Julius Mtatiro: Mawaziri wa CCM wanaendesha vikao vya siri na kugawa bahasha kwa wajumbe!

Julius Mtatiro: Mawaziri wa CCM wanaendesha vikao vya siri na kugawa bahasha kwa wajumbe!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kwenye ukurasa wake wa facebook,Mtatiro ameandika ujumbe ufuatao akiwatuhumu mawaziri wa CCM kuhujumu mchakato wa katiba mpya.

Mh.Mtatiro ameandika:

Jana waziri Maghembe amewaita wawakilishi wa wafugaji waliomo kwenye bunge la katiba,amewaandalia chakula cha kutosha,vinywaji vya kutosha na viburudisho vingine,huku wakipewa bahasha za nauli baada ya vikao vya siri.

Waziri wa elimu,Shukuru Kawambwa,jana pia amewaita wawakilishi wa vyuo vya elimu ya juu walioko katika bunge la katiba na kuendelea na mchezo huo.

Mhe.Lowassa pia leo amekutana na wafugaji na wakulima walio wajumbe wa bunge la katiba kwa mfumo huo huo.

Hoja zao wanapokutana na makundi hayo ni kupiga chapuo kura ya wazi na kupinga ya siri,huku wakieleza namna CCM inavyopinga baadhi ya mapendekezo muhimu yaliyomo katika rasimu ya katiba.

Mh.Mtatiro ameongeza kuwa,wanachofanya mawaziri hawa ndicho kinachofanywa na mawaziri wengine wa CCM,ni agizo la lazima ambalo hivi sasa linatumika hapa Dodoma.

Leo,CCM na mawaziri wanatumia fedha na kutoa rushwa ili kupitisha matakwa yao.Masuala haya yana ushahidi,kesho nitayasema bungeni kwa uwazi kabisa.

MY TAKE:
Hizi ni tuhuma nzito sana!

Je,TAKUKURU wanachukua hatua gani?

Je,Raisi Kikwete hajua kinachoendelea?

Je,ni kweli Raisi Kikwete ana nia njema ya kupata katiba mpya kama anavyosifiwa?

Yetu macho na masikio!
 
Hiki chama cha c.c.yem kilaaniwe kwa kuhodhi mchakato mzima wa katiba yetu tuitakayo na pia hao wahusika nawaombea mungu awavune vyema kwani wamekuwa ni miti isiyo na matunda mbele za mungu!

Akina majembe,kalambwa na lowaza wanaenda kufanya nini makanisani na misikitini ikiwa wana roho mbaya kiasi hiki?
 
Kuna umuhimu wa kwenda mahakamani kupinga huu mchakato "fake"!
 
hii ni aibu sana halafu ipo na mijitu inayojinadi kutaka kuongoza nchi inaongoza katika uchafu huu wa rushwa.nakuunga mkono mtatiro walipue leo umma uwajue

c.c.yem ni kichaka cha watenda maovu.

Mtanzania kiogope kama ukoma!
 
Ccm bila kufanya uhalifu hawajisikii kama wako vizuri
 
Kwenye ukurasa wake wa facebook,Mtatiro ameandika ujumbe ufuatao akiwatuhumu mawaziri wa CCM kuhujumu mchakato wa katiba mpya.

Mh.Mtatiro ameandika:

Jana waziri Maghembe amewaita wawakilishi wa wafugaji waliomo kwenye bunge la katiba,amewaandalia chakula cha kutosha,vinywaji vya kutosha na viburudisho vingine,huku wakipewa bahasha za nauli baada ya vikao vya siri.

Waziri wa elimu,Shukuru Kawambwa,jana pia amewaita wawakilishi wa vyuo vya elimu ya juu walioko katika bunge la katiba na kuendelea na mchezo huo.

Mhe.Lowassa pia leo amekutana na wafugaji na wakulima walio wajumbe wa bunge la katiba kwa mfumo huo huo.

Hoja zao wanapokutana na makundi hayo ni kupiga chapuo kura ya wazi na kupinga ya siri,huku wakieleza namna CCM inavyopinga baadhi ya mapendekezo muhimu yaliyomo katika rasimu ya katiba.

Mh.Mtatiro ameongeza kuwa,wanachofanya mawaziri hawa ndicho kinachofanywa na mawaziri wengine wa CCM,ni agizo la lazima ambalo hivi sasa linatumika hapa Dodoma.

Leo,CCM na mawaziri wanatumia fedha na kutoa rushwa ili kupitisha matakwa yao.Masuala haya yana ushahidi,kesho nitayasema bungeni kwa uwazi kabisa.

MY TAKE:
Hizi ni tuhuma nzito sana!

Je,TAKUKURU wanachukua hatua gani?

Je,Raisi Kikwete hajua kinachoendelea?

Je,ni kweli Raisi Kikwete ana nia njema ya kupata katiba mpya kama anavyosifiwa?

Yetu macho na masikio!
Simiyu Yetu wewe upo kwenye bunge la katiba saidia hapa na weka ushabiki wa chama pembeni
 
Last edited by a moderator:
Pole sana mkuu, nadhani hajiamini kwa nn atutafute maneno ya kwenda kusema mjengoni? nilidhani kama ana hoja angeanza kwenda kuisema ndani ili tuone anajengaje hoja katika hili. sasa kwa vile anawaogopa hao cc yemu ndio maana anatafuta sapoti
 
Tamko la nec ya ccm lilikuwa wazi.. wanataka serikali mbili na ndo hiyo itakayopatikana huko Dodoma.. Wanaodhani kutakuwa hoja za kupambanishwa wanajidanganya.. Matokeo yalishapangwa..
 
Malalamiko kila siku wizara hazina fedha, miradi ya maendeleo haitekelezwi, watumishi hawalipwi stahili zao.
But haya ndio matumizi ya fedha za walipa kodi... Mimi ntaichukia CCM milele...
 
Wala hapo sishangai, lakini Waj ue kuwa: kura ya wazi ikipita bungeni nasi uraian tutapiga kura ya wazi
 
Ukizungumzia rushwa kama ni kweli iweyo yeyote ile na inapata baraka ya viongozi wa nchi hii ujue hao TAKUKURU wameshaagizwa wakae pembeni..lakini ki ukweli CCM yetu imeharibu nchi katika suala la RUSHWA..ni vigumu tena sana kupata haki kwa mtoa haki bila kutoa rushwa..ni vigumu kuwa kiongozi ndani ya chama bila rushwa. Yaani asilimia 90 ya wanachama wa ccm kwanaamini rushwa ni haki yao wqlq sio adui wa haki..viongozi wetu wamewafundisha hayo ati..da siamini hilo linalosemwa km liko na ukweli lakini mwenendo wa CHAMA chetu siku hizi mmmh yawezekana kabisa
 
haya mambo nilijua tu yatatokea,ccm hawapendi haki kwa sababu mapendekezo yao yamekaa kimslahi ya chama tu na si kwa wananchi wote,so wanatumia rushwa kuwashawish wajumbe,Mungu wape mioyo migumu hawa wajumbe na uwape roho ya kuwa wazalendo zaidi ktk nchi yao.
 
Back
Top Bottom