Pre GE2025 Jumuiya ya Wanafunzi wa Sayansi ya Siasa: Tumesikitishwa Wanafunzi UDSM kutakiwa kuwa na kadi ya CCM ili wasaidiwe kupata mkopo

Pre GE2025 Jumuiya ya Wanafunzi wa Sayansi ya Siasa: Tumesikitishwa Wanafunzi UDSM kutakiwa kuwa na kadi ya CCM ili wasaidiwe kupata mkopo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
photo_2024-08-17_16-20-00.jpg


YAH: TAARIFA KWA UMMA.​
Jumuiya ya Wanafunzi wa Sayansi ya Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUPSA) tumesikitishwa na kulaani matukio na taarifa zifuatazo.

Mosi, Tangazo la Kiongozi wa Chama Cha Mapinduzi Tawi la Chuo Kikuu Dar es Salaam ndugu Goodluck Evarist la kuwataka wanafunzi ambao hawajapata mkopo na walio na mkopo mdogo wawe na kadi ya Chama ili wasaidiwe, sisi DUPSA tunalaani Tangazo hilo la kibaguzi lenye lengo la kutugawaya hivyo tunaungana na taarifa ya bodi ya mkopo (HESLB) la tarehe 13/08/2024 kupinga kauli hiyo.

Pili, Tunalaani Tangazo la DARUSO MLIMANI kupitia wizara ya Habari, sayansi na teknolojia la tarehe 14/08/2024 la kuzuia wanafunzi kutoka na kupokea taarifa kwani ni kinyume cha katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 18(1) na (2). pia ni kinyume cha katiba ya DARUSO Mlimani ibara ya 1(v). Hivyo Tangazo hilo lipuuzwe.

Tatu, Tunalaani na kupinga kauli zote za kibaguzi, kichochezi na zenye lengo la kutugawanya, kusambaza chuki au kuminya haki za msingi za watu zinazotolewa na viongozi wa DARUSO Mlimani na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa kwani ni

kinyume cha falsafa ya Mh. Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya 4R. Aidha, DUPSA inawataka wanafunzi, viongozi wa DARUSO Mlimani na vyama vya siasa kufuata Katiba, sheria, taratibu, kanuni na miongozo tuliyonayo iliyopo chuoni. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki DUPSA Asanteni.

Pia soma:
~ Wanafunzi UDSM tuliokosa mikopo 2023 na waliopata mikopo kidogo tunaambiwa lazima tuwe na Kadi ya CCM ndio tutahudumiwa
~ HESLB yafafanua madai ya Wanafunzi UDSM kutakiwa kuwa na Kadi ya CCM ili wapate mkopo
 
Back
Top Bottom