ni CRIMINAL CASE NO.128 OF 2016 imetolewa hukumu leo tarehe 18 april 2017 katika mahakama ya wilaya ya mbozi ambayo mtuhumiwa alikuwa ni mpaluka said nyagali almaarufu mdude nyagali na...
Maria Sarungi: Bila shaka waliomteka Mdude Nyagali ni Polisi, kwanini watumie nguvu badala ya sheria? Siku 5 nyuma alisema waliomtia ukilema ni Polisi
Siku 5 zilizopita Mdude Chadema aliandika haya maneno katika akaunti yake ya Twitter kuhusu utekaji aliofanyiwa mwaka uliopita na mateso aliyopewa na kusema wazi walikuwa ni polisi. Hii ndo nchi aliyotuachia Mwalimu Nyerere? Na jana usiku wamemchukua safari hii na silaha. Kwa nini tusiamini...