JWTZ mpaka leo imeshindwa kuajiri wasomi wenye vipaji halisi, sababu hizi hapa...

JWTZ mpaka leo imeshindwa kuajiri wasomi wenye vipaji halisi, sababu hizi hapa...

mada ilikua nzuri ila mmeiaribu kwa mashindano yasiyona maana.sijui lini watanzania mtatumia akili
 
Ukiangalia mfumo mzima wa ajira utabaini yafuatayo
1. Waalimu waliopo vyuoni 90% ni kikwazo kwa wasomi wengi wanaojiunga na jeshi hilo, akitokea mwanafunzi mwenye elimu kubwa hata Phd watafanya kila mbinu wamfukuze kwa kisingizio cha utovu wa nidhamu au watacomment kuwa kafeli.

2. Trainning zao hazija base kutafuta vipaji vya kweli katika nyanja muhimu kitaifa, kama vile madaktari, Eng, nk. Mfano Nyumbu mpaka leo wameshindwa kuifanya iwe ya kizalishaji toka enzi za mwalimu. Lugalo mpaka leo hawana hata blood bank sababu wanasayansi tiba hawapo ndio maana wanashindwa kukabiliana na migomo ya MH, sababu huko wengi 80% ni AMO na CO.

3. TMA ni kikwazo kikubwa sana katika kuwapata wasomi wazuri ndani ya jeshi hilo, elimu ya rasilimali watu kwa waalimu inawezekana ikawa ni issue. So they are trying to reduce the number of students kwa visingizio vya nidhamu ambayo ukifuatilia kiundani sio nidhamu as such but ni kutojua ubaya wakumfundisha mtu at certain level na kumwachisha mafunzo. HILO N BOMU BAADAYE.

4. Mazingira dhaifu kuwawezesha wenye vipaji kubuni kwa uhuru na kutumia taaluma zao, kufanya tafiti chanya maeneo yao ya kazi, mpaka leo hatujaziona.

5. Officer aliyetokea uraiani moja kwa moja I mean those who have got a little knowledge kuwa mkufunzi, atafundisha nini kama sio kupika majungu na kukosa comfidence?

Hayo machache yaliyobainishwa hapo juu ni chanzo kikubwa cha jeshi letu kuwa kama lilivyo hivi leo.


jeshi waanajiri watu....makini kutoko vyuo makini ...kwa mfano kama mfano vyuo kama
1.udsm
2.mzumbe
3.d.i.t
4.sua
ni vyuo ambavyoo hutoa wasomi bora....ndo maana jeshi huamini vijana toka huku sasa kama wewe ulisoma chuo cha kizushi karisit mitihani ya form 4 na 6...ili uende ukasome vyuo hivi vyenye ubora utapata tuu kazi tuu jeshini
 
Wanaojua mambo ya jeshi na wajue na wasiojua mtafute nafasi muingie kama mna qualifications zinazohitajika maana hata kwa kosoma mitandaoni sidhani kama mtajua ile reality ya ukiwa mafunzoni jeshini. Mtoa mada nadhani atakuwa alishindwa pale TMA au hakupita kwenye interview pale KUNDUCHI. Huko kinachoangaliwa ni OBEDIENCE TO LAW, RULES AND AUTHORITY ONLY.
Sasa kama wewe ulienda na degree au masters yako then ukawa unajifanya wewe ni mjuaji kwa wale maaskari, hiyo imekula kwako kaka. Jambo la kwanza ni lazima utolewe URAIA kwa mambo ambayo unaweza sema wanakudhalilisha na wengi hapa ndipo wanapotorokaga au kuonesha jeuri zao ambazo zinawaletea shida na mwisho kufukuzwa kama si kuishi maisha ya taabu na wakufunzi. Yangu hayo na Heri ya mwaka mpya
 
Sio siasa fikiri kwa kutumia akili kichwa na sio ma...
Huwa makalio yangu yanafikiri kwa kina zaidi kuliko kichwa chako, na wewe unajua hilo ndio maana uka refer!
sasa nikija tumia kuchwa hutaona ndani!
 
Maisha si lazima uwe mwajiriwa wa JWTZ tu, kama unajiona una CV ya kutisha tafuta Taasisi zingine ambazo zitakunyenyekea pamoja na unanga wako, kiburi chako na utovu wako wa nidhamu, kisha na mavyeti vya kununua toka ulikotoka !!
Kwa taratibu za kkawaida tu, ukishindwa kumheshimu mdogo, je huyo wa juu yako utamheshimu kweli kwa dhati au ndio unafiki !!
Jiunge na siasa uingie Bungeni, ili umalizapo tu kiapo uanze kuwahadaa Wa-tz kwa Mikataba ya kuliuza Taifa !!
 
