TWisheshagi
Member
- May 2, 2020
- 14
- 209
MAKALA hii nimeanza kuandika jana, nikiwa kwenye jukwaa la CCM, mjini Musoma.
Mengi nimeyashuhudia kwa macho yangu, lakini kwa nafasi yangu hususan kwenye timu ya kampeni ya mgombea wetu nitajadili machache:
Nimeshuhudia baadhi ya watu muhimu kwenye timu yetu wakifuatilia hotuba za Lissu kwa siri katikati ya Hotuba ya mgombea wetu!
Yaani, hatumsikilizi mgombea wetu, tuna msikiliza Lissu! Mgombea wetu amebakia kwenye mabago nchi nzima huku Lissu akitawala kwenye MIOYO ya watu!
Aliposimama "Mama wa TAIFA" Mama Maria Nyerere, kuongea ndani ya dakika moja, tayari alianza kuumbua watu kabla ya kumaliza hotuba yake fupi yenye masimango ndani yake!
Hotuba fupi ya Mama Nyerere, ili beba ujumbe mzito na muhimu kuliko hotuba za makada wengi wa CCM walio panda jukwani kuzungumza!
Wengi tulibaki vichwa chini baada ya Mama Maria Nyerere, kuzungumza!
Mama huyu amebakia na chembe chembe za ukweli kutoka kwa Marehemu Mume wake! Huwezi kupanga naye jambo la uongo, anaweza kukubalia mwanzoni na kisha kukana baadaye kwa staili ya aina yake! Hicho ndicho kilichotokea jana.
Kupanga jambo na watu wenye umri mkubwa unapaswa kuwa mwangalifu! Ukizoea ghiriba uwe makini, ukipenda uongo uwe mwangalifu!
Lipo jambo jingine linalojitokeza kwenye kampeni zetu! Mgombea wetu, pamoja na kupendelewa na vyombo vya habari vyote muhimu, bado hotuba zeke zinafuatiliwa na watu wachache sana, ukilinganisha na wale wanavyofuatilia hotuba za Lisu kwenye mtandao ya kijamii! Ipo haja ya kujipanga upya!
Jambo jingine tumeanza kujibu Lissu, badala ya kueleza sera zetu, na mambo mengi mazuri tuliyofanya! Tumesahau sisi ndiyo wenye serikali. Tuliaminiwa kukusanya kodi za Watanzania kwa miaka mitano. Wajibu wetu ni kueleza utekelezaji zaidi kuliko kuahidi jambo jingine jipya wakati kuna mengi hatujatimiza!
Tunasikiliza Lisu, kasema kitu gani ili kesho yake tujibu! tena kwa vijembe!
Tumekosa kumbukumbu kabisa! tulichokesema jana tunakikataa leo, na tunachosema leo tunakipinga kesho asubuhi!
Ushauri wangu: Naomba kutoa ushauri ambao hauwezi kukubalika! Tunahitaji kuongezewa nguvu ya timu ya kampeni. Tupunguze watu wenye blabla tuite watu wenye uwezo wa kumsaidia mgombea wetu!
Wasanii wanapoteza muda mwingi, tunashindwa hata kuwanadi wagombea ubunge na udiwani vizuri. Jana tumeacha malalamiko mengi Musoma.
Kuna baadhi ya wagombea ubunge hata sisi wenyewe tulioko kwenye timu ya kampeni hatuwajui!
Pili, tumuombe Mzee Kinana ATUSAIDIE! Mipango mingi ya Dkt. BASHIRU imefeli kabla ya utekelezaji. Ni yeye aliyetutangazia kuwa hakutakuwa na wasanii badala yake bendi ya Chama itatumika kutumbuiza. Hilo limeshindikana kabla halijaanza kutekelezwa!
Mzee Kikwete, toka kwenye mashamba ya mananasi Msoga, njoo kwenye kampeni ili ukoe jahazi! Ushawishi wako kwa umma ni muhimu sana kuliko porojo na kelele za Humphrey Polepole!
