Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
MHE. JULIANA SHONZA APOKEA VYETI KWA KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA JUMUIYA YA WAZAZI CCM
Mbunge wa Viti Maalumu CCM Mkoa wa Songwe, Mhe. Juliana Danieli Shonza amepokea vyeti viwili vya shukurani kwa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Taifa Ndugu Gilbert Kalima. Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Songwe wamemshukuru Mhe. Shonza kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali za Jumuiya ya Wazazi ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
Wakati huo huo, Mhe. Shonza ameshiriki ziara ya Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi Taifa (CCM) katika Mkoa wa Songwe. Katika ziara hiyo, Mhe. Shonza alipata nafasi ya kuzungumza na wananchi wa Kata ya Hasanga katika Mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi Taifa na kusema; "Jumuiya ya Wazazi ni mojawapo ya nguzo muhimu sana katika kusimamia Malezi na Maadili ya Watoto na Vijana"
Aidha, katika ziara hiyo; Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Ndugu Gilbert Kalima (MNEC) na viongozi wa CCM na jumuiya ya wazazi wa Mkoa wa Songwe walishona Nguo walipotembelea Chuo cha Ufundi cha Veta - Ileje, amewasisitiza wazazi kuona umuhimu wa Chuo hicho kwa kuwaleta watoto wao wapate ujuzi.
#MTOTO UMLEAVYO, NDIVYO AKUAVYO.
#UCGUNGU WA MWANA, AUJUAYE MZAZI
#KAZIIENDELEE