Joseverest
JF-Expert Member
- Sep 25, 2013
- 52,812
- 71,392
Wasalaam wakuu,
Hatimaye nimerudi tena baada ya kimya cha mwezi mzima. Natumai mnaendelea vyema na shughuli zenu hapa jamvini na hata za nje ya jukwaa. Katika mwezi huo mmoja niliokaa kimya kumeibuka 'Sintofahamu' nyingi juu yangu kwa wale ndugu, jamaa na rafiki zangu wa humu Jukwaani
Lengo la kuandika uzi huu ni 'KUWEKA MAMBO SAWA' na SIO 'SIFA' au sijui wengine mnaita 'KIKI' kwani baada ya kuingia kwenye account yangu nimekuta 'taarifa tata' zinazonihusu mimi kutoka kwa members wa hili jukwaa.. Hadi thread nimeanzishiwa kuhusu uwepo wangu, nimeona si vibaya kuweka mambo sawa yakae kwenye mstari ili kuondoa 'utata' kwa maana haiwezekani nizushiwe mambo 'AMBAYO SIO SAWA' nikae kimya tu
{ Najua zimesemwa taarifa nyingi tu ila hapa najaribu kuainisha chache tu }
Miongoni mwa taarifa hizo nilizoziona na ambazo nimezushiwa ni;
1. Nimebadili ID na avatar
2. Nimetekwa na watu wa usalama na kufichwa kusipojulikana
3. Nilienda Zimbabwe wengine wakasema Kenya kwenye uchaguzi
4. Nimemaliza kazi niliyotumwa na 'watu wa system'
5. Nipo chuo Tandabui
6. Mke wangu kanizuia kuingia JF
7. Simu yangu imeharibika au kudondokea kwenye maji
8. Nimetongoza mwanamke wa mojawapo ya mods ndio maana nimezuiwa kupost
9. Nipo Kibiti napimwa mkojo kwa ajili ya uchochezi au nipo magereza
10. Nipo nchini China/Canada kikazi/kimasomo ambapo baadhi ya mitandao ya kijamii imefungiwa (kupigwa BAN)
11. Wengine walidiriki kwenda mbali na kusema Nimefariki katika ajali ya pikipiki (iliyotokea ubungo riverside ikimuhusisha ndugu yetu Johanes [RIP])
Sasa, napenda KUKANUSHA TAARIFA HIZO KAMA IFUATAVYO kwa maana sio za kweli
1. Sihusiki na hizo ID mpya kama mbili/tatu hivi ( ya kike na ya kiume) nimeziona zinazotumia Avatar kama hii ya kwangu..Ya kwangu ni hii tu (Joseverest) hamna nyingine kwa maana siwezi kumiliki ID zaidi ya moja na sioni faida yake.
2. Sijatekwa na mtu yeyote wala kutishiwa maisha kwa namna yoyote ile ndani ya huu mwezi mmoja niliokuwa kimya
3. Sikwenda Zimbabwe wala Kenya, taarifa za uchaguzi wa Kenya nilizipata hapahapa Tanzania kupitia vyombo vya habari
4. Sina kazi maalumu niliyotumwa na hao watu wa system, mimi ni kijana najitegemea na maisha yangu binafsi na Sihusiki kwa namna moja au nyingine na hao watu mnaowaita ni wa System
5. Sisomi chuoni Tandabui, mambo ya kusoma yaliisha kitambo ila hapo mbeleni nitajiendeleza kielimu kwa neema za Mungu akijaalia
6. Sina mke au mpenzi ambae ananizuia kulog in (kuingia JF)
7. Simu yangu ipo sawa haijaharibika wala kudondokea kwenye maji
8. Sijihusishi kimapenzi na mwanamke yeyote wa mods kwa maana siwajui na haitakaa itokee
9. Sipo Kibiti kwa ajili ya kupimwa haja ndogo kwa maana sikuhusika kwa namna yoyote kwenye masuala ya uchochezi katika mojawapo ya machapisho yangu humu jukwaani, Pia sipo/sikuwepo gerezani kwa maana mimi sio mhalifu
10. Sipo nchini China wala Canada kikazi/kimasomo nipo hapahapa Nchini Tanzania
11. SIJAFA wala SIJAPATA ajali ya aina yoyote iliyotokea hivi karibuni mahala popote(Japokuwa sipingi kifo, najua kila nafsi itaonja mauti)...hadi muda huu ninavyoandika uzi huu ( Nipo Physically and Mentally Fit, nikimaanisha niko sawa kimwili na kiakili[timamu] )
Mwisho kabisa napenda kutoa RAI kwa baadhi ya watu kuwa, mtafute TAARIFA SAHIHI na sio ' Uzushi au taarifa mbaya zenye lengo la kumdhalilisha/kumchafua mtu aonekane mbaya/muongo/mfitini miongoni mwa wanajamii wanaomzunguka.
-Tuendelee kutumia JF kama sehemu muhimu na maalum ya kujifunza, kuelimika, kupata habari na hata kuburudika..
