JWTZ: Baada ya siku 7 atakayepatikana amevaa, anatumia au anauza mavazi ya Jeshi atapatiwa adhabu kali

JWTZ: Baada ya siku 7 atakayepatikana amevaa, anatumia au anauza mavazi ya Jeshi atapatiwa adhabu kali

Waliotunga sheria za Dunia hawana noma maana unaweza kuta kifaru cha jeshi kinauzwa mnadani
Nguo ndio kabisa mpaka makazini watu wanavaa tu
Ila kama kwetu watu wanazivaa kwa ujambazi na utapeli au kujionyesha kuwa na wewe ni mjeda basi wapigwe tu
 
Nguo zenyewe zinashonwa na kina Manji na mihuri yote mlimpa huku mnakuja kunyanyasa wachimba chumvi tuu kama mna maadili mngeanza kutengeneza wenyewe hizo nguo zenu maana hazina hata fashion wala kubadilisha rangi mnashindwaje kutengeneza wenyewe ninyi mpo busy kuwapa wahuni wawatengenezee harafu hao hao baadhi wanaziuza kwenye maduka ya mtaani...
 
Nataka nione Mbowe,Lissu,Mnyika,UVCCM n.k wakizipeleka,na picha zipigwe,wakikabidhi.Isije ikawa tamko tu,jeshi la wananchi wataanza kuonekana wa kawaidakawaida endapo tamko limetolewa,halafu likachukuliwa tofautitofauti.
 
Ni haki kabisa kupewa adhabu kali hata fazi laki polisi hadi waombe ruhusa kama wanaigiza
 
Wenzao wanapambana kujiongeza kwenye technology wao wamebaki na nguo.Kila siku nguo hivi nguo vile Afrika bhn
 
inahusisha aina zote za majeshi au n sare za jeshi la hapa tz tu?
Yote mtu akikutapeli kavaa hayo manguoya majeshi utakuwa mgeni wa nani wewe?

Ukiona yeyote kavaa miguo ya jeshi lolote wakati sio mwanajeshi jeshi lolote ripoti polisi haraka kituo.karibu yako cha polisi

Mpige hadi picha chap kama una simu jana kisha waonyeshe
 
Mnatafuta raia wa kufanyia mazoezi, ombeni Sudan 🇸🇩 mkasaidie kurudisha amani
 
wakimaliza kutoa adhabu waombe mechi hata na congo silaha zitashika kutu
 
Yote mtu akikutapeli kavaa hayo manguoya majeshi utakuwa mgeni wa nani wewe?

Ukiona yeyote kavaa miguo ya jeshi lolote wakati sio mwanajeshi jeshi lolote ripoti polisi haraka kituo.karibu yako cha polisi

Mpige hadi picha chap kama una simu jana kisha waonyeshe
sawa mkuu nmekuelewa
 
Kama wanaongelea kufuata sheria, na wanasisitiza hivyo, basi Jeshi linapaswa kuwa mfano wa kufuata hizo sheria. Kwa kuanzia waanze kwa kupeleka malalamiko yao Polisi.

Polisi ndiyo wenye mamlaka ya kufuatilia hilo, waachane na jungle minds, zama zimebadilika hizi wanapaswa kujua majukumu yao yanapoishia. Tunalipenda na kuliheshimu Jeshi letu, so linapaswa kutambua misingi, sheria kanuni na mipaka ya majukumu yao.

Kwa Jeshi kupeleka malalamiko yao Polisi, siyo unyonge, bali itadhihirisha kuwa ni Jeshi linalojitambua, na linalotambua majukumu yake na ya wengine, na mipaka yake, zaidi itaibua hali ya Wananchi kufuata sheria na kwamba kumbe kufuata sheria siyo unyonge au utumwa bali ni ustaarabu na kujitambua.

Nguvu za hizi taasisi zinaundwa kutokana na sheria. Uhamiaji ilikua ni idara tu, sasa hivi baada ya muswada kupitishwa na kuwa sheria, Uhamiaji hivi sasa ni Jeshi kwa mujibu wa sheria iliyoliunda, na kuna sheria zinazoelekeza aina ya silaha wanazopaswa kutumia wawapo kazini, pia wanazoruhusiwa kuwa nazo popote hata majumbani.

Sheria ndiyo inaelekeza aina ya mafunzo gani yatolewe kwa Jeshi lipi, siyo kwa sababu labda Jeshi fulani ni noma kuliko lingine.

Sheria ikibadilishwa inaweza kupelekea JW inakua Polisi na Polisi wakawa JW. Tuachane na jungle minds, those days are long gone.
Mkuu hongera kuwa open minded.

Huu mjadala siyo mpya, wala matamko ya Jwtz kuhusu mavazi yenye kufanana na sare za jeshi siyo mapya, huibuliwa na kusinyaa kwa sababu si ya kisheria, huu ni mwendelezo tu wa ubabe wa kunyanyasa raia.

Huyo mwanajeshi aliyesimama kwenye mimbari kutoa msimamo huo wa jeshi kuhusu jambo hilo, hakuandaliwa.

Nimesema hivyo kwa sababu, maswali yote muhimu aliyoulizwa na waandishi wa habari ambao ni ma lay man katika masuala ya kijeshi hakuyajibu ipaswavyo kiweledi ama aliyakwepa.

