Joyce Kiria na akaunti yake ya Facebook

Nimeweka picha ili kila mtu ajue.

Leo nimeamini kuwa mwanamke ni sehemu ya mafanikio ya mwanaume.


Lazima tujue kuwa mke na familia zetu zinatoa taswira maisha yetu ya leo hata baadaye. Nimepita FB nikaona maajabu makubwa sana. Nikaunganisha matukio mengi sana nikapata jibu.

Wengi walisema, ila kwa vile sikutilia maanani hicho kilichokuwa kinasemwa sikufuatailia.

Tukio la kwanza ilikuwa kuonyesha nyeti za mtoto wa kike katika runinga. La pili kutuma kwenye mitandao akihesabu fedha zilizochangwa na watu aliowaita marafiki waliomchangia kuuwinda Ubunge kwa mme wake. La tatu ni la hivi karibuni kuiishi maisha ya umalaya yaliyopitiliza.

Huwezi ukawa na mwanamke anashindwa kuvaa hata "skintight", ukasema umeoa. Anakaa uchi hata Ulaya hawako hivyo.

Bila kubadilika hautafika unakokwenda. Zaidi ataendelea kufanya vituko na wewe ukidhalilika wa watu unaotaka kuwaongoza.



 
Duuu ni kweli, maana mi kichapo ninachopewa na baba watoto wangu nikivaa nguo za uchi, hata vipindi vya huyu Dada nimwiko kuangalia alishanipiga marufuku, kuna siku nilikaidi agizo lake akanikuta naangalia nilipigwa kofi la shavu niliona nyotanyota za blue na njano machoni mwangu, tangu hapo nilikoma kabisa.
 
Uzuri Yumo humu Labda kuna kitu atakua amejifunza pia.
 
Mambo mengine kwakweli yanasikitisha na kuhuzunisha.Mwanamke au mke wa mtu inabidi aendane na falsafa na mitazamo ya mumewe.Sasa inapotokea kwa bahati mbaya au makusudi mtu unakosea kuoa aina ya mwanamke unae endana nae,hakika ni matatizo makubwa.

Ndugu yetu,kijana mwenzetu inabidi ajitafakari sana juu ya mke alie nae.Unapohitaji kuwa public figure kuna baadhi ya principles ambazo inatakiwa uzizingatie.Sasa unapoacha baadhi ya masharti lazima jamii unayotaka kuiongoza ikuone kituko kama alivyo mwenza wako.

Hayo ni maisha yao binafsi lakini lazima yatazamwe na jamii,kwa sababu mtu anataka kuitumikia jamii.Kiukweli hapo kaka yangu lazima afanye mabadiliko kwa kupenda au kutokupenda kama anahitaji awe kiongozi wa wananchi.

Heri kuishi bila mke kuliko kuwa na mke ambaye nikutuko katika jamii,kama anahitaji kuendelea kuwa na ndoto za uongozi katika jamii kuna baadhi ya vitu inabidi avitoe sadaka.

Mke sio mama yako kiasi kwamba ukimuacha hutopata mwingine.Za kuambiwa achanganye na zake(in JK voice).

KALINZI NYUMBANI.
 
Ila mwambie asiwe anakupa kichapo physically, mwanaume huwezi kukipiga kiumbe dhaifu unajishusia hadhi mwenyewe.

Au shem huelewi bila kichapo nini?
 
Ila mwambie asiwe anakupa kichapo physically, mwanaume huwezi kukipiga kiumbe dhaifu unajishusia hadhi mwenyewe.

Au shem huelewi bila kichapo nini?
Akitoa agizo nikakaidi kichapo lazima kinihusu.
 
Naona nyota nyota. Hapa JF ni uwazi,siku hizi ni mafumbo
 
mwache mdada ndo wakati wake huu, inawezekana aliruka stage, alikimbilia kuolewa mapema kabla hajamaliza ujana!!! Ila kisura anacho tatizo mkuu hana , vigimbi kama vimekojolewa na popo
 
Mbona unamshauri amuache mkewe usimshauri aongee nae Ili abadilike? Na hii inategemea Kama kamanda anaona tabia za mkewe zinamkwaza.
 
Ni uwazi kabisa. Unajua tunaojuana inatakiwa tuambiane hata kwa maandishi kama haya. Angalia pichakwa taarifa zaidi.
Nimeona mkuu. Huyu si ni mwanamke live? Anaishi falsafa yake,yuko live. Jamaa yake alilalamika kuwa alibanwa makengele baada ya kutuhumiwa jinai,labda performance imekuwa chini. Biashara matangazo.
 
Sijashauri amuache hata kidogo. Ila nimeshauri mabadiliko, ingawa dhana ya mabadiliko ni pana sana.

Aidha, lazima ajue watu wanaweza kwazwa na tabia ya familia au wewe na ikaadhiri malengo yako. Hivyo, mtaji mkubwa ni kusikiliza jamii hasa kwa mtu wa kaliba yake.
Mbona unamshauri amuache mkewe usimshauri aongee nae Ili abadilike? Na hii inategemea Kama kamanda anaona tabia za mkewe zinamkwaza.
 
Kama ni hivi historia inamuhukumu kamanda wetu. Angalia hapa
Inaonyesha ni shida tangu zamani.
Nimeona mkuu. Huyu si ni mwanamke live? Anaishi falsafa yake,yuko live. Jamaa yake alilalamika kuwa alibanwa makengele baada ya kutuhumiwa jinai,labda performance imekuwa chini. Biashara matangazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…