Joyce Kiria arudi kimya kimya kwa mumewe baada ya kumdhalilisha mitandaoni

Joyce Kiria arudi kimya kimya kwa mumewe baada ya kumdhalilisha mitandaoni

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,386
Mwanaharakati na mtangazaji wa kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria ameonekana kufurahishwa na mumewe ikiwa ni miezi sita sasa imepita tangu atangaze mitandaoni kuwa mumewe haudumii familia yake na majukumu yote ya kulea watoto ameachiwa yeye.


Kwanza nakuomba radhi kwa kushare hii ulinikataza nisiposti… ulivyoniambia umelipa hii ela shuleni sikuamini. Tena siku uliyotuletea chakula ukanipa na ela nilichanganyikiwa machozi ya furaha pamoja na kuniomba nisiposti lakini ninafikiri ni vyema niendeleze elimu kwamba INAWEZEKANA KUBADILIKA! Dunia wakajua wewe ni baba bora sasa! Umeanza kuchukua WAJIBU WAKO Asante sana kwa kusikia kilio changu! I am emotional.
Namshukuru Mungu sana kwa hatua hii kubwa sana ya kulipa sehemu ya ada ya watoto wetu na kuwaletea chakula! We love you so much [emoji177] tunakuombea ufanikiwe zaidi na utukumbuke kama ivi[emoji120][emoji120][emoji120]
Kinababa mtaniwia radhi lakini nasisitiza kwamba, hii ni awareness niliamua kufanya kwa wanaNdoa wengi kuna mengi ya kujifunza! Mabaya yangu ya kubwatabwata niachie mwenyewe maana mimi nipo kazini napigana na UKATILI WA KIJINSIA, na mazuri yangu ya kuwakumbusha wababa kuwajibika muyachukue kwa faida ya familia zetu! Na HESHIMA yenu pia.
Naimani wababa wengi sana wamejirekebisha na maisha yanaenda kwa Amani… nami nawaombea kwa dhati ya moyo wangu mfanikiwe katika kazi zenu ili mzidi kutenda mema kwa familia zenu!!! NAWAPENDA [emoji177][emoji177][emoji177][emoji177][emoji177]
kiria.jpg
 
Niliwahi ambiwa na babu kuwa mwanamke si wa kuamini akanipa kisa flani hivi; kuna jamaa alikua akisumbuliwa na mbwa wa jirani yule mbwa alikua na tabia ya kuua vifaranga vya kuku sasa akawa anamwinda ili ikiwezekana amuue, siku moja kukiwa na kigiza akasikia kitu kinatikisa majani ya mahindi kuja kwake jamaa alipo sikia mahindi yanatikisika akachukua rungu akampiga nalo akijua ni mbwa wa jirani kumbe ni mtoto wa huyo jirani na akafa palepale.

Alipogundua kuwa alichopiga si mbwa bali ni mtoto wa jirani akakimbia kwenda kumwambia mkewe tukio, basi wakakubaliana wafiche maiti ili ikifika usiku sana wakautupe mbali ili isijulika mtoto kaenda wapi, wazazi wa yule mtoto walimtafuta mtoto wao bila mafanikio.
Ilipofika usiku wa manane wakakubaliana wakamzike mtoto mbali huko vichakani, walimzika wakarudi maisha yakaendelea. Kwa bahati nzuri jamaa akaenda akamsimulia ndugu yake kilichompata nae ndugu yake akamuuliza kama mkewe anajua nae akamkubalia huyo ndugu yake akamwambia kama Mke anajua basi afanye jitihada usiku tena akahamuamishe huyo marehemu akamzike sehemu nyingine mbali anayojua mwenyewe Kwa sababu mwanamke si wa kuamini.

Na jamaa akafanya alivyoelekezwa na ndugu yake, siku zikapita nyingi baada ya tukio siku moja kukatokea ugomvi jamaa akampiga mkewe mwanamke akakimbilia polisi kusimulia kila kitu.

Polisi wakamkamata jamaa na mwanamke akawapeleka hadi walipomzika huyo mtoto lakini hawakumpata.

Huyu kaambiwa asipost yeye mbiyo kupost.
 
Back
Top Bottom