Kabla ya ndoa ujifunze lipi



Mbu i do agree na mengi ya ulio sema.... interest yangu ilikua piqued na
ile ya kusema tunaelekea kubaya... source Post # 51 ambapo nimenukuu hii

..mmetoka mbali na huko mnakoelekea kama siko?!

Which in some way nakubali... ila tu nilitaka nijue unaposema tunaelekea pabaya
ni sawa na mimi ninavyo elewa... karibu mengi umeongea ni kweli thus the No
Comment....



 
Reactions: Mbu


Mr Rocky haya basi kama kweli wanaume walikua wanafuata dini inavyosema
kwanini tu wameshikilia yale ya wao kua superior lakini mengine wasisitize
na hali yoote yametoka katika vitabu??

Na haya ya mfumo dume au jike ndio tatizo linakuja katika hizo concepts...
tatizo sio kwamba woote wawe juu... haiwezekani kabisa!!! Tatizo ni kua wanawake
wawe treated fairly... kuna mambo ambayo mwanamke anaweza kua juu
na mengine haipaswi kabisa awe juu... kikubwa awe treated fairly kama mwanadamu.
 
Mimi nitakuwa nina-refer kwenye maandiko tu lolz!!!

.....♫........♫.......'whistling!'......♫.....♫........


Sasa Mbu naona dada zangu wamekukalia kooni lol!!!

...si ndio ulivyotaka, ona sasa...aarrgghh!


Lol!!! Mbu unataka ku-revoke maandiko ya kwenye biblia unajua Mungu hapendi eheee lol!!!

...lol,...hivi wewe The Finest, kwanini hukunisomea "Miranda Law" kabla sijaanza kuchangia humu?
 

Ashadii nakubali mfumo dume umekuwa mbaya na unagharama zake
Ila tuu ni maelewano maana ndani ya familia hata mkielewana mwanaume anaweza kumsujudia mke wake na ikawa poa kabisa
tatizo ni lile la kuwapa nafasi kubwa na wengine kutaka kuchukua nafasi kubwa au waonekane wako juu na wao wawe na sauti katika mammbo yote kitu ambacho hakiwezekani
Tukubali mwanaume ana nafasi yake katika familia na mwanamke ana nafasi yake na kila mmoja aplay his or her game kwenye ndoa na mambo yote yatakuwa mema
 


Lol, ...hii ni mada yenye uzito tofauti na hii.
AD, kwenye maisha ya nyumba Mume na Mke kwa kujitambua au la
mtakuwa mnaishi mkiwa governed na miongozo ya kidini, kiserikali, kimila na tamaduni...

Matatizo ya ndoa yanasababishwa na misingi hiyo kuachwa kwa makusudi/bahati mbaya na mmoja,
au wote wawili mnaohusika kwenye ndoa. Bahati mbaya, baadhi ya wanawake wa kisasa haswa mjini
hawana uoga tena wa misingi ya kiimani, tofauti na zamani.

Hapo ndipo zinapo clash hii mambo ya kumtii mume kama vitabu vya dini, mila, desturi zinavyotuongoza
compared na "misinterpretation" ya baadhi ya maazimio ya kikao cha Beijing kuhusiana na usawa.
FYI, Beijing Declaration
 


Mr Rocky bado tuna safari ndefu... lakini dunia ni hii hii mambo yanaenda
yana evolve for the beta or worse... Katika eneo/jamii/institution yoyote ile
ni lazima awepo ambae ni kiongozi.. vivyo hivyo katika ndoa...

IMO naamini saana kua mwanaume lazima awe nguzo ya familia na awe juu yangu
lakini anapokua juu yangu sina maana anidharau/aniendeshe/aniamulie yooote/anitawale
au kunichukulia tu kama mwanadamu ambae niko kwa ajili yake... Lah!

Nataka awe juu yangu kua aniheshimu mimi kama mke na kama mwanadamu...
athamini mchango wangu woote (wa production and reproduction..).. anishirikishe
na kuniona ni rafiki, ajue kua nami kuna mambo nina msimamo nayo hivyo nae
a compromise pia... na most importantly anioneshe kweli yeye ni kiongozi kwa matendo
ndani na nje ya nyumba na kwamba mimi ni msaidizi ambae anataka niwepo na
nishiriki kwa yoote 24/7...
 

Mr Rocky kwa nini unahisi hivyo kuwa klama maandiko yangesemwa mwanamke badala ya mwanaume ingekuwa ajabu?? Sio kuwa ingezoeleka tu kama ilivyozoeleka kwa ilivyo sasa? What would be wrong kama mwanamke ndie angetakiwa kusujudiwa na mwanaume? nini mbaya ingekuwa na ingetofautianaje na ilivyo kwa wanaume sasa hivi??

Mwe!! Its just construction of something bana.......
 