Kwanza kabisa nasikitika sana kwa kauli zako za kipumbavu na za mtu asiyeelewa kile anachokizungumzia. Wewe uko nje ya mfumo wa kijeshi unafahamu nini kuhusu jeshi wewe? Hivi unajiona wewe ni bora kiasi gani kuliko wasomi walioko jeshini? Kweli mjinga atabaki mjinga tu hata kama akipitia chuo. Hizo kauli ulizozitoa zinadhalilisha taaluma yako. Jeshi ni mfumo unaojiendesha kwa utaratibu wake, na ndio maana mtu anakuwa tayari kukutana na adui ambaye hata kama wewe ungekuja na kipaji chako (cha kupiga majungu??) ungeishia kupoteza fahamu. Hiyo peke yake ni profession, ambayo ina mfumo wake. Sasa kama unafikiri kuwa na vipaji maalum ndio kufit jeshini, ni heri ukafunga domo lako na ukamwaga heshima kwa watu waliojitolea kukulinda mburura kama wewe. Si tu kwamba hufai jeshini, ni kwamba hata kwenye ajira binafsi hutofaa kwa vile huna nidhamu na pia uelewa wako ni mfinyu mno. A fool at his best!

(Nimesimama mguu sawa na kupiga saluti) Afande umeua!
 
inaonekana kama ulifukuzwa monduli...,

kwa kifupi, pamoja na kipaji ulichonacho nidhamu ndiyo pillar ya mafunzo yako,, jeshi ni nidhamu, period! Na nidhamu ndio inaleta ufanisi kwenye uwanja wa vita, unapotoa amri mfuasi akatumbukize hand grenade kwny kifaru cha adui, hatakiwi kujiuliza hata kwa sekunde moja.., na hii nidhamu inajengwa kwenye mafunzo, ndio maana jeshini kuna adhabu za kipuuzi kabisa,, mfano unaambiwa umwagilie maua wakati mvua inanyesha,,, ukileta mambo ya logic utaona kua mkufunzi wako ni mpuuzi hana akili,,,, lakn thts part of disciplining you,, ufanye ulichoamrishwa hata kama hupendi,, na hii sio kwa jwtz tu, proffesional armies zote wana namna mbalimbali ya kufundisha nidhamu..,

Kuhusu kuajiri vipaji,,, kwa hili nakubaliana na ww kabisa kwamba japo jeshi linaajiri wasomi na siku za karibuni wanaajiri kwa wingi zaidi, ila bado kuna upungufu mkubwa sana wa wasomi wa fani mbalimbali,, lakini pia tutambue jwtz ipo kwenye transition period,,, kuna individuals ambao hawapendi kabisa hawa watoto wasomi wanaingia na kutoka na manyota fasta,, resistance kwenye change lazima iwepo, ila in general jeshi limeamua liwe dogo na la kisomi na ndio maana kwa sasa hakuna std 7 anaajiriwa wote ni form four and above unless ni mwanamichezo au ana kipaji flani cha sanaa...,

Ukiondoa isolated incidents za wakufunzi wachache kuwachukia wasomi,,, wakuu ngazi za juu wanataka jeshi dogo la kisasa na la wasomi..., na pale monduli bana ukichukiwa na wakufunzi,,, chances za kumaliza ni ndogo sana,,,

Nawaasa watakaopita interview inayokuja hivi karibuni,, pale monduli jishushe,, ni yes sir, yes staff, hata kama task ulopewa logically doesnt make sense

For me, this is the best comment

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ratio nota Masada amekurupuka,
anaongea vitu ambavyo Hana detail navyo,kutengeneza ofisa aw jeshi sio kazi raisi Kama unavyodhani, ukija module degree Chako unakiacha Getini, pale wote ni cadet
 
For me, this is the best comment

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Good comments, lakini msiwalaumu wakufunzi wa JWTZ kwani mfumo mzima wa vyuo vyetu ni wa kivita kati ya mwalimu na mwanafunzi, mwalimu anajisikia raha au bingwa kufelisha kundi kubwa la wanafunzi na anapata support kubwa na maelezo ni kuwa wanafunzi ni vilaza. Inakuaje mwanafunzi tangu darasa la kwanza anafanya vizuri mpaka form six, halafu chuo anakua kilaza???

