Uchaguzi 2020 Juhudi za kuua upinzani nchini kwenye uchaguzi ujao ni kwa maslahi ya nani?

Uchaguzi 2020 Juhudi za kuua upinzani nchini kwenye uchaguzi ujao ni kwa maslahi ya nani?

stigajemwa

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2016
Posts
449
Reaction score
430
Wanabodi,

Kutokana na vitendo vinavyofanywa na viongozi wa serikali na vyombo vya dola kuna kila dalili kuwa upinzani hauhitajiki tena nchini na kwamba mfumo wa chama kimoja ndio unaohitajika kwa sasa.

Mfano mzuri ni huu wa kuzuia wabunge wa upinzani kufanya mikutano kwa Uhuru na wapiga kura wao. Hii imetokea Mara kwa Mara kwa wabunge kama Msigwa,Mbowe,Mnyika na wengine wengi.

Mfano mwingine ni huu wa viongozi waandamizi wa serikali kutokuwapa ushirikiano wabunge wa upinzani. Hii imejidhihirisha pale wanapowaambia wananchi kuwa hawatapewa maendeleo sababu walichagua upinzani,huku pia wakiwaandalia mazingira ya kuonekana ni wezi wanaokula pesa za ruzuku ya jimbo na sitting allowance bila kuwajali wala kuwasemea wananchi waliowachagua.

Mfano mwingine ni huu wa kuwabambikia kesi za jinai na kuzuia mikutano ya hadhara kwa viongozi wa vyama vya upinzani nchini.

Matukio yote hayo yanaashiria shughuli za vyama vya upinzani hazihitajiki tena nchini na kwamba wabunge wa upinzani hawapaswi kurudi bungeni 2020.

Swali ni je, kuondoa wabunge wote wa upinzani bungeni na kuua vyama vya upinzani ni kwa maslahi mapana ya nani? Je,Watanzania wote?aAu kikundi? Au mtu fulani?

Nawasilisha.
 
Swali ni je, kuondoa wabunge wote wa upinzani bungeni na kuua vyama vya upinzani ni kwa maslahi mapana ya nani? Je,Watanzania wote?aAu kikundi? Au mtu fulani?
Nawasilisha.

Mbona hayo maslahi yanajulikana mkuu kwani wewe ni mgeni Tanzania.
 
[emoji30][emoji30][emoji30]
Screenshot_20191016-224559-picsay.jpeg
 
Kwa mtazamo wangu ni kuwa hawa waccm wanafikiria wanajua kile kitatokea kesho, na hio ni wao tu ambao wanajindangaya maana ni mungu tu ajuae kesho, yaani ccm inataka kutuambia tz kuwa masikini ni sababu ya upizani??siwezi ombea mtu mabaya lakini ili tz iondoke kweye hii shinda, heli huyu mtu mungu amutupe kule wakakae na rafiki yake shetani
 
stigajemwa,

Rais Magufuli aliahidi kwamba kufikia 2020 atakuwa ameua upinzani. ukitazama vitendo vya serikali yake ni katika kutimiza azma hiyo. lakini anasema pia kwamba MAENDELEO HAYANA VYAMA!!
Halafu kuna haka ka mtindo ka kuwafanya wapinzani ni majuha. eti IGP anasema hajawahi kupata malalamiko. Lugola amenukuliwa kwanza akipiga marufuku mikutano ya siasa kwa vyama vya upinzani, halafu akanukuliwa tena kudai kwamba hajawahi kuletewa malalamiko.

Natambua kwamba kuwepo kwa upinzani wenye nguvu kunahitaji watanzania wasimame imara kukataa kulazimishwa kuwa na chama kimoja tu. watanzania wenyewe wafungue kesi kama alivyokuwa anafanya Mtikila. akina Fatuma Karume wasiachwe peke yao
 
Upinzani wanajiua wenyewe, kama Serikali ingeamua kuwaua, wangelikuwa wamekufa siku nyingi.
 
Weka picha ya hicho choo cha Tandale tuone, halafu tulinganishe na ya sura ya ZK tuone ukweli.
 
Your analysis is correct but the conclusions quite erroneous. Samahani kwa lugha hiyo sasa tupitie mifano yako. Wabunge wa upinzani hawajazuiwa kwenye majimbo YAO, wote wamejikita majimbo mengine. Nassari na Mbowe tuliambiwa hawajafika kwao. Haya mengine ni mambo ya kuambiwa, kwa nini unyimwe forum, si nenda kashitaki? Na Nassari alihongwa na nani shilingi ngapi? Hili la ushirikiano sikuelewi. Umeona barabara za Arusha? Umeona shule za Iramba chini ya muti? Na miundombinu ya Mbeya, na Airport, na shule za Iringa zinachomwa moto? Huwezi kubagua, toa hoja nyingine majimbo ya wapinzani yamependelewa sana kwa maendeleo.
 
Back
Top Bottom