Uchaguzi 2020 Kadiri siku zinavyosogea wanachama na wafuasi wa CHADEMA wanatepeta

Uchaguzi 2020 Kadiri siku zinavyosogea wanachama na wafuasi wa CHADEMA wanatepeta

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Sio siri wafuasi na wanachama wa CHADEMA walijitutumua kuonyesha chama chao kipo hai na hili walilikomalia zaidi pale Lissu aliporejea toka Ubelgiji na kisha kuteuliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA.

Lakini kadiri siku za kupiga kura zinapokaribia,wanakata tamaa,nini kimewasabu? Au kwa sababu kila hoja wanayoibua inaonekana haina mashiko? Mfano waliibua hoja kuwa uwanja wa ndege Chato ulijengwa kwa upendeleo wa rais JPM kupendelea eneo analotoka, lakini CCM waliijibu hii hoja vizuri na kueleza jinsi ilivyojenga viwanja vya ndege sehemu mbali mbali kwa manufaa ya umma.

Ikaja hoja nyingine ambayo mpaka leo imewafanya waonekane ni majuha wa kisiasa, kwamba CCM inatekeleza miradi mikubwa kama kujenga Hospital, SGR, JNHPP kuwa ni miradi ya vitu na haina manufaa kwa watu, mgombea wao akaita ni white elephant projects. Hili limewatia aibu sababu miradi yote inayotekelezwa na CCM ni kwa manufaa ya watu. Na hili lipo wazi na wala halihitaji ufafanuzi. (Hii ni mifano tu).

Sasa wana hoja gani ya kuwanyanyua siku hizi 19 zilizobaki? Maana wanaibua mambo ambayo kwenye box la kura hayana msaada,mfano Lissu kuongea kiingereza na balozi wa Usa, je Maalim Seif na Mbatia hawakuongea nae Kiingereza?

Lakini hoja kuu hapa mbona wamekata tamaa na kutepeta maana bado kama wiki mbili.
 
Tulishaambiwa kufikia 2020 CHADEMA kitakuwa kimekufa,ongea habari za TLP/UDP vyama ambavyo viko hai,vyama ambavyo vina wagombea na wafuasi makini achana na CHADEMA chama kilichokufa.
 
Sema wamezidi kuimarika na kuwa na hamasa zaidi.
 
Tundu anaponzwa na ulimi wake
FB_IMG_16021517377590271.jpeg
 
Unapenda kuandika pumba tu kila wakati, mmeshalipwa buku saba naona Lumumba mmekuja kwa spidi.
 
Huu uzi huu mmmh walioutoa wanajua wanachokifanya kweli???
 
Kuna baadhi ya wagombea kidogo wa CHADEMA, wanafanya kampeni za kistarabu sana, kama huyu ndo pekee mpaka sasa naona kampeni zake wananchi wanafurahi kumskiliza! wengine wote ni wa kuonea huruma sana
 
Naona mlipigiana simu kabla ya kuanzisha uzi huu....
Haya MATAGA yanajaribu kujitutumua na kujifariji. Yanafahamu fika yalifanya siasa yenyewe tu na mgombea wao kwa miaka mitano!

Lakini mpaka sasa hayaelewi imekuaje bado kuna kundi kubwa la Watanzania wanataka mabadiliko na kuunga mkono upande wa pili wa shilingi. CCM itakufa tu. Hakuna namna. Imeshajichokea na kuzeeka.

Haina jipya kwa Watanzania na ndiyo maana kwenye kampeni zao za mwaka huu, wameona wakodi kundi kubwa la Wasanii wa Bongo fleva ili liwasaidie kuvutia Wahudhuriaji. Bila kutumia mbinu hii, aibu ingewaandama kwenye mikutano yao.
 
Back
Top Bottom