Pre GE2025 Joseph Haule 'Prof. Jay: Nitagombea Ubunge Mikumi 2025

Pre GE2025 Joseph Haule 'Prof. Jay: Nitagombea Ubunge Mikumi 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Msanii maarufu wa muziki wa hip-hop, Joseph Haule, anayejulikana kama Profesa Jay, ametangaza rasmi kuwa atagombea tena ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Akizungumza kwenye kipindi cha The Throne kinachorushwa na redio Crown FM leo Ijumaa, Oktoba 11, 2024, Profesa Jay ameeleza kuwa bado anaamini anazo nguvu za kutosha za kuwatumikia wananchi wa Mikumi.

“Mwenyezi Mungu ameniweka hai, ninaamini ana kazi na mimi, naona bado nina nguvu, na ninaona kuna kazi ya kufanya kwa wananchi wa Mikumi," alisema Profesa Jay.

Ameongeza kuwa atashiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivi karibuni na kwamba mwakani atawania tena ubunge ili kuendelea kuwatumikia wananchi wa Mikumi.

Alisema kwa kujiamini, "Naamini siku ya kwenda Mikumi hata Twiga watatoka mbugani kuja kunilaki."

Jambo
 
Msanii maarufu wa muziki wa hip-hop, Joseph Haule, anayejulikana kama Profesa Jay, ametangaza rasmi kuwa atagombea tena ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Akizungumza kwenye kipindi cha The Throne kinachorushwa na redio Crown FM leo Ijumaa, Oktoba 11, 2024, Profesa Jay ameeleza kuwa bado anaamini anazo nguvu za kutosha za kuwatumikia wananchi wa Mikumi.

“Mwenyezi Mungu ameniweka hai, ninaamini ana kazi na mimi, naona bado nina nguvu, na ninaona kuna kazi ya kufanya kwa wananchi wa Mikumi," alisema Profesa Jay.

Ameongeza kuwa atashiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivi karibuni na kwamba mwakani atawania tena ubunge ili kuendelea kuwatumikia wananchi wa Mikumi.

Alisema kwa kujiamini, "Naamini siku ya kwenda Mikumi hata Twiga watatoka mbugani kuja kunilaki."
Huu Uzi unabidi kuunganishwa
 
Sometime watu wafanye vitu kulingana na nyakati sio matamanio hasa unaopokuwa kwenye mambo yanayohusu ofisi za umma!!!

Professor anaheshimika Sana angepumzika afanye mambo mengine ubunge unahitaji mchaka mchaka Sana na watu ambao fit physically na mentally!!.

Nashauri angejipumzisha na awekeze kwenye faundation yake!!!
 
Sidhani kama hata madaktari wataruhusu hili, kwa zile video alizoposti kwenye mapito yake nadhani angepumzika aangalie afya yake kwa umakini. Ajitunze, kwa hali aliyopitia ilikuwa " chupuchupu" atangulie...
Bado hayuko fiti akae kwa kutulia.
 
Sometime watu wafanye vitu kulingana na nyakati sio matamanio hasa unaopokuwa kwenye mambo yanayohusu ofisi za umma!!!

Professor anaheshimika Sana angepumzika afanye mambo mengine ubunge unahitaji mchaka mchaka Sana na watu ambao fit physically na mentally!!.

Nashauri angejipumzisha na awekeze kwenye faundation yake!!!
Kuugua ni mojawapo ya mapito ya mwanadamu. Prof. Jay ni kweli aliugua lkn haimfanyi kukatisha michakato na ndoto zake za maisha.

Aliugua , amepona na hivyo aachwe afanye anachokipenda.
 
Back
Top Bottom