Mimi hapa nitajikita katika mambo kadhaa kwa kuwa siyakumbuki yote yaliyoongelewa:

La kwanza na la muhimu likiwa ni mapungufu ya wazi ya kisheria katika jambo hilo.

Katika kumiliki haki ya bidhaa(brand)yoyote, kuna process za kufuatwa ili mtu ama taasisi kupata haki miliki.

Jambo hilo linafahamika na sitalielezea.

Je Jwtz ina haki miliki ya mavazi wanayoyatumia kwa sasa ambayo wanaagiza tu kupitia mzabuni yeyote ambaye huyanunua popote kutoka kiwanda chochote cha ndani ama nje ya nchi?

Je ni rangi gani ama maua gani ya mavazi ambayo rasmi kisheria yanayotajwa kuwa ni ya jeshi katika context yake hiyo?

Na ni jeshi gani aliloliongelea yeye?

Labda tumkumbushe taratibu ambazo kwamfano sare gani za Jwtz zivaliwe ambazo hufuatwa, yeye msemaji hakuzielezea!

Katika sheria za kijeshi, The Defence forces regulations Vol.1, zimeeleza wazi kuwa sare zinazovaliwa na staff wa Jwtz kwa wakati husika kibali chake hutolewa na mkuu wa majeshi.

Kwa hiyo wanavyoonekana leo, kesho waweza kuta wamebadilishiwa kutokana na matakwa ya mkuu wao wa majeshi(Cdf) na bila majadiliano yoyote.

Pia katika The Defence forces regulations vol.1 hiyo, Sheria zinajibu swali la mwandishi wa habari kuhusu wasanii na waigizaji, ambalo yeye alishindwa kulijibu.

Ni kwamba wasanii ama waigizaji wanapotaka kutumia mavazi ama vifaa vya kijeshi kuigizia,sheria zinawaelekeza wapeleke maombi yao Makao makuu ya jeshi kwa kibali period!

Sasa mitaani kwenye maduka ya nguo kumejaa vitambaa vyenye rangi mbali mbali ambazo zinatumiwa na majeshi yetu, vikiwemo vya kijani, vyeupe, blue, vyekundu na vyeusi vinavyotumiwa na wanajeshi.

PT na uhamiaji ni vyeupe, blue, khaki na jungle green.

Ugoro na kijani wanavyotumia MT nk nk.

Kwa hiyo rangi zote za maana wameziwin wanajeshi, sasa sisi raia tuvae rangi gani sasa!

Je kutoa tamko la jumla jumla haoni kwamba analeta mtafaruku kwa wafanya biashara wa nguo nchini?

Je marobota ya nguo hizo yakizuiliwa kuuzwa ni nani atakayefidia hasara hiyo?

Hiyo sheria anayoitetea ama "makosa" aliyokemea yameanza leo?

Kwanini kipindi hiki?

Au kwa sababu hivi karibuni Mbowe alionekana kuhutubia kwenye mkutano flani, nyuma yake kasimama mtu kama mpambe katinga gwanda?

Je tukisema Jeshi letu limeanza kujiingiza kwenye siasa ama kutumiwa na wanasiasa watasemaje?

Suala la mavazi ni mtambuka, asilione lirahisi namna hiyo, maana linagusa mpaka uchumi wa nchi ajue!

Hivi kufanya uhalifu ama mhalifu anaweza kuvaa sare za kijeshi mchana bila ya kugundulika kirahisi?

Au raia lay man anaweza kuvaa vazi la kijeshi na kujfanya mwanajeshi, yaweza pita kutwa nzima hajadakwa?

Uanajeshi siyo mavazi tu, ajiulize concentration ya vita namna wanajeshi wasiofahamiana ambavyo hukusanywa na kuchanganywa pamoja kumkabili adui, hufahamiana kwa mavazi pekee?

Kitu gani huwafanya watambuane?

Jamani acheni raia wema wajivalie mitumba yao waliyoinunua kwa jasho jingi.

Kwa wapenda makesi wakiingia kizimbani kwa issue kama hizi hakuna sheria hapo itakayo waadabisha.
 
Mkuu anzisheni kitengo cha technology...mfanye project za kitechnology kama kutengeneza drones...
Mtengeneze OS yenu..mtumie jeshini na sio windows OS
Alafu kambini..wanajesh wasiingie na smartphone
 
Je, watatoa fidia kwa walionunua kwenye mitumba? Tupo ambao tunazo pochi, peni, fulana, tochi, chupi na vingine vingi vinavyikuja kwenye vifaru vikiwemo vifaru na vigari vya watoto.
Umeuliza swali zuri sana.

Hilo la kwanza, la pili ni kwamba rangi zinazotumiwa na majeshi yetu ni nyingi sana, kuna nyeupe, nyeusi, kijani, bluu, nyekundu, ugoro, grey, njano nk nk.

Sasa rangi hizo ndiyo rangi pendwa za vitambaa vya suti madukani, kwa hiyo raia wafunge biashara?
 
Jeshi limeshindwa kukaa bandarini na border kuhakikisha sare haziingii au wao kazi yao kutisha raia???


Kwamba waleta unga wapo salama mateja ndo wakukimbizwa???
 
Swali langu je vipi kwa nguo za watoto wa miaka 2, 3 nazo ni haramu? hizo wanazoita zenye ufanano, ili tujue mapema tuzigeuze pyjama.
 
Back
Top Bottom