Samahani kama nimewakwaza kwa thread hii ndefu( nimejaribu kufupisha kadiri niwezavyo)
Original Joseverest ✓
Sent using Tapatalk
Hatimaye nimerudi tena baada ya kimya cha mwezi mzima. Natumai mnaendelea vyema na shughuli zenu hapa jamvini na hata za nje ya jukwaa. Katika mwezi huo mmoja niliokaa kimya kumeibuka 'Sintofahamu' nyingi juu yangu kwa wale ndugu, jamaa na rafiki zangu wa humu Jukwaani
Lengo la kuandika uzi huu ni 'KUWEKA MAMBO SAWA' na SIO 'SIFA' au sijui wengine mnaita 'KIKI' kwani baada ya kuingia kwenye account yangu nimekuta 'taarifa tata' zinazonihusu mimi kutoka kwa members wa hili jukwaa.. Hadi thread nimeanzishiwa kuhusu uwepo wangu, nimeona si vibaya kuweka mambo sawa yakae kwenye mstari ili kuondoa 'utata' kwa maana haiwezekani nizushiwe mambo 'AMBAYO SIO SAWA' nikae kimya tu
{ Najua zimesemwa taarifa nyingi tu ila hapa najaribu kuainisha chache tu }
Miongoni mwa taarifa hizo nilizoziona na ambazo nimezushiwa ni;
1. Nimebadili ID na avatar
2. Nimetekwa na watu wa usalama na kufichwa kusipojulikana
3. Nilienda Zimbabwe wengine wakasema Kenya kwenye uchaguzi
4. Nimemaliza kazi niliyotumwa na 'watu wa system'
5. Nipo chuo Tandabui
6. Mke wangu kanizuia kuingia JF
7. Simu yangu imeharibika au kudondokea kwenye maji
8. Nimetongoza mwanamke wa mojawapo ya mods ndio maana nimezuiwa kupost
9. Nipo Kibiti napimwa mkojo kwa ajili ya uchochezi au nipo magereza
10. Nipo nchini China/Canada kikazi/kimasomo ambapo baadhi ya mitandao ya kijamii imefungiwa (kupigwa BAN)
11. Wengine walidiriki kwenda mbali na kusema Nimefariki katika ajali ya pikipiki (iliyotokea ubungo riverside ikimuhusisha ndugu yetu Johanes [RIP])
Sasa, napenda KUKANUSHA TAARIFA HIZO KAMA IFUATAVYO kwa maana sio za kweli
1. Sihusiki na hizo ID mpya kama mbili/tatu hivi ( ya kike na ya kiume) nimeziona zinazotumia Avatar kama hii ya kwangu..Ya kwangu ni hii tu (Joseverest) hamna nyingine kwa maana siwezi kumiliki ID zaidi ya moja na sioni faida yake.
2. Sijatekwa na mtu yeyote wala kutishiwa maisha kwa namna yoyote ile ndani ya huu mwezi mmoja niliokuwa kimya
3. Sikwenda Zimbabwe wala Kenya, taarifa za uchaguzi wa Kenya nilizipata hapahapa Tanzania kupitia vyombo vya habari
4. Sina kazi maalumu niliyotumwa na hao watu wa system, mimi ni kijana najitegemea na maisha yangu binafsi na Sihusiki kwa namna moja au nyingine na hao watu mnaowaita ni wa System
5. Sisomi chuoni Tandabui, mambo ya kusoma yaliisha kitambo ila hapo mbeleni nitajiendeleza kielimu kwa neema za Mungu akijaalia
6. Sina mke au mpenzi ambae ananizuia kulog in (kuingia JF)
7. Simu yangu ipo sawa haijaharibika wala kudondokea kwenye maji
8. Sijihusishi kimapenzi na mwanamke yeyote wa mods kwa maana siwajui na haitakaa itokee
9. Sipo Kibiti kwa ajili ya kupimwa haja ndogo kwa maana sikuhusika kwa namna yoyote kwenye masuala ya uchochezi katika mojawapo ya machapisho yangu humu jukwaani, Pia sipo/sikuwepo gerezani kwa maana mimi sio mhalifu
10. Sipo nchini China wala Canada kikazi/kimasomo nipo hapahapa Nchini Tanzania
11. SIJAFA wala SIJAPATA ajali ya aina yoyote iliyotokea hivi karibuni mahala popote(Japokuwa sipingi kifo, najua kila nafsi itaonja mauti)...hadi muda huu ninavyoandika uzi huu ( Nipo Physically and Mentally Fit, nikimaanisha niko sawa kimwili na kiakili[timamu] )
Mwisho kabisa napenda kutoa RAI kwa baadhi ya watu kuwa, mtafute TAARIFA SAHIHI na sio ' Uzushi au taarifa mbaya zenye lengo la kumdhalilisha/kumchafua mtu aonekane mbaya/muongo/mfitini miongoni mwa wanajamii wanaomzunguka.
-Tuendelee kutumia JF kama sehemu muhimu na maalum ya kujifunza, kuelimika, kupata habari na hata kuburudika..
Samahani kama nimewakwaza kwa thread hii ndefu( nimejaribu kufupisha kadiri niwezavyo)
Original Joseverest ✓
Sent using Tapatalk