Reactions: Mbu

Ashadii nakubaliana na wewe bado tuna safari ndefu sana
Ndoa ni shule ni darasa kwa watu ambao wako kwenye institution hiyo na kama mnakubaliana kuwa wote mko darasani mnajifunza ndoa yenu itakuwa nzuri sana na mtaishi maisha ya kupendana na kusahihishana kwa kila jambo.
Tukubali kuwa hakuna mbabe kwenye maisha ya ndoa si mwanaume si mwanamke wote mnatakiw amuwe kwenye status moja hapo mnawez akuona maisha ya ndoa ni mazuri ila mkiwa na ule ubwana na utwana maisha yatakuwa hovyo sana maana hakuna atakayekubali kushuka na kuwa mpole kwa mwenzake.
Kuna mambo mengi ambayo kila mmoja wenu anahitaji kujifunza kwa mwenzake na mkiwa katika hali hiyo ni furaha sana ila akiwemo mmoja wenu anayejiona yeye ni wa kutoa amri au kutoa maagizo na kuna wa kuyafuata bila kuuliza kama jeshini hiyo sio ndoa
 

...Loh...loh...lahasha!
Maandiko nimeyakuta na huenda yakanihukumu.

Ila kuna hii Beijing Declaration bro,...kwani unadhani mpaka
kina mama walipokaa chini kupanga maazimio yao hawakukumbuka kuna
miongozo tayari ya kidini? Hebu pitia tena hizo Declarations uone kama
zinapingana na maandiko au la,...
FYI; Beijing Declaration
 

Mwanajamiione duh umeniamulia
Ni just hisia tuu ila hata maandiko yanasema tukae na wanawake kwa akili
Mwanamke kupewa nguvu au kuambiwa kiuhalisia kuw ayuko juu ya mwanaume nafikiri unajua ni kitu gani kingetokea
Ila yaache maandiko yakae the way yalivyo kuwa mwanamke amsujudie mwanaume na mwanaume amheshimu mkewe
 

Mbu mkuu walijua na wanajua kuwa maandiko yanasema wazi kuwa mwanaume ni kichwa cha nyumba na mwanamke amsujudie mumewe.
Walijua kabisa kuwa wao wameambiwa kuwa watakuwa chini yetu ila kwa jeuri wakaweka hizo declaration zao ambazo mpaka leo zinashindwa kufanya kazi kwa kuwa hawajiamini na hawajaamini kuwa wanaweza bado wanahitaji wanaume kuwaambia kuwa wanaweza
 


I recipocrate 100% kwa hio black bolded... ni kweli kabisaa!!

In blue nafikiri kua sio wanaweke pekee hata wanaume pia hasa katika maswala ya imani...
But i have to differ with you kua haiendani na maswala ya Beijing Declaration.... Bahati
mbaya saana hio declaration was so mis intepreted na wanawake wenyewe (thus many
sides of feminism zipinganazo...) na kuchukuliwa very negatively na wanaume world over...

Whether kufuata vitabu vya dini au lah! (hata ki mila...) kumtii mume muhimu... for
their to be harmony hapo ndani kwenu... tatizo ni kwamba interpretation ya utii ndio
inakua issue... which line to cross na ipi usi cross ndio tatizo... kwamba unapo sema
utii ni kua uwe some kind of slave au kwamba umuheshim na kumtreat accordingly...
 


Mr Rocky sasa haya maneno uloongea ingekua wanaume na wanawake woote
tunaamini na kufuata hivyo unafikiri kungekua na shida katika ndoa??
Ushindani umekua mwiiingi mno - weeengi hata kujitapa na kujisifia
kua hawezi jishusha kwa mwenzie... inasikitisha kweli, kama once in a while
huwezi jishusha kwa mkeo/mumeo hamuwezi fika popote pale... labda
kama ndio wale wanaishi ndoa za kundimba dimba....
 
Asante sana mkuu,
Umetukumbusha ngoja tuanze mazoezi ambao hatujaingia kwenye ndoa
 
MJ1 kipindi hicho thamani ya mwanmke ilikua kwa ajili ya uwepo wa mwanaume yaani yeye hata naona alikua haruhusiwi hata kushika maandiko alikua anasomewa tu...yaani wanawake kweli tumetoka mbali aiseee...
Dada,lengo la kuumbwa mwanamke halijabadilika tangu mwanzo yaliyoandikwa kuhusu mwanamke na malengo ni yaleyale tangu karne ya kwanza mpaka leo hayabadiliki!Unless unamawazo kuwa vitabu vya Mungu vimepitwa na wakati!
 
Dada,lengo la kuumbwa mwanamke halijabadilika tangu mwanzo yaliyoandikwa kuhusu mwanamke na malengo ni yaleyale tangu karne ya kwanza mpaka leo hayabadiliki!Unless unamawazo kuwa vitabu vya Mungu vimepitwa na wakati!


You brother of mine labda kabla sijajibu hebu nipe lengo la mwanamke kuumbwa..??
 
According to the Bible mwanamke aliumbwa kama msaidizi wa mwanaume,full stop!!!!Kitakachozidi hapo ni ubatili!
 
According to the Bible mwanamke aliumbwa kama msaidizi wa mwanaume,full stop!!!!Kitakachozidi hapo ni ubatili!


Tuko pamoja ... kama msaidizi eeeh?? Sio mtumwa... ila zile mbavu tuliomba zile zinatu cost sometimes... Dah!
 
According to the Bible mwanamke aliumbwa kama msaidizi wa mwanaume,full stop!!!!Kitakachozidi hapo ni ubatili!

...lol, now this is getting interesting...!
awe msaidizi wa nini? naamini kuna nyongeza humo...
na huo usaidizi si una mipaka yake, una masharti na malengo yake, nk nk?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…