Inawezekana wanafunzi ni tatizo lakini nafikiri kunahaja yakuangalia kwa undani hili suala. Mwalimu akimchukia mwanafunzi basi atafeli, why? kwa maslahi ya nani??? Taifa kweli litaendelea hivi!!!! Nionavyo mimi wengi wanaofanya hii kazi ya uwalimu/ukufunzi wamelazimishwa aidha na mazingira au na mfumo, kwani binadamu wakawaida atapenda kusifiwa au kujisifu kwa matokeo ya kazi nzuri aliyoifanya.

Kwakweli itokee mwanafunzi amefeli kwakuwa hana uwezo. Implication ya mfumo huu wa wakunfunzi kuwafelisha au kujisikia hodari kwa kufelisha unawafanya wanafunzi vyuoni kote iwe jeshini au uraiani wasijifunze kwani wakati wote wanawaza kupambana na audui yake mwalimu. Therefore, cheating, hongo na rushwa vinakidhiri kwakuwa kipimo nikufaulu au kufeli kwenye makaratasi. Tubadilikeni jamani, nidhamu isijengwe kwa vitisho, ije yenyewe automatically.
 
Siku zingine ukileta mada hata kama ni ya majungu jitahidi kuukaribia ukweli kuliko huu ----- uliouandika,kuuliza sii ujinga penda kujifunza inaonekana mtoa hoja huna ufahamu wa uliyoyaandika .
 
Nimeupenda huu uzi, unafundisha.unaburudisha na unaghabisha!
 
Moshe Dayan najua when it comes to mambo ya JWTZ uko very deep.
Swali langu kwako ni hili, kama kweli jeshi linafanya reform na kuanza kuajiri wasomi wengi lakini kwa utaratibu wa jeshi hao wasomi lazima wafaulu shughuli ya monduli, na huko monduli ndiko kunatuhumiwa kuwa na matrainer wanoko hasa wale wa vteo vya chini.
JWTZ inafanya juhudi gani kuondoa huo unoko/uonevu ili wataalamu/waomi hao watumie taaluma zao kwa manufaa ya jeshi na nchi kwa ujumla.
Na kwa nchi zilizoendelea wasomi wanaojiunga na majeshi wanakuwa treated ''kinyaninyani'' kama mnavyowafanyia monduli?

Mkuu Mwita Maranya nikuhakikishie tu kuwa duniani kote hakuna kozi za wasomi na wasiosoma. Mafunzo ya kijeshi yako standard no matter what. Ukiwa katika uwanja wa medani bahati mbaya masters yako haitokusaidia kama hujaiva kimbinu. Ndo maana hata corporal ambaye ni competent anaweza kuitikisa nchi. (Nadhani unamkumbuka Iddi Amini). Tena ukihudhuria vyuo vya nje huwezi amini, ni balaa zaidi. Wanakuambia kwamba technology fails, that is why we don't use it in training. Kule kila kitu ni manual tofauti uongo wanaopeana watu. Technology utafundishwa kwenye unit yako sio chuoni. Tatizo wabongo wanafikiri digitali ina affect basic soldiering, no way.Wale wanaotamani kuonda maisha wavumilie kupitia katika kikaango kwanza, ndo wakakae maofisini na bachelors na masters za mambo ya utawala.

Na pale mnaposema vipaji maalum I can't understand what you are driving at? Jeshini vipaji maalum hupelekwa Commando, PT na sehemu nyingine zinazohitaji outstanding performance. Sasa hivi vipaji maalum sijajua ni nini. Nadhani mnamfahamu Balati. He was the greatet leader of all time katika commando, na huyo ni mmoja tu. Alipata bachelor na masters akiwa karibu kabisa na kustaafu. Kumbe basi jeshini kuna askari wengi sana wenye military knowledge ya hali ya juu kuliko most of graduates. Siwapondi hawa, isipokuwa tu kuna notion fulani imejengeka kwamba wasomi wanachukiwa jeshini, lakini ukweli ni kwamba wanaojiita wasomi wengi wao hawapendi kupitia rigorous training. Wanataka watambuliwe usomi wao wakati wa mafunzo kwamba mimi ni daktari, mhasibu, mchimi, n.k. Wakati wa training haya mambo hayana maana yoyote, na ndipo competent corporal ukimtishia elimu yako atakuwa willing kukudhihirishia kuwa katika kile ulichofuata pale, yeye ni zaidi yako. Guys, it is the matter of self discipline, that's all it takes. Otherwise mtabaki ku-lament kila siku kama hamtaki kutambua kuwa military knowledge is a profession in itself.

