John Mnyika: Watu wenye silaha wamemchukua Mwanachama wa CHADEMA, Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA)

John Mnyika: Watu wenye silaha wamemchukua Mwanachama wa CHADEMA, Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA)

Wasiojulikana kile kitengo maarufu cha Dikteta pale Ikulu ili kuwanyamazisha wanaomkosoa kwa kuwateka, kuwatesa na hata kuwaua kimeibuka tena kwa kasi ya kutisha.
Atakuwa kadhulumu watu huyo, acha wamshikishe adabu
 
Mbunge wa Kibamba kupitia CHADEMA, John Mnyika kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Twitter amesema kuwa Chadema Mdude amechukuliwa na Watu wenye silaha
Aidha, yeye mwenyewe amesema CHADEMA inafuatiloa suala hilo na taarifa zaidi itatolewa muda si mrefu
View attachment 1088177
Itafutwe suluhu la yote, kwa Mwendo huu hatiwezi kufika salama kama Taifa, tujali utu, Mungu anatuona siku akianza kujibu tukubali matokeo.
 
Watawakana kumteka kisha baada ya mwezi waseme alikua anahojiwa.

Wiki nzima wakili wa arusha alikua anatafutwa bila mafanikio, baada ya jamii kuanza kupiga kelele ndo wanajitokeza kusema hakutekwa bali ana hojiwa .

Kama nia yao ni nzuri kwanini wawavizie katka ukamataji. ? . Kwanini iwe siri. ? kwanini watumie magari yasiyo na namba za utambulisho? .


Kwanini serikali isihusishwe na utekaji. ?
Unawafundisha namna ya kumkamata mtuhumiwa??
 
Magari mawili aina ya Nissan Patrol na Toyota Landcruzer (yasiyo na namba za usajili) yakiwa na watu kadhaa wenye silaha za moto wamevamia eneo la kazi la Ndugu Mpaluka Mdude Nyagali, maarufu kama Mdude Chadema dakika chache zilizopita. Mdude ni fundi wa Computer na masuala ya IT na ofisi yake ipo maeneo ya Vwawa, huko Mbozi.

Watu hao wamefyatua risasi moja hewani na kuwaamuru watu wote waliokuwemo kulala chini kisha wakamchukua Mdude na kuondoka nae kwa mwendo wa kasi. Baada ya kuondoka mashuhuda wa tukio hilo wameenda kutoa taarifa kituo cha polisi Vwawa lakini bado hawajachukua hatua yoyote.

Nimezungumza na baadhi ya mashuhuda waliokua eneo la tukio, Mbunge wa Viti maalumu Songwe mama Sophia Mwakagenda, na Mgombea ubunge wa Vwawa Ndg.Fanuel Mkisi ambao wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo. Tunaomba tupaze sauti kwa nguvu ili Mdude apatikane akiwa salama.!
 
Screenshot_2019-05-04-20-22-22~2.png
 
Ni nani huyo jamaa anayejiita Chadema Mdude? Maana niliposoma heading nikadhani ni typing erra kumbe ni jina la mtu!

Ndio kwanza namsikia leo. Naomba kujua matukio yake au baadhi ya maneno au kauli alizowahi kutamka au kusema.
 
Magari mawili aina ya Nissan Patrol na Toyota Landcruzer (yasiyo na namba za usajili) yakiwa na watu kadhaa wenye silaha za moto wamevamia eneo la kazi la Ndugu Mpaluka Mdude Nyagali, maarufu kama Mdude Chadema dakika chache zilizopita. Mdude ni fundi wa Computer na masuala ya IT na ofisi yake ipo maeneo ya Vwawa, huko Mbozi.

Watu hao wamefyatua risasi moja hewani na kuwaamuru watu wote waliokuwemo kulala chini kisha wakamchukua Mdude na kuondoka nae kwa mwendo wa kasi. Baada ya kuondoka mashuhuda wa tukio hilo wameenda kutoa taarifa kituo cha polisi Vwawa lakini bado hawajachukua hatua yoyote.

Nimezungumza na baadhi ya mashuhuda waliokua eneo la tukio, Mbunge wa Viti maalumu Songwe mama Sophia Mwakagenda, na Mgombea ubunge wa Vwawa Ndg.Fanuel Mkisi ambao wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo. Tunaomba tupaze sauti kwa nguvu ili Mdude apatikane akiwa salama.!
I say fight now!all are criminals
 
Back
Top Bottom