BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) imekemea vitendo vya utekaji, ukatiili na mauaji yanayofanywa na genge la watu wasiojulikana na kulaani tukio la kuchukuliwa na kuuawa kikatili kwa kada wa Chadema, Ally Kibao.
CCT ni Taasisi inayowakilisha Umoja wa Madhehebu ya Kikristo ya Kiprotestanti pia inaundwa na makanisa mbalimbali wanachama na vyama vya Kikristo au vyenye mwelekeo wa kikanisa kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Tayari Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameeleza kusikitishwa na mauaji hayo na kuagiza vyombo vya uchunguzi kumpelekea haraka taarifa ya kina juu ta tukio hilo na mengine ya aina hiyo.
Katika ujumbe wake kwa Mwananchi jana usiku, Septemba 8, 2024, Mwenyekiti wa CCT, Askofu Fredrick Shoo amesema sasa ifike mwisho kwani inaumiza kila kukicha kusikia taarifa za watu kutekwa, kufanyiwa ukatili na kuuawa na watu wasiojulikana.
“Watanzania tumefika huko? Ndio njia tumeamua kuiendea? Hao wafanyayo hayo sasa wanaonyesha wazi, tena mchana kweupe kuwa hawamwogopi yeyote, chochote, wala hawana hofu ya Mungu tena,” amesema Askofu Shoo na kuongeza.
“CCT tumesikitishwa sana na mauaji na ukatili wanaofanyiwa Watanzania wasio na hatia. Tunakemea vikali utekaji, ukatili na mauaji yanayoendelea nchini kwa sasa.”
“Mnaofanya hayo iwe ni kwa sababu yoyote ile, mjue yupo Mungu, nasi tutamwomba adhihirishe wazi uwezo na mamlaka yake. Mungu hadhihakiwi,” amesema.
"Kama mnayafanya hayo ili kuwajaza watu hofu, jueni Watanzania tunasema kwa haya hatuogopi wala hatutaogopa. Tunayakataa, kuyapinga na kuyakemea wazi,” amesaema Askofu Shoo ambaye pia ni Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya KKKT.
Katika maelezo yake, kiongozi huyo wa kiroho amesema: “Kama lengo lenu ni kumchafua Rais wetu ili mikono yake ijae damu za watu, jueni kuwa mmeshashindwa na mtashindwa vibaya, kwa maana Mungu atatenda jambo."
Mkuu huyo wa KKKT mstaafu amesema: “Tunatoa wito kwa Watanzania wote waombe kwa dhati na kukemea vitendo hivi viovu vinavyotaka kutishia usalama, haki na amani kwa raia wa nchi yetu."
MWANANCHI
CCT ni Taasisi inayowakilisha Umoja wa Madhehebu ya Kikristo ya Kiprotestanti pia inaundwa na makanisa mbalimbali wanachama na vyama vya Kikristo au vyenye mwelekeo wa kikanisa kutoka Tanzania Bara na Visiwani.
Tayari Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameeleza kusikitishwa na mauaji hayo na kuagiza vyombo vya uchunguzi kumpelekea haraka taarifa ya kina juu ta tukio hilo na mengine ya aina hiyo.
Katika ujumbe wake kwa Mwananchi jana usiku, Septemba 8, 2024, Mwenyekiti wa CCT, Askofu Fredrick Shoo amesema sasa ifike mwisho kwani inaumiza kila kukicha kusikia taarifa za watu kutekwa, kufanyiwa ukatili na kuuawa na watu wasiojulikana.
“Watanzania tumefika huko? Ndio njia tumeamua kuiendea? Hao wafanyayo hayo sasa wanaonyesha wazi, tena mchana kweupe kuwa hawamwogopi yeyote, chochote, wala hawana hofu ya Mungu tena,” amesema Askofu Shoo na kuongeza.
“CCT tumesikitishwa sana na mauaji na ukatili wanaofanyiwa Watanzania wasio na hatia. Tunakemea vikali utekaji, ukatili na mauaji yanayoendelea nchini kwa sasa.”
“Mnaofanya hayo iwe ni kwa sababu yoyote ile, mjue yupo Mungu, nasi tutamwomba adhihirishe wazi uwezo na mamlaka yake. Mungu hadhihakiwi,” amesema.
"Kama mnayafanya hayo ili kuwajaza watu hofu, jueni Watanzania tunasema kwa haya hatuogopi wala hatutaogopa. Tunayakataa, kuyapinga na kuyakemea wazi,” amesaema Askofu Shoo ambaye pia ni Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya KKKT.
Katika maelezo yake, kiongozi huyo wa kiroho amesema: “Kama lengo lenu ni kumchafua Rais wetu ili mikono yake ijae damu za watu, jueni kuwa mmeshashindwa na mtashindwa vibaya, kwa maana Mungu atatenda jambo."
Mkuu huyo wa KKKT mstaafu amesema: “Tunatoa wito kwa Watanzania wote waombe kwa dhati na kukemea vitendo hivi viovu vinavyotaka kutishia usalama, haki na amani kwa raia wa nchi yetu."
MWANANCHI