Daktari akifuzu mafunzo atatakiwa kutibu majeruhi mstari wa mbele, bunduki begani.
Mhasibu atatumia bachelor yake kulipa mishahara mstari wa mbele (vitani mishahara hulipwa kama kawaida).
Logistician atafanya kazi kupeleka logistics frontline (tena hawa huwindwa sana vitani).
N.k. Sasa usipokuwa trained utaperform vipi majukumu hayo? Tusilewe na kazi za jeshi wakati wa amani, kikinuka watu huvua kombati na kujificha, don't be one of them! Just do your part and everything should be fine.

MILITARY TEACHES YOU HOW NOT TO DIE!!!!!!!!!!


Military-Training-Desktop-Wallpaper-1024x768.jpg
 
Asante Nyenyere,

Kama maandishi hayatoshi, picha imefunga kazi! Tatizo la wasomi vijana la kujiona bora kuliko wengine haliko jeshini tu! Hata uraiani ni hivyo! Maofisini ndo kabisa, na bahati mbaya huko wanadekezwa. Pelekeni hoja Serikalini, vijana wote wasomi waende jeshi miezi 4 kabla ya kupata ajira si serikalini tu bali hata Makampuni binafsi.
 
Asante Nyenyere,

Kama maandishi hayatoshi, picha imefunga kazi! Tatizo la wasomi vijana la kujiona bora kuliko wengine haliko jeshini tu! Hata uraiani ni hivyo! Maofisini ndo kabisa, na bahati mbaya huko wanadekezwa. Pelekeni hoja Serikalini, vijana wote wasomi waende jeshi miezi 4 kabla ya kupata ajira si serikalini tu bali hata Makampuni binafsi.

Mkuu unajua kuna watu wnapotoshana sana humu JF. Mwaka 2005 ilivuja video inayoonyesha royal marines (COmmando) wa uingereza wakifanya mazoezi ya magumi uchi wa mnyama. Magazeti na mitandao ilishutumu sana kitendo hicho cha "kidhalilishaji." Hasa kwenye ile sehemu ambapo kuruta alikula mkono hadi akazirai. Sasa "wasomi" wakaanza kuhoji mantiki ya kufanya vitendo kama vile.

_41065204_marines_must_credit.jpg

Kuna jamaa mmoja katika kutoa maoni yake aliandika sentensi moja tu, lakini yenye majibu yoote:

"Gee, army guys being army guys... go figure. "
Na ujumbe huu uwafikie wale woooooote wanaonung'unikia mafunzo ya jeshi. Siri kubwa ya mwanajeshi ni kuwa Mentally tough. Na hii inapimwa kwa kuwa exposed kwenye mambo ambayo logic ya kawaida itayaita upuuzi. Na mambo haya yataendelea kuwa ni upuuzi mtupu kwa wasomi wetu mpaka pale watakapojikuta ni mateka mikononi mwa adui. Hapo watakumbuka kumbe yale yalikuwa mafunzo muhimu mno kwa kukujenga kisaikolojia. Huko watakutana na mambo ambayo kama wasingepitia hivi vipimo vidogo vidogo vya kuambiwa wenye digrii wadeki vyoo, wasingeweza kusurvive hata dakika tano tu. Wangemwaga yooote.

When the going gets tough, the tough get going. What about the weak? Hawa wanakuwa eliminated na ndo hawa hawa wanakimbilia JF kutafuta huruma. No way!
 
Nina master ya Sheria ya LLB natarajia kujiunga na JWTZ mwakani. Inaonekana huyu mdau alisoma chuo Kikuu cha kata cha UDOM na alipata degree ya sheria ya Pichu. Amedhalilisha professional ya Law
 
Wakuu, wengine mnajadili vizuri na baadhi mnapotosha maada. La msingi tuangalie kwanini kama fedha na rasili mali kibao mnazopewa na serikali kuendeshea jeshi letu mpaka leo hatuioni chochote. Mfano Irani wanafanya mambo makubwa sana na kila mtu humu jf analijua. Lkn hili letu halina hata kimoja cha mfano vyote nyie mnababaisha tu. Angalia pale Lugalo hakuna hata research moja inayofanyika kwanini kama kweli mmna weza kufundisha kwa weledi? Msibishe kwa kasumba ambazo hazina maana jitathimini je hiki ninachokisema sio kweli. Sisi tunawajua udhaifu wenu. mnadfai kulifanyia jeshi reform wakati hamjui sababu ya nyinyi kuwa kama mlivyo. JWTZ hamuwezi bila kufanya research mkabadilika kama mnavyotaka. Mawazo mapya lazima muyakubali.
 
Back
Top Bottom