Juventus Torino waweza waita Juve.
Jina lao la utani ni Bianconeri.
Kama ilivyo kwa rossoneri yaani nyekundu na nyeusi Bianconeri inamaanisha nyeupe na nyeusi.
1888 ndipo chama hili lilianzishwa.
Bibi kizee Lavecchia Signora mzaliwa wa jiji la Rome ndio alietoa wazo na pesa kwa ajili ya vijana wa mji wa Torino kuanzisha timu yao.
Hatimae Juve ilianzishwa. Kwa heshima, hatimae wakaazi wa mji huu waliamua kuiita timu Juventus wakiwa na maana ya bibi kizee.
Kwa kuwa bibi alikuwa na kisu basi mara moja Juve iliikamata italy na kutawala soka la nchini humo mpaka miaka 11 iliofuata yaani mwaka 1899 ndipo Juve walianza kuonja shubiri
Kwani tarehe 16 ya mwezi wa 12 klabu ya AC Milan ikaanzishwa
Umaarufu wa Bibi Lavecchia ni mkubwa mno katika mji wa Torino
Kiasi kwamba ukifika katika mji huo kisha ukamuuliza mtu yeyote yule kuwa unamtafuta Bibi mmoja hivi...basi utajibiwa Bibi Lavecchia Signora?
Lakini kwa miaka ya hivi karibuni umaarufu wa Bibi huyu umekuwa ukizidi kupotea kutokana na vijana wengi kutojuwa ama kutojali mchango wake.
Kwa sasa huko katika mji wa Torino kuna Mfalme...
Kuna wakati ilipendekeza wimbo wa klabu ya Juve ufanyiwe marekebisho ili jina la Mfalme huyu liwepo.
Mfalme huyu ni Alexander Peter.
Lakini kwa wenyewe kule Italia anafahamika kama Alesandro del Piero. Katika mahubiri ya Dominica moja huko katika kanisa la Mt Petro lililopo katika Taifa la Vatcan ndani ya Mji wa Roma Papa Yohane Paolo wa pili alionesha kushangazwa kwake na kufuru ya pesa iliofanywa na kampuni ya kutengeneza njumu ya Diadora.
Hayati Papa alionesha kushangazwa kwake na mkataba wa Diadora kwamba watamlipa Del Piero akicheza kwa kila Dakika, watamlipa akifunga goli la kawaida na watamlipa akitupia kwa free kick...
Del piero akawa mchezaji anaelipwa mpunga mtamu kuliko mcheza soka yeyote Duniani...
*dominica = Jumapili
Basi umaarufu wa Del Piero ukawa mkuubwa zaidi baada ya alfajiri moja iliokuwa ya majonzi kwa wakazi wa mji wa Torino.
Majonzi hayo yalitokana na chama cha soka cha Italia kuafiki klabu ya Juve ishushwe daraja kwa kosa la kupanga matokeo...
Andrea Agnelli bosi wa Juve wakati huo anasema alikuwa macho usiku kucha akiwaza maisha mapya ya serie B yatakavyokuwa. Ghafla mapema alfajiri akapokea simu kutoka kwa nahodha wa klabu yake...anasema kabla hajapokea simu hio akawaza kuwa Del alikuwa anataka kumwambia kuwa ataondoka klabuni hapo hivyo atafute nahodha mwingine...
Lakini la hasha haikuwa hivyo. Baada ya kupokea simu na kusalimiana na Del Piero hatimae Del akamwambia kuwa yeye ni Juve na Juve ni yeye, hivyo yupo tayari kufa na Juve hata wngetakiwa washuke hadi serie C
.
Agnelli anasema hakuweza yaamini maneno ya Del..
Na mara alipokata simu akapokea simu nyingine toka kwa mdogo wake akimtaarifu kuwa atazame chanel moja ya TV ya mji wa Torino..
Na alipowasha TV akakutana na breaking news kuwa Golikipa Gigi Buffon amekubali kushuka na timu.
Anasema baada ya usiku wa huzuni hatimae aliaanza kurukaruka kwa furaha...
Na furaha yake ilikamilika mwendo wa saa tano asubuhi baada nyota wawili Nedved na Trezeguet kukubali kushuka na timu hio.
Wasaliti walikuepo tangu enzi ya Yesu na wasaliti hawatoisha, kwani wasaliti walijitokeza hata baada ya Juve kushuka daraja...Ibrahimovic, Canavaro, Thuram, Zambrotta, Vieira hawa ni wasaliti wakubwa na laana litawaandama milele
Forza Juve
Sempre Juve