JWTZ yafundisha askari toka Kenya, Rwanda, na Uganda

JWTZ yafundisha askari toka Kenya, Rwanda, na Uganda

Mbona sioni hoja ya msingi ya kujadili hapa?
 
..ni mafunzo ya Officer Cadet course ya mwaka mmoja inayotolewa Tanzania Military Academy, Monduli.

..zaidi ya askari toka CoW, nchi nyingine zilizofaidika na mafunzo toka kwa jeshi letu ni Seychelles, DRC, Mozambique, na Zimbabwe.

..habari hii inazima zile propaganda kwamba Tanzania ina mahusiano mabaya na majirani zake.


habari nzima soma hapa: Home

habari nyingine hii hapa:http://www.dailynews.co.tz/index.ph...congo-president-in-arusha-for-special-mission

cc lawmaina78, jMali, Ngongo, Nguruvi3, Bulldog, Kishimbe wa Kishimbe
kwani wanasoma bure! labda muwe vitani ndio tungeweza kukataa.
 
Last edited by a moderator:
Eti mnamtishia nyau halafu nyau huyohuyo mnaiga stail yake mh
 
Hata mimi sioni hoja hisiyo ya msingi ya kutojadili hapa
Suala la maofisa wa kijeshi kwenda kujifunza mbinu za kivita kwenye nchi nyingine ni la kawaida hivyo siyo ajabu maafisa wa jeshi la Kenya kujifunza kwenye chuo cha maafisa wa kijeshi Tanzania kama ambavyo sio ajabu kwa maafisa wa JWTZ kujifunza kwenye chuo cha maafisa wa kijeshi cha Kenya. Hilo Linatokea kwa nchi nyingi na siyo kwa Kenya, Tanzania, Rwanda! na Uganda pekee.
 
Ukiona Alumni yeyote ta tanzania iko katika nchi ya kigeni, basi ujue kuna mission za udukuzi za ki-intel zinafanyaka.. tanzania has nothing to learn from anycountry in the field ya militarism.

hahahah...Thank you Mkuu, Once again you have revived my strength as patriot and statesman. Thank you once again
 
Tanzania haiana la kujifunza kwenye majeshi legevu ya Rwanda , Kenya wala Uganda wao ndo wanajifunza kwetu sisi tuko imara sana
 
kwani wanasoma bure! labda muwe vitani ndio tungeweza kukataa.

..we have to give credit where credit is due.

..majuzi kuna ma-cadet zaidi ya 300 toka DRC wamemaliza mafunzo yao Monduli.

..huo ni mchango wa Tz ktk masuala ya ulinzi na usalama kwa wananchi wa DRC, na zaidi eneo letu la maziwa makuu.

NB:

..kabla ya hapo JWTZ walifundisha mamia ya askari wa Uganda ambao walikwenda kuanzisha jeshi la nchi hiyo baada ya kuangushwa kwa utawala wa Iddi Amini.
 
..ni jambo la kawaida lakini nani alikuwa anajua?

..nimeileta habari hii ile ku-balance habari mbaya zinazoandikwa dhidi ya Tz ktk magazeti ya wenzetu.

..kuna vyombo vya habari kama rwanda newtimes, the eastafrican magazine, na blog mbalimbali zimekuwa zikiwaaminisha wasomaji wao kwamba hakuna jema linaloweza kufanywa na Tanzania au Mtanzania.

..kwa mfano, kulikuwa na habari ya Tanzania kujitenga, na kutokuchangia chochote kile, ktk East Africa Standby Force. Sasa hailezwi kwamba Tanzania tayari tuko kwenye Souther African/SADC standby force, na zaidi imekuwa ikishirikiana ktk mafunzo na mazoezi ya pamoja na majeshi mbalimbali ya East Africa na Afrika kwa ujumla.

..lakini kitu cha ajabu, na ambacho sikukitegemea, ni reaction ya baadhi ya wachangiaji ambao ni ndugu zetu toka baadhi ya nchi majirani. michango yao inaonyesha kwamba wamekerwa sana na kitendo cha cadets wao kupata mafunzo toka kwa majeshi yetu.

cc mossad007, lawmaina78, waltham, Geza Ulole, Ab-Titchaz


Usiwawaze sana JF ina-attract fanatics wa nchi jirani, sio wananchi wa kawaida, au general population. General population mara chache wakawa n amud awa kutafuta mabaya ya nchi flani wakayapost kwenye mtandandao wa nchi jirani.

Binafsi nina access ya internet 24/7/365 lakini sina muda wa kupost kwenye website ya rwanda,kenya au uganda. kwa kuwa yanayoendelea kule hayanihusu kama mtanzania. Lakini kuna njemba za rwanda na Kenya zinaamkia na kulala JF.kwa hiyo usiwatumie hawa kama barometer ya sentiments za wananchi wa nchi zao.Ingawa nakubaliana na wewe kuwa ni wachafuaji, but well, visebengo hawakosekani.
 
Back
Top Bottom