Ndimi mkulima wa bamia, bonde la mto Simiyu Magu-MWanza. Safarini CCM KIRUMBA
Mengi nimeyashuhudia kwa macho yangu, lakini kwa nafasi yangu hususan kwenye timu ya kampeni ya mgombea wetu nitajadili machache:
Nimeshuhudia baadhi ya watu muhimu kwenye timu yetu wakifuatilia hotuba za Lissu kwa siri katikati ya Hotuba ya mgombea wetu!
Yaani, hatumsikilizi mgombea wetu, tuna msikiliza Lissu! Mgombea wetu amebakia kwenye mabago nchi nzima huku Lissu akitawala kwenye MIOYO ya watu!
Aliposimama "Mama wa TAIFA" Mama Maria Nyerere, kuongea ndani ya dakika moja, tayari alianza kuumbua watu kabla ya kumaliza hotuba yake fupi yenye masimango ndani yake!
Hotuba fupi ya Mama Nyerere, ili beba ujumbe mzito na muhimu kuliko hotuba za makada wengi wa CCM walio panda jukwani kuzungumza!
Wengi tulibaki vichwa chini baada ya Mama Maria Nyerere, kuzungumza!
Mama huyu amebakia na chembe chembe za ukweli kutoka kwa Marehemu Mume wake! Huwezi kupanga naye jambo la uongo, anaweza kukubalia mwanzoni na kisha kukana baadaye kwa staili ya aina yake! Hicho ndicho kilichotokea jana.
Kupanga jambo na watu wenye umri mkubwa unapaswa kuwa mwangalifu! Ukizoea ghiriba uwe makini, ukipenda uongo uwe mwangalifu!
Lipo jambo jingine linalojitokeza kwenye kampeni zetu! Mgombea wetu, pamoja na kupendelewa na vyombo vya habari vyote muhimu, bado hotuba zeke zinafuatiliwa na watu wachache sana, ukilinganisha na wale wanavyofuatilia hotuba za Lisu kwenye mtandao ya kijamii! Ipo haja ya kujipanga upya!
Jambo jingine tumeanza kujibu Lissu, badala ya kueleza sera zetu, na mambo mengi mazuri tuliyofanya! Tumesahau sisi ndiyo wenye serikali. Tuliaminiwa kukusanya kodi za Watanzania kwa miaka mitano. Wajibu wetu ni kueleza utekelezaji zaidi kuliko kuahidi jambo jingine jipya wakati kuna mengi hatujatimiza!
Tunasikiliza Lisu, kasema kitu gani ili kesho yake tujibu! tena kwa vijembe!
Tumekosa kumbukumbu kabisa! tulichokesema jana tunakikataa leo, na tunachosema leo tunakipinga kesho asubuhi!
Ushauri wangu: Naomba kutoa ushauri ambao hauwezi kukubalika! Tunahitaji kuongezewa nguvu ya timu ya kampeni. Tupunguze watu wenye blabla tuite watu wenye uwezo wa kumsaidia mgombea wetu!
Wasanii wanapoteza muda mwingi, tunashindwa hata kuwanadi wagombea ubunge na udiwani vizuri. Jana tumeacha malalamiko mengi Musoma.
Kuna baadhi ya wagombea ubunge hata sisi wenyewe tulioko kwenye timu ya kampeni hatuwajui!
Pili, tumuombe Mzee Kinana ATUSAIDIE! Mipango mingi ya Dkt. BASHIRU imefeli kabla ya utekelezaji. Ni yeye aliyetutangazia kuwa hakutakuwa na wasanii badala yake bendi ya Chama itatumika kutumbuiza. Hilo limeshindikana kabla halijaanza kutekelezwa!
Mzee Kikwete, toka kwenye mashamba ya mananasi Msoga, njoo kwenye kampeni ili ukoe jahazi! Ushawishi wako kwa umma ni muhimu sana kuliko porojo na kelele za Humphrey Polepole!
Ndimi mkulima wa bamia, bonde la mto Simiyu Magu-MWanza. Safarini CCM KIRUMBA