I was talking about his dark side
Even dark of his, umeweka uwongo mwingi sana. Juma Njemba aliowa wake kwa dini ya kiislam, aliishi an wake wanne, akihitilafiana au kufiwa na mke aliongeza mke kwa kuoa mwingine. Hakudhulum mke wa mtu, alichumbia na kukubaliwa akaowa, alipokataliwa posa take hakuoa na hakudhuru mtu.
Pia umeandika kuhusu kuacha na kudhuru wenzi wake aliotalakiana nao, jambo ambalo si la kweli, mke wake wa kwanza akiitwa Bi. mtumwa bint Ali Saad, mwanamke huyu aliishi toka ujana hats kifo na mumewe na hawakujaliwa kupata mtoto.
Mke wake wa pili akiitwa Hawa bint Almas Msano mpaka leo anaishi Sengerema Mwanza amekuwa ajuza kwa umri wake alizaa nae bint aliyeitwa Asha.
Mke wa tatu sikumbuki jina lake lakini alizaa watoto wawili mmoja akiitwa Lwamba na Mwingine Mwamvua. Mwanamke huyu waliachana muda mrefu kwa mke huyu kurejea kwao Urambo ambako kaka yake alikuwa na uchumi hivyo aliamua kuachana na ndoa kuendelea kusimamia uchumi (pengine walikuwa na yao) lakini hakumuuwa wala hakukuwa na madhara, mama huyu kafa mwaka juzi 2016 Tanga Mjini.
Alimuoa pia mama wa kisenegal akazaa bint akiitwa Johari, mama Yule walitengana na hakumdhuru alifariki mwaka 2014 akiwa mtu mzima.
Alimuoa mwanamke mwingine akazaa nae mtoto wa kiume akiitwa Mwinyimbegu yupo mtu huyu pale Kigoma Ujiji na mama yake yu hai na hana madhara.
Alioa mwanamke wa kiha akiitwa Bora bint Maulid mungo mkuyu huyu kazaa nae watoto wanne. Wawili wa kiume wapo Dar Es salaam pale jiran ya Meeda Bar Sinza. Tena wapo na mama yao ambaye aliishi na marehemu mpaka kufa kwake. Na wawili wa kike mmoja ni mwalimu Mwanza na mwingine yupo huko Ujiji kwao.
Hivyo umeweka chumvi ya kutosha.
Lipo suala la kuuwa watu, lipo suala la uchawi nk tote uzushi.
Ila yupo aliandika hapa kuwa zama zile za ufanyaji wa biashara za magendo, mzee Yule alikuwa na ujuzi wa kukupa maandishi katika elimu yake ya kitabu na sio mti wala kizimba wala tunguri wala uchawi Bali ni katika uwezo wa elimu yake ya kitabu, basi utakuwa salama bila kukwaruzana na askari wala kukamatwa kwa Mali yako.
Ni hakika kuwa hakuna aliyekuwa akijipendekeza kwake, Bali aliheshimiwa mno, maana hakuwa akipenda waha na wamanyema kuonewa, maskini kuonewa, wanawake na watoto kuonewa hakupenda.
Siku moja akiwa darasani kwake akisomesha elimu zake, alitokea mama mmoja akamshitakia kuwa mwanafunzi wa huyu mzee akiitwa xxxxxxx Kamo (amekuwa marehemu),alikuwa akimtaka kimapenzi kwa lazima akisema anapata masomo yenye kuburi kubwa za Juma Njemba akikataliwa atamfanyia kisomo na kumdhuru.
Mzee Juma alimuondoa masomoni mtu huyu kwa tuhuma ile akisema elimu yake ni kinga kwa watu dhaifu kutokana na mabavu ya wenye nguvu.
Kesho nitasimulia kiss chake na Mkuu wa Mkoa Kannal Mahhawa aliyeonjeshwa joto la jiwe la elimu ya mzee huyu.
Pia nitasimulia kiss cha mtumishi mwenye dharau kwa wazee alivyoikimbia ofisi kwa kuona Simba.