Johnny Innis, Mswahili wa New York

Johnny Innis, Mswahili wa New York

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
JOHN INNISS MSWAHILI WA NEW YORK

Nimemfahamu John Inniss miaka ya 1980 mwishoni kwa kutambulishwa na Bi. Riziki Shahari miaka hiyo yeye mwanafunzi Columbia University, New York ambako ndiko "Waswahili," hawa wawili walijuana.

John Innis ambae nikipenda kumwita kwa jina lake la utani "Mtembezi," alikuwa anakisema Kiswahili kiasi ukitoa ile "accent" ya Kimarekani utadhani kazaliwa Kariakoo.

Basi alipokuja Dar es Salaam tukakutana.

Mtu mstaarabu na muungwana sana.

Juu ya ulemavu wake alikuwa anajimudu vizuri akitembea bila ya msaada wa mtu.

Mungu akajaalia kuwa wenyeji wake Dar es Salaam mimi ni ndugu zangu pale Mission Quarter alipofikia.

Katika kufahamiana huku tulizungumza mengi na hivyo ndivyo alivyonihadithia maisha yake kwa yale yaliyomfika Vietnam akiwa askari Marine Corps na akapoteza mkono na mguu katika umri mdogo sana wa ujana.

Naamini nilikuwa nikimstaajabisha vile nikiwafahamu rafiki zake kutoka Dar es Salaam aliojuananao Marekani katika 1960s.

Aliniuliza kama namfahamu Abdul Nanji.

Nikamtajia hadi mtaa aliozaliwa na historia yake kama mwanachama wa Chipukizi Club na akina Badrin na Hussein Shebe.

Badrin alihamia Marekani miaka hiyo ya 1960 miaka ambayo Vita Vya Vietnam vilikuwa vimepamba moto.

Mazungumzo yetu yalikuwa yakistawi kwa kweli na mini nikistarehe sana kumsikiliza anavyokimwaga Kiswahili tena cha ndani kabisa.

Alikuwa haishi kunishangaza.

Innis ananambia, "Mohamed jana nilikwenda kwa Mita."

Huyu Mita ni katika vijana wa Kidaresalaam na alikuwa JWTZ.

John Innis Mtembezi anaendelea, "Zamani kila nikikutana na Mita hapa Dar es Salaam mazungumzo yetu makubwa ni mambo ya jeshi na silaha mpya.

Safari hii nikashangaa Mita kanishikilia na mambo ya biashara na miradi yake."

Nikamwambia, "Mita wewe utaweza kucheza ngoma na mzigo kichwani?"

Kashangaa vipi Mita atakuwa mwanajeshi na hapo hapo mfanya biashara.

Tabu kuamini semi kama hii ya "ngoma na mzigo kichwani," inatoka kwenye kinywa cha Mmarekani aliyejifunza Kiswahili kama lugha ya pili.

Mtembezi akifahamiana na Prof. Sengo ambae kama yeye ni bingwa wa Kiswahili.

Basi akaniuliza hali yake nk. nk.
Innis akanishangaza kupita kiasi.

Katika kumsifia Dr. Sengo kuhusu ujuzi wake wa lugha akaniambia, "Mimi Dr. Senior ni nyakanga wangu."

Hapa alinimaliza.

Hakuna kijana wa kiume Mswahili asiyelijua zimwi hili.

Nyakanga heshima yake kwenye kumbi ni kubwa mno kwa wali wake.

Nyakanga ndiye mwalimu wao wa kuwafunza yale ambayo baba wala mjomba hawezi.

Huyu ndugu yetu alikipenda Kiswahili na akajua hadi mila zetu.

Da Ummie pole sana na nakuomba tuwekee yale mahojiano yako na John Inniss.

FB_IMG_1616648280654.jpg
 
Mohamed ni muislam attached to Middle Eastern islamic traditions,ila let not deny this,Mohamed upo fascninated na utamaduni wa America na especially wa mabishoo Black Americans

Mohamed wewe ni bishoo na una leanings kali sana za niggas maana kuna kipindi ulileta uzi wa wanamuziki wa zamani wa America you guys are always in love with.

Kwa kifupi it happened ulizaliwa kwenye uislam of which umekulia na unaupenda kama jukumu,ila mzee mwenzangu American softpower imekukaa kama sisi wengine!

Hahahaha
😆😆😆Hamtaki unafiki
 
Mohamed ni muislam attached to Middle Eastern islamic traditions,ila let not deny this,Mohamed upo fascninated na utamaduni wa America na especially wa mabishoo Black Americans

Mohamed wewe ni bishoo na una leanings kali sana za niggas maana kuna kipindi ulileta uzi wa wanamuziki wa zamani wa America you guys are always in love with.

Kwa kifupi it happened ulizaliwa kwenye uislam of which umekulia na unaupenda kama jukumu,ila mzee mwenzangu American softpower imekukaa kama sisi wengine!

Hahahaha
Wyatt,
Umesema kweli.

Makuzi yangu kidogo hayakuwa typical Kariakoo.

Baba yangu alinilea tofauti na kunipa "exposure," si wengi katika rika langu walipata.

Ndiyo sababu wewe umeona kuwa kuna kitu kwangu hakiendani na kawaida ya Waswahili.

Hii imeniathiri sana hadi leo sasa nimekuwa mzee.
 
Bwa
JOHN INNISS MSWAHILI WA NEW YORK

Nimemfahamu John Inniss miaka ya 1980 mwishoni kwa kutambulishwa na Bi. Riziki Shahari miaka hiyo yeye mwanafunzi Columbia University, NEW York ambako ndiko "Waswahili," hawa wawili walijuana.

John Innis ambae nikipenda kumwita kwa jina lake la utani "Mtembezi," alikuwa anakisema Kiswahili kiasi ukitoa ile "accent" ya Kimarekani utadhani kazaliwa Kariakoo.

Basi alipokuja Dar es Salaam tukakutana.

Mtu mstaarabu na muungwana sana.

Juu ya ulemavu wake alikuwa anajimudu vizuri akitembea bila ya msaada wa mtu.

Mungu akajaalia kuwa wenyeji wake Dar es Salaam mimi ni ndugu zangu pale Mission Quarter alipofikia.

Katika kufahamiana huku tulizungumza mengi na hivyo ndivyo alivyonihadithia maisha yake kwa yale yaliyomfika Vietnam akiwa askari Marine Corps na akapoteza mkono na mguu katika umri mdogo sana wa ujana.

Naamini nilikuwa nikimstaajabisha vile nikiwafahamu rafiki zake kutoka Dar es Salaam aliojuananao Marekani katika 1960s.

Aliniuliza kama namfahamu Abdul Nanji.

Nikamtajia hadi mtaa aliozaliwa na historia yake kama mwanachama wa Chipukizi Club na akina Badrin na Hussein Shebe.

Badrin alihamia Marekani miaka hiyo ya 1960 miaka ambayo Vita Vya Vietnam vilikuwa vimepamba moto.

Mazungumzo yetu yalikuwa yakistawi kwa kweli na mini nikistarehe sana kumsikiliza anavyokimwaga Kiswahili tena cha ndani kabisa.

Alikuwa haishi kunishangaza.

Innis ananambia, "Mohamed jana nilikwenda kwa Mita."

Huyu Mita ni katika vijana wa Kidaresalaam na alikuwa JWTZ.

John Innis Mtembezi anaendelea, "Zamani kila nikikutana na Mita hapa Dar es Salaam mazungumzo yetu makubwa ni mambo ya jeshi na silaha mpya.

Safari hii nikashangaa Mita kanishikilia na mambo ya biashara na miradi yake."

Nikamwambia, "Mita wewe utaweza kucheza ngoma na mzigo kichwani?"

Kashangaa vipi Mita atakuwa mwanajeshi na hapo hapo mfanya biashara.

Tabu kuamini semi kama hii ya "ngoma na mzigo kichwani," inatoka kwenye kinywa cha Mmarekani aliyejifunza Kiswahili kama lugha ya pili.

Mtembezi akifahamiana na Prof. Sengo ambae kama yeye ni bingwa wa Kiswahili.

Basi akaniuliza hali yake nk. nk.
Innis akanishangaza kupita kiasi.

Katika kumsifia Dr. Sengo kuhusu ujuzi wake wa lugha akaniambia, "Mimi Dr. Senior ni nyakanga wangu."

Hapa alinimaliza.

Hakuna kijana wa kiume Mswahili asiyelijua zimwi hili.

Nyakanga heshima yake kwenye kumbi ni kubwa mno kwa wali wake.

Nyakanga ndiye mwalimu wao wa kuwafunza yale ambayo baba wala mjomba hawezi.

Huyu ndugu yetu alikipenda Kiswahili na akajua hadi mila zetu.

Da Ummie pole sana na nakuomba tuwekee yale mahojiano yako na John Inniss.

View attachment 1733889
Bwana Muhammad ni nini kimejificha nyuma ya malingo yako juu ya utoto wa daslama? Au ni sawa na jahliya ile ya maanswar dhidi ya muhajirina' kipi kitakufaa juu ya utoto wako wa daslama kwa Mola wako? Allah Ampe kauli Thabit ndugu yetu mtembezi
 
Mohamed Said mbona John Magufuli hujamuandikia Tazia?
Nilisikia akimnanga DW japo alitia na nifaq kwa uchache Kuna mahali akijifanya kumsifia, huenda ukastaajabu aliandika juu ya kitwana kondo kibaraka wa wakoloni lakini ameshindwa kwa magufuli
 
Nilisikia akimnanga DW japo alitia na nifaq kwa uchache Kuna mahali akijifanya kumsifia, huenda ukastaajabu aliandika juu ya kitwana kondo kibaraka wa wakoloni lakini ameshindwa kwa magufuli
Ni haki yake ya kikatiba kumsifia anayemtaka na kumsema vibaya anayemtaka, si lazima amsifu unayempenda wewe.

Hii gia ya "kibaraka wa wakoloni" inatumiwa kwa propaganda sana na meshapitwa na wakati.
 
Bwa

Bwana Muhammad ni nini kimejificha nyuma ya malingo yako juu ya utoto wa daslama? Au ni sawa na jahliya ile ya maanswar dhidi ya muhajirina' kipi kitakufaa juu ya utoto wako wa daslama kwa Mola wako? Allah Ampe kauli Thabit ndugu yetu mtembezi
Makala...
Huangalia nyuma na kushukuru kwani yapo pia majuto.

Mengi wazee wetu walitufanyia kwa mapenzi na mategemeo kuwa iko siku sisi tutakuwa watu muhimu katika jamii.
 
Nilishawahi kutana na huyu mwamba
Wakati nikiwa mdogo alikuwa na urafiki
Na anty zangu

Ova
 
Back
